Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 141,485
- 283,881
Nimeona niliweke hili ili kuondoa sintofahamu inayozunguka nchini Tanzania kwa sasa.
Hakuna haja yoyote ya mtu yeyote kupanic kwa sababu yeyote ile .
CHADEMA ni kama Jeshi, hakuna kamanda yeyote ambaye ni mkubwa kuliko Jeshi lenyewe, si Mbowe wala Mashinji ama labda Erythrocyte ambaye aweza kuushinda ukubwa wa CHADEMA.
Bila kujali yanayoendelea, na naomba niweke wazi kwamba hapa sijadili malumbano yanayojadiliwa na wengine, naweka angalizo kwamba CHADEMA ambayo inaongoza kata yangu kule Kyela na imefika mpaka kijijini kwetu Kajunjumele ni kubwa sana kuliko individuals.
=================
Tumbo, said:
Wakuu amani ya Bwana iwe pamoja nanyi.
Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA ni taasisi imara ambayo imejijengea uwezo, himaya ya kitaasisi tangu pale mfumo wa vyama vingi uliporejeshwa nchini mwaka 1992 hadi sasa.
CHADEMA kama taasisi haimtegemei mtu/kiongozi mmoja ama kundi la watu wachache wenye maslahi yao binafsi ndani ya chama ili iendelee kuwepo, bali hutegemea nguvu ya UMMA na wanachama kwa ujumla wao, na hapa ndipo nguvu ya taasisi inapoonekana, hakuna wakuliteteresha/liyumbisha CHADEMA kwa kuondoka mwenyewe ama kufukuzwa na chama.
Kwa nyakati tofauti tangu kuanzishwa kwake mwaka 1992, CHADEMA imepata kuwa na viongozi wengi na wenye ushawishi mkubwa ndani na nje ya chama, CHADEMA imepata kuwa na viongozi ndani ya chama wenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja na kuweza kushawishi Jamii juu ya agenda za chama/taasisi na hatimae kueleweka vyema kwa UMMA.
Pamoja na hao viongozi kuwa na ushawishi ndani na nje ya chama, kuwa na uwezo mkubwa wa kujenga hoja; lakini bado hawakuwa juu ya chama ama wakubwa kuliko chama/taasisi. Walipokwenda kinyume na taratibu za chama aidha walifukuzwa ama walijiondoa wenyewe na chama /taasisi ikaendelea kuwepo na pengine kuimarika zaidi.
Mfano mzuri ni akina M1&Co, walipotimuliwa baada ya kwenda kinyume na maadili na taratibu za chama bado CHADEMA haikutetereka bali iliimarika mara dufu. Kuelekea uchaguzi mkuu 2015 aliondoka Dr.Slaa CHADEMA haikupasuka kama miccm ilivyo tarajia na hatimae CHADEMA kwa chini ya UKAWA ilipata takriban 6m kwa nafasi ya Urais na idadi kubwa ya wabunge na madiwani hali iliyopelekea CHADEMA /UKAWA kuongoza baadhi ya halmashauri nchini ikiwemo Dar es Salaam.
Hili swala la Lowassa kwenda tofauti na mtazamo/ misimamo ya chama /taasisi haikubaliki, aitwe mbele ya kamati kuu ajieleze ni agenda zipi alienda nazo ikulu na kwani nini afanye jambo hilo kuwa siri? Kwa nini hakushirikiana na viongozi wa CHADEMA ili wawe na agenda ya pamoja? Apewe nafasi ya kusikilizwa asipotoa maelezo yanayo jitosheleza, milango iwe wazi kwake iwe ni kwa hiari yake ama kwa nguvu ya UMMA ili kulinda maslahi cha chama/taasisi na chama bado itabaki salama.
Kusifia serikali pale inapofanya jambo jema kwa wananchi wake siyo vibaya, ila kwa hali ilivyo hivi sasa kila raia amekata tamaa mtaani hali ni mbaya changamoto lukuki, maisha kwa ujumla ni magumu mno! Usalama wetu upo mashakani, huduma za Jamii hairidhishi, ajira, mikopo elimu ya juu balaa tupu, uhuru wa vyombo vya habari, kujieleza, bunge kabatini, unapataje ujasiri wa kupongeza serikali kwa hali hiyo?. Unless otherwise atueleze alienda ikulu kwa maslahi yake binafsi na yale yote aliyoyaongea ni maoni yake binafsi.
