Adolph Jr
JF-Expert Member
- Nov 5, 2016
- 5,560
- 8,638
Kamuanzishia biashara ya M-Pesa mke wake hapo kijiweni, baada ya kuona inalipa akaenda kukopa million 2.5 kuongezea mtaji.
Picha linaanza mara baada ya kukopa tu, siku ya kwanza kaenda kutoa 100k ili aandae mazingira, arudi nyumbani anapatwa na dalili za malaria.
Akaenda kununua paracetamol kupunguza homa mara mafua na nguvu kukosa nguvu.
Kaenda kupima U.T.I, Malaria hakuna kitu basi daktari kamshauli kununua dawa za vidonda vya tumbo (PPI).
Kurudi nyumbani siku ya pili mke akafuata dalili ni zile zile homa, joto kali na mafua kupima hakuna ugonjwa, kachukua dawa za kutuliza homa na mafua pia alikuwa anatapika.
Siku ya tatu mtoto wa miaka mitatu naye homa na mafua hakuna ugonjwa sasa jamaa kachoka millioni 2.5 imebakia laki nane.
Kachoka amekuja kuomba ushauri nimemjibu kama nilivyoandika title kashindwa kuongeza mtaji maana bado wanaumwa wote watatu.
Tumshauri biashara ya kurejesha deni licha ya kuwa ni mgonjwa mwanaume kujikaza, muda unasonga eti, daaaaah!
Picha linaanza mara baada ya kukopa tu, siku ya kwanza kaenda kutoa 100k ili aandae mazingira, arudi nyumbani anapatwa na dalili za malaria.
Akaenda kununua paracetamol kupunguza homa mara mafua na nguvu kukosa nguvu.
Kaenda kupima U.T.I, Malaria hakuna kitu basi daktari kamshauli kununua dawa za vidonda vya tumbo (PPI).
Kurudi nyumbani siku ya pili mke akafuata dalili ni zile zile homa, joto kali na mafua kupima hakuna ugonjwa, kachukua dawa za kutuliza homa na mafua pia alikuwa anatapika.
Siku ya tatu mtoto wa miaka mitatu naye homa na mafua hakuna ugonjwa sasa jamaa kachoka millioni 2.5 imebakia laki nane.
Kachoka amekuja kuomba ushauri nimemjibu kama nilivyoandika title kashindwa kuongeza mtaji maana bado wanaumwa wote watatu.
Tumshauri biashara ya kurejesha deni licha ya kuwa ni mgonjwa mwanaume kujikaza, muda unasonga eti, daaaaah!