Hadithi ya umslopagaas

Mwishowe, akaanza kusema, na sauti yake ilikuwa ya unyenyekevu, wala si kama yake ya desturi, akasema, ‘’Sijawahi kufikiri ya kuwa ipo siku nita fundishwa wajibu wangu na Mzulu lakini mambo yaonyesha namna tunavyoweza kushawishiwa.

Labda mtaweza kufahamu jinsi ninavyoona aibu, tena nimestahili kuaibika. Kweli ilikuwa wajibu wangu kumshika Sorais na kumweka katika mikono ya askari wa zamu, lakini sikuweza, basi.

Nilimwacha aende zake, nikaahidi sitaitoa nje habari hiyo, ndiyo aibu yangu, Aliniambia ya kuwa nikijipanga upande wake atakubali nimwooe na kunifanya mfalme wa nchi hii, lakini nashukuru ya kuwa nilikataa hata alipoahidi nimwoe, nikasema kuwa siwezi kuwahaini rafiki zangu,Basi,ndugu zangu mnaweza kufanya mnayotaka kunifanyia, nimeyastahili yote.

Nitasema haya nawaomba nanyi mjilinde msipende mwanamke kwa moyo wenu wote na kujaribiwa naye kama mimi nilivyojaribiwa,’’ akageuka ili aende.

Sir Henry akasema, ‘’Mwenzangu, ngoja kwanza. Mimi nina hadithi ninayotaka kusimulia.’’

Akamsimulia habari ya mambo yale yaliyotokea jana baina ya yeye na Sorais. Basi, habari za mambo yale zilimvunja moyo zaidi maskini Good. Akasema, ‘’Nadhani habari hizi zimekwisha niponya,’’ akageuka akaenda zake, nami nilimsikitikia sana.


Siku ile ilikuwa siku ya baraza ambayo Malkia walizoea kukaa katika sebule kubwa na kusikiliza haja za watu, na kufanya mashauri mengineyo ya sheria na fedha, na mambo kadha wa kadha, basi baadaye kidogo tulikwenda sebuleni, na Bwana Good akafuatana nasi.

Tulipofika tulimkuta Nyleptha amekwisha kaa kitini pake, na mambo yanaendelea kama kawaida, amezungukwa na washauri, wakuu, wana sheria, makuhani, na jeshi kubwa kidogo la askari.


Lakini ilikuwa dhahiri kwa nyuso za watu na kwa namna watu walivyoongeaongea, ya kuwa hawaangalii mambo ya kawaida ila wanatazamia mengine, maana habari zimekwisha enea kuwa vita vya kindanindani vi karibu.

Basi, tukamwamkia Nyleptha, tukakaa katika mahali petu pa siku zote, pia muda mambo yaliendelea kama kawaida, mara tarumbeta zilianza kupigwa nje ya jumba, na mlio mkubwa uliwatoka umati wa watu waliokuwa wamehudhuria nje kutazama mambo yatakayotokea:

‘’Sorais! Sorais! Ndipo mingurumo ya magurudumu ya magari iliposikika na halafu pazia kubwa mwisho wa sebule lilivutwa upande, na Sorais ‘’Bibi wa Usiku’’ aliingia, wala hakuja peke yake.


Agon kuhani mkuu alimtangulia amevalia mavazi yake yaliyo bora, na kila upande wake makuhani walishindamana.


Sababu ya kuwako makuhani ilikuwa dhahiri, maana kwa kuwa amefuatana nao, hawezi kuzuiliwa, kwa kuwa kuwazuia makuhani ni kufanya mambo ya kufuru. Nyuma yake walikuwako wakuu wengine na kundi la askari waliochaguliwa.

Kumtazama tu ikawa dhahiri kuwa Sorais hakuwa na amani, maana badala ya mavazi yake ya siku zote amevaa mavazi namna ya kiaskari, tena alikuwa amechukua mkuki mdogo wa fedha mkononi mwake.


Basi, alipita katikati ya sebule na watu walijitenga wampishe njia, na alipofika karibu na mwamba mtakatifu alisimama, akaweka mkono wake juu yake, akasema kwa sauti kubwa. ‘’Salamu, Ee Malkia!’’

