Kuna habari zinasambaa eti kuna watia nia wa kugombea ubunge kupitia CHADEMA wanajiita G55, na wanadai kuwa wapo watia nia 200. Hawa watu ni waongo na matapeli.
CHADEMA wana utaratibu wa kuwatambua watia nia kwa ngazi zote. Utaratibu wenyewe ni kama ifuatavyo:
1. Kwa ngazi ya ubunge, mwenye nia ya kugombea nafasi ya ubunge, anaandika barua kwa katibu wa chama wa Kanda, na nakala anaipeleka kwa Katibu Mkuu wa Chama.
2. Kwa wagombea wa udiwani, wanaandika barua kwa Katibu wa Chama Wilaya, na nakala wanaituma kwa Katibu wa Chama wa Kanda na kwa katibu wa chama wa Kata.
Mimi nilihudhuria kikao kilichoitishwa na Katibu Mkuu cha tarehe 03 APRIL 2025, kilichojumuisha watia nia wote na waliokuwa wagombea kwenye uchaguzi wa 2020.
Majimbo yote ya Tanganyika, na baadhi ya Zanzibar na Pemba, watia nia wake walihudhuria mkutano huo ulioitishwa na Katibu Mkuu, na hakuna hata jimbo moja kwa upande wa Tanganyika ambalo halina watia nia. Baadhi ya majimbo yalionekana kuwa na watia nia zaidi ya mmoja. Ukumbi ulijaa kwa kiasi cha baadhi kufikia hatua ya kukosa viti, na kutafutiwa toka nje.
Baada ya hotuba za viongozi wakuu wa chama, wanahabari waliombwa watoke ukumbini ili watia nia wawe huru kuongea lolote kuhusiana na msimamo wa chama uliopitishwa na Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu, wa NO REFORM NO ELECTION. Na nafasi ilitolewa kwa watia nia kwa kufuata kanda baada ya kanda.
MATOKEO:
Hakuna hata mtia mmoja aliyesema anapinga au hakubaliani na msimamo huo wa chama wa NO REFORM NO ELECTION. Ilifikia mahali mpaka naibu katibu mkuu akaomba anyoshe mkono yule tu ambaye anapinga msimamo wa NO REFORM NO ELECTION, kama unaunga mkono usinyoshe mkono, na kwamba chama kinataka kusikia maoni ya wanaotaka twende kwenye uchaguzi kwa mazingira yaliyopo. Mtia nia mmoja wa jimbo la Kilosa alinyosha mkono. Aliponyosha tu mkono, wengi wakageuka nyuma kutaka kumwona huyo anayepinga NO REFORM NO ELECTION. Naibu katibu mkuu alisistiza sana kuwa watu watulie, na wampe uhuru wote aliye na mawazo tofauti, na wajumbe wawe tayari kusikia hoja zake. Watu wakati wakisubiria kusikia hoja za huyo mtia nia, wakaishiwa nguvu, na kuishia kwenye vicheko, baada ya kumsikia mtia nia huyo akisema kuwa, yeye hataki tuingie kwenye uchanguzi kwa mazingira yaliyopo, ila anapinga mikutano ya NO REFORM NO ELE3CTION kutofika kwenye jimbo lake.
Kabla ya kikao, makatibu wote wa Kanda waliwakilisha orodha ya watia nia wote kwa katibu mkuu, na majina yale yalikuwa na makarani wanaotick kama mtia nia ayeandikwa amefika kwenye kikao. Hao wanaojiita watia nia wa G55, majina yao hayakuonekana kwenye orodha ya watia nia. Kimsingi, kwa taratibu za CHADEMA, kwa sababu hawakutimiza matakwa ya taratibu za kuweza kutambuliwa kama watia nia, hao G55 ni watia nia fake, bila shaka wamejipachika majina ya watia nia kwa lengo maalum, bila shaka, la kuvuta pesa kutoka upande ule wa giza, maana kipindi cha kuelekea kwenye uchaguzi kunakuwa na utapeli mwingi wa kujipatia malipo binafsi yasiyo halali, kupitia uchaguzi.
Wakati huu ambao CCM ipo desperate, yeyote ambaye yupo CHADEMA kitapeli, anaweza kuivuta pesa ya CCM kiurahisi sana, kwa kuiiaminisha CCM kuwa anao uwezo wa kuzuia au kuharibu maamuzi ya umma wa Watanzania kuunga mkono programu ya ukombozi wa Taifa ya NO REFORM NO ELECTION.
NO REFORM NO ELECTION, hakika inaenda kushinda. Ninashangaa sana ilivyopata mwitikio mkubwa sana kutoka kwa wananchi wa vyama vyote, mpaka baadhi ya wanaCCM. Leo hii pekee wanaCCM watatu tofauti wamenipigia simu na kuniambia, "jamani pambaneni sana ili tujikomboe". Hawa wanaCCM, mmoja aliwahi kuwa mbunge kipindi cha Mkapa, mmoja aliwahi kuwa DC wakati wa kipindi cha Magufuli.
