Hakika Mbowe ni Mwanasiasa Mahiri, Msikilize;

Hakika Mbowe ni Mwanasiasa Mahiri, Msikilize;

Kwa kujifariji tu hamjambo.
Kwani mateso yanatoka kwako nyumbani au mateso yaneletwa na Mtukufu malaika toka chato na Naibu Rais Maliyamungu Bashite? au ni kujifariji kivipi? Huko CCM mkisikia mpinzani kawambia Ukweli mnatafasiri ni kujifariji? ina maana mnafanya makusudi kuwanyanyasa Wapinzani?
 

Huu ndio uwezo wa kisiasa unaohitajika. Hotuba haina kejeli, matusi wala maneno ya kuudhi wengine.
Kumbe ndio maana wale wanao muogopa kwa kusema kwake ukweli bila woga wala Uchadema bali Utanzania hawataki aendelee kuwepo siasani na pengine hata duniani.

Aendelee kua siasani ila asiwe mwenyekiti tu, anatia doa demokrasia.
 
Hiyo spichi ni ya mwaka juzi kabla hajachanganyikiwa na kuota mvi nyeupe. Sasa hivi ni full matusi, uchochezi na uhaini! Hata bungeni hahudhurii tena, bila ruhusa ya spika. Bunge la bajeti karibu linaisha hajahudhuria hata siku moja. Spika atakapomchukulia hatua matusi atakayoyatoa itatubidi tuzibe masikio!
Dr Akili ungetumia akili kidogo ingekusaidia. Hivi mfano kama hiyo ya kuchoma vifaranga ni mwaka juzi?
Muwe wakweli kidogo na Mbowe ni Mtamzania mwenzenu Hakuna haja ya kuwa na chuki naye namna hiyo hasa kwenye ukweli
 
Kwani mateso yanatoka kwako nyumbani au mateso yaneletwa na Mtukufu malaika toka chato na Naibu Rais Maliyamungu Bashite? au ni kujifariji kivipi? Huko CCM mkisikia mpinzani kawambia Ukweli mnatafasiri ni kujifariji? ina maana mnafanya makusudi kuwanyanyasa Wapinzani?
Jipangeni aisee ili msiishie kudanganywa na utamu wa pilau mkashindwa kuhoji mengi yaliyojificha nyuma ya pazia.

Mbowe ni fundi wa kuongea na kujenga hoja, lakini vipi kuhusu chama chake kuwapa nafasi vijana wakaleta mawazo na mchango mpya?. Tangu 2004 mpaka leo ni miaka 14, jamaa bado kashikilia nafasi yake huku akiwadanganya kwa eloquence taaamu kama sukari!!.

Badilikeni, vinginevyo mtabakia mkikosa muelekeo mpya wa uongozi, mtabakia mkikosa busara mpya za kiuongozi.

Miaka 14 madarakani ndio yale yale kina Kagame, Mugabe na Museveni, ni kudumaa kwa demokrasia katika chama chenye neno demokrasia kama utambulisho wake.
 
nimepitia baadhi ya maoni humu nabaki kuangalia na kutafakari aina ya mtu
nadhani iwepo dislike button pia
 
Mbona yuko sahihi kabisa!
Yupo sahihi kwa vipi wakati kila mtu ameona Mbowe hahudhurii vikao vya bunge vya bajeti. Kila mtu aliona na kusikia jinsi Mbowe alivyoporomosha matusi alipotoka rumande akiwa na ndevu nyeupe! Ametoka rumande akiwa 'a totally changed person mentally and physically'.
 
Maskini hapendwi na watu wa dunia wala wa dini. Kwa hiyo Magu asitudanganye kwamba anawapenda maskini, akisema anawapenda wapiga kura tutamwamini.
 
Yupo sahihi kwa vipi wakati kila mtu ameona Mbowe hahudhurii vikao vya bunge vya bajeti. Kila mtu aliona na kusikia jinsi Mbowe alivyoporomosha matusi alipotoka rumande akiwa na ndevu nyeupe! Ametoka rumande akiwa 'a totally changed person mentally and physically'.
Weka ushahidi hapa!
 
Jipangeni aisee ili msiishie kudanganywa na utamu wa pilau mkashindwa kuhoji mengi yaliyojificha nyuma ya pazia.

Mbowe ni fundi wa kuongea na kujenga hoja, lakini vipi kuhusu chama chake kuwapa nafasi vijana wakaleta mawazo na mchango mpya?. Tangu 2004 mpaka leo ni miaka 14, jamaa bado kashikilia nafasi yake huku akiwadanganya kwa eloquence taaamu kama sukari!!.

Badilikeni, vinginevyo mtabakia mkikosa muelekeo mpya wa uongozi, mtabakia mkikosa busara mpya za kiuongozi.

Miaka 14 madarakani ndio yale yale kina Kagame, Mugabe na Museveni, ni kudumaa kwa demokrasia katika chama chenye neno demokrasia kama utambulisho wake.
Talk is cheap kama huumizi akili kufikiri!

Nguvu anazotumia kujenga chama, kuna nguvu nyingine kubwa zaidi on the opposite side inayotumika kukisambaratisha. Kwa wasio ona mbali ni shida kutambuwa hilo. Labda kama chama kingekuwa kimeshawahi kushika madaraka ndo ungesema unalosema likamake sense.

Umiza akili endapo haijapofushwa bado.
 
Kweli nyani haoni makalio yake yeye alipobadilisha gia angani alimshauri nani? Mbona hakuenda twitter kutafuta maoni. Viongozi kama hawa ni liabilities kwa Taifa. Inauzi sana wakati mwingine. Anatakiwa ajue kuwa upinzani nchi hii hauta simama kama utakuwa na viongozi wajuu walaghai na wababaishaji kama huyu. Kuongea kwa hisia huku moyoni umejawa na unafiki ni useless.

Watanzania tatizo letu ni usahaulifu kasahau mara tu tumesahau kelele za mahakama ya kaadhi, ni wadini yetu nk. Mtu wa ajabu huyu kasahau TRA tu hapo Wachaga ilikuwa ni kama X-mass Moshi Au makao makuu NSSF ukienda pale ijumaa utazania ni mshuko wa ijumaa hayo mavazi utakayo kutana nayo

Tuwe wa kweli tuone tulijikwaa wapi sio kuangalia tulipo angukia. Kauli kama hizi za huyu mbowe ni ushahidi tosha kutufumbua macho na masikio wale tuliojifanya vipofu na viziwi kuelewa kwamba kulikuwa na upendeleo ukiendelea kimya kimya/chini chini na wale walio kuwa wanapendelewa ndio hao wanapiga kelele sasa. Hata kauli hizi za hovyo eti "nchi imepewa iongozwe na washamba ni katika ule ubaguzi uliokuwa unaendelea chini kwa chini. Ushamba kwa sababu ya kabila la mtu!!!? Hovyoo sanaa tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom