Hakuna tatizo miradi mikubwa ya kimkakati kuelekezwa Chato

Hata mkitaka kuhamishia Bunge la Tanzania Chato hakuna TATIZO.
Nimekaa nakutafakari sasa tunakoelekea sio pazuri.

Serikali inajenga hospitali ya rufaa Chato, wafuasi wa upinzani wanazodoa na kupinga.

Kwani hii Hospitali haitawahudumia Watanzania?

Kwani kujengwa Chato ndio tatizo?

Mfano, mkazi wa Dar es Salaam akiwa Runzewe anaendesha truck kwenda Rwanda,ghafla anapata ajali,Je hawezi kupelekwa Chato na kupata huduma za tiba? Huu ni mfano.

Nini hasa kinawafanya mzodoe na kupinga ujenzi wa hii hospitali muhimu? Rais JPM kuwa ametokea Chato?

Nadhani ni kipindi muafaka Askofu Bagonza na Askofu Mwamakula kuwaombea hawa vijana waliokengeuka kisiasa ili uzalendo uwarudie na kuipenda nchi yao.
 
Lile jengo la TRA chato,yani nyerere aliona mbali ndugu zetu wasukuma,wachaga,wahaya na wanyakusya hawapaswi kupewa madaraka makubwa ya ukuu wa Nchi

Hivi unayo yasema hapa yameandikwa kwenye katiba hipi?

Mbona Nyerere mwenyewe alikuwa anakemea dhana ya kubaguwa watu kwa misingi ya ukabila - Nyerere alisema wazi wazi kwamba tusimkatae mtu kuteuliwa kiti cha Urais kutokana na asili ya kabila lake.
 
Mwafrika akiwa kwenye nafasi kupapendelea kwao hiyo ni jambo la kawaida
Asipopapendelea napo mtakuja mlaumu na kumsema+kumcheka
Kuna mwingine yuko kwenye nafasi kubwa lakini kwao hapafanyi lolote huo ni ubinafsi

Nyumbani kwanza kwa maisha ya badaye

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
Umenena kweli.
 
Kwani anayepeleka miradi ni Magufuli au serikali?
Unakosea kusema sehemu nyingine hakuna miradi. Mradi wa maji Shinyanga to Tabora? Mradi wa meli ziwa Nyassa?

Flyover ya Ubungo ni sawa na bil 9 zinazojenga Hosp Chato?
Hospital ya Chato ni zaidi ya bil 30. Halafu flyover ni mkopo pia.
 
Hospitali ya rufaa kanda ya ziwa iko Bugando Mwanza.
Kanda ambazo hazina hospitali za rufaa za kanda ni:
1. Kanda ya magharibi: mikoa ya Kigoma, Rukwa, Katavi (hata Tabora ni mbali na Dodoma na Mwanza)
2. Kanda ya kusini mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma

Nilitarajia kama hospitali za rufaa za kanda ni kipaumbele, basi zingeanzia katika kanda hizo ambazo hazina
Right. Mtwara iko kwenye ujenzi mwaka wa tatu huu na sidhani kama ya mabilioni yote.

Huko kigoma wangewapelekea ingekuwa jambo la heri sana.
 
Jirani yake kuna hospitali kubwa ya rufaa ya kanda, Bugando! Nani ataenda chato Na si Bugando?
Next. Serikali itajitoa Bugando halafu iwatake wafanyakazi waende Chato. Watahama ila hawatamisha familia zao kijijini.
 
Yaani hospital ya rufaa ya kanda inajengwa kijijini na still huoni tatizo? Tupe sababu za msingi on why ni chato na si mwanza, Shinyanga, Tabora Geita au Kigoma mjini.
Kwani tuwabague watu wa vijijini? Watoke kijijini kufata huduma bora mjini, kwani tukibadilika itakuaje jamani? Yaani huduma zote kubwa ziwepo mjini tu?
 
Yaani hospital ya rufaa ya kanda inajengwa kijijini na still huoni tatizo? Tupe sababu za msingi on why ni chato na si mwanza, Shinyanga, Tabora Geita au Kigoma mjini.
Ingejengwa msoga au Kijiji unachotoka wewe pia ungelalamika mkuu?
 
Hospitali ya rufaa kanda ya ziwa iko Bugando Mwanza.
Kanda ambazo hazina hospitali za rufaa za kanda ni:
1. Kanda ya magharibi: mikoa ya Kigoma, Rukwa, Katavi (hata Tabora ni mbali na Dodoma na Mwanza)
2. Kanda ya kusini mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma

Nilitarajia kama hospitali za rufaa za kanda ni kipaumbele, basi zingeanzia katika kanda hizo ambazo hazina
Yani umejibu kisomi sana...!
 
Kuna miradi mingine angepeleka Geita Mji (Mjini), yeye kaitenga Geita live live anapeleka wilayani chato na wala sio mkoani yaani Geita Mji (mjini) , mfano uwanja wa ndege chato, hospital ya rufaa chato, chuo cha utumishi chato, Veta chato, Burigi chato, Mwalo chato, nilikuwa naongea na jamaa wa Geita anasema anfanya hivyo kwa sababu kina msukuma na group lake kipindi anaomba udhamini walimkimbia akakuta Hewa office ya ccm , lakini yeye ameshakuwa Rais tayari hakuna umuhimu wa kuitenga Geita , angetawanya ili watu wote wale, mimi sina shida na Burigi hifadhi, Rubondo, Mwalo wa chato maana haya yako chato huwezi hamisha, laikini uwanja wa Ndege , hospital ya rufaa, chuo cha utumishi, hivi vitatu pia kimojawapo au viwili angepeleka Geita mjini.

Hatukatai Chato sio Tanzania, ni Tanzania ,lakini mtawanyo wa maendeleo kwa wote ni vema zaidi, hapa tunaongea kigoma, tabora, mpanda hakuna hospital ya kanda basi nako sio afikirie ajenge walau watu watakuwa na imani na anavyofanya.
 
Hakuna mfumuko wa bei na PAYE ilirekebishwa budget ya 2020 so kuna increment ya Net Pay
1610443274614.png
 
Nimekaa nakutafakari sasa tunakoelekea sio pazuri.

Serikali inajenga hospitali ya rufaa Chato, wafuasi wa upinzani wanazodoa na kupinga.

Kwani hii Hospitali haitawahudumia Watanzania?

Kwani kujengwa Chato ndio tatizo?

Mfano, mkazi wa Dar es Salaam akiwa Runzewe anaendesha truck kwenda Rwanda,ghafla anapata ajali,Je hawezi kupelekwa Chato na kupata huduma za tiba? Huu ni mfano.

Nini hasa kinawafanya mzodoe na kupinga ujenzi wa hii hospitali muhimu? Rais JPM kuwa ametokea Chato?

Nadhani ni kipindi muafaka Askofu Bagonza na Askofu Mwamakula kuwaombea hawa vijana waliokengeuka kisiasa ili uzalendo uwarudie na kuipenda nchi yao.
Mtu mzima anapotoa mifano ya kitoto tunamwita mwehu! Nchi hii kuna miji mingi mikubwa iliyo na idadi kubwa ya watu lakini imeachwa kwa sababu za ubinafsi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom