Hadithi za babu yangu mzee Aweda na uchaguzi wa 2014/2015

Hadithi za babu yangu mzee Aweda na uchaguzi wa 2014/2015

Mikael Aweda

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2010
Posts
3,129
Reaction score
4,285
Hadithi ya babu yangu Mzee Aweda na Uchaguzi wa mwaka 2014/2015.

Babu yangu Aweda aliwahi kuniambia kuwa kuna watu kumi walikuwa wanasafiri baharini kwa kutumia boti au mtumbwi. Mmojawao ni mhunzi halafu ni mtundu sana. Kutokana na tabia yake hiyo, akawa ana ng'oa mabati na mbao kwenye boti. Wao walimwacha wakisema hawezi kungóa mabati kiasi cha mtumbwi/boti letu kuzama kwa kuwa na yeye pia atazama na sisi majini. Wakamwacha, akaendelea. Wakiwa wamefikia robo tatu ya safari yao mtumbwi/boti likaanza kuingiza maji, nao wakaanza kujiokoa kwa kurudishia kila mbao na bati lililongólewa huku wakimlaumu mwenzao, lakini haikusaidia – walichelewa na maji yakawazidi. Wote wakazama na kufa baharini. Hadithi ya babu yangu Aweda inatufudisha nini kwenye kipindi hiki tunapoendelea na mchakato wa uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu wa 2015?

Kuna watu wanadhani kuwa wao si wanasiasa, kwa hiyo mtaani/kijijini kwao, haijalishi mtu anayechaguliwa wala chama anachotoka. Haiwahusu. Mwaka kesho nani atakuwa Diwani, Mbunge au Rais haiwahusu – wengine hata kura hawapigi – wanasema haiwahusu. Kuna mwingine anajisemea moyoni kuwa yeye si mwanasiasa, yeye ni mwalimu, mkulima, mwanafunzi, Dakatari, mtanzania asiyetaka vurugu za wanasiasa, mwajiriwa katika shirika nzuri nk nk – wasichojua ni kwamba wanakosea sana kama wale wasafiri tisa wa hadithi ya Mzee Aweda.

Ukweli ni kwamba wanasiasa na viongozi serikalini, ndo wanaoamua ubora wa dawa unazokula iwe feki au nzuri, (Refer ARV Feki ziliripotiwa wiki hii), aina ya vifaa unayojengea iunguze nyumba au la, bei ya chakula chako iwe juu au chini, maji yawepo au la, Amani iendelee au vita vije, shule zifaulishe au zifelishe, ubora wa hospitali, bara bara, bei ya umeme ipande au ishuke, nauli ipande au ishuke nk nk. Hii ina maanisha kuwa kukaa kimya ni kufanya uamuzi mbaya kama wale wasafiri 9 na mwenzao.

Kwa hiyo basi,
Busara ya kawaida na mantiki au logiki, inanisukuma nihitimishe kuwa, kila mwenye busara hawezi kuacha kwenda kuchagua viongozi wazuri wa mtaa wake, na hawezi kuacha kupiga kura mwaka 2015 kwa sababu siasa inamhusu kuanzia anataka mpaka hataki - tofauti yetu itakuwa ni kiwango cha ushiriki tu. Na mtu makini hawezi kufanya ushabiki wa kivyama katika uamuzui wake bali hoja na sera nzuri za mgombea zinazotekelezeka na kubadili maisha yake ya kila siku.

Kutofanya hivyo rafiki zangu, ni sawa na kusema, mwenzetu huyu hawezi kutoboa boti letu likazama baharini kwa sababu na yeye atazama.
Wasiasa wengi tulio nao ni sawa na mhunzi mtundu niliyemtaja hapo juu. Watu wema ni lazima tuwajibike ili boti letu Kijijini au Tanzania yetu isizame-huu si muda wa kulaumu tu.

Ni ombi langu basi kwenu nyote,
kila moja akajiandikishe kuanzia tarehe 23 nov, 2014 hadi 28 Nov, 2014 na umshawishi na jirani yako ili tusiwe kama wasafiri 9 waliompuuza mwenzao akawazamisha, wakafa.

Mwanafalsafa mmoja alisema, Dunia inaharibika siyo kwa sababu ya uwepo wa watu wabaya (mafisadi), Hapana, Dunia inaharibika kwa sababu watu wema wamekaa kimya.
Tafakari,
Chukua hatua.
 
Hadithi ya babu yangu Mzee Aweda na Uchaguzi wa mwaka 2014/2015.

Ni ombi langu basi kwenu nyote,
kila moja akajiandikishe kuanzia tarehe 23 nov, 2014 hadi 28 Nov, 2014 na umshawishi na jirani yako ili tusiwe kama wasafiri 9 waliompuuza mwenzao akawazamisha, wakafa.

Mwanafalsafa mmoja alisema, Dunia inaharibika siyo kwa sababu ya uwepo wa watu wabaya (mafisadi), Hapana, Dunia inaharibika kwa sababu watu wema wamekaa kimya.
Tafakari,
Chukua hatua.
Mkuu Mikael P Aweda, asante kwa elimu murua ya uraia.

Pasco
 
Mbona Mzee wako kaongea vitu vya busara, though ilikuwa kama hadithi, SIJAONA AKIWA WAZI KUWA #Lowassa ndie anafaa urais, ningefurahi zaidi kusikia hilo, sbb nchi hii tunataka kiongozi WA KUTOA MAAMUZI AINA YA #Lowassa...ebu ukiongea nae tena mgusie hilo..na mweleze alivyo mchapa kazi, na pia akisema alisikia Richmond cjui nn, mwambie alibebeshwa mzigo na kutolewa kafara, mwenye Richmond hata ww Mikael unamjua...!!! Asante mfikishie ujumbe!!!
 
Nimekubali mkuu kila mtu atimize wajibu wake.
 
Mbona Mzee wako kaongea vitu vya busara, though ilikuwa kama hadithi, SIJAONA AKIWA WAZI KUWA #Lowassa ndie anafaa urais, ningefurahi zaidi kusikia hilo, sbb nchi hii tunataka kiongozi WA KUTOA MAAMUZI AINA YA #Lowassa...ebu ukiongea nae tena mgusie hilo..na mweleze alivyo mchapa kazi, na pia akisema alisikia Richmond cjui nn, mwambie alibebeshwa mzigo na kutolewa kafara, mwenye Richmond hata ww Mikael unamjua...!!! Asante mfikishie ujumbe!!!

Huna hoja zaidi ya povu tu,msome Aweda umuelewe vizuri!
 
Yeah ni elimu nzuri ya uraia na kwa kila aliye tayari kwa umri wa miaka 18+ ikiwa hana tatizo lolote la kiakili basi ni haki yake ya msingi kabisa kujiandikisha na hatimaye kupiga kura. Tatizo wa Tz wanapenda kuchaguliwa na ukiwachagulia bado watakulaumu sana na kunung'unika kila siku wakati fursa walikua nayo hapo awali ya kupinga maamuzi yako ya kuwachagulia.
 
Hadithi hii ni reflection ya yanayotokea ndani ya chadema. Kuna watu walichekelea wakati akina Zitto, Mwigamba na Kitila wanashughulikiwa. Leo chadema inahaha kupandisha hadhi yake kwa kuitumia ukawa tunapoelekea 2015. Mbowe anatamani suluhu na Zitto lakini wapi. Too late. Wanachama wao wamehamia ACT na wengine kurudi nyumbani CCM. Aweda, ahsante kwa hadithi yako tamu ambayo kila mmoja anaweza kuitafsiri kwa angle yake
 
Huna hoja zaidi ya povu tu,msome Aweda umuelewe vizuri!
Mkuu, kila mtu anaweza kumsoma Aweda kwa perception yake na akamuelewa. Nami nimemuelewa kwa muktadha nilioueleza hapo juu
 
mkuu Aweda,kwa mara yangu ya kwanza nakuona ukiandika kama kamanda wa ukweli (mwanamageuzi halisi).nakupa like ya moyoni kaka,ila zaidi ushauri wangu kwako ni kujitahidi kuifikisha elimu hii ya uraia na kujitambua kwa watanzania wengi kwa kadri inavyowezekana kwani elimu hii tu ndiyo inayoweza kuharakisha ukombozi wa pili na wa kweli. ''KEEP IT UP''.
 
Hadithi ya babu yangu Mzee Aweda na Uchaguzi wa mwaka 2014/2015.

Babu yangu Aweda aliwahi kuniambia kuwa kuna watu kumi walikuwa wanasafiri baharini kwa kutumia boti au mtumbwi. Mmojawao ni mhunzi halafu ni mtundu sana. Kutokana na tabia yake hiyo, akawa ana ng’oa mabati na mbao kwenye boti. Wao walimwacha wakisema hawezi kungóa mabati kiasi cha mtumbwi/boti letu kuzama kwa kuwa na yeye pia atazama na sisi majini. Wakamwacha, akaendelea. Wakiwa wamefikia robo tatu ya safari yao mtumbwi/boti likaanza kuingiza maji, nao wakaanza kujiokoa kwa kurudishia kila mbao na bati lililongólewa huku wakimlaumu mwenzao, lakini haikusaidia – walichelewa na maji yakawazidi. Wote wakazama na kufa baharini. Hadithi ya babu yangu Aweda inatufudisha nini kwenye kipindi hiki tunapoendelea na mchakato wa uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu wa 2015?

