Haka ndiko kabinti kangu...

Watoto wanaolelewa na HG's tu peke yao bila guidance ya wazazi. Sometimes akiwakataza kutoka wakisema kwa mama au baba mnamuwakia HG as if amekosea. Sasa nyie wenye hiyo tabia ndioy hapo fataki anapopata upenyo wa kuwakamata. Tutaibika jamani oooh! shauri yetu
 
Habari wana JF!!

Kama title inavyosema ni kabinti kangu yaani katoto kangu ka kike kenye umri wa miaka 9.5 sasa.

Majuzi nimekaa nako kwenye gari nikisubiri bidhaa nilizoagiza huku nataniana nae, kiukweli nampenda sana mwanangu ndiyo maana akawa rafiki yangu mkubwa!!!

Katika kucheza cheza pale akanitupia swali, namnukuu `Hivi baba kwanini yule baba dukani kwa kina Robu hupenda kuniita ita kule uani kwao halafu anapenda kunishika shika matakoni na kifuani?` Kwani ndo nini hivyo?

Kidogo nianguke kwa presure.....huyo baba mwenyewe ni mtu mzima sawa tu na mzazi wangu mimi!!! Na sikumjibu kitu ila nikamwambia nitakuelezea nyumbani tukifika, mama mtu akataka kumpiga but nikamwambia no!! Mwache

Nilijaribu kumdadisi kama kuna anachopewa na huyo mzee akajibu hajawahi kupewa kitu chochote zaidi ya pipi na gumz basi.

Natafuta namna ya kumjibu na kumwelekeza madhara yake na kuweka mtego wa kumnasa fataki!!

Mama hataki mtoto aelekezwe kwa sasa juu ya swala zima la mapenzi kisa bado mdogo sana!!! Wana JF mnadhani ni sahihi?

Nimeweka hapa pia kama tahadhari kwetu wana JF coz najua wengi wetu hapa ni wazazi na sikujua jambo kama hili lingeweza linitokee kwangu ila ndiyo hivyo limenifika!! So take care na watoto wetu jamani

...awe ni mtoto wa kike au wakiume. Anapokujia kwa uwazi na kukueleza haya,Busara tu ndiyo itayoweza kumuokoa au kumpoteza mwanao. "mwana umleavyo....!" ...kwanini achapwe kwa kusema ukweli? Huo ni udhaifu uliopitiliza ambako sana sana kutampelekea kudadisi hilo lililomponza.

Ingelikuwa ni mimi, ningekaa nae kitako na kusikiliza maelezo yote, na matendo anayofanyiwa.

Kisha kulingana na umri wake, ningemuelekeza Ubaya wa tukio hilo kulingana na
  • imani ya dini
  • matakwa ya wazazi
  • mila, desturi na tamaduni ya jamii husika.
Mwisho, ningempongeza kwa ujasiri wake wa kuwa mkweli, na wakati huo kumu encourage asisite kuuliza lolote ambalo anahisi linamtatiza, kwani sote tumepitia umri wake wa udadisi.

Kisha, nitakwenda kuongea "kiutu uzima" na huyo babu!
 
Kaka nimekuheshimu sana umewezaje kutofungwa hadi leo? Ila umenisaidia sana mzee kesho ninarudisha bastola yangu kunako wahusika nimegundua kumbe siwezi kuimiliki na nikawa salama.Lakini kabla ya kufanya hivy kama unaweza kutoa namba yako ya simu,itakuwa bora nikupigie unionyesha tu huyo mtu halafu mengine nitajua mwenyewe nitachomfanya hatasahau maisha yake yote.
 