Na Nyleptha akajibu ‘’Salamu dada yangu! Karibu usiogope hutadhurika.’’
Sorais hakusema neno, akapita mpaka akasimama mbele ya viti vya kifalme, kisha akasema, ‘’Nina haja Ee Malkia!’’

Nyleptha akajibu, ‘’Sema, dada yangu, kuna kitu gani zaidi ninachoweza kukupa nawe unao nusu ya ufalme wote.’’

Akajibu, ‘’Unaweza kuniambia mimi na watu wote wa Zuvendi habari za kweli. Utamtwaa Yule mgeni mbwa mwitu kuwa mume wako ama sivyo?’’

Akamwelekezea mkuki wake mdogo Sir Henry.

Sir Henry akaukunja uso wake, akageuka akamwambia Sorais kwa sauti ndogo, ‘’Nakumbuka ya kuwa jana ulikuwa na majina mengine ya kuniita wala si mbwa mwitu, Ee Malkia.’’

Basi, hapo Nyleptha aliona mambo hayawezi kifichika tena, akaondoka, akashuka katika kiti chake, akaenda mpaka pale Sir Henry alipokuwepo, akasimama pale pamoja naye.


Akaiondoa bangili ya dhahabu mfano wa nyoka katika mkono wake, akamwambia Sir Henry apige magoti, akapiga goti moja, kisha, akaitwaa bangili ile ya dhahabu akaikunjua akaiweka shingoni mwa Sir Henry, akambusu pajini, akamwita ‘’Bwana mpenzi.’’

Kisha akasema, ‘’Waona, nimeiweka bangili yangu katika shingo ya mbwa mwitu, na tazama! Atakuwa mbwa wa kunilinda, ndilo jibu langu kwako wewe Malkia Sorais dada yangu, na kwa watu waliyofuatana nawe.’’

Kisha, akageuka akawaambia wote waliopo kwa sauti thabiti, ‘’Ndiyo, Bibi wa Usiku, na wakuu, na makuhani na watu wote mliopo , hii ndiyo dalili mbele yenu nyote, ya kuwa nimemtwaa mgeni huyu awe mume wangu.’’ Akamshika mkono wake akawatazama watu wote kwa ujasiri.

Tendo alilolitenda lilikuwa la uhodari, na Wazuvendi, kama watu wote walivyo, hupenda ujarisi, basi walipaza sauti zao kwa shangwe.

Lakini Sorais alisimama akitazama chini, maana hakuweza kustahimili kuiona furaha ya dada yake, na jinsi alivyomwibia mwanaume aliyetumaini kumpata, akatetemeka kwa hasira ya wivu aliouona.

Kisha, aliuinua uso wake, akaunyosha juu mkuki wake mdogo, akautikisa, akasema.
‘’Na wewe Nyleptha, unafikiri kuwa mimi Sorais, Malkia wa Zuvendi nitakubali mgeni huyo akikaliye kiti cha kifalme cha baba yangu? Hasha! Hasha! Kifua changu kingali na uzima ndani yake, na watu wangalipo wa kunifuata na mkuki upo wa kupigia, sitakubali! Nani, nani watakaonifuata mimi?


Sasa Nyleptha, mtoe mgeni mbwa mwitu na wale waliokuja pamoja naye wauawe kwa moto, maana sio hawa waliyofanya dhambi ya kufisha juu ya Jua kama sivyo, basi nitapigana vita! Vita vya damu! Nakuambia Nyleptha nitakubandua katika kiti chako, nawe utatupwa, utatupwa toka juu ya ngazi kuu mpaka chini yake, kwa sababu umetia aibu nyumba ya kifalme.


Na ninyi wageni, nawaambieni nyote isipokuwa Bougwan, ambaye kwa kuwa alinitumikia nitamwokoa akiwaacha wenzake, (na Bwana Good alikitikisa kichwa chake sana kukataa) nitawafunika kwa mabati ya dhahabu na kuwafungia minyororo mngali hai katika ncha za panda za sanamu zile nchani mwa dari, iliiwe dalili na maonyo kwa watu wote.


Na wewe Inkubu, wewe utakufa kwa namna nyingine ambayo sitakuambia sasa.’’
Basi, akanyamazana akitweta, maana ghadhabu yake ilimtikisa kama tufani, na mnong’ono wa nusu hofu na nusu kumsifu, ulivuma katika sebule.

