Zitto
Former MP Kigoma Urban
- Mar 2, 2007
- 1,562
- 10,880
MSIMAMO WA ACT-WAZALENDO;
“HAKUNA TUME HURU, HAKUNA UCHAGUZI UTAKAOKUBALIKA NCHINI” WAZIRI SELEMANI JAFO AWAJIBIKE KWA KUHARIBU UCHAGUZI.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Imetolewa leo Tarehe 11/11/2019
1. Mchakato wote wa Uchaguzi uanze upya: Lazima yote yaliyofanyika chini ya utaratibu wa sasa yafutwe, uchaguzi uahirishwe na mchakato wa uchaguzi uanze upya.
2. Wasimamizi wa Uchaguzi wote walioharibu mchakato wa uchaguzi huu wawajibishwe ili kukomesha tabia hii inayoharisha amani ya nchi.
3. Zitungwe Kanuni Mpya za Uchaguzi kwa maridhiano na makubaliano na Wadau wote hususani vyama vya siasa.
4. Iundwe Kamati Huru ya kusimamia Uchaguzi: Lazima maamuzi katika hatua zote za Uchaguzi yawe ya maridhiano na makubaliano ya vyama sio TAMISEMI, ambao hawana uhuru, uwazi na wala uwezo wa kutenda haki.
5. Waziri Selemani Jafo aitishe kikao cha pamoja cha vyama vyote vya siasa ili kukubaliana juu ya namna ya kusonga mbele Kwa utekelezaji wa mapendekezo yetu hayo. Kinyume na hivyo sisi ACT Wazalendo hatutashiriki Uchaguzi huu wa Tarehe 24 Novemba, 2019.
6. Kutokana na O-TAMISEMI kuwa Wizara iliyopo chini ya OFISI YA RAIS, tunamtaka Rais Magufuli afikirie upya kuiondoa ofisi hii Ikulu na kuirejesha kwa Waziri Mkuu kama ilivyokuwa awali ili ‘TAASISI YA URAIS IEPUKANE NA KASHFA ZA UHARIBIFU WA DEMOKRASIA NCHINI’
7. Tunatoa wito kwa Vyama vyote vya Siasa kutokubali hadaa ya Waziri Jafo na kutumia nafasi hii kuwa pamoja kudai Tume Huru ya Uchaguzi ili Uchaguzi wa mwaka 2020 usiwe na dosari tulizoshuhudia sasa. Bila Tume Huru ya Uchaguzi pasiwe na Uchaguzi wowote nchini. Viongozi wa Kitaifa wa vyama watoke na tamko la pamoja kutaka TUME HURU YA UCHAGUZI.
HITIMISHO
Ndugu wanahabari, ni wazi mchakato wa uchaguzi huu wa serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji, hauwezi kuendelea kwa haki hasa baada ya wananchi kuonyesha hisia zao za kuichoka CCM katika hatua za awali katika uandikishaji wapiga kura. Serikali ya CCM itaendelea na gilba zake kuhakikisha inapoka demokrasia ili kujihalalishia ushindi kwa kutumia mabavu ya dola na mtandao mpana uliowekwa kwa kazi hiyo. Ndio maana vitisho vya waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola na DCI Robert Boaz vinaendelea kila uchao.
Tunaendelea kusisitiza msimamo wetu wa kujitoa kwenye uchaguzi na kuwataka wanachama wetu wote nchi nzima kuendelea kutekeleza agizo la Chama la kuandika barua za kujitoa kwenye uchaguzi. Aidha tunatoa wito kwa wanachama wetu kubaini wagombea bandia wa CCM waliopewa fomu kwa kugushi mihuri na barua za utambulisho maeneo kadhaa nchini ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.”
….
Joran Bashange
MWENYEKITI WA KAMATI YA KAMPENI NA UCHAGUZI TAIFA.
“HAKUNA TUME HURU, HAKUNA UCHAGUZI UTAKAOKUBALIKA NCHINI” WAZIRI SELEMANI JAFO AWAJIBIKE KWA KUHARIBU UCHAGUZI.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Imetolewa leo Tarehe 11/11/2019
1. Mchakato wote wa Uchaguzi uanze upya: Lazima yote yaliyofanyika chini ya utaratibu wa sasa yafutwe, uchaguzi uahirishwe na mchakato wa uchaguzi uanze upya.
2. Wasimamizi wa Uchaguzi wote walioharibu mchakato wa uchaguzi huu wawajibishwe ili kukomesha tabia hii inayoharisha amani ya nchi.
3. Zitungwe Kanuni Mpya za Uchaguzi kwa maridhiano na makubaliano na Wadau wote hususani vyama vya siasa.
4. Iundwe Kamati Huru ya kusimamia Uchaguzi: Lazima maamuzi katika hatua zote za Uchaguzi yawe ya maridhiano na makubaliano ya vyama sio TAMISEMI, ambao hawana uhuru, uwazi na wala uwezo wa kutenda haki.
5. Waziri Selemani Jafo aitishe kikao cha pamoja cha vyama vyote vya siasa ili kukubaliana juu ya namna ya kusonga mbele Kwa utekelezaji wa mapendekezo yetu hayo. Kinyume na hivyo sisi ACT Wazalendo hatutashiriki Uchaguzi huu wa Tarehe 24 Novemba, 2019.
6. Kutokana na O-TAMISEMI kuwa Wizara iliyopo chini ya OFISI YA RAIS, tunamtaka Rais Magufuli afikirie upya kuiondoa ofisi hii Ikulu na kuirejesha kwa Waziri Mkuu kama ilivyokuwa awali ili ‘TAASISI YA URAIS IEPUKANE NA KASHFA ZA UHARIBIFU WA DEMOKRASIA NCHINI’
7. Tunatoa wito kwa Vyama vyote vya Siasa kutokubali hadaa ya Waziri Jafo na kutumia nafasi hii kuwa pamoja kudai Tume Huru ya Uchaguzi ili Uchaguzi wa mwaka 2020 usiwe na dosari tulizoshuhudia sasa. Bila Tume Huru ya Uchaguzi pasiwe na Uchaguzi wowote nchini. Viongozi wa Kitaifa wa vyama watoke na tamko la pamoja kutaka TUME HURU YA UCHAGUZI.
HITIMISHO
Ndugu wanahabari, ni wazi mchakato wa uchaguzi huu wa serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji, hauwezi kuendelea kwa haki hasa baada ya wananchi kuonyesha hisia zao za kuichoka CCM katika hatua za awali katika uandikishaji wapiga kura. Serikali ya CCM itaendelea na gilba zake kuhakikisha inapoka demokrasia ili kujihalalishia ushindi kwa kutumia mabavu ya dola na mtandao mpana uliowekwa kwa kazi hiyo. Ndio maana vitisho vya waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola na DCI Robert Boaz vinaendelea kila uchao.
Tunaendelea kusisitiza msimamo wetu wa kujitoa kwenye uchaguzi na kuwataka wanachama wetu wote nchi nzima kuendelea kutekeleza agizo la Chama la kuandika barua za kujitoa kwenye uchaguzi. Aidha tunatoa wito kwa wanachama wetu kubaini wagombea bandia wa CCM waliopewa fomu kwa kugushi mihuri na barua za utambulisho maeneo kadhaa nchini ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.”
….
Joran Bashange
MWENYEKITI WA KAMATI YA KAMPENI NA UCHAGUZI TAIFA.