Soma Pre GE2025 - DSM - CHADEMA yaandaa kikao maalum kuwaita viongozi wanaotaka kugombea Ubunge na Udiwani "kuwafundisha" kuhusu No Reforms No Election
CHADEMA wana utaratibu wa kuwatambua watia nia kwa ngazi zote. Utaratibu wenyewe ni kama ifuatavyo:
1. Kwa ngazi ya ubunge, mwenye nia ya kugombea nafasi ya ubunge, anaandika barua kwa katibu wa chama wa Kanda, na nakala anaipeleka kwa Katibu Mkuu wa Chama.
2. Kwa wagombea wa udiwani, wanaandika barua kwa Katibu wa Chama Wilaya, na nakala wanaituma kwa Katibu wa Chama wa Kanda na kwa katibu wa chama wa Kata.
Mimi nilihudhuria kikao kilichoitishwa na Katibu Mkuu cha tarehe 03 APRIL 2025, kilichojumuisha watia nia wote na waliokuwa wagombea kwenye uchaguzi wa 2020.
Majimbo yote ya Tanganyika, na baadhi ya Zanzibar na Pemba, watia nia wake walihudhuria mkutano huo ulioitishwa na Katibu Mkuu, na hakuna hata jimbo moja kwa upande wa Tanganyika ambalo halina watia nia. Baadhi ya majimbo yalionekana kuwa na watia nia zaidi ya mmoja. Ukumbi ulijaa kwa kiasi cha baadhi kufikia hatua ya kukosa viti, na kutafutiwa toka nje.
Baada ya hotuba za viongozi wakuu wa chama, wanahabari waliombwa watoke ukumbini ili watia nia wawe huru kuongea lolote kuhusiana na msimamo wa chama uliopitishwa na Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu, wa NO REFORM NO ELECTION. Na nafasi ilitolewa kwa watia nia kwa kufuata kanda baada ya kanda.
MATOKEO:
Hakuna hata mtia mmoja aliyesema anapinga au hakubaliani na msimamo huo wa chama wa NO REFORM NO ELECTION. Ilifikia mahali mpaka naibu katibu mkuu akaomba anyoshe mkono yule tu ambaye anapinga msimamo wa NO REFORM NO ELECTION, kama unaunga mkono usinyoshe mkono, na kwamba chama kinataka kusikia maoni ya wanaotaka twende kwenye uchaguzi kwa mazingira yaliyopo. Mtia nia mmoja wa jimbo la Kilosa alinyosha mkono. Aliponyosha tu mkono, wengi wakageuka nyuma kutaka kumwona huyo anayepinga NO REFORM NO ELECTION. Naibu katibu mkuu alisistiza sana kuwa watu watulie, na wampe uhuru wote aliye na mawazo tofauti, na wajumbe wawe tayari kusikia hoja zake. Watu wakati wakisubiria kusikia hoja za huyo mtia nia, wakaishiwa nguvu, na kuishia kwenye vicheko, baada ya kumsikia mtia nia huyo akisema kuwa, yeye hataki tuingie kwenye uchanguzi kwa mazingira yaliyopo, ila anapinga mikutano ya NO REFORM NO ELE3CTION kutofika kwenye jimbo lake.
Kabla ya kikao, makatibu wote wa Kanda waliwakilisha orodha ya watia nia wote kwa katibu mkuu, na majina yale yalikuwa na makarani wanaotick kama mtia nia ayeandikwa amefika kwenye kikao. Hao wanaojiita watia nia wa G55, majina yao hayakuonekana kwenye orodha ya watia nia. Kimsingi, kwa taratibu za CHADEMA, kwa sababu hawakutimiza matakwa ya taratibu za kuweza kutambuliwa kama watia nia, hao G55 ni watia nia fake, bila shaka wamejipachika majina ya watia nia kwa lengo maalum, bila shaka, la kuvuta pesa kutoka upande ule wa giza, maana kipindi cha kuelekea kwenye uchaguzi kunakuwa na utapeli mwingi wa kujipatia malipo binafsi yasiyo halali, kupitia uchaguzi.
Wakati huu ambao CCM ipo desperate, yeyote ambaye yupo CHADEMA kitapeli, anaweza kuivuta pesa ya CCM kiurahisi sana, kwa kuiiaminisha CCM kuwa anao uwezo wa kuzuia au kuharibu maamuzi ya umma wa Watanzania kuunga mkono programu ya ukombozi wa Taifa ya NO REFORM NO ELECTION.
NO REFORM NO ELECTION, hakika inaenda kushinda. Ninashangaa sana ilivyopata mwitikio mkubwa sana kutoka kwa wananchi wa vyama vyote, mpaka baadhi ya wanaCCM. Leo hii pekee wanaCCM watatu tofauti wamenipigia simu na kuniambia, "jamani pambaneni sana ili tujikomboe". Hawa wanaCCM, mmoja aliwahi kuwa mbunge kipindi cha Mkapa, mmoja aliwahi kuwa DC wakati wa kipindi cha Magufuli.
Soma Pre GE2025 - DSM - CHADEMA yaandaa kikao maalum kuwaita viongozi wanaotaka kugombea Ubunge na Udiwani "kuwafundisha" kuhusu No Reforms No Election