Kisha, Nyleptha akajibu kwa madaha na utulivu, akasema, ‘’Dada yangu, heshima yangu ingevunjika kabisa kama ningesema maneno kama hayo uliyoyasema, na kuogofya kama wewe ulivyoogofya.

Lakini ukifanya vita, basi, mimi nitajaribu kupigana nawe, maana ingawa mikono yangu huonekana kuwa nyororo, lakini itakuwa kama chuma cha kukaba koo za jeshi lako. Sorais, sikuogopi!

Nahuzunika kwa mambo utakayoyaleta juu ya watu wetu na juu yako mwenyewe, lakini kwangu mimi, nasema, sikuogopi. Na wewe jana tu ulijaribu kumvuta Bwana wangu awe mpenzi wako na Bwana wako, ambaye leo unamwita mgeni mbwa mwitu.


Tena, usiku huu huu ulininyemelea kama nyoka mpaka katika chumba changu cha kulala kwa njia ya siri, nawe ulijaribu kuniua, mimi dada yako, katika usingizi wangu’’
Sauti ya Agon na watu wapatao ishirini wengine zililia, ‘’Uwongo! Uwongo!’’

Basi, hapo nilisimama mbele, na huku ninakiinua kile kipande cha kisu, nikasema, ‘’Si uwongo, je, kipini cha kisu hiki ki wapi Ee Sorais?’’


Na Bwana Good akajitokeza ili authibitishe uaminifu wake tena, akasema, ‘’Si uwongo. Nilimshika ‘Bibi wa Usiku’ pale kitandani pa Malkia Nyleptha, na kisu chake kilivunjikia kifuani pangu.’’

Basi Sorais aliona kuwa mioyo ya watu inageuka upande mwingine, akautikisa mkuki wake, akasema, ‘’Nani wako upande wangu? Je, Bougwan?’’ Hivi akageuka kumuuliza kwa sauti ndogo, kisha akaendelea.


‘’Wewe mwoga, kama ungalinifuata mimi ungeweza kuwa mfalme wangu na mume wangu’’


Akalia, ‘’Vita! Vita! Vita! Hapa nimesimama na mkono wangu juu ya mwamba mtakatifu utakaodumu mpaka Wazuvendi watakapojiinamisha chini ya mgeni. Nani watamfuata Sorais katika kushinda na kujipatia heshima.’’


Mara umati wa watu ulianza kufumukana kwa ghasia. Wengi waliokuwapo walijipanga upande wa Sorais, lakini wengine walitoka upande wake wakajipanga upande wetu. Katika hao waliotutoka, kiongozi mmoja wa askari wa Nyleptha aliyegeuka alijaribu kukimbia mlangoni walimopita watu wa Sorais.


Lakini Umslopogaas alikuwapo anatazama, akamshika, maana aliona kuwa akitoka, basi wengine watamfuata. Basi, Yule askari aliufuta upanga wake akajaribu kumpiga Umslopogaas.

Hapo, Mslopogaas alirudi nyuma kwa mlio mkali akauepuka upanga, akalizungusha shoka lake, akampiga, na Yule askari akaanguka chini amekufa.


Basi, hii ilikuwa damu ya kwanza kumwagika katika vita. Nikalia, ‘’Fungeni milango’’ nikifikiri kuwa labda tutaweza kumzuia Sorais, na kwa namna hii kuzuia matata.

Lakini tulichelewa; basi yeye na askari zake walikuwa katika kupita, na mara walikuwa wakienda mbio katika njia zao, zikajaa sauti za farasi na mingurumo ya magurudumu ya magari yake.

Basi, Sorais, akapita akivuta nusu ya watu nyuma yake kama chamchela katika mji, akashika njia yake kuiendea Marstuna iliyo ngome kadiri ya maili mia moja na thelathini upande wa kaskazini wa Milosis.

Baada ya hayo, mji ulijaa sauti za vishindo vya vikosi na matengenezo ya vita, Mzee Umslopogaas alianza tena kukaa katika jua na kuyanoa makali ya Inkosikazi.
 
Mwishowe, akaanza kusema, na sauti yake ilikuwa ya unyenyekevu, wala si kama yake ya desturi, akasema, ‘’Sijawahi kufikiri ya kuwa ipo siku nita fundishwa wajibu wangu na Mzulu lakini mambo yaonyesha namna tunavyoweza kushawishiwa.

