Husna Muba
JF-Expert Member
- Jan 28, 2017
- 14,524
- 44,567
- Thread starter
- #61
THE ISLAMIC WIFE
(Mke Muislamu)
Sehemu Ya 28
Mtunzi... MoonBoy
Simu No, +255714419487 WhatsApp
Ilipoishia Jana →→↓↓
"rahim, "As Salaam Aleykum mama"
Alisalimia zena huku akimpa mkono mama yake rahim,... Wakati huo rahim ndio anainua kichwa chake na kusema...
"mama... Huyu ndio mchumba wangu.. Sasa mbona huupokei mkono wake"
Aliongea rahim huku mama kashikwa na butwaa kwa jinsi alivyokuwa anamuona mtoto wake..... Masikini zena hajachoka kuunyoosha mkono wake, japo haukuwa na majibu ya kupokelewa na mama mkwe.... Na wakati huo sasa,.. Yale majamaa ndio yanakuja kwa nyuma nyuma taaratibu ili kumkamata rahim,... Sasa Mbaya zaidi kumbe wamempangia zena mabaya pale watakapo fanikiwa kuondoka na rahim wao....
ENDELEA.........
Ujio wa mama rahim sio wa kwenda kwa wakwe, bali alikuja kumchukuwa mtoto wake ili aende shule, mana baba yake anamfokea sana kwa rahim kuwepo Tanga huku shule zikiwa zimefunguliwa,... Na rahim ni mwanafunzi mzuri sana sema pombe ndizo zilizomharibu, na huu ndio ulikuwa mwaka wake wa mwisho ikiwa ni mwezi wa 9 sasa yaani ameshapitwa na masomo sana tu,....
Sasa leo mama kaja kumchukuwa mwenyewe, na nia yake ni kumchukua hapo hapo Airport, na pia hakuja mwenyewe kaja na vijana wa nguvu kama watano hivi, na vijana hao tayari wamesha wazunguka akina rahim baada ya mama yake kusimama nao...
Wakati huo zena kanyoosha mkono kumsalimia mama mkwe,.. Lakini mama rahim alikuwa kama hauoni mkono huo, yaani macho yake yalikuwa kwa rahim jinsi alivyobadirika....
"ivi ni wewe rahim mwanangu ninaekujua au naota"
"ni mimi mama...... Mama lakini zena anakusalimia"
Aliongea rahim mana zena hakuchoka kunyoosha mkono kwa mama mkwe japo mama mkwe kama vile hauoni,..
"nani kasababisha kuwa hivyo"
Aliuliza mama rahim huku rahim akinyoosha kidole kwa zena, kumaanisha kuwa aliefanya yeye kuwa mtu wa dini, ni zena...
Huezi amini mama aliona hata kuupokea ule mkono wa zena, bado haitoshi, mana kitu alichokifanya ni kikubwa mno.... Huezi Amini mama rahim alimkumbatia kabisa zena, yaani hata ule mkono aliona ni mdogo sana,... Mama hata machozi yalimtoka,...
"mwanangu.. Ahsante sana kwa kunibadilishia mtoto wangu.... Sio kuwa nilikuwa sitaki uwe hivyo, ila upendo wetu kwako ulizidi mpaka tukawa tunakuacha sasa ufanye utakalo"
Aliongea mama rahim huku akiwa kamkumbatia zena,... Sasa wale jamaa nao ndio walikuwa wanakaribia ili wamkamate rahim, lakini mama aliwazuia
"jamani? Basi.... Nitawalipa pesa zenu, lakini basi msikamate mtu tena"
Aliongea mama rahim huku akitoa pochi yake na kutoa burungutu la pesa na kuwapa wale majamaa waliokuwa tayari kufanya kazi ya kumkamata rahim.... Sasa wakati mama anatoa pesa, huku zena alitoa kitenge ambacho alikuwa nacho kwenye mkoba wake,.... Mama rahim alishangaa anafungwa kanga,.. Kana kwamba nguo aliovaa ni fupi mno.. Machozi yalizidi kumtoka huku akizidi kuingiwa na imani ya hutuma..
"Ahsante mwanangu"
Mama rahim alimshukuru zena kwa kumfunga kanga,... Sasa wale jamaa wakatafuta usafiri wao, na kurudi arusha... Ila mama Safari ya kurudi arusha ilikufa, na alikuwa hana nia ya kubaki tanga, lakini ilimghalimu aendelee kubaki...
Wakati huo huku nyumbani bibi anamuulizia rahim kwa jamali
"we jamali mdogo wako kaenda wapi"
Aliuliza bibi mzungu huku akiwa na wasiwasi,...
"aaahhhhh kwa sasa, nadhani atakuwa anakaribia kufika arusha"
Bibi alitoa macho,
"Unasemaje wewe??... Kaenda kufanya nini"
"bibiiiii.... Yule bado ni wakusoma... Nashangaa mnakaa nae tu huku"
"mungu wangu mjukuu wangu anakwenda kurudia pombe tena"
"bibi... Hata mimi hapa Nasubiri tu simu ya mama aniambie nikachukue gari Airport"
"kwahio mama yako nae alikuja"
"tena kaja na wanajeshi ili wamkamate rahim"
"mbona mimi sijui, na hamjaniambia"
"sasa we si hutaki aende utaambiwa vip"
Mara ghafla wanasikia sauti ya honi iliopiga nje ya geti,...
