Haka ndiko kabinti kangu...

Haka ndiko kabinti kangu...

Pole sana , halafu mshukuru Mungu kuwa binti amekuambia, ni wajibu wenu wazazi kuongea na binti yenu, unavyojua watoto wanakua haraka, wanashinda na mahousegirls, mtoko wao ni dukani na housegirls mara nyingi wazazi busy kutafuta hela, hivyo mshukuru Mungu kuwa umefahamu,

Naomba baada ya kumpa elimu binti yenu, huyo fataki umwambie kisha umtembezee noma mtaa mzima kwa kuwajulisha watu litabia lake libovu asiendelee kutafuna vibinti vya watu...zee zima! Anakuwa kama yule 'Ali Maumba' sina hakika na jina aliyekuwa anaharibu vivulana vidogo...usimvumilie!!!lazima ahame mtaa kwa aibu!

Mwisho natoa rai wazazi tujaribu kuwa close na wanetu, mimi mabinti zangu nimewaelekeza sana kuwa usikubali kuvua chupi, kushikwa hapa etc...lakini pia kikubwa ni kuwaombea maana TV na fb na utandawazi unawakuza wanetu
 
naona umfungulie kesi huyu mtu akafie jela.ili iwe fundisho kwa watu wengina wenye tabia kama izi.
 
Mtegeshee huyo mbaba na uwe na mashahidi ili akamatwe vizuri na kuchukuliwa hatua za kisheria. Maana mtoto pia hadanganyi, anaweza kuelezea kila kitu huyo binti yako.
kwanza nikupongeze kitu kimoja, kuwa rafiki na mwanao ambaye yupo free kuongea na wewe mana akipatwa na chochote kingine lazima atakushirikisha. Inawezekana huyo mbaba kamwambia asiseme kwa mtu.
Kama bado ni mapema, naomba mwanao akae mbali na huyo mbaba mana anapoelekea atamfanyia kitendo kibaya..Hakikisha nyumbani kwako hawaji vijana wa ajabu ajabu au mtoto kucheza nje muda mrefu bila kuonekana nyumbani.
Endelea kuwasiliana na mwanao, hata shuleni na mazingira mengine kama amewahi kukumbana na hiyo hali..pole sana!!
 
Mkuu chukua hatua za kisheria. Hii ni very serious matter. Kwenda kumpa onyo huyo babu sidhani kama itatosha. Kwa sababu mtoto wako akikua halafu ajue kuwa pamoja na kukueleza uliishia kwenda kumpa huyo babu onyo tuu atakuwa very very dissapointed. Chukua hatua za kisheria, lakini inabidi uwe makini sana. Sijui nikushauri ukaripoti polisi kwanza, lakini polisi wetu ndio hivyo tena. Labda wasiliana na watu wa utawi wa jamii au wanashighulika na child protection wanaweza kukupa mwongozo mzuri. Na hapa ndio pia ndugu and marafiki wako wa karibu wanapomatter. Wanaweza kukupa ushauri mzuri pia. Lolote utakalofanya be focused na usitetereke na hasira za watu hapa. We're living in a crazy world anyway.
 
Mwanaume mwenzenu huyo.............
Usijekuta hata rafiki/ndugu ya mtu hapa wa karibu..................
Mi hapa ndo huwa siwaelewagi viumbe wanaoitwa wanaume duniani.

LD si Wanaume wote wana mawazo ya kipumbavu kama ya huyu mshenzi/hayawani ambaye badala ya kutafuta wanawake watu wazima ili aweze kukidhi matamanio yake ya kimwili anakavizia kabinti kadogo ili akaharibu. Si ajabu huyu mshenzi ameshafanyia uhuni wake kwa vibinti vingi hapo mtaani. Ni vizuri huyu adhibitiwe kwa namna moja au nyingine ili kuepusha vibinti vingine visiharibiwe na huyu kichaa.
 
u must be a very passion person ..

nimekosa la kukujibu kwa kweli
maana nina swali kuliko jibu
"kwanini tu ulimwacha"...
at list ungempa hata ngeu ..
Kweli hii imenipa hasira kupita kiasi..
 
Yaani ukiwahamisha wanaume wanawake wenzio watakushuhulikia. Kuna wanawake ambao hawawezi kupita siku mbili bila hiyo huduma!

Ha ha ha, wanaotaka huduma ya kiume kila siku na wenyewe wahame nao.

Back to topick. Hicho kibabu sio cha kuchekea manake hata watoto wetu wa kiume wanaweza pata tabu aisee.
Sijui ni laana gani imeingia kwa hawa wazee.
 