Labda mtaweza kufahamu jinsi ninavyoona aibu, tena nimestahili kuaibika. Kweli ilikuwa wajibu wangu kumshika Sorais na kumweka katika mikono ya askari wa zamu, lakini sikuweza, basi.

Nilimwacha aende zake, nikaahidi sitaitoa nje habari hiyo, ndiyo aibu yangu, Aliniambia ya kuwa nikijipanga upande wake atakubali nimwooe na kunifanya mfalme wa nchi hii, lakini nashukuru ya kuwa nilikataa hata alipoahidi nimwoe, nikasema kuwa siwezi kuwahaini rafiki zangu,Basi,ndugu zangu mnaweza kufanya mnayotaka kunifanyia, nimeyastahili yote.

Nitasema haya nawaomba nanyi mjilinde msipende mwanamke kwa moyo wenu wote na kujaribiwa naye kama mimi nilivyojaribiwa,’’ akageuka ili aende.

Sir Henry akasema, ‘’Mwenzangu, ngoja kwanza. Mimi nina hadithi ninayotaka kusimulia.’’

Akamsimulia habari ya mambo yale yaliyotokea jana baina ya yeye na Sorais. Basi, habari za mambo yale zilimvunja moyo zaidi maskini Good. Akasema, ‘’Nadhani habari hizi zimekwisha niponya,’’ akageuka akaenda zake, nami nilimsikitikia sana.


Siku ile ilikuwa siku ya baraza ambayo Malkia walizoea kukaa katika sebule kubwa na kusikiliza haja za watu, na kufanya mashauri mengineyo ya sheria na fedha, na mambo kadha wa kadha, basi baadaye kidogo tulikwenda sebuleni, na Bwana Good akafuatana nasi.

Tulipofika tulimkuta Nyleptha amekwisha kaa kitini pake, na mambo yanaendelea kama kawaida, amezungukwa na washauri, wakuu, wana sheria, makuhani, na jeshi kubwa kidogo la askari.


Lakini ilikuwa dhahiri kwa nyuso za watu na kwa namna watu walivyoongeaongea, ya kuwa hawaangalii mambo ya kawaida ila wanatazamia mengine, maana habari zimekwisha enea kuwa vita vya kindanindani vi karibu.

Basi, tukamwamkia Nyleptha, tukakaa katika mahali petu pa siku zote, pia muda mambo yaliendelea kama kawaida, mara tarumbeta zilianza kupigwa nje ya jumba, na mlio mkubwa uliwatoka umati wa watu waliokuwa wamehudhuria nje kutazama mambo yatakayotokea:

‘’Sorais! Sorais! Ndipo mingurumo ya magurudumu ya magari iliposikika na halafu pazia kubwa mwisho wa sebule lilivutwa upande, na Sorais ‘’Bibi wa Usiku’’ aliingia, wala hakuja peke yake.


Agon kuhani mkuu alimtangulia amevalia mavazi yake yaliyo bora, na kila upande wake makuhani walishindamana.


Sababu ya kuwako makuhani ilikuwa dhahiri, maana kwa kuwa amefuatana nao, hawezi kuzuiliwa, kwa kuwa kuwazuia makuhani ni kufanya mambo ya kufuru. Nyuma yake walikuwako wakuu wengine na kundi la askari waliochaguliwa.

Kumtazama tu ikawa dhahiri kuwa Sorais hakuwa na amani, maana badala ya mavazi yake ya siku zote amevaa mavazi namna ya kiaskari, tena alikuwa amechukua mkuki mdogo wa fedha mkononi mwake.


Basi, alipita katikati ya sebule na watu walijitenga wampishe njia, na alipofika karibu na mwamba mtakatifu alisimama, akaweka mkono wake juu yake, akasema kwa sauti kubwa. ‘’Salamu, Ee Malkia!’’

Na Nyleptha akajibu ‘’Salamu dada yangu! Karibu usiogope hutadhurika.’’
Sorais hakusema neno, akapita mpaka akasimama mbele ya viti vya kifalme, kisha akasema, ‘’Nina haja Ee Malkia!’’

Nyleptha akajibu, ‘’Sema, dada yangu, kuna kitu gani zaidi ninachoweza kukupa nawe unao nusu ya ufalme wote.’’