Jamali alistuka, ina maana mama yake wamemshindwa kumkamata?? Mana alitegemea kupata simu ya kwenda kuchukuwa gari Airport,..
Jamali haraka haraka anakwenda kufungua geti,.. Alishangaa kumwona mama yake, akiwemo rahim na zena..
Jamali kashindwa kuelewa kwanini imekuwa hivyo,... Bibi alifurahi sana kumwona rahim karudi, mana tayari bibi keshaingiwa na wasiwasi juu ya mjukuu wake, kana kwamba kumtengeneza kote huko leo anarudi kuanza tena...
Waliingia ndani lakini jamali bado haamini, kama rahim karudi tena hapa,...
"shkamoo mama"
Mama rahim alimsalimia mama mkwe wake, kisha wakaingia ndani...
Walipokaa tu, jamali kaja na maswali yake
"mama vipi tena... Huyu mtu shule zimefunguliwa tayari"
Jamali aliongea hayo kwa kumwambia mama yake
"jamali mwanangu.... Kweli nimejiskia raha sana rahim kuwa katika hali hii... Binafsi hata baba yako akilijua hili, litamfurahisha sana"
"kwahio mama, Unasemaje kuhusu shule"
Aliuliza jamali lakini mama hakumjibu,... Mama rahim alimgeukia mama mkwe wake na kumuuliza...
"mama.... Rahim anatakiwa kwenda shule... Unaonaje nikaonana na wazazi wa huyu mschana tukaongea"
Zena alifurahi sana kusikia hivyo,....
"sawa nitakupeleka ukawaone"
"rahim.... Nataka uoe, lakini Tuende arusha ukamalizie masomo yako huku ukiwa na mkeo, hilo nimeliona ni sahihi, kwasababu baba yako anagomba san kuhusu shule"
Rahim kusikia aoe, alitamani hata muda huo huo
"mama... Shakira je"
Rahim alimuuliza mama yake kama mtego tu
"hapana rahim.... Huyu huyu anakufaa"
"lakini ni masikini hawa"
"sitaki kujua...."
Rahim aliongea hivyo kwa maana asije wakaenda huko wakakuta maisha ya ajabu wakaanza kuleta mambo ya Kiswahili...
Jioni ilipofika, familia yote ya akina rahim, ilikwenda kwa akina zena,.. Na wakati huo na familia ya akina zena nayo yote ilikuwepo, mana waliambiwa kuwa kuna ugeni utakuja jioni,... Hivyo maandalizi ya kuwapokea wageni yalikuwepo,.. Mama yake rahim alijua anakwenda kwa wakwe wenzie, hivyo alitakiwa kuvaa kiheshima... Rahim hata yeye leo anamshangaa mama yake kavalia nguo ndefu ndefu,.. Hata jamali haamini kama leo mama yake kavaa hivyo....
Maongezi yalianza... Baina ya wazee wazima, wazazi akina kaka.....
"jamani wazazi wenzangu... Mtoto wetu kapenda kwenu... Hivyo anataka jiko... Na kwakuwa wanapendana,... Sioni kama kuna tabu"
Aliongea bibi wakati huo bibi zake na zena pia wapo na ndio waliokuwa wanaongea wenyewe,...
"sisi hatuna shaka... Ni nyinyi tu kukubaliana na matakwa yetu"
Aliingea bibi yake zena, huku rahim na zena wanaomba mungu tu wakubaliane,... Mana wao hawaruhusiwi kuongea ispokuwa zena ataulizwa..
"matakwa gani tena jamani... Tuwaozesheni watoto wakayaanze yakwao"
Aliongea bibi yake rahim huku wakiendelea kunywa chai, si unajua vikao vya tanga vilivyo...
"mtoto wetu katunzwa haswa... Ana kila kitu yule, hamjui mwanaume toka kuzaliwa kwake"
Mama rahim alitoa macho kuskia zena alikuwa hamjui mwanaume toka kuzaliwa kwake,...
"mnasemaje... Ivi karne hiii mabinti hao wapo kweli"
Aliuliza mama yake rahim huku akishangaa kwa kauli hizo..
"haaaaa mbona huku tanga wapo wengi sana... Kiukweli kwa mjini huko sidhani lakini huku tanga ndani ndani wapo weengi mno"
Aliongea bibi yake zena huku akisubiri majibu toka kwa mume, yaani wazazi wa mume... Lakini mama hajaridhika ikabidi amuangalie mtoto wake amuulize.... Kwa macho macho, kuwa ni kweli zena ni bikra...
