Hakuna kazi ngumu kama kuwatetea Simba na coach Fadlu

Hakuna kazi ngumu kama kuwatetea Simba na coach Fadlu

ngara23

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2019
Posts
15,774
Reaction score
35,994
Simba imepokea kipigo cha 6 mfululizo na coach Fadlu akifingwa mara 4 mfulilizo peke yake bila kupata goli lolote Kwa Yanga,

Coach Fadlu amefungwa na makocha 4 tofauti wa Yanga
Gamondi kamfunga
Ramovic kamfunga
Milouf Hamdi kamfunga
Roman Folz kamfunga

Tuliaminishwa
1. Usajili huu kuafanya coach mwenyewe.
Kwamba alikutana na tajiri Mo Dubai akampa mkwanja asajili mwenyewe

2. Uongozi mpya
Cresencius Magori na Babra ndani ila kipigo kimeendelea

3 Kambi Bora zaidi huko Egypt wakati wenzako wakiwa Avic town Kigamboni

4. Maboresho ya bench la ufundi

5. Wadhamini wakubwa betway, diadora na jayrutty wamemwaga mapesa

6. Bonuses na hamasa Kwa wachezaji.
Zamani tuliambiwa wachezaji walicheza vibaya Kwa kuwa hawakulipwa Kwa wakati, Sasa jayrutty pekee alitangaza kuweka milion 100 na bunus ya kipa 10m

7 Simba walidai wamefukuza maduka, yaani wachezaji walikuwa wakiuza mechi kama wanavodai na Kwa Sasa Simba ni safi, akina Inonga, Mkude, Tshabalala, Chama n.k

8. Mo alitangaza kurudi Kwa kushindo, baada ya kuwa alitangaza kususia timu

9 Simba walimuunga mkono Rais Karia kwenye uchaguzi tofauti na Yanga waliogoma na kuonekana watakuwa na msimu magumu kutokana na kumkataa Karia na uchaguzi wake wa kihuni

10. Simba wana wachezaji waliocheza FIFA world cup kama Rushaina, Maema na Mwalimu ila Bado wanapakatwa na Yanga ambaye hana mchezaji hata mmoja huko FIFA world cup
 
Nikitulia nitarejea hapahapa🥴
IMG-20250917-WA0080.jpg
 
Na mashabiki Wa simba tumekataa kabisa kukiri kua ushambuliaji tuna wachezaji wabovu ambao hawawezi kukupa matokeo

Ilianza simba day tukasema mbona mpira Wa hovyo huu pre season Egypt ilikua na maana gani hasa wakati pre season ndo inatumika kuandaa timu
Unajua wakasemaje!!!!! Hili lilikua ni bonanza na pia simba ana mechi dhidi ya yanga tar 16 kocha huwezi kuexpose mbinu
Wakati huo mjumbe Wa bodi ya wakurugenzi azim dewji alikua kakiri simba day wamecheza mpira Wa hovyo asa sijui na yeye alikua hajui hili

Haya imefika siku ambayo ulikua umeficha mbinu umepigwa then kisingizio kimekua ni refa kwamba goli lilikua offside Haya we hata ambalo ulifunga likakataliwa hamna

Yani kukubali kwamba kuna mapungufu tumegoma kabisa intake ya mwisho ambayo simba ilisajili viungo washambuliaji at least wenye football IQ ilikua ni intake ya kina sakho,Duncan nyoni,banda,inonga baada ya hapo hamna kitu

Kuna chali Fulani nakumbuka aliwahi Fanya vibaya mtihani Wa form 4 kumuuliza vipi akadai coz alikataliwa kufanya mitihani ya sayansi phy na chem then nikamuuliza vipi Haya masomo yaliyobaki mbona na yenyewe ulifeli kulikua na uhusiano gani hana majibu mentality hii ndo iliyopo simba nw

KILA unapofungwa unaona tatizo ni wengine ila we umecheza vizuri na ulistahili kushinda mentality hiyo imekuwepo since game zote na yanga faunal CAF mechi zote 2
 
12. Mechi 4 dakika 360 ... SIMBA HAWAJAPATA GOLI HATA LA OFFSIDE

Mnapenda sana kujitoa ufahamu lile goli ambalo kayoko alilikataa kwenye mechi ya kwanza ya ligi msimu uliopita ulifunga wewe au, anyway jitahidini mfanye vizuri na kimataifa kuwazidi simba ili watu wasitilie mashaka huu ushindi wenu wa ndani, maana msimu uliopita mlisingizia tulicheza mashindano ya kina mama na timu ndogo safari hii sijui mtasingizia nini
 
Mnapenda sana kujitoa ufahamu lile goli ambalo kayoko alilikataa kwenye mechi ya kwanza ya ligi msimu uliopita ulifunga wewe au, anyway jitahidini mfanye vizuri na kimataifa kuwazidi simba ili watu wasitilie mashaka huu ushindi wenu wa ndani, maana msimu uliopita mlisingizia tulicheza mashindano ya kina mama na timu ndogo safari hii sijui mtasingizia nini
Kipigo cha 6 mfululizo 😅🤣😂
 
Back
Top Bottom