Tlaatlaah
JF-Expert Member
- May 18, 2023
- 36,155
- 30,836
Ndugu wadau wa heshima na wa maana sana JF,
Ni vizuri kama waTanzania kuelimishana na kufahamishana kinagaubaga kwamba maandamano ya aina yoyote nchini kwetu ni haki ya kila kundi, na ni shartiyafanyike kulingana na sheria za nchi, lakini pia yawe yenye kibali kutoka kwenye vyombo vya ulinzi na usalama hususani polisi, ili hatimae yapewe baraka za kisheria, yalindwe na yafanyike katika hali ya utulivu, usalama na amani.
Kwamfano yapo maandamano yaliyofanyika mwaka mwaka uliopita 2024, yakiongozwa na miongoni mwa vyama vya siasa nchini, ambayo kwakweli yalifuata utaratibu wote wa kisheria na kiusalama na hatimae yakafanyika kwa amani karibu katika majiji yote humu nchini. Hapakutokea vurugu wala uharibifu wa aina yoyote wa mali au miundombinu bali yalifanyika kwa utulivu na usalama wa kiwango cha juu sana na viongozi wa maandamano yale walijulikana kote nchini, lakini pia malengo ya maandamano yale hayakua ya kificho bali yalikua ya wazi kwa umma na dunia nzima.
Kama mTanzania mzalendo,
napenda kuwafahamisha wadau wa JF na waTanzania wote wema kwa ujumla kwamba, sina shaka yoyote kwamba maandamano yasiyo na kibali wala ulinzi wa vyombo vya ulinzi na usalama nchini, kamwe hayataruhusiwa kufanyika Tanzania, zaidi sana maandamano yasio na uongozi unaotambulika na yaliyo na malengo ya kificho, kamwe hayataruhusiwa kufanyika kwenye ardhi ya amani ya Tnazania.
Niwasihi tu mamluki wote wa maandamo haramu Tanzania,
Hakuna kikundi cha mercenaries, vibaraka, maharamia au magaidi kitakachoruhusiwa kufanya aina yoyote ya maandamano popote Tanzania. Hakuna maandamano duniani yenye lengo la kudai uhuru na haki ya kupora mali, kuharibu mali na miundombinu ya umma na binafsi au kuvuruga amani na uTulivu miongoni mwa wananchi Tanzania, hiyo haitatokea Tanzania.
Amani na utulivu miongoni mwa waTanzania vitalindwa kwa nguvu na gharama yoyote ile.
Na muhalifu yeyote atakaethubutu kulazimisha yaliyo kinyume na sheria au kufanya mikusanyiko yenye viashiria vya fujo, vurugu uharibifu au kuhatarisha amani ya nchi atakabiliwa kwa mujibu wa sheria na kushughulikiwa na vyombo vya ulinzi na usalama bila kumchelewesha, kumuonea haya wala huruma kulingana na taratibu za kiusalama.
Mungu Ibariki Tanzania
Ni vizuri kama waTanzania kuelimishana na kufahamishana kinagaubaga kwamba maandamano ya aina yoyote nchini kwetu ni haki ya kila kundi, na ni shartiyafanyike kulingana na sheria za nchi, lakini pia yawe yenye kibali kutoka kwenye vyombo vya ulinzi na usalama hususani polisi, ili hatimae yapewe baraka za kisheria, yalindwe na yafanyike katika hali ya utulivu, usalama na amani.
Kwamfano yapo maandamano yaliyofanyika mwaka mwaka uliopita 2024, yakiongozwa na miongoni mwa vyama vya siasa nchini, ambayo kwakweli yalifuata utaratibu wote wa kisheria na kiusalama na hatimae yakafanyika kwa amani karibu katika majiji yote humu nchini. Hapakutokea vurugu wala uharibifu wa aina yoyote wa mali au miundombinu bali yalifanyika kwa utulivu na usalama wa kiwango cha juu sana na viongozi wa maandamano yale walijulikana kote nchini, lakini pia malengo ya maandamano yale hayakua ya kificho bali yalikua ya wazi kwa umma na dunia nzima.
Kama mTanzania mzalendo,
napenda kuwafahamisha wadau wa JF na waTanzania wote wema kwa ujumla kwamba, sina shaka yoyote kwamba maandamano yasiyo na kibali wala ulinzi wa vyombo vya ulinzi na usalama nchini, kamwe hayataruhusiwa kufanyika Tanzania, zaidi sana maandamano yasio na uongozi unaotambulika na yaliyo na malengo ya kificho, kamwe hayataruhusiwa kufanyika kwenye ardhi ya amani ya Tnazania.
Niwasihi tu mamluki wote wa maandamo haramu Tanzania,
Hakuna kikundi cha mercenaries, vibaraka, maharamia au magaidi kitakachoruhusiwa kufanya aina yoyote ya maandamano popote Tanzania. Hakuna maandamano duniani yenye lengo la kudai uhuru na haki ya kupora mali, kuharibu mali na miundombinu ya umma na binafsi au kuvuruga amani na uTulivu miongoni mwa wananchi Tanzania, hiyo haitatokea Tanzania.
Amani na utulivu miongoni mwa waTanzania vitalindwa kwa nguvu na gharama yoyote ile.
Na muhalifu yeyote atakaethubutu kulazimisha yaliyo kinyume na sheria au kufanya mikusanyiko yenye viashiria vya fujo, vurugu uharibifu au kuhatarisha amani ya nchi atakabiliwa kwa mujibu wa sheria na kushughulikiwa na vyombo vya ulinzi na usalama bila kumchelewesha, kumuonea haya wala huruma kulingana na taratibu za kiusalama.
Mungu Ibariki Tanzania
