Mukulu wa Bakulu
JF-Expert Member
- Aug 12, 2014
- 4,052
- 12,906
Katika eneo unaweza kukuta watu wanajisifu basi ni wacheza drafti.
Ukifika kijiwe cha wacheza drafti kwa mara ya kwanza kama hujawahi kufika basi unaweza kukimbia ukijua hawa watu ni wauaji wakubwa maan hutaacha kusikia kauli kama nakuua, hili umekufa, usinichezee mimi mtu mbaya sana, mimi sio mtu wa kuchezea, hili huponi, hili sikuachi nakuua, yaani kwenye drafti kila mtu ni mbaya.
Binafsi napenda drafti, hua nikitoka kazini mapema nikafika maeneo ya nyumbani lazima nende kwenye vijiwe vya drafti nikafunge watu,pamoja na kua mimi sio mtaalam sana ila ukiingia kwenye 18 nakuua, huponi.
Mimi sio mtu mzuri kabisa kwenye drafti.
Wale wapenda drafti tupeane majina ya madrafti magumu kwenye play store niwe nacheza kuchangamsha akili.
Nakumbuka nikiwa form one niliwahi kumfunga bingwa wa kijiwe kwa ambae alikua anawapanga watu kama nyanya, hakuamini wakaenda kunishtaki home kua nimekalia draft sisomi, hiii ni baada ya mimi kudhalilisha wazee wa kijiweni😂😂.
Ukifika kijiwe cha wacheza drafti kwa mara ya kwanza kama hujawahi kufika basi unaweza kukimbia ukijua hawa watu ni wauaji wakubwa maan hutaacha kusikia kauli kama nakuua, hili umekufa, usinichezee mimi mtu mbaya sana, mimi sio mtu wa kuchezea, hili huponi, hili sikuachi nakuua, yaani kwenye drafti kila mtu ni mbaya.
Binafsi napenda drafti, hua nikitoka kazini mapema nikafika maeneo ya nyumbani lazima nende kwenye vijiwe vya drafti nikafunge watu,pamoja na kua mimi sio mtaalam sana ila ukiingia kwenye 18 nakuua, huponi.
Mimi sio mtu mzuri kabisa kwenye drafti.
Wale wapenda drafti tupeane majina ya madrafti magumu kwenye play store niwe nacheza kuchangamsha akili.
Nakumbuka nikiwa form one niliwahi kumfunga bingwa wa kijiwe kwa ambae alikua anawapanga watu kama nyanya, hakuamini wakaenda kunishtaki home kua nimekalia draft sisomi, hiii ni baada ya mimi kudhalilisha wazee wa kijiweni😂😂.