THE ISLAMIC WIFE
(Mke Muislamu)
Sehemu Ya 13
Mtunzi... MoonBoy
Simu No, +255714419487 WhatsApp
Ilipoishia Jana →→↓↓
Sasa rahim anatafuta gia ya kuendea pale dukani ili amuulize kwanini jana kaenda kulala nae wakati akiwa kalewa, hilo tu ndio swali kwake,... Sasa rahim akakaza moyo mpaka pale dukani, na hapo alikuwa hajalewa, na duka hilo lipo hapo hapo nyumbani, hivyo mzee akitoka tu atamuona rahim,...
"mambo zena"
"sema As salama Aleykum warahmatullah wabarakatuh"
"mmmhhhhhh hio ndefu sitoweza kuitaamka"
"afu umekujaje sa hii wazazi wangu wapo"
Rahim mwanamke akishakuwa wake hua kuongea anaweza lakini ni kwa upole utafikiri kondoo,..
"kuna kitu nataka nikuulize zena... Kizuri sana ila sijui kwanini umenivizia nikiwa nimelewa"
"nimefanya nini"
Sasa wakati huo huo fadhila nae anatokea nae alikuwa anakuja kwa zena, lakini alipomwona rahim pale dirishani, alibana mahali, na alikuwa akisikia yaliokuwa yakiongelewa na rahim....
"mmmhhh eti unajifanya hujui... Jana ulinifanyia nini... Mpaka saa saba za usiku"
Sasa zena yeye anashangaa maneno ya rahim,... Lakini sasa kule kwa fadhila nae alikuwa anajiuliza kuwa
"khaaa... Ina maana rahim hakumbuki tukio la jana??.... Safi sana.... Wacha amwambie ili zena akasirike na waachane..... Rahim. Lazima awe wangu"
ENDELEA...........
Maneno ya fadhila aliokuwa akijisemea mwenyewe baada ya kusikia kuwa rahim hakumbuki mtu aliyekuwa nae mpaka saa saba za usiku,... Fadhila alifurahi sana kuskia hivyo kuwa rahim hakumbuki tukio la jana,... Na rahim wakati huo hajui kama fadhila yupo jirani na anasikia... Hivyo mpaka sasa tunajua fadhila ndio alikuwa na rahim jana usiku kucha, sasa ni pombe gani hizo mtu asijui
"we rahim wewe, jana mimi si nilikuacha mwenyewe"
Rahim ukumbuke ni mpole sana mana hajalewa, ila dharau za pesa zipo pale pale hata kama hajalewa,
"sikiliza zena,.. Mi najua unaona aibu lakini unafahamu ulichonifanyia jana usiku... Afu kwani kulikuwa na haja gani unipeleke nyumbani saa saba hio.. Ungeniacha tu nimalize afu na asubuhi safi tu"
Aliongea rahim kama tunavyomjua tabia yake, hua hachagui cha kuongea hata kidogo,... Lakini wakati huo zena anashangaa kwa kile anachokiongea rahim.... Kwahio kutokana na maongezi ya rahim, zena keshajua jana rahim kafanya nini.... Sasa zena ile anajiandaa tu kumjibu rahim, ghafla mzee mvungi huyo katokea kwa uwani
"we kijana wataka nini hapa"
Aliongea baba yake zena asiotaka zena awe karibu na huyu kijana
"shkamoo mzee..."
Rahim alimsalimia, na nilishakwambia kuwa rahim akiwa hajalewa, anakuwa mzuri sana ila dharau za chini chini kutokana na pesa zao, haziishagi siku zote... Na rahim hawezi kupitisha siku bila ya kulewa, yaani ni lazima,... Iwe kalewa tilalila au kagusa kidogo, lakini haachi hata siku moja,...
"nakuuliza unataka nini hapa nyumbani kwangu"
"Samahani mzee, nimekuja kununua kalamu"
Rahim aliongea kwa upole, na hapo kidogo hata mzee akashangaa,.. Mbona jana kajibiwa kihuni na leo hali imekuwa tofauti,...
"ina maana koote hakuna maduka umeliona hili tu au"
"Samahani mzee... Zena, basi usinipe hio kalamu"
Rahim akajifanya kasusa kabisa kuchukuwa hio kalamu, lakini pia sio kuwa aliitaka hio kalamu, ni basi tu gia zake za kuondokea baada ya kukutwa na mzee
Rahim aliondoka zake taaratibu kisha huyooo, fadhila nae kuona hivyo akaamua kumfuata rahim kule kule alipoelekea,..