Akajibu, ‘’Unaweza kuniambia mimi na watu wote wa Zuvendi habari za kweli. Utamtwaa Yule mgeni mbwa mwitu kuwa mume wako ama sivyo?’’

Akamwelekezea mkuki wake mdogo Sir Henry.

Sir Henry akaukunja uso wake, akageuka akamwambia Sorais kwa sauti ndogo, ‘’Nakumbuka ya kuwa jana ulikuwa na majina mengine ya kuniita wala si mbwa mwitu, Ee Malkia.’’

Basi, hapo Nyleptha aliona mambo hayawezi kifichika tena, akaondoka, akashuka katika kiti chake, akaenda mpaka pale Sir Henry alipokuwepo, akasimama pale pamoja naye.


Akaiondoa bangili ya dhahabu mfano wa nyoka katika mkono wake, akamwambia Sir Henry apige magoti, akapiga goti moja, kisha, akaitwaa bangili ile ya dhahabu akaikunjua akaiweka shingoni mwa Sir Henry, akambusu pajini, akamwita ‘’Bwana mpenzi.’’

Kisha akasema, ‘’Waona, nimeiweka bangili yangu katika shingo ya mbwa mwitu, na tazama! Atakuwa mbwa wa kunilinda, ndilo jibu langu kwako wewe Malkia Sorais dada yangu, na kwa watu waliyofuatana nawe.’’

Kisha, akageuka akawaambia wote waliopo kwa sauti thabiti, ‘’Ndiyo, Bibi wa Usiku, na wakuu, na makuhani na watu wote mliopo , hii ndiyo dalili mbele yenu nyote, ya kuwa nimemtwaa mgeni huyu awe mume wangu.’’ Akamshika mkono wake akawatazama watu wote kwa ujasiri.

Tendo alilolitenda lilikuwa la uhodari, na Wazuvendi, kama watu wote walivyo, hupenda ujarisi, basi walipaza sauti zao kwa shangwe.

Lakini Sorais alisimama akitazama chini, maana hakuweza kustahimili kuiona furaha ya dada yake, na jinsi alivyomwibia mwanaume aliyetumaini kumpata, akatetemeka kwa hasira ya wivu aliouona.

Kisha, aliuinua uso wake, akaunyosha juu mkuki wake mdogo, akautikisa, akasema.
‘’Na wewe Nyleptha, unafikiri kuwa mimi Sorais, Malkia wa Zuvendi nitakubali mgeni huyo akikaliye kiti cha kifalme cha baba yangu? Hasha! Hasha! Kifua changu kingali na uzima ndani yake, na watu wangalipo wa kunifuata na mkuki upo wa kupigia, sitakubali! Nani, nani watakaonifuata mimi?


Sasa Nyleptha, mtoe mgeni mbwa mwitu na wale waliokuja pamoja naye wauawe kwa moto, maana sio hawa waliyofanya dhambi ya kufisha juu ya Jua kama sivyo, basi nitapigana vita! Vita vya damu! Nakuambia Nyleptha nitakubandua katika kiti chako, nawe utatupwa, utatupwa toka juu ya ngazi kuu mpaka chini yake, kwa sababu umetia aibu nyumba ya kifalme.


Na ninyi wageni, nawaambieni nyote isipokuwa Bougwan, ambaye kwa kuwa alinitumikia nitamwokoa akiwaacha wenzake, (na Bwana Good alikitikisa kichwa chake sana kukataa) nitawafunika kwa mabati ya dhahabu na kuwafungia minyororo mngali hai katika ncha za panda za sanamu zile nchani mwa dari, iliiwe dalili na maonyo kwa watu wote.


Na wewe Inkubu, wewe utakufa kwa namna nyingine ambayo sitakuambia sasa.’’
Basi, akanyamazana akitweta, maana ghadhabu yake ilimtikisa kama tufani, na mnong’ono wa nusu hofu na nusu kumsifu, ulivuma katika sebule.

Kisha, Nyleptha akajibu kwa madaha na utulivu, akasema, ‘’Dada yangu, heshima yangu ingevunjika kabisa kama ningesema maneno kama hayo uliyoyasema, na kuogofya kama wewe ulivyoogofya.