Kuna watu wanadhani kuwa wao si wanasiasa, kwa hiyo mtaani/kijijini kwao, haijalishi mtu anayechaguliwa wala chama anachotoka. Haiwahusu. Mwaka kesho nani atakuwa Diwani, Mbunge au Rais haiwahusu – wengine hata kura hawapigi – wanasema haiwahusu. Kuna mwingine anajisemea moyoni kuwa yeye si mwanasiasa, yeye ni mwalimu, mkulima, mwanafunzi, Dakatari, mtanzania asiyetaka vurugu za wanasiasa, mwajiriwa katika shirika nzuri nk nk – wasichojua ni kwamba wanakosea sana kama wale wasafiri tisa wa hadithi ya Mzee Aweda.

Ukweli ni kwamba iwanasiasa na viongozi serikalini, ndo wanaoamua ubora wa dawa unazokula iwe feki au nzuri, (Refer ARV Feki ziliripotiwa wiki hii), aina ya vifaa unayojengea iunguze nyumba au la, bei ya chakula chako iwe juu au chini, maji yawepo au la, Amani iendelee au vita vije, shule zifaulishe au zifelishe, ubora wa hospitali, bara bara, bei ya umeme ipande au ishuke, nauli ipande au ishuke nk nk. Hii ina maanisha kuwa kukaa kimya ni kufanya uamuzi mbaya kama wale wasafiri 9 na mwenzao.

Kwa hiyo basi,
Busara ya kawaida na mantiki au logiki, inanisukuma nihitimishe kuwa, kila mwenye busara hawezi kuacha kwenda kuchagua viongozi wazuri wa mtaa wake, na hawezi kuacha kupiga kura mwaka 2015 kwa sababu siasa inamhusu kuanzia anataka mpaka hataki - tutofautiana tu kiwango cha ushiriki. Hawezi kufanya ushabiki wa kivyama katika uamuzui wake bali hoja na sera nzuri zinazotekelezeka na kubadili maisha yake ya kila siku.

Kutofanya hivyo rafiki zangu, ni sawa na kusema, mwenzetu huyu hawezi kutoboa boti letu likazama baharini kwa sababu na yeye atazama.
Wasiasa wengi tulio nao ni sawa na mhunzi mtundu niliyemtaja hapo juu. Watu wema ni lazima tuwajibike ili boti letu Kijijini au Tanzania yetu isizame-huu si muda wa kulaumu tu.

Ni ombi langu basi kwenu nyote,
kila moja akajiandikishe kuanzia tarehe 23 nov, 2014 hadi 28 Nov, 2014 na umshawishi na jirani yako ili tusiwe kama wasafiri 9 waliompuuza mwenzao akawazamisha, wakafa.

Mwanafalsafa mmoja alisema, Dunia inaharibika siyo kwa sababu ya uwepo wa watu wabaya (mafisadi), Hapana, Dunia inaharibika kwa sababu watu wema wamekaa kimya.
Tafakari,
Chukua hatua.
Mkuu vipi zile hadithi zako za mtonyaji wa serikalini? Sijazisikia kitambo
 
Mkuu vipi zile hadithi zako za mtonyaji wa serikalini? Sijazisikia kitambo
Mkuu, hata Babu Slaa naye aliwahi kusema kuwa nusu ya Maafisa Usalama wanaripoti kwake. Naye siku hizi analia lia tu kwa vile hapati tena taarifa nyeti. Amebaki tu kusema eti amenyaka taarifa kuwa Rais Kikwete atakuwa ziarani China na Marekani. Hiyo kwake ni taarifa ua Siri
 
Mbona Mzee wako kaongea vitu vya busara, though ilikuwa kama hadithi, SIJAONA AKIWA WAZI KUWA #Lowassa ndie anafaa urais, ningefurahi zaidi kusikia hilo, sbb nchi hii tunataka kiongozi WA KUTOA MAAMUZI AINA YA #Lowassa...ebu ukiongea nae tena mgusie hilo..na mweleze alivyo mchapa kazi, na pia akisema alisikia Richmond cjui nn, mwambie alibebeshwa mzigo na kutolewa kafara, mwenye Richmond hata ww Mikael unamjua...!!! Asante mfikishie ujumbe!!!

Asante nimekusikia lakini sijashawishika bado
 
Back
Top Bottom