Rahim alitikisa kichwa kuashiria hajawahi kumjua... Lakini pia bibi yake zena hakutaka kudhibitisha sana, hivyo alimuuliza zena kuwa
"zena... Uko sawa au umeshaharibu"
"bibi, nipo sawa... Fanyeni mnachojua tu ila mimi na rahim tunajuana vizuri"
Aliongea zena, huku bibi yake zena akimrudia bibi yake rahim
"unasikia huko.. Vijana wenyewe wanajuana wapo vizuri... Sasa kazi ni kwenu kwa kile tunachokitaka"
"haya semeni mnataka nini"
Hapo bibi yake zena akatulia na kumwachia baba mwenye mtoto wa kike..
"kwa mimi... Nataka ng'ombe saba madume manne na majike matatu.. Hapo mimi nimemaliza"
Alipomaliza baba, akaja mama yake zena
"Kiukweli kwa mimi mama mtu... Ninachokitaka kwenu, naomba muishi na mtoto wangu vizuri,.. Anakwenda kuwa wenu, hivyo muishi kama mtoto wenu... Hicho ndicho kitu ninachokitaka kwenu"
Sasa baada ya mama yake zena kuongea hayo... Mama rahim akamjibu kuwa
"hilo umelipata mama.... Enhee kwa upande wa mabibi na mababu"
Aliuliza mama zena,... Huku bibi akijiandaa
"mimi nataka vitenge pea saba, na kanga zangu kama pea tatu... Nataka na hijabu,.. Hivyo tu vinatosha"
Baada ya bibi kuongea,.. Alifuata babu yake zena,..
"mimi bwanaaaaaaaaa..... Nataka kondoo wawili ili nichunge chunge kidogo... Nataka bakora... Mana nimezeheka sasa.... Kingine nataka koti... Bila kusahau kilo 50 za sukari.. Kuna baridi jamani"
Sasa wale wakubwa wote waliisha kutaja matakwa yao, na yote hayo ni kwasababu zena amejitunza usichana wake na ndio maana wana uhuru wa kutaja watakacho... Jamani kujitunza usichana raha kweli,.. Sasa nyie hayeni
Kaka mtu nae na mdogo mtu nae kila mtu alitaamka kitu akitakacho.... Sasa ikafika zamu ya zena kutaka kitu chochote kwa mume
"mimi nataka mswahafu tu"
Baba alitoa macho, mwanae kutaka mswahafu peke yake...
Lakini baba ikabidi atulie tu mana ni maamuzi yake yeye mwenye kuolewa
"ok, nadhani mumemaliza mambo yenu,... Sasa uwezekano wa kulipa pesa badala ya hivyo vitu si upo"
Aliuliza mama rahim, ili kama uwezekano wa kulipa pesa upo, alipe pesa badala ya vitu,.... Familia ikakubali walipwe pesa zao zote, hivyo mahesabu yakapigwa, mama rahim hapo hapo akatoa pesa keshi, huku akisema
"ndoa, nataka ifungwe kesho... Ili huyu aende shule"
Kuanzia saa hio maandalizi yalianza,.. Walialikwa watu wengei sana na sehemu ya kufungia ndoa iliandaliwa vizuri sana, mpaka usiku saa nne watu wapo bize,... Kila kitu kilinunuliwa kasoro mavazi ya wana harusi yalikuwa bado,... Familia zote zilikuwa na furaha sana, lakini sasa mama yake rahim hakutaka baba yake rahim alijue hilo, kwasababu lazima ataleta pingamizi... Yaani mama rahim alimpenda zena kwa nusu siku tu, baada ya kumuona mtoto wake amekuwa Muislamu safi, na sababu ya kumrudia mungu ni kwasababu ya zena, hivyo mama alimoenda kwa kumbadirishia mwanae,.... Lakini sasa mbaya zaidi jamali yeye anataka mdogo wake amalize shule kwanza hivyo hajapenda kitendo cha rahim kupewa mke ingali bado ni mwanafunzi,.... Mama yake rahim, na bibi yake rahim, na rahim mwenyewe, simu zao zilikuwa zimezimwa kwa siku hio, ila kasoro jamali, kwani yeye alikuwa na simu ya pembeni tofauti na ile iliozimwa,... Jamali hakupenda mdogo wake aoe kwa wakati huo na istoshe jamali na baba yake vinaivana vizuri,.... Huezi amini usiku huo huo simu kwa baba yake, ambae kwa sasa yupo dubai...
"haloo dady shkamoo"
Alisalimia jamali huku akiangaza macho huku na kule ili asije akasikiwa na mmoja wao,....
"Marahaba, vipi saa hizi"
Baba yake aliuliza kuna nini muda huu,
"mzee, huku unapatiwa mkwe"
"mkwe Kivipi"
"rahim anaoa kesho"
"Whaaaaaat?"
