MTK
JF-Expert Member
- Apr 19, 2012
- 8,927
- 6,850
Tht sounded like a bad dream, mhusika hana jinsi ya kukwepa dhambi ya mautiWana JF.
Mkasa huu haunihusu mimi kwa namna yoyote ile.
Nime upata toka kwa mtu aliye kua akitoa ushuhuda na ulinitoa machozi sana.
Soma mwenyewe.
###############....MWANZO....######################################
Hakukuwa na mwanamke ambaye nilikuwa simpendi
kama mama yangu.
Yeye alikuwa masikini wa kutupwa huku uso wake ukiwa unatisha
kwa kuwa tu hakuwa na jicho moja.
Kila nilipokuwa nikimuona nilikuwa nikimkasirikia sana.
Alikuwa akijaribu kunionyesha mapenzi kama mtoto wake lakini
kwangu sikuwa nikitaka kumuona kabisa.
Kuna siku nilikaa nae chini na kumwambia kwamba
nilitamani sana kuwa na furaha katika maisha, akaniuliza kitu gani
kifanyike ili niwe na furaha, kiukweli nikamwambia kwamba kama
angekufa muda huo, hakika ningefurai milele.
Nikafanikiwa kusoma chuo na kwenda nchini Afrika Kusini
kusomea sheria, nilifurahi sana. Sikutaka kurudi nyumbani,
nikaoa huko huko na kupata watoto.
Katika maisha yangu yote hayo hakika sikumkumbuka kabisa mama
yangu, nilikuwa nikitamani sana afe ili niwe na furaha.
Nikafanikiwa kupata watoto wawili huku nikiwa nimejenga
nyumba ya kifaari na kuwa na utajiri mkubwa.
Kuna siku nikasikia mlango ukigongwa, watoto wangu wakaenda
kuufungua mlango, ALIKUWA NI MAMA YANGU amekuja
kunitembelea.
Watoto wangu wakaanza kulia kwani
walikuwa wakimuogopa sana mama yangu kutokana na hali
ya kukosa jicho aliyokuwa nayo, nikaamua kwenda
mlangoni, nilipomuona, alifikiri ningetabasamu, nikamfokea
kwa haira sana "TOKA NYUMBANI KWANGU KINYAGO
WEWE UNAWATISHA WATOTO
WANGU".
Kwa sauti iliyojaa upole, mama yangu akaniambia
"SAMAHANI BABA. NAFIKIRI NITAKUWA NIMEKOSEA NJIA" hapo hapo akaondoka.
Nikafanikiwa kutembelea nchini Tanzania, na moja kwa
moja nikaanza kwenda kwenye nyumba ile tuliyokuwa
tunakaa.
Majirani zangu wakaniambia kuwa mama yangu alikuwa amefariki kwa
kuwa tundu la jicho lake lilikuwa limeharibu hadi mishipa ya fahamu,
WALA SIKUHUZUNIKA KABISA ZAIDI YA KUTABASAMU. Hapo ndipo
waliponiletea barua ambayo aliiandika mama yangu na kunipa.
Barua ile ilikuwa imeandikwa hivi.
Mwanangu mpendwa.
Najua kwamba katika maisha yako ulikuwa ukinichukia sana
ila amini kwamba nilikuwa nikikupenda sana.
Ulipokuwa mtoto ulipata ajali, jicho lako likapasuka ila kwa kuwa
nilikuwa sitaki uishi maisha ya kuwa na jicho moja, nikaamua
kutoa jicho langu na kuwekewa wewe ili tu uweze
kuuona ulimwengu kwa macho yote mawili.
Sikutaka kujali ningepata matatizo gani lakini
niliamini kwamba wewe ndiye ungekuwa furaha yangu hasa
kila nitakapokuona unauangalia ulimwengu huu huku ukitumia jicho langu moja.
Mimi mama yako Mpendwa....
###########.....MWISHO...########################
Labda kwa namna moja ama nyingine ume waacha wazazi wako kijijini
wakiteseka huku wewe ukila maisha matamu mjini.
Unajua walitoa upendo kiasi gani kwako kukusaidia kufika hapo ulipo fikia?
Labda hawakukusaidia,....lakini unadhani kuwachunia ni adhabu inayo faaa kabisa?
Mungu na akufungue ufahamu wako,UITAMBUE AMRI YAKE PEKEE YENYE AHADI,....uwapende
na kuwaheshimu baba na mama yako ili upate heri na miaka mingi duniani.
God bless you.