Huwezi kulinganisha enzi za Nyerere na hizi za sasa. Nyerere aliongoza chama chenye kupigania uhuru, enzi zile taasisi zilikuwa sio imara, wenye elimu walikuwa wachache, umoja wa waliotafuta uhuru ulihitaji mtu mmoja imara ili muendelezo wa madai ya kupewa uhuru usiweze kupoteza muelekeo.
Nyakati za Mbowe ni tofauti kabisa, nchi ipo huru, wenye elimu ni wengi, wenye kuweza kuhoji mambo wakiwa na uelewa ni wengi. Taasisi za uongozi ni imara.
Yaani kwa sababu Nyerere aliongoza kuanzia nyakati za TANU mpaka mwaka 1987 basi Mbowe nae aongoze CDM kwa miaka 33!!, poleni sana kwani mtaendelea kuwa bendera hufuata upepo mpaka mwisho wa uhai wenu.
Hayo yote ambayo unasema anakutana nayo kama vile kupewa kesi na kutupwa mahabusu ni kielelezo tosha kwa CDM kuhitaji kiongozi mpya mwenye maono mapya, ambaye atakuja na mikakati inayoendana na wakati.
Mbowe bado ana ile ile mikakati ya kiuanaharakati, mikakati ambayo inazidi kupitwa na wakati kila kukicha.