Lakini ukifanya vita, basi, mimi nitajaribu kupigana nawe, maana ingawa mikono yangu huonekana kuwa nyororo, lakini itakuwa kama chuma cha kukaba koo za jeshi lako. Sorais, sikuogopi!

Nahuzunika kwa mambo utakayoyaleta juu ya watu wetu na juu yako mwenyewe, lakini kwangu mimi, nasema, sikuogopi. Na wewe jana tu ulijaribu kumvuta Bwana wangu awe mpenzi wako na Bwana wako, ambaye leo unamwita mgeni mbwa mwitu.


Tena, usiku huu huu ulininyemelea kama nyoka mpaka katika chumba changu cha kulala kwa njia ya siri, nawe ulijaribu kuniua, mimi dada yako, katika usingizi wangu’’
Sauti ya Agon na watu wapatao ishirini wengine zililia, ‘’Uwongo! Uwongo!’’

Basi, hapo nilisimama mbele, na huku ninakiinua kile kipande cha kisu, nikasema, ‘’Si uwongo, je, kipini cha kisu hiki ki wapi Ee Sorais?’’


Na Bwana Good akajitokeza ili authibitishe uaminifu wake tena, akasema, ‘’Si uwongo. Nilimshika ‘Bibi wa Usiku’ pale kitandani pa Malkia Nyleptha, na kisu chake kilivunjikia kifuani pangu.’’

Basi Sorais aliona kuwa mioyo ya watu inageuka upande mwingine, akautikisa mkuki wake, akasema, ‘’Nani wako upande wangu? Je, Bougwan?’’ Hivi akageuka kumuuliza kwa sauti ndogo, kisha akaendelea.


‘’Wewe mwoga, kama ungalinifuata mimi ungeweza kuwa mfalme wangu na mume wangu’’


Akalia, ‘’Vita! Vita! Vita! Hapa nimesimama na mkono wangu juu ya mwamba mtakatifu utakaodumu mpaka Wazuvendi watakapojiinamisha chini ya mgeni. Nani watamfuata Sorais katika kushinda na kujipatia heshima.’’


Mara umati wa watu ulianza kufumukana kwa ghasia. Wengi waliokuwapo walijipanga upande wa Sorais, lakini wengine walitoka upande wake wakajipanga upande wetu. Katika hao waliotutoka, kiongozi mmoja wa askari wa Nyleptha aliyegeuka alijaribu kukimbia mlangoni walimopita watu wa Sorais.


Lakini Umslopogaas alikuwapo anatazama, akamshika, maana aliona kuwa akitoka, basi wengine watamfuata. Basi, Yule askari aliufuta upanga wake akajaribu kumpiga Umslopogaas.

Hapo, Mslopogaas alirudi nyuma kwa mlio mkali akauepuka upanga, akalizungusha shoka lake, akampiga, na Yule askari akaanguka chini amekufa.


Basi, hii ilikuwa damu ya kwanza kumwagika katika vita. Nikalia, ‘’Fungeni milango’’ nikifikiri kuwa labda tutaweza kumzuia Sorais, na kwa namna hii kuzuia matata.

Lakini tulichelewa; basi yeye na askari zake walikuwa katika kupita, na mara walikuwa wakienda mbio katika njia zao, zikajaa sauti za farasi na mingurumo ya magurudumu ya magari yake.

Basi, Sorais, akapita akivuta nusu ya watu nyuma yake kama chamchela katika mji, akashika njia yake kuiendea Marstuna iliyo ngome kadiri ya maili mia moja na thelathini upande wa kaskazini wa Milosis.

Baada ya hayo, mji ulijaa sauti za vishindo vya vikosi na matengenezo ya vita, Mzee Umslopogaas alianza tena kukaa katika jua na kuyanoa makali ya Inkosikazi.
Mapenzi ni sumu kali.
 
SURA YA KUMI NA TISA


Lakini palikuwa na mtu mmoja ambaye hakuweza kutoka kwa haraka kabla milango haijafungwa , ndiye kuhani mkuu Agon, ambaye tulisadiki ya kuwa ni msaidizi mkuu na mwongozi wa kundi la Sorais.

Mtu mkali mwereve huyu alikuwa hajatusamehe jambo lile la kuwaua viboko, ndivyo alivyosema. Sirini kwa kweli hakuweza kustahimili tulete maarifa ya kigeni, yaani ikiwa anaweza kuyazuia.