Mungu ibariki Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Africa kwa ujumla.
Hakuna haja yoyote ya mtu yeyote kupanic kwa sababu yeyote ile .
CHADEMA ni kama Jeshi, hakuna kamanda yeyote ambaye ni mkubwa kuliko Jeshi lenyewe, si Mbowe wala Mashinji ama labda Erythrocyte ambaye aweza kuushinda ukubwa wa CHADEMA.
Bila kujali yanayoendelea, na naomba niweke wazi kwamba hapa sijadili malumbano yanayojadiliwa na wengine, naweka angalizo kwamba CHADEMA ambayo inaongoza kata yangu kule Kyela na imefika mpaka kijijini kwetu Kajunjumele ni kubwa sana kuliko individuals.
=================
Tumbo, said:
Wakuu amani ya Bwana iwe pamoja nanyi.
Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA ni taasisi imara ambayo imejijengea uwezo, himaya ya kitaasisi tangu pale mfumo wa vyama vingi uliporejeshwa nchini mwaka 1992 hadi sasa.
CHADEMA kama taasisi haimtegemei mtu/kiongozi mmoja ama kundi la watu wachache wenye maslahi yao binafsi ndani ya chama ili iendelee kuwepo, bali hutegemea nguvu ya UMMA na wanachama kwa ujumla wao, na hapa ndipo nguvu ya taasisi inapoonekana, hakuna wakuliteteresha/liyumbisha CHADEMA kwa kuondoka mwenyewe ama kufukuzwa na chama.
Kwa nyakati tofauti tangu kuanzishwa kwake mwaka 1992, CHADEMA imepata kuwa na viongozi wengi na wenye ushawishi mkubwa ndani na nje ya chama, CHADEMA imepata kuwa na viongozi ndani ya chama wenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja na kuweza kushawishi Jamii juu ya agenda za chama/taasisi na hatimae kueleweka vyema kwa UMMA.
Pamoja na hao viongozi kuwa na ushawishi ndani na nje ya chama, kuwa na uwezo mkubwa wa kujenga hoja; lakini bado hawakuwa juu ya chama ama wakubwa kuliko chama/taasisi. Walipokwenda kinyume na taratibu za chama aidha walifukuzwa ama walijiondoa wenyewe na chama /taasisi ikaendelea kuwepo na pengine kuimarika zaidi.
Mfano mzuri ni akina M1&Co, walipotimuliwa baada ya kwenda kinyume na maadili na taratibu za chama bado CHADEMA haikutetereka bali iliimarika mara dufu. Kuelekea uchaguzi mkuu 2015 aliondoka Dr.Slaa CHADEMA haikupasuka kama miccm ilivyo tarajia na hatimae CHADEMA kwa chini ya UKAWA ilipata takriban 6m kwa nafasi ya Urais na idadi kubwa ya wabunge na madiwani hali iliyopelekea CHADEMA /UKAWA kuongoza baadhi ya halmashauri nchini ikiwemo Dar es Salaam.
Hili swala la Lowassa kwenda tofauti na mtazamo/ misimamo ya chama /taasisi haikubaliki, aitwe mbele ya kamati kuu ajieleze ni agenda zipi alienda nazo ikulu na kwani nini afanye jambo hilo kuwa siri? Kwa nini hakushirikiana na viongozi wa CHADEMA ili wawe na agenda ya pamoja? Apewe nafasi ya kusikilizwa asipotoa maelezo yanayo jitosheleza, milango iwe wazi kwake iwe ni kwa hiari yake ama kwa nguvu ya UMMA ili kulinda maslahi cha chama/taasisi na chama bado itabaki salama.
Kusifia serikali pale inapofanya jambo jema kwa wananchi wake siyo vibaya, ila kwa hali ilivyo hivi sasa kila raia amekata tamaa mtaani hali ni mbaya changamoto lukuki, maisha kwa ujumla ni magumu mno! Usalama wetu upo mashakani, huduma za Jamii hairidhishi, ajira, mikopo elimu ya juu balaa tupu, uhuru wa vyombo vya habari, kujieleza, bunge kabatini, unapataje ujasiri wa kupongeza serikali kwa hali hiyo?. Unless otherwise atueleze alienda ikulu kwa maslahi yake binafsi na yale yote aliyoyaongea ni maoni yake binafsi.
Mungu ibariki Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Africa kwa ujumla.