Hakijaeleweka bado....

Hakijaeleweka bado....

Lavit

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2011
Posts
16,372
Reaction score
37,938
Wakuu haya maisha unaweza pata kila (material things) na bado furaha usiipate. Mara nyingi huwa nacheka sana watu wanapopewa ushauri wa tafuta pesa baada ya kutendwa.

Nikirudi nyuma katika wakati kipindi hicho nikiwa hoehae na kwanza ndo niko shule, nikatokea kumpenda sana binti mmoja, nilihangaika sana kumshawishi na nikakutana na vitimbwi vya kila aina, sikukata tamaa nikiamini ndio fungu langu..

Toka 2006 akaja kunikubali 2008 ila bad enough baada ya miezi kadhaa akaja kunibwaga kwa madai kwamba siko moyoni mwake na hata akiniita mpenzi nafsi inamsuta. Niliyapokea haya katika muda ambao sikuutaraji tena nikiwa nimefunga safari ndefu kumfata yeye.

Niliondoka kishingo upande huku sumu ya penzi nikiwa nimeshailamba, hakika aliuvunja moyo wangu vipande vipande, tokea hapo sikuwa tena na imani na hawa viumbe. Na kila aliyekatiza anga zangu alionja joto ya jiwe, hata sikuona thaman ya penzi..

Baada ya miaka kadhaa yule yule aliyeuvunja moyo vipande vipande akarudi na kudai ananipenda sana, anataka nimuoe na ndani ya wiki akadai anitambulishe kwa baba ake. Nilimkubalia lakini lengo lilikuwa kumuumiza tu, alifunga safari na kunifata, nilikaa naye kama wiki na alipoondoka ndo ukawa mwisho wa mapenzi..

Nikajifanya kauzu ihali nampenda, sasa tangu aondoke bado nauguza moyo wangu na siamini kama utapoa. Mbaya zaidi huyu mwanamke kashaolewa na ana watoto wawili sasa.

Kila nilikojaribu kwenda najikuta sifiki kokote, kwa kifupi hakijaeleweka bado, kuna muda nafikiri pengine wengine hatupo duniani kwa ajiri ya kuoa. Kifupi ni kwamba ni miaka 10 sasa ila bado hakijaeleweka.

 
Usiwe na wasiwasi ndugu, Kuoa sio lazima kwamba wote lazima tuoe. Still Life Goes on.
 
Kweli mkuu acha maisha yaendelee..
 
Mapenzi bwanaa unaempendaa kwadhati anampendaa mwingineee
Jitahidii kukubali kuwa ushamkosaa na usifuatiliee maisha yakee Wala usiwee na mawasiliano nayeee
 
Nafikiri hicho ndo kinanicost.. Maana leo kanipigia video call, kicheko chake kikarudisha machungu upya!
Mapenzi bwanaa unaempendaa kwadhati anampendaa mwingineee
Jitahidii kukubali kuwa ushamkosaa na usifuatiliee maisha yakee Wala usiwee na mawasiliano nayeee
 
Kuna mwanamke wangu nampenda kinoma. Home kwetu wanaleta vikwazo kibao mara hivi mara vile, mara umri mara kabila na huko kwa mwanamke na yeye mara wamuambie mimi sijui mdogo bado sijamaliza ujana, mara kabila lakini sisi tunapendana hakuna mfano

Sasa hapa next Month anakuja Tutiane mimba af tuone hao wanaongea watafaidiaka nn
 
Na sio lazima upende ndio uoe, nawajua wengi sana wameoa vigezo, na sio mapenzi.
 
Usije ukampoteza huyo mtu mkuu
Kuna mwanamke wangu nampenda kinoma. Home kwetu wanaleta vikwazo kibao mara hivi mara vile, mara umri mara kabila na huko kwa mwanamke na yeye mara wamuambie mimi sijui mdogo bado sijamaliza ujana, mara kabila lakini sisi tunapendana hakuna mfano

Sasa hapa next Month anakuja Tutiane mimba af tuone hao wanaongea watafaidiaka nn
 
Kuna mwanamke wangu nampenda kinoma. Home kwetu wanaleta vikwazo kibao mara hivi mara vile, mara umri mara kabila na huko kwa mwanamke na yeye mara wamuambie mimi sijui mdogo bado sijamaliza ujana, mara kabila lakini sisi tunapendana hakuna mfano

Sasa hapa next Month anakuja Tutiane mimba af tuone hao wanaongea watafaidiaka nn
Wazee wako sahihi ww bado mtoto "next month" "mtiane mimba" akifanikiwa kukutia mimba naomba unitag
 
Hii wikiendi story nying zilikuwa za mabaharia kupenda nadhan wadada mtambue mabaharia nao wanapenda

Ila ule uzi wa kula kimasihara nyie achanen nao nna uhakika kuna watu wamesharudia demu mmoja ila sehem tofaut[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna mwanamke wangu nampenda kinoma. Home kwetu wanaleta vikwazo kibao mara hivi mara vile, mara umri mara kabila na huko kwa mwanamke na yeye mara wamuambie mimi sijui mdogo bado sijamaliza ujana, mara kabila lakini sisi tunapendana hakuna mfano

Sasa hapa next Month anakuja Tutiane mimba af tuone hao wanaongea watafaidiaka nn
Haya unayopitia mm yalinikuta ilibid n give up lakn bado nampenda sana yule mwanamke na yeye mpk leo ananipenda lakin no way out acha ikae
 
Back
Top Bottom