Ni vizuri kuwa karibu na mtoto maana amekuwa wazi kukueleza. Cha muhimu ni kutafuta mbinu za kumuweka ndani huyo Baradhuli fataki wako wengi kama hao wajibu wetu kuhakikisha wanakwisha. Mtoto ni kumtia moyo kuwa muwazi na kumweleza ni nini ilikuwa nia ya fataki na njia madhubuti za kuepuka tabia hatarishi kama hizi.
Mafanikio mema
 
Hivi vizee vilivyopoteza maadili vilikua wapi wakati wa gharika ya Nuhu? Kwanini wanasababisha tutoe matamshi mabaya ambayo yatakua madoa hadi kwa wazee wetu wengine wenye heshima na hekima zilizotukuka?
Nitoe tu angalizo kwa wazazi kuwa na utamaduni wa kusikiliza watoto ili kubaini uchafu wa aina hii kabla wachafuzi hawajafika mbali na azma zao mbaya! Pole mzazi mwenzetu!
 
Habari wana JF!!

Kama title inavyosema ni kabinti kangu yaani katoto kangu ka kike kenye umri wa miaka 9.5 sasa.

Majuzi nimekaa nako kwenye gari nikisubiri bidhaa nilizoagiza huku nataniana nae, kiukweli nampenda sana mwanangu ndiyo maana akawa rafiki yangu mkubwa!!!

Katika kucheza cheza pale akanitupia swali, namnukuu `Hivi baba kwanini yule baba dukani kwa kina Robu hupenda kuniita ita kule uani kwao halafu anapenda kunishika shika matakoni na kifuani?` Kwani ndo nini hivyo?

Kidogo nianguke kwa presure.....huyo baba mwenyewe ni mtu mzima sawa tu na mzazi wangu mimi!!! Na sikumjibu kitu ila nikamwambia nitakuelezea nyumbani tukifika, mama mtu akataka kumpiga but nikamwambia no!! Mwache

Nilijaribu kumdadisi kama kuna anachopewa na huyo mzee akajibu hajawahi kupewa kitu chochote zaidi ya pipi na gumz basi.

Natafuta namna ya kumjibu na kumwelekeza madhara yake na kuweka mtego wa kumnasa fataki!!

Mama hataki mtoto aelekezwe kwa sasa juu ya swala zima la mapenzi kisa bado mdogo sana!!! Wana JF mnadhani ni sahihi?

Nimeweka hapa pia kama tahadhari kwetu wana JF coz najua wengi wetu hapa ni wazazi na sikujua jambo kama hili lingeweza linitokee kwangu ila ndiyo hivyo limenifika!! So take care na watoto wetu jamani

Mkuu hii habari kwanza imenifanya nicheke nusura nitokwe na machozi, later ikanifanya nichukie nusura niibwage PC down..,
Hilo zee...., n'wayz nilichotaka kuongea kingenipeleka kifungoni kwa mara ya kwanza, mkuu huyo mbwiga anastahili kuzikwa kiwiliwili na kuachwa kichwa tu juu.......!
 
Habari wana JF!!

Kama title inavyosema ni kabinti kangu yaani katoto kangu ka kike kenye umri wa miaka 9.5 sasa.

Majuzi nimekaa nako kwenye gari nikisubiri bidhaa nilizoagiza huku nataniana nae, kiukweli nampenda sana mwanangu ndiyo maana akawa rafiki yangu mkubwa!!!

Katika kucheza cheza pale akanitupia swali, namnukuu `Hivi baba kwanini yule baba dukani kwa kina Robu hupenda kuniita ita kule uani kwao halafu anapenda kunishika shika matakoni na kifuani?` Kwani ndo nini hivyo?

Kidogo nianguke kwa presure.....huyo baba mwenyewe ni mtu mzima sawa tu na mzazi wangu mimi!!! Na sikumjibu kitu ila nikamwambia nitakuelezea nyumbani tukifika, mama mtu akataka kumpiga but nikamwambia no!! Mwache

Nilijaribu kumdadisi kama kuna anachopewa na huyo mzee akajibu hajawahi kupewa kitu chochote zaidi ya pipi na gumz basi.

Natafuta namna ya kumjibu na kumwelekeza madhara yake na kuweka mtego wa kumnasa fataki!!