"ndio hivyo mzee... Na kesho saa saba ndoa inafungwa msikitini"
"hivi huyu mtoto ana akili kweli... Na mama enu nae yupo wapi"
"mama ndio kipau mbele mzee"
"pumbavu sana.... Hebu ngoja nimpigie"
"kazima simu, yaani hii yenyewe hawajui kama nina simu ndogo, mana tumezima wote simu zikawekwa mahali ili wewe usijue"
"hapana.. Haiwezekani... Mimi nataka mwanangu asome... Yaani nitahakikisha hio ndoa haikamiliki"
"sasa utafanyeje mzee"
"kesho nakuja na ndege ya private... Nataka uje Airport na hio gari uje unichukue"
"sasa watanishtukia wasiponiona mzee"
"shiiiiit,... Ngaoja nina jamaa wangu hapo Airport nitamwazima gari yake, ila usizime simu.... Mama yako hana akili kabisa huyu"
Kesho yake sasa mida kama saa tano za asubuhi akina rahim na zena walikuwa ndani, wakiangalia nguo za kufungia ndoa walizoenda kununua muda mfupi uliopita,... Katika viwanja vya ndoa, mashekhe walikuwa wamesha wasili eneo hilo,.. Wana madrasa walikuwa wakifanya yao kwa kupiga vidufu,... Palikuwa hapatoshi, kama unavyojua watu wa tanga kwa harusi usipime.....
Sasa huku kwa fadhila kaanzisha balaa jipya, baada ya kusikia kuwa leo ndio ndoa ya akina rahim, na yite hio ni kwasababu ya rahim ili kumpa ukweli juu ya ujauzito ule kuwa sio wakwake,...
"ivi unajua kinachoendelea fadhila"
Minah alimwambia fadhila kama anajua kuwa rahim anafunga ndoa,...
"ndio, si zena wanafunga ndoa"
"sasa kwanini unaangalia tu na wewe ndio unastahili"
"nastahili kivipi??.."
"unajua fadhila wewe ni mwana madrasa, lakini hukuwa makini na hilo, ulikuwa bize na mambo mengine huzingatiii... Kisheria mwenye mimba ndio wa kwanza kuolewa kwasababu yeye ndio kaanza kuleta familia.. Sasa unaachaje nafasi kama hio"
Sasa fadhila kweli ni mwana madrasa lakini swala hilo halijui...
"unasemaje minah???"
"we zubaa tu"
"lakini pia sheria ya dini yetu inasema mwanamke mwenye ujauzito haruhusiwi kuolewa mpaka atakapojifungua"
"wewe nenda kavuruge tu... Tena pale kuna watu wengi sana, ndio pazuri yaani kila mtu ajue una ujauzito wa rahim... Nenda wewe utapoteza haki yako.. Na sasa kumebakia nusu saa tu ndoa ifungwe"
Kweli huku kwenye jukwaa, la ndoa wanandoa wakiwa wamependeza mno.. Rahim na kanzu yake ya kifahari, bila kusahau zena alivalia vizuri mpaka raha.... Jamali alikuwa mahali hivi, akampigia baba yake simu kuwa kila kitu kinakwenda kuisha
"baba... Ndoa inakwenda kufungwa hivyo"
Aliongea jamali huku akiwa na woga woga kiasi..
"mbona mimi nimeshafika... Nipo jirani na msikiti mkuu"
"ati unasemaje?? Tayari upo tanga mzee"
"yaani hapa naulizia tu hilo jukwaa lipo wapi"
"baba, jukwaa lipo jirani na msikitini.."
"basi... Ngoja niulize hapa"
Simu ilikata huku mzee akitafuta mtu wa kumuuliza....
Sasa mbaya zaidi mtu anaemuuliza alikuwa ni fadhila aliokuwa na haraka ya kuwahi kuvuruga ndoa isifanyike... Mana yeye akisema tu kuwa ana ujauzito wa rahim, basi ni kweli ndoa itaahirishwa, mana kidini yeye ndio anatakiwa kuanza kuolewa yeye...
"samahani mwanangu... Eti kwenye huu mtaa kuna kijana anaoa"
Mzee rashidi au baba yake rahim aliuliza kama vile sio mzaliwa wa eneo hilo, na fadhila yeye hajui kama huyu ndio baba yake na rahim, hilo halijui kabisaa,...
"ndio.. Ni hapo mbele tu"
"unaweza ukanielekeza"
Aliongea mzee ambae ndio baba mzazi wa rahim.. Ila Zena hajui
"ndio... Twende"
Fadhila alipanda kwenye gari huku akiwa na hamu ya kuwahi, na ni kweli watawahi mana bado hawajaanza lolote,... Fadhila ndani ya gari, na wote baba yake rahim na fadhila lengo lao ni moja kuistopisha ndoa isifungwe,... Ila sema hawajuani, fadhila anajua huyu mzee ni mualikwa tu... Na huyu mzee anajua huyu dada anamuelekeza tu.. Kumbe nia yao ni moja... Sasa kule jukwaani zena na rahim ndio wanaamshwa kwenye viti vyao, na kila Mtu kashika pete kwa ajili ya kumvisha mwenza wake..... Kwa mbaali gari ya mzee rashidi ilionekana,... Maana yake ni kwamba wameshafika eneo la tukio, na uwezekano wa ndoa kustopishwa ni mkubwa... Mana mzee na fadhila tayari wapo eneo hilo japo hawajuani kuwa lengo lao ni moja tu...