Sasa huku dukani mzee alimfokea sana mtoto wake, lakini licha ya kumfokea, pia alimuuliza kuwa
"mbona leo kaita mzee, na jana aliita dingi"
"hapo bado hajanywa vitu vyake"
"kumbe akiwa hajanywa ni kondoo"
Mzee ndio anashangaa kusikia habari hio...
Huku sasa fadhila kamkuta rahim kakaa mahari kwenye kivuli, wakati huo jua kali la saa saba hivi inakwenda saa nane...
"mambo rahim"
"poa nambie"
"safi tu.... Naona leo umemfua umpendae mpaka dukani kwao"
"ndio... Na jana kanipa vitu we acha tu"
Sasa fadhila roho ilikuwa inamuuma, kitendo afanye yeye, afu sifa apewe zena,... Aliona ni kitu kibaya sana ambacho hawezi kukikalia kimya...
"kwaio rahim unamaanisha jana ulipata utamu"
"ahh we acha... Zena ata..."
Sasa kabla rahim hajamalizia kuongea, fadhila kamstopisha
"basi, basi basi... Inatosha.. Huyo zena na Uislamu wake ule aje alale na wewe ana kichaa...ulevi ulionae wewe, zena kweli asubutu kuja kulala na wewe na hali ile ya jana"
Fadhila alivunja ukimya, mana sifa zote hizo zinamfaa yeye na sio zena.. Lakini sasa rahim nae anashangaa kuwa, fadhila kajuaje kama jana alilewa bwax,...
"we umejuaje kama jana mi nililewa"
"kwani uliolala nae jana ni nani kama sio mimi"
Rahim alitoa macho kuskia kuwa jana kumbe alilala na fadhila afu keshaenda kusema ujinga kule kwa zena...
"unasemaje wewe?"
"jana ulilala na mimi, na sio zena... Ila nakushangaa sana kwanini hukumbuki"
"fadhila? Ivi una akili kweli wewe"
"ina mana mimi sistahili kuwa nawe.. Au mimi sio mwanamke"
"hata kama.... Lakini unajua kabisa mimi nampenda zena, kwanini umefanya ujinga kama huo,... Fadhila sema asee we chalii umenikera kinoma asee"
Rahim ameongea utafikiri anaongea na mwanaume mwenzake, kumbe ni mwanamke,.. Na kitu anachokililia rahim ni kwamba, kwanini asingesema mapema, mpaka akaenda kuropoka kule
"kwahio hujapenda ram"
"ndio... Kwasababu hukusema mapema mpaka nikaenda kuropoka kwa zena kule"
"usijali.. Mimi nitalimaliza kwa zena"
Unajua rahim ni mtoto wa kiume na mpenda starehe sana, hivyo kulala na fadhila sio kuwa kachukia, kufurahia sana mana ni moja kati sehemu ya starehe zake, lakini sasa kitu anachokililia ni kuwahi kumwambia zena na mbaya zaidi zena keshajua kuwa rahim kamaanisha nini...
"hata kama lakini hawezi kuelewa hata kidogo... Afu umeniwekea nini?, yaani Sikumbuki kitu kabisa jana"
Rahim aliuliza tena akiwa na hasira mno,.. Na fadhila alionekana kusita kuongea, kana kwamba kweli jana kuna kitu alimfanyia rahim mpaka kutokujitambua,...
"utanisamehe rahim... Lakini na mimi ni mwanamke, nilishindwa tu kukuambia hata mimi nakupenda"
"nataka nijue jana ilikuwaje"
SASA HAPA FADHILA ANATUPA HISTORIA YA JANA JINSI ILIVYOKUWA
Wakati ule rahim akiwa anamuuliza fadhila kuwa
"wewe unamjua mtu alielewaaaaaa"
Papo hapo akadondoka chini kwa ulevi kumzidia,.. Sasa fadhila akaanza kuogopa mana rahim ni mtoto wa tajiri mno, sasa akikutwa nae hapo ataambiwa kamfanya nini, roho ya kumuacha akawa hana,...
"mungu wangu... Rahim.... We rahim... Ram... Jamani ram amka basi"
Wakati huo rahim alikuwa akikoroma mno,...