LD si Wanaume wote wana mawazo ya kipumbavu kama ya huyu mshenzi/hayawani ambaye badala ya kutafuta wanawake watu wazima ili aweze kukidhi matamanio yake ya kimwili anakavizia kabinti kadogo ili akaharibu. Si ajabu huyu mshenzi ameshafanyia uhuni wake kwa vibinti vingi hapo mtaani. Ni vizuri huyu adhibitiwe kwa namna moja au nyingine ili kuepusha vibinti vingine visiharibiwe na huyu kichaa.

Usikute ndo kachuma ulete kake kanamwambia akifanya hivyo pesa inaongezaka BA.
 
Jamani kama kuna wanasheria humu MMU hebu tusaidieni,katika kesi kama hii hili fataki ukilifungulia RB na mtoto akatoa ushahidi huwezi kupata conviction kweli? Mbona Babu Seya alichukua mvua 30 pamoja na kwamba hakukamatwa live? Mi naona dawa ni kumpeleka central tu yakajulikane mbele kwa mbele.
 
Poleni kwani huo ni mshtuko mkubwa.
Yaani watu wazima wengine hovyo kabisa,kila ua zuri linalochipua hutaka tu kuliharibu,sijui ni pepo au ushetani yaani wanaudhi sana.
Dunia tunayoishi sasa,mazingira yamebadilika sana,ni vyema kuwa wazi kwa watoto wetu katika masuala ya afya ya uzazi na vishawishi vinavyowazunguka,hasa huyo wa miaka 9 bado hujachelewa,akaelewa nini kinaendelea kwa upole na hali ya urafiki na atazidi kuwa muwazi tu kwako.

Kinachotuponza hasa akina mama ni kupanic,na kuchukulia binti ndiyo mwenye kosa na kuwa bado hilo ni jambo la aibu kusema.
Wakati fataki yeye kwake haoini haya kabisa kuharibu,hivyo siyo wakati wa kuona haya kwenye hili.

Ikibidi mfuate fataki huyo ,mweleze huo uchafu anaoufanya utamgharimu kwani upo mbioni kumchukulia hatua za kisheria,utakuwa umewaokoa binti wengi sana ambao hawana fursa za kuzungumza na wazazi wao kama binti yako.
Kila la kheri katika malezi
 
Aisee!

Nimemkumbuka Matesha wangu....almost same age.

Haki Ya Mungu Ntaua mtu. Nimesemaje? and I mean it!
 
Hii thread imenipa baridi kabisa yaani, nimechoka hata sielewi, masikini binti yangu. Hebu nijifunze kuanza kuzungumza nae mwe! nitaanzaje sasa kuzungumza nae kuhusu haya mambo ya mapenzi wajameni kwamba ............................ jamani mtihani hebu nipeni mwongozo maana wangu ana 10 sasa ila huwa naona kama bado mdogo sana.

Asante mleta mada, shukrani kwa wachangiaji kuhusu malezi ya watoto kwani nimejifunza mengi kwa hii thread. Ila hilo la kuanza kuzungumza na binti wajameni mtihani, Nisaidieni ndio naanza anza anzaje?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hii thread imenipa baridi kabisa yaani, nimechoka hata sielewi, masikini binti yangu. Hebu nijifunze kuanza kuzungumza nae mwe! nitaanzaje sasa kuzungumza nae kuhusu haya mambo ya mapenzi wajameni kwamba ............................ jamani mtihani hebu nipeni mwongozo maana wangu ana 10 sasa ila huwa naona kama bado mdogo sana.

Asante mleta mada, shukrani kwa wachangiaji kuhusu malezi ya watoto kwani nimejifunza mengi kwa hii thread. Ila hilo la kuanza kuzungumza na binti wajameni mtihani, Nisaidieni ndio naanza anza anzaje?
Pole kwa kupata baridi. Jenga sana urafiki na binti yako. Mimi naamini wazazi wakiwa marafiki wa watoto wao, watoto wanakuwa hawana siri, akiwa na tatizo anajua mtu wake wa kwanza kumweleza tatizo lake ni Mama/ Baba yake. We fikiria kama Kijana juzi angekuwa hana urafiki / ukaribu na binti yake angemwelezaje hicho alichofanyiwa na huyo babu mtu mzima hovyo? Wazazi wasiwatenge watoto wao. Waonyesheni mnawajali na kuwathamini. Mtoto inabidi siku zote ajue kuwa rafiki yake wa kwanza huku Duniani ni Baba / Mama yake. Hatatokea wa kumdhuru / kumdanganya kwa chochote. Mungu awatangulie watoto wote humu duniani. Amina.
 
Hii thread imenipa baridi kabisa yaani, nimechoka hata sielewi, masikini binti yangu. Hebu nijifunze kuanza kuzungumza nae mwe! nitaanzaje sasa kuzungumza nae kuhusu haya mambo ya mapenzi wajameni kwamba ............................ jamani mtihani hebu nipeni mwongozo maana wangu ana 10 sasa ila huwa naona kama bado mdogo sana.