Je? Watafanikiwa kwa jambo hilo??.. Na je itakuwaje??.... USIKOSE
ITAENDELEA...........
(Mke Muislamu)
Sehemu Ya 28
Mtunzi... MoonBoy
Simu No, +255714419487 WhatsApp
Ilipoishia Jana →→↓↓
"rahim, "As Salaam Aleykum mama"
Alisalimia zena huku akimpa mkono mama yake rahim,... Wakati huo rahim ndio anainua kichwa chake na kusema...
"mama... Huyu ndio mchumba wangu.. Sasa mbona huupokei mkono wake"
Aliongea rahim huku mama kashikwa na butwaa kwa jinsi alivyokuwa anamuona mtoto wake..... Masikini zena hajachoka kuunyoosha mkono wake, japo haukuwa na majibu ya kupokelewa na mama mkwe.... Na wakati huo sasa,.. Yale majamaa ndio yanakuja kwa nyuma nyuma taaratibu ili kumkamata rahim,... Sasa Mbaya zaidi kumbe wamempangia zena mabaya pale watakapo fanikiwa kuondoka na rahim wao....
ENDELEA.........
Ujio wa mama rahim sio wa kwenda kwa wakwe, bali alikuja kumchukuwa mtoto wake ili aende shule, mana baba yake anamfokea sana kwa rahim kuwepo Tanga huku shule zikiwa zimefunguliwa,... Na rahim ni mwanafunzi mzuri sana sema pombe ndizo zilizomharibu, na huu ndio ulikuwa mwaka wake wa mwisho ikiwa ni mwezi wa 9 sasa yaani ameshapitwa na masomo sana tu,....
Sasa leo mama kaja kumchukuwa mwenyewe, na nia yake ni kumchukua hapo hapo Airport, na pia hakuja mwenyewe kaja na vijana wa nguvu kama watano hivi, na vijana hao tayari wamesha wazunguka akina rahim baada ya mama yake kusimama nao...
Wakati huo zena kanyoosha mkono kumsalimia mama mkwe,.. Lakini mama rahim alikuwa kama hauoni mkono huo, yaani macho yake yalikuwa kwa rahim jinsi alivyobadirika....
"ivi ni wewe rahim mwanangu ninaekujua au naota"
"ni mimi mama...... Mama lakini zena anakusalimia"
Aliongea rahim mana zena hakuchoka kunyoosha mkono kwa mama mkwe japo mama mkwe kama vile hauoni,..
"nani kasababisha kuwa hivyo"
Aliuliza mama rahim huku rahim akinyoosha kidole kwa zena, kumaanisha kuwa aliefanya yeye kuwa mtu wa dini, ni zena...
Huezi amini mama aliona hata kuupokea ule mkono wa zena, bado haitoshi, mana kitu alichokifanya ni kikubwa mno.... Huezi Amini mama rahim alimkumbatia kabisa zena, yaani hata ule mkono aliona ni mdogo sana,... Mama hata machozi yalimtoka,...
"mwanangu.. Ahsante sana kwa kunibadilishia mtoto wangu.... Sio kuwa nilikuwa sitaki uwe hivyo, ila upendo wetu kwako ulizidi mpaka tukawa tunakuacha sasa ufanye utakalo"
Aliongea mama rahim huku akiwa kamkumbatia zena,... Sasa wale jamaa nao ndio walikuwa wanakaribia ili wamkamate rahim, lakini mama aliwazuia
"jamani? Basi.... Nitawalipa pesa zenu, lakini basi msikamate mtu tena"
Aliongea mama rahim huku akitoa pochi yake na kutoa burungutu la pesa na kuwapa wale majamaa waliokuwa tayari kufanya kazi ya kumkamata rahim.... Sasa wakati mama anatoa pesa, huku zena alitoa kitenge ambacho alikuwa nacho kwenye mkoba wake,.... Mama rahim alishangaa anafungwa kanga,.. Kana kwamba nguo aliovaa ni fupi mno.. Machozi yalizidi kumtoka huku akizidi kuingiwa na imani ya hutuma..
"Ahsante mwanangu"
Mama rahim alimshukuru zena kwa kumfunga kanga,... Sasa wale jamaa wakatafuta usafiri wao, na kurudi arusha... Ila mama Safari ya kurudi arusha ilikufa, na alikuwa hana nia ya kubaki tanga, lakini ilimghalimu aendelee kubaki...
Wakati huo huku nyumbani bibi anamuulizia rahim kwa jamali
"we jamali mdogo wako kaenda wapi"
Aliuliza bibi mzungu huku akiwa na wasiwasi,...
"aaahhhhh kwa sasa, nadhani atakuwa anakaribia kufika arusha"
Bibi alitoa macho,
"Unasemaje wewe??... Kaenda kufanya nini"
"bibiiiii.... Yule bado ni wakusoma... Nashangaa mnakaa nae tu huku"
"mungu wangu mjukuu wangu anakwenda kurudia pombe tena"
"bibi... Hata mimi hapa Nasubiri tu simu ya mama aniambie nikachukue gari Airport"
"kwahio mama yako nae alikuja"
"tena kaja na wanajeshi ili wamkamate rahim"
"mbona mimi sijui, na hamjaniambia"
"sasa we si hutaki aende utaambiwa vip"
Mara ghafla wanasikia sauti ya honi iliopiga nje ya geti,...
