Dr leader
JF-Expert Member
- Jun 28, 2016
- 1,041
- 1,294
Acha tufunge maneno vizuri leo.
Hivi unajua kuna watu wanaoa kama vile wanafanya biashara ya madawa ya kulevya? Yaani, kimyakimya, bila mashahidi, bila kujulisha hata mbwa wa jirani. "ndoa ya siri."
Sasa hivi bwana, kuna mtu anaweza kupata ndoa nyuma ya pazia alafu kesho anaanza kusema "Nimeoa," huku hata dada zake hawajui kama alitoa mahari au alienda kanisani/msikitini. Ukimuuliza anasema, "tulielewana, ndoa ni kati ya watu wawili." Hapo ndo unajua ulimwengu umeharibika.
Ndoa si kamchezo ka bahati nasibu. Ndoa ni heshima, inataka uiheshimu na uiheshimishe. Siri ni kwa mapenzi, si kwa ndoa. Ukioa kimya kimya, kesho utalia kimya kimya. Ukiolewa kwa siri, kesho ukiachwa huwezi hata kuandikwa WhatsApp status.
Jamii yetu inahitaji uwazi. Utu, siyo ughost.
Hakuna ndoa ya siri. Kama huna ujasiri, usiingie kwenye ndoa.
🖋️ Abuuabdillah
#Mahusianoseason
Hivi unajua kuna watu wanaoa kama vile wanafanya biashara ya madawa ya kulevya? Yaani, kimyakimya, bila mashahidi, bila kujulisha hata mbwa wa jirani. "ndoa ya siri."
Sasa hivi bwana, kuna mtu anaweza kupata ndoa nyuma ya pazia alafu kesho anaanza kusema "Nimeoa," huku hata dada zake hawajui kama alitoa mahari au alienda kanisani/msikitini. Ukimuuliza anasema, "tulielewana, ndoa ni kati ya watu wawili." Hapo ndo unajua ulimwengu umeharibika.
Ndoa si kamchezo ka bahati nasibu. Ndoa ni heshima, inataka uiheshimu na uiheshimishe. Siri ni kwa mapenzi, si kwa ndoa. Ukioa kimya kimya, kesho utalia kimya kimya. Ukiolewa kwa siri, kesho ukiachwa huwezi hata kuandikwa WhatsApp status.
Jamii yetu inahitaji uwazi. Utu, siyo ughost.
Hakuna ndoa ya siri. Kama huna ujasiri, usiingie kwenye ndoa.
🖋️ Abuuabdillah
#Mahusianoseason