Mama hataki mtoto aelekezwe kwa sasa juu ya swala zima la mapenzi kisa bado mdogo sana!!! Wana JF mnadhani ni sahihi?

Nimeweka hapa pia kama tahadhari kwetu wana JF coz najua wengi wetu hapa ni wazazi na sikujua jambo kama hili lingeweza linitokee kwangu ila ndiyo hivyo limenifika!! So take care na watoto wetu jamani
Duh mungu wangu huyo siku moja anataka aje ambake hivo anamsogeza karibu ili awe confortable nae, kwanza mfate umwambie umesikia hicho kitu kwa mtoto na akiendelea utampoteza, pia inakuwaje mnamwacha mtoto anaenda enda hapo mara kwa mara? siku hizi dunia imeharibika, na usiacha kumwambia mtoto black and white cause cheleachelea yaumiza matumbo, utakuja kuta mwana si wako huyo, mie watoto wangu nimewaweka chini na kuwaambia yote bila kificho na ni wadogo tu kama huyo wakati nawaambia
 
umenifanya nishike bastola yangu ghafla kucheki kama iko tayari tayari. doh hapo ningeshastakiwa kwa kuua bila ya kukusudia. sina huruma na mijitu ya aina hii asilani!
 
Ndugu yangu, huyo babu ni mtu hatari sana. Kwanza nakuomba umweleze huyo mtoto kuwa asiende tena kwa huyo babu hata kama atamwita na kwamba asijaribu kufanya chochote na huyo babu. Mwambie akifanya ataumwa sana. Mweleze katika hali itakayomfanya hapaswi kwenda na hata kufanya chochote. Pia nenda ukamweleze babu kuwa njama zake umezipata. Mweleze kwa msisitizo na si kwa ukali akuone mtu makini usiyetaka mzaha wala kuharibiwa mali au watu wako. Akiendelea mpeleke kwa mamlaka za juu kisheria. Kumbuka usichukue hukumu mwenyewe kwa kumpiga au kumpa madhara kwani mambo yatakugeukia. Mpeleke kwenye mamlaka husika.
 
Ili kumsaidia huyo fatakina jamii pia dawa ni kumwendea na kumjulisha juu ya tabia yake mbaya bila kujali kama atakubali kuhusika au la. La maana ni kwamba ajue kuwa jamii na wewe kama mzazi mnajua. Pia mtoto ajengewe mazingira ya kuwa mbali naye. Si binadamu huyo!
 
sijui ningekuwa mimi ningefanyaje....Mungu atusaidie sana...mkuu,mtel huyo mama asikataze mtoto kuujua ukweli hizi ni zama za uwazi,..mwambie mwanao madhara ya huo uchafu ambao huyo fataki asiye na aibu anamfanyia.....pole sana kaka
 
Ndugu mpendwa KJ pole sana kwa presha naamini ingekuwa mm walah, ningerudia njiani nakumpa blac & white huyo fataki, Mungu amekufungulia njia kujua mbaya wa mwanao kwa kufungua kinywa cha kinda wako kukuambia ukweli, wengine huhongwa mengi nakuambiwa wasiseme nyumbani, chamsingi, usichelewa. kamwambie wazi ukimuonya nakumwambia kuwa mvua 30 ziko nje ya nyumba yk, km anaendelea kumfata au kuwafuata watoto wadogo, au km unaona huwezi basi waeleze Takukuru yaani majirani wamtumie mtoto wako au wajirani kumnasa huyu mzee akajifie rupango, ni ujinga mkubwa kwa wazee km hawa kuachwa wakiwaharibu wanetu, mm ninamtoto wangu wa miaka 10 pia inaniweka wakati mgumu sn kuamini kuwa yuko safe kama wako amefanyiwa haya, inanitesa akilini pia.
usingoje wakati mwizi aje kukuibia km unaweza mshoot maadamu unauhakika ni mwizi.
 