Jamali alistuka, ina maana mama yake wamemshindwa kumkamata?? Mana alitegemea kupata simu ya kwenda kuchukuwa gari Airport,..
Jamali haraka haraka anakwenda kufungua geti,.. Alishangaa kumwona mama yake, akiwemo rahim na zena..
Jamali kashindwa kuelewa kwanini imekuwa hivyo,... Bibi alifurahi sana kumwona rahim karudi, mana tayari bibi keshaingiwa na wasiwasi juu ya mjukuu wake, kana kwamba kumtengeneza kote huko leo anarudi kuanza tena...
Waliingia ndani lakini jamali bado haamini, kama rahim karudi tena hapa,...
"shkamoo mama"
Mama rahim alimsalimia mama mkwe wake, kisha wakaingia ndani...
Walipokaa tu, jamali kaja na maswali yake
"mama vipi tena... Huyu mtu shule zimefunguliwa tayari"
Jamali aliongea hayo kwa kumwambia mama yake
"jamali mwanangu.... Kweli nimejiskia raha sana rahim kuwa katika hali hii... Binafsi hata baba yako akilijua hili, litamfurahisha sana"
"kwahio mama, Unasemaje kuhusu shule"
Aliuliza jamali lakini mama hakumjibu,... Mama rahim alimgeukia mama mkwe wake na kumuuliza...
"mama.... Rahim anatakiwa kwenda shule... Unaonaje nikaonana na wazazi wa huyu mschana tukaongea"
Zena alifurahi sana kusikia hivyo,....
"sawa nitakupeleka ukawaone"
"rahim.... Nataka uoe, lakini Tuende arusha ukamalizie masomo yako huku ukiwa na mkeo, hilo nimeliona ni sahihi, kwasababu baba yako anagomba san kuhusu shule"
Rahim kusikia aoe, alitamani hata muda huo huo
"mama... Shakira je"
Rahim alimuuliza mama yake kama mtego tu
"hapana rahim.... Huyu huyu anakufaa"
"lakini ni masikini hawa"
"sitaki kujua...."
Rahim aliongea hivyo kwa maana asije wakaenda huko wakakuta maisha ya ajabu wakaanza kuleta mambo ya Kiswahili...
Jioni ilipofika, familia yote ya akina rahim, ilikwenda kwa akina zena,.. Na wakati huo na familia ya akina zena nayo yote ilikuwepo, mana waliambiwa kuwa kuna ugeni utakuja jioni,... Hivyo maandalizi ya kuwapokea wageni yalikuwepo,.. Mama yake rahim alijua anakwenda kwa wakwe wenzie, hivyo alitakiwa kuvaa kiheshima... Rahim hata yeye leo anamshangaa mama yake kavalia nguo ndefu ndefu,.. Hata jamali haamini kama leo mama yake kavaa hivyo....
Maongezi yalianza... Baina ya wazee wazima, wazazi akina kaka.....
"jamani wazazi wenzangu... Mtoto wetu kapenda kwenu... Hivyo anataka jiko... Na kwakuwa wanapendana,... Sioni kama kuna tabu"
Aliongea bibi wakati huo bibi zake na zena pia wapo na ndio waliokuwa wanaongea wenyewe,...
"sisi hatuna shaka... Ni nyinyi tu kukubaliana na matakwa yetu"
Aliingea bibi yake zena, huku rahim na zena wanaomba mungu tu wakubaliane,... Mana wao hawaruhusiwi kuongea ispokuwa zena ataulizwa..
"matakwa gani tena jamani... Tuwaozesheni watoto wakayaanze yakwao"
Aliongea bibi yake rahim huku wakiendelea kunywa chai, si unajua vikao vya tanga vilivyo...
"mtoto wetu katunzwa haswa... Ana kila kitu yule, hamjui mwanaume toka kuzaliwa kwake"
Mama rahim alitoa macho kuskia zena alikuwa hamjui mwanaume toka kuzaliwa kwake,...
"mnasemaje... Ivi karne hiii mabinti hao wapo kweli"
Aliuliza mama yake rahim huku akishangaa kwa kauli hizo..
"haaaaa mbona huku tanga wapo wengi sana... Kiukweli kwa mjini huko sidhani lakini huku tanga ndani ndani wapo weengi mno"
Aliongea bibi yake zena huku akisubiri majibu toka kwa mume, yaani wazazi wa mume... Lakini mama hajaridhika ikabidi amuangalie mtoto wake amuulize.... Kwa macho macho, kuwa ni kweli zena ni bikra...
Rahim alitikisa kichwa kuashiria hajawahi kumjua... Lakini pia bibi yake zena hakutaka kudhibitisha sana, hivyo alimuuliza zena kuwa
"zena... Uko sawa au umeshaharibu"
"bibi, nipo sawa... Fanyeni mnachojua tu ila mimi na rahim tunajuana vizuri"
Aliongea zena, huku bibi yake zena akimrudia bibi yake rahim
"unasikia huko.. Vijana wenyewe wanajuana wapo vizuri... Sasa kazi ni kwenu kwa kile tunachokitaka"
"haya semeni mnataka nini"
Hapo bibi yake zena akatulia na kumwachia baba mwenye mtoto wa kike..
"kwa mimi... Nataka ng'ombe saba madume manne na majike matatu.. Hapo mimi nimemaliza"
Alipomaliza baba, akaja mama yake zena
"Kiukweli kwa mimi mama mtu... Ninachokitaka kwenu, naomba muishi na mtoto wangu vizuri,.. Anakwenda kuwa wenu, hivyo muishi kama mtoto wenu... Hicho ndicho kitu ninachokitaka kwenu"
Sasa baada ya mama yake zena kuongea hayo... Mama rahim akamjibu kuwa
"hilo umelipata mama.... Enhee kwa upande wa mabibi na mababu"
Aliuliza mama zena,... Huku bibi akijiandaa
"mimi nataka vitenge pea saba, na kanga zangu kama pea tatu... Nataka na hijabu,.. Hivyo tu vinatosha"
Baada ya bibi kuongea,.. Alifuata babu yake zena,..
"mimi bwanaaaaaaaaa..... Nataka kondoo wawili ili nichunge chunge kidogo... Nataka bakora... Mana nimezeheka sasa.... Kingine nataka koti... Bila kusahau kilo 50 za sukari.. Kuna baridi jamani"
Sasa wale wakubwa wote waliisha kutaja matakwa yao, na yote hayo ni kwasababu zena amejitunza usichana wake na ndio maana wana uhuru wa kutaja watakacho... Jamani kujitunza usichana raha kweli,.. Sasa nyie hayeni
Kaka mtu nae na mdogo mtu nae kila mtu alitaamka kitu akitakacho.... Sasa ikafika zamu ya zena kutaka kitu chochote kwa mume
"mimi nataka mswahafu tu"
Baba alitoa macho, mwanae kutaka mswahafu peke yake...
Lakini baba ikabidi atulie tu mana ni maamuzi yake yeye mwenye kuolewa
"ok, nadhani mumemaliza mambo yenu,... Sasa uwezekano wa kulipa pesa badala ya hivyo vitu si upo"
Aliuliza mama rahim, ili kama uwezekano wa kulipa pesa upo, alipe pesa badala ya vitu,.... Familia ikakubali walipwe pesa zao zote, hivyo mahesabu yakapigwa, mama rahim hapo hapo akatoa pesa keshi, huku akisema
"ndoa, nataka ifungwe kesho... Ili huyu aende shule"
Kuanzia saa hio maandalizi yalianza,.. Walialikwa watu wengei sana na sehemu ya kufungia ndoa iliandaliwa vizuri sana, mpaka usiku saa nne watu wapo bize,... Kila kitu kilinunuliwa kasoro mavazi ya wana harusi yalikuwa bado,... Familia zote zilikuwa na furaha sana, lakini sasa mama yake rahim hakutaka baba yake rahim alijue hilo, kwasababu lazima ataleta pingamizi... Yaani mama rahim alimpenda zena kwa nusu siku tu, baada ya kumuona mtoto wake amekuwa Muislamu safi, na sababu ya kumrudia mungu ni kwasababu ya zena, hivyo mama alimoenda kwa kumbadirishia mwanae,.... Lakini sasa mbaya zaidi jamali yeye anataka mdogo wake amalize shule kwanza hivyo hajapenda kitendo cha rahim kupewa mke ingali bado ni mwanafunzi,.... Mama yake rahim, na bibi yake rahim, na rahim mwenyewe, simu zao zilikuwa zimezimwa kwa siku hio, ila kasoro jamali, kwani yeye alikuwa na simu ya pembeni tofauti na ile iliozimwa,... Jamali hakupenda mdogo wake aoe kwa wakati huo na istoshe jamali na baba yake vinaivana vizuri,.... Huezi amini usiku huo huo simu kwa baba yake, ambae kwa sasa yupo dubai...
"haloo dady shkamoo"
Alisalimia jamali huku akiangaza macho huku na kule ili asije akasikiwa na mmoja wao,....
"Marahaba, vipi saa hizi"
Baba yake aliuliza kuna nini muda huu,
"mzee, huku unapatiwa mkwe"
"mkwe Kivipi"
"rahim anaoa kesho"
"Whaaaaaat?"
"ndio hivyo mzee... Na kesho saa saba ndoa inafungwa msikitini"
"hivi huyu mtoto ana akili kweli... Na mama enu nae yupo wapi"
"mama ndio kipau mbele mzee"
"pumbavu sana.... Hebu ngoja nimpigie"
"kazima simu, yaani hii yenyewe hawajui kama nina simu ndogo, mana tumezima wote simu zikawekwa mahali ili wewe usijue"
"hapana.. Haiwezekani... Mimi nataka mwanangu asome... Yaani nitahakikisha hio ndoa haikamiliki"
"sasa utafanyeje mzee"
"kesho nakuja na ndege ya private... Nataka uje Airport na hio gari uje unichukue"
"sasa watanishtukia wasiponiona mzee"
"shiiiiit,... Ngaoja nina jamaa wangu hapo Airport nitamwazima gari yake, ila usizime simu.... Mama yako hana akili kabisa huyu"
Kesho yake sasa mida kama saa tano za asubuhi akina rahim na zena walikuwa ndani, wakiangalia nguo za kufungia ndoa walizoenda kununua muda mfupi uliopita,... Katika viwanja vya ndoa, mashekhe walikuwa wamesha wasili eneo hilo,.. Wana madrasa walikuwa wakifanya yao kwa kupiga vidufu,... Palikuwa hapatoshi, kama unavyojua watu wa tanga kwa harusi usipime.....
Sasa huku kwa fadhila kaanzisha balaa jipya, baada ya kusikia kuwa leo ndio ndoa ya akina rahim, na yite hio ni kwasababu ya rahim ili kumpa ukweli juu ya ujauzito ule kuwa sio wakwake,...
"ivi unajua kinachoendelea fadhila"
Minah alimwambia fadhila kama anajua kuwa rahim anafunga ndoa,...
"ndio, si zena wanafunga ndoa"
"sasa kwanini unaangalia tu na wewe ndio unastahili"
"nastahili kivipi??.."
"unajua fadhila wewe ni mwana madrasa, lakini hukuwa makini na hilo, ulikuwa bize na mambo mengine huzingatiii... Kisheria mwenye mimba ndio wa kwanza kuolewa kwasababu yeye ndio kaanza kuleta familia.. Sasa unaachaje nafasi kama hio"
Sasa fadhila kweli ni mwana madrasa lakini swala hilo halijui...
"unasemaje minah???"
"we zubaa tu"
"lakini pia sheria ya dini yetu inasema mwanamke mwenye ujauzito haruhusiwi kuolewa mpaka atakapojifungua"
"wewe nenda kavuruge tu... Tena pale kuna watu wengi sana, ndio pazuri yaani kila mtu ajue una ujauzito wa rahim... Nenda wewe utapoteza haki yako.. Na sasa kumebakia nusu saa tu ndoa ifungwe"
Kweli huku kwenye jukwaa, la ndoa wanandoa wakiwa wamependeza mno.. Rahim na kanzu yake ya kifahari, bila kusahau zena alivalia vizuri mpaka raha.... Jamali alikuwa mahali hivi, akampigia baba yake simu kuwa kila kitu kinakwenda kuisha
"baba... Ndoa inakwenda kufungwa hivyo"
Aliongea jamali huku akiwa na woga woga kiasi..
"mbona mimi nimeshafika... Nipo jirani na msikiti mkuu"
"ati unasemaje?? Tayari upo tanga mzee"
"yaani hapa naulizia tu hilo jukwaa lipo wapi"
"baba, jukwaa lipo jirani na msikitini.."
"basi... Ngoja niulize hapa"
Simu ilikata huku mzee akitafuta mtu wa kumuuliza....
Sasa mbaya zaidi mtu anaemuuliza alikuwa ni fadhila aliokuwa na haraka ya kuwahi kuvuruga ndoa isifanyike... Mana yeye akisema tu kuwa ana ujauzito wa rahim, basi ni kweli ndoa itaahirishwa, mana kidini yeye ndio anatakiwa kuanza kuolewa yeye...
"samahani mwanangu... Eti kwenye huu mtaa kuna kijana anaoa"
Mzee rashidi au baba yake rahim aliuliza kama vile sio mzaliwa wa eneo hilo, na fadhila yeye hajui kama huyu ndio baba yake na rahim, hilo halijui kabisaa,...
"ndio.. Ni hapo mbele tu"
"unaweza ukanielekeza"
Aliongea mzee ambae ndio baba mzazi wa rahim.. Ila Zena hajui
"ndio... Twende"
Fadhila alipanda kwenye gari huku akiwa na hamu ya kuwahi, na ni kweli watawahi mana bado hawajaanza lolote,... Fadhila ndani ya gari, na wote baba yake rahim na fadhila lengo lao ni moja kuistopisha ndoa isifungwe,... Ila sema hawajuani, fadhila anajua huyu mzee ni mualikwa tu... Na huyu mzee anajua huyu dada anamuelekeza tu.. Kumbe nia yao ni moja... Sasa kule jukwaani zena na rahim ndio wanaamshwa kwenye viti vyao, na kila Mtu kashika pete kwa ajili ya kumvisha mwenza wake..... Kwa mbaali gari ya mzee rashidi ilionekana,... Maana yake ni kwamba wameshafika eneo la tukio, na uwezekano wa ndoa kustopishwa ni mkubwa... Mana mzee na fadhila tayari wapo eneo hilo japo hawajuani kuwa lengo lao ni moja tu...
Je? Watafanikiwa kwa jambo hilo??.. Na je itakuwaje??.... USIKOSE
ITAENDELEA...........