Yaani usingizi jumlisha pombe, yaani ni usingizi wa pono,... Sasa fadhila kwao hua hakuna jam sana, yeye ana chumba chake cha nje,.. Yani nyumba yao imeungana na chumba chake, kama vile nyumba iliojengwa mfano wa ( L ).. Lakini nyumba ni hio hio moja, sasa fadhila alifikiria ampeleke Kwao, yaani kwao huyu rahim, lakini sasa kwakina rahim ni mbali kidogo kuliko kwa akina fadhila..... Aliona kwa akina rahim ni mbali, Bora ampeleke kwao akampe hata huduma ya kwanza, mana ukiona mlevi kazidiwa na pombe basi ujue hajala akashiba au hajala kabisa
Dakika tano mbele wakawa wamefika katika chumba cha fadhila, na hapo wazazi wa akina fadhila hawajui kwasababu hicho ni chumba cha nje, kama nilivyokwambia malezi ya fadhila ni ya kawaida tu, sio kama ya zena,... Hivyo mambo ya wanaume anayajua sana, ila sio kuwa kazidisha hapana yaani ni mtu ambaye keshawahi kuwa na mwanaume, simaanishi kuwa ni wengi,... Sasa alipomfikisha hapo chumbani kwake alimlaza vizuri kitandani kwake kisha akaenda nyumba kubwa yaani kwa wazazi wake, akakoroga uji saafi tena wa maziwa, huku ukiwa umejazwa nazi.. Kisha akaja kumnywesha rahim,... Dakika tano mbele rahim kapata fahamu, kumbe ni kweli alikunywa unywaji bila kula, na yote hayo ni kwasababu ya kumuwahi zena kule chini ya mti.. Sasa rahim kapata fahamu, lakini kuamsha macho au kuamka hawezi kwa kuchoshwa na kemikali za unywaji mana ni kali na ukali wake ni wa taratibu sana... Sasa kitu alichokosea fadhila, alijisahau kabisa kama rahim nae ni mwanaume,.. Kumbe alipokuwa anamnywesha ule uji, alikuwa kamkalia kwa juu katika haya maeneo ya flaizi,... Mwanaume hata kama hujaona lakini kuna hali lazima utahisi ni tofauti, sasa utofauti wa hali hio fadhila aliujua, kwasababu alimkali,.... Sasa fadhila aliipenda ile hali huku akijisemea kuwa
"heeeeeeee.... Yamekuwa hayo tena?"
Aliongea fadhila huku tabasamu zito likimshuka, lakini sasa aliwaza, mtu huyo kwa jinsi anavyompenda zena,hatokubali kulala nae,.. Fadhila ni mtoto wa kitanga, anajua aingie wapi atokee wapi,.. Kuna dawa alikwenda kuichukuwa, na rahim hawezi kujua kiwa ni dawa au ni tiba bado inaendelea,... Huezi amini rahim alijikuta anapatwa na usingizi wa pono, yaani bora hata mwanzo alivyozidiwa na pombe, sasa hivi ni zaidi ya mara tatu ya wakati uliopita..
Ilipofika Saa saba za usiku,.. Fadhila alikuwa anafikiria alale nae mpaka asubuhi au inakuwaje,... Lakini akajua tu lazima rahim akasirike pale atakapogundua kuwa usiku mzima alilala na fadhila,... Huezi amini usiku huo huo alimkurupua... Kwa bahati nzuri alikutana na bajaji, aliiita kisha wakaseidiana na dereva bajaji,... Walipofika nyumbani kwa akina rahim, fadhila alikuwa hana hata shilingi tano,.. Fadhila alimsachi rahim na kuitoa pochi yake iliokuwa imejaa pesa nyingi sana Elfu kumi kumi zilizomtia uvivu fadhila kwa kuzihesabu... Fadhila alitoa noti ya shilingi elfu kumi moja tu, kisha akampa dereva bajaji aondoke zake,.. Fadhila aliirudisha ile pochi, lakini dereva toyo hakuridhika kuona pochi imerudi mfukoni na kuna burungutu la pesa
"we vipi, unarudishaje pochi kirahisi hivyo"
"sikiliza wewe, mimi nimekulipa ujira wako, swala la pochi halikuhusu sawa"
"aahhh mbona unanikolomea sasa?.. Hawa ndio mafisadi wa nchi hawa, sio wa kuwaacha tu"
"huyu kaka ni Mpenzi wangu sawa, naomba uondoke"
Sasa dereva kuona huyu ni mwanamke tu kwanini ashindwe kuchukuwa pesa yote hio"
"kwanza pesa ulionipa ndogo hii... Nataka nyingine"
Ghafla dereva bajaji akatoa chuma katika bajaji yake... Fadhila alianza kuogopa, na wakati huo ni saa saba za usiku, kumetuliaaa
"mtu mwenyewe fisadi tu huyu afu unamlegezeeea"
Sasa wakati huo dereva bajaji anamsogelea rahim pale chini,.. Fadhila alikuwa tayari keshaogopa maskini ya mungu,.. Kajibana kwenye nguzo ya geti, na ubaya wa nyumba hio haikuwa na mlinzi, mana tanga ni raha tu...
Je? Nini kitaendelea??... Dereva atafanikiwa kuchukuwa burungutu la pesa???... USIKOSE
ITAENDELEA...