pole sana,

ni vyema tukiwa tunawaeleza watoto wetu (wakike na kiume) ni maeneo gani
ya mwili ni "no go areas" kwa mtu yeyote yule labda aruhusiwe na mama
(kutegemeana na umri kwani wakati mwingine hawezi jisafisha anahitaji msaada).
hii ni kutokana na ukweli kwamba mharibifu mara nyingi ni yule ambaye mtoto anamuamini.
na waharibifu huanza kwa kushika shika sehemu hizo za "no go" .

katika kundi la watu ambao mtoto huwaamini wapo majirani, ndugu wa karibu wa rafiki za mtoto,
ndugu wa karibu wa wazazi, wasaidizi wa ndani n.k. katika hawa ndimo waharibifu hutokea. ni
mara chache sana mtu wa mbali akafanya uharibifu kwa mtoto na ikitokea hivyo basi nguvu
itakuwa imetumika.

inabidi uwe muangalifu juu ya hatua utakazochukua, kwani ikiwa ya mikikimikiki basi unaweza
muathiri mtoto kisaikolojia mfano ukienda kumpandishia huyo babu na pakatokea vurugu
binti yako anaweza kukosa amani hapo mtaani kwa kunyoshewa kidole na kila mtu na
wengine wakageuza stori kabisa. aidha watoto wenzake hapo mtaani wanaweza wakampa na
jina la utani. si unajua watoto wakianza kutania huwa "wakatili sana"

ingekuwa mimi, basi ningemfuata huyo babu na kumueleza kwa ustaarabu kabisa ila
kwa msisitizo, kwamba nimesikia kwa huwa anamazoea na binti yangu na si vyema kwa mtu wa umri wake kuwa naukaribu
na watoto wadogo na kwamba binafsi nisingependa ukaribu huo uendelee.
 
Yaani huyo mama naona hajui dunia ilivyo, yakimkuta ndio atajua umuhimu wa kuongea na watoto mambo yote
 
Habari wana JF!!

Kama title inavyosema ni kabinti kangu yaani katoto kangu ka kike kenye umri wa miaka 9.5 sasa.

Majuzi nimekaa nako kwenye gari nikisubiri bidhaa nilizoagiza huku nataniana nae, kiukweli nampenda sana mwanangu ndiyo maana akawa rafiki yangu mkubwa!!!

Katika kucheza cheza pale akanitupia swali, namnukuu Hivi baba kwanini yule baba dukani kwa kina Robu hupenda kuniita ita kule uani kwao halafu anapenda kunishika shika matakoni na kifuani? Kwani ndo nini hivyo?

Kidogo nianguke kwa presure.....huyo baba mwenyewe ni mtu mzima sawa tu na mzazi wangu mimi!!! Na sikumjibu kitu ila nikamwambia nitakuelezea nyumbani tukifika, mama mtu akataka kumpiga but nikamwambia no!! Mwache

Nilijaribu kumdadisi kama kuna anachopewa na huyo mzee akajibu hajawahi kupewa kitu chochote zaidi ya pipi na gumz basi.

Natafuta namna ya kumjibu na kumwelekeza madhara yake na kuweka mtego wa kumnasa fataki!!

Mama hataki mtoto aelekezwe kwa sasa juu ya swala zima la mapenzi kisa bado mdogo sana!!! Wana JF mnadhani ni sahihi?

Nimeweka hapa pia kama tahadhari kwetu wana JF coz najua wengi wetu hapa ni wazazi na sikujua jambo kama hili lingeweza linitokee kwangu ila ndiyo hivyo limenifika!! So take care na watoto wetu jamani
Nimemind utadhani ni mwanangu ndo kafanyiwa.....ila nenda kaongee na huyu mzee mshenzi kitaratibu kabisa aache hiyo tabia....kisha ongea na mwanao kama ataendelea akueleze....akiendelea nina Colt4...njoo tumalize kisa.
 
Hivi binti wa miaka 9 anakua na matiti gani mpaka baba wa duka ashike kifuani, hii kamba nimeikataa bana labda matakoni huko ulikosema lakini kifuani UONGO
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom