1kush africa
JF-Expert Member
- Dec 13, 2016
- 9,326
- 12,691
Mkuu umenihamasisha kwelikweliHii movie nimeiona zamani hebu nijaribu kukumbuka leo...
Utamu wa hii movie kwanza ni story yake ambayo ni kisa cha kweli kilichotokea katika vita kuu ya pili ya dunia.
Story iko hivi, wanajeshi wa Marekani wakiwa vitani wanapigwa kipondo cha kufa mtu hali iliyopelekea wengi wao kupoteza maisha.
Sasa baadhi ya miili inarejeshwa kwenda kuzikwa Marekani.
Mama mmoja anapewa habari kuwa watoto wake watatu wamefariki katika uwanja wa kivita, mama analia sana lakini anawaambia watoto wake walikuwa wanne, hivyo kuna mmoja atakuwa aksalia kwenye uwanja wa kivita.
Basi kinatumwa kikosi kwa ajili ya kwenda kumtafuta mtoto wa nne wa yule mama, ambaye ni private ryan.
Wanamkuta private ryan katika uwanja wa vita anakiwasha kweri kweriiii (in mwendazake's voice) katika hali ya kushangaza private ryan anagoma kurudi nyumbani
Balaa sasa lipo hapo...
Ngoja niipakue