Hebu twende taratibu mkuu, umesema mtu mwingine akitaka hicho cheo basi inakuwa mbinde.
OK, hayo ni maoni yako (yenu) na tuuaache mubaki nayo.
Lakini nakumbuka kuna watu walikuwa ndani ya Chadema wakafanya njama kubwa sana kutaka ZZK agombee cheo hicho. Watu hao nadhani unawakumbuka, Kitila, Mgwamba, Msando kwa uchache.
Lakini baada ya zoezi lao kushindwa na kufukuzwa wakaenda kuanzisha ACT. Jee bado wapo ACT? Ni kuwa hata huyo ZZK wamemtosa na kwa vile hawakuwa na mioyo ya upinzani dhidi ya ccm bali special assignment ya kuvuruga wamerudi CCM.
Hapo ndio nataka kukuambia kuwa Chadema ni chama kubwa na kinajua mbinu chafu, wakiona wakati wa kufanya mabadiliko ya mwenyekiti watafanya. Hujawahi kuona Mbowe anafanya lobbying kubaki madarakani bali ni wanachama wenyewe ndio wanataka.
Hakuna mambo kama yale ya Dodoma eti kura zote ndio halafu mamia wanajitokeza kudai kura zao za hapana zimeenda wapi?