kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,319
- 12,622
Kweli Simba na Yanga wana utani ambao wote tumeukuta, lakini wakati huu ambao timu zinaingia kwenye uwekezaji wa kibiashara hazihitaji msemaji kama Manara mwenye utani ule wa kale wa uhasama na uhasimu.
Utani wa Manara ulipitiliza kiasi kwamba shabiki wa Yanga unashindwa kuinunua bidhaa ya mdhamini wa Simba. Yaani bidhaa za watu wa Simba unaziona haramu kuzitumia au kuzinunua unapokutana nazo sokoni.
Biashara haitakiwi ibague wateja lakini Chuki anayoipandikiza Haji inamtia hasara mo kibiashara sokoni.
Utani wa jadi usisababishe kichefuchefu kwa mashabiki wa timu pinzani kiasi Cha kushindwa kununua magodoro ya GSM hata kama yana ubora mkubwa.
Wawekezaji epukeni wasemaji kama Jerry Muro na Haji Manara. Wana utani wa wakizamani sana unaofaa kwenye timu za mitaani za makombe ya mbuzi. Hata Azam kama mtaruhusu wasemaji wa vile mtapunguza mapato.
Utani wa Manara ulipitiliza kiasi kwamba shabiki wa Yanga unashindwa kuinunua bidhaa ya mdhamini wa Simba. Yaani bidhaa za watu wa Simba unaziona haramu kuzitumia au kuzinunua unapokutana nazo sokoni.
Biashara haitakiwi ibague wateja lakini Chuki anayoipandikiza Haji inamtia hasara mo kibiashara sokoni.
Utani wa jadi usisababishe kichefuchefu kwa mashabiki wa timu pinzani kiasi Cha kushindwa kununua magodoro ya GSM hata kama yana ubora mkubwa.
Wawekezaji epukeni wasemaji kama Jerry Muro na Haji Manara. Wana utani wa wakizamani sana unaofaa kwenye timu za mitaani za makombe ya mbuzi. Hata Azam kama mtaruhusu wasemaji wa vile mtapunguza mapato.