Asante mleta mada, shukrani kwa wachangiaji kuhusu malezi ya watoto kwani nimejifunza mengi kwa hii thread. Ila hilo la kuanza kuzungumza na binti wajameni mtihani, Nisaidieni ndio naanza anza anzaje?

Pole sana Maty,


Hata na mimi Mungu amenijalia mabinti…kweli ni kazi sana kuongea na mambo haya, lakini inabidi tu ujitahidi.
Mimi nilianza kuongea naye kuhusu mabadiliko ya mwili yanayotokea jinsi anavyokua (mambo ya MP), then nikaendelea na kumpa tahadhari ya akina Fataki…


Kitu kingine ambacho ni cha muhimu, ni kuwa karibu na binti yako, ili chochote kikitokea akuambie, kama mwanzisha sredi. Kwangu mimi, najitahidi kutengeneza urafiki nao, japo sijafanikiwa sana, lakini angalau kidogo…siku moja binti yangu mmoja akaniambia kuna mvulana amemwandikia barua na kumwambia kuwa anampenda. Kwa kweli nilifurahi sana kupata taarifa kama hizo, maana nilipata nafasi na kuongea naye na kumwelekeza jinsi gani kuhandle masuala hayo ya malove…! Kwa kweli naendelea kumwomba Mungu anisaidie, na pia awalinde mabinti zangu.


Kila la heri dear, Mungu akupe hekima ya kuongea na binti yako.
 
Nakupongeza sana kwa kuwa karibu na binti yako.Huyo mzee umkanye kwa kuwashirikisha majirani wenzako wawili watatu iv;Pia nashauri mkae na mkeo mumuulize taratibu binti yenu awaeleze zaidi kwani usikute huyo baazazi alikwishapiga hatua ;
Pili mama wa mtoto yaani mkeo ajitahidi kuwa karibu na bintiye kwani kuna mambo mengi yeye kama mama anapaswa kumwambia binti yake.
Ni vema kila siku asubuhi na jioni kuwakabithi watoto wetu kwa Mwenyezi Mungu awalinde kwani
Ulimwengu wa sasa umeharibika vibaya mno.
 
Habari wana JF!!

Kama title inavyosema ni kabinti kangu yaani katoto kangu ka kike kenye umri wa miaka 9.5 sasa.

Majuzi nimekaa nako kwenye gari nikisubiri bidhaa nilizoagiza huku nataniana nae, kiukweli nampenda sana mwanangu ndiyo maana akawa rafiki yangu mkubwa!!!

Katika kucheza cheza pale akanitupia swali, namnukuu `Hivi baba kwanini yule baba dukani kwa kina Robu hupenda kuniita ita kule uani kwao halafu anapenda kunishika shika matakoni na kifuani?` Kwani ndo nini hivyo?

Kidogo nianguke kwa presure.....huyo baba mwenyewe ni mtu mzima sawa tu na mzazi wangu mimi!!! Na sikumjibu kitu ila nikamwambia nitakuelezea nyumbani tukifika, mama mtu akataka kumpiga but nikamwambia no!! Mwache

Nilijaribu kumdadisi kama kuna anachopewa na huyo mzee akajibu hajawahi kupewa kitu chochote zaidi ya pipi na gumz basi.

Natafuta namna ya kumjibu na kumwelekeza madhara yake na kuweka mtego wa kumnasa fataki!!

Mama hataki mtoto aelekezwe kwa sasa juu ya swala zima la mapenzi kisa bado mdogo sana!!! Wana JF mnadhani ni sahihi?

Nimeweka hapa pia kama tahadhari kwetu wana JF coz najua wengi wetu hapa ni wazazi na sikujua jambo kama hili lingeweza linitokee kwangu ila ndiyo hivyo limenifika!! So take care na watoto wetu jamani
Kwanza nakupa pole kwa hilo na hongera kwa hatua ulizochua. Mara nyingi hasira huwa ni hasara, huenda ungempiga mtoto wako paleplale kwa hasira tu. Lakini pia naomba huyo fataki muwekee mtego halafu mfundushe mtoto wako ili asimuambie kwamba amewekewa mtego kisha ukimkamata mpige picha tena uwe na mashahidi watakaosaidia kumkamata na kutoa ushahidi halafu mpeleke kituo cha polisi na hatimaye mahakamani.
Kwa upande wa mtoto mfundishe ili ajue ubaya wa kushikwa na wanaume, usipomfundisha wewe au mama yake dunia itamfundisha sasa itakuwa balaa!!!!!!!!!!! tutaomba feedback
 
una kifua kaka, aisee singeweza kuvumilia hivyo!!!
 
Mmh! Kuna wazee mishapa yao ya hekima imenyofoka.
 
Back
Top Bottom