Tena, alijua ya kuwa dini yetu si dini yake, naye hakosi aliogopa kuwa tutajaribu kuifundisha, dini yetu katika nchi ya Zuvendi. Siku moja aliniuliza kama iko dini katika nchi yetu, nikamwambia ya kuwa kadiri ninavyoweza kukumbuka yapo madhehebu ya dini zipatazo tisini na tano. Aliposikia hivyo alistaajabu sana.


Basi, tulipopata habari ya kuwa Agon amekamatwa, Nyleptha, na Sir Henry na mimi tulifanya shauri tumfanye nini? Mimi nilitaka kumfunga asiweze kutoka tena, lakini Nyleptha alikitikisa kichwa chake akasema tukifanya hivyo tutaleta ghasia katika nchi nzima, akasema ‘’Lakini! Nikishinda na mimi peke yangu ni Malkia, basi nitazivunja nguvu za makuhani hawa, na kuondoa ibada na michezo na matendo yao ya giza na siri.’’


Basi, Sir Henry akasema, ‘’Basi kama hatumfungi, ni afadhali tumwache aende zake, maana hatatusaidia kitu hapa.’’ Nyleptha alimtazama upande upande akasema, ‘’Ndiyo unavyofikiri bwana wangu?’’ Sir Henry akajibu, ‘’Ndiyo, sioni faida ya kumweka hapa.’’


Nyleptha hakujibu neno ila alimtazama na huku anakiinamisha kichwa chake kwa haya, ndipo alipofahamu akasema, ‘’Nisamehe Nyleptha. Ni kweli kuwa utaolewa nami sasa?’’


Nyleptha akajibu, ‘’Sijui bwana, lakini kama bwana wangu unataka, basi, kuhani yupo, madhabahu ipo,’’ akakielekeza kidole chake kulinyoshea hekalu dogo lililokuwa karibu, ‘’na mimi nipo tayari kufanya utakavyo bwana wangu.


Ee bwana wangu, katika muda wa siku nane au muda mfupi zaidi huda budi kuniacha kwenda vitani, maana ndiwe utakayewaongoza watu vitani, na katika vita watu pengine huuawa, na ikiwa mambo haya yatatokea, basi, ningependa niolewe nawe ili niweze kuwa na kumbukumbu,’’ aliposema hivyo machozi yalimtoka machoni yakamtiririka usoni kama umande katika moyo wa ua.


Akaendelea, akasema, ‘’Tena, ikitokea kuwa nitashindwa, na taji itanipotea, na maisha yangu pamoja na taji, na maisha yako pamoja na yangu.

Sorais ana nguvu nyingi, tena ana uchungu sana, na akishinda hatakuwa na huruma.’’ Basi niliwaacha nikarudi chumbani nikifikiri juu ya mambo, nikamtazama mzee Umslopogaas akilinoa shoka lake.

Na baada ya kupita kadiri ya muda wasaa moja, Sir Henry akaja mbio amefurahi sana, akatuuliza mimi na Bwana Good na Umslopogaas kama tutapenda kushuhudia arusi ya kweli kweli.


Tukasema tutapenda, tukamfuata mpaka hekaluni, tukamkuta Agon na uso wake ulikuwa una hasira sana. Ikatokea ya kuwa yeye na Nyleptha walipambana juu ya arusi hii.


Agon alikataa kabisa kumwoza, wala hakukubali kumpa kuhani mmojawapo wake ruhusa ya kumwoza, na kwa hivi Nyleptha alikasirika, akamkumbusha kuwa yeye ni Malkia, tena mkuu wa dini, naye amenuia ya kuwa watamtii, Agon alizidi kukataa, basi mwishowe Nyleptha akasema.

‘’Vyema, siwezi kumuua kuhani mkuu kwa sababu watu wataona uchungu , wala siwezi kumfunga kwa sababu makuhani wadogo watafanya kelele na ghasia lakini naweza kumwacha hekaluni mbele ya madhabahu ya Jua atafakari bila chakula cho chote, maana hii ndiyo kazi yake; nawe, ee Agon, usipokubali kunioza, utawekwa mbele ya madhabahu ile pamoja na maji kidogo tu ya kunywa, hata upate nafasi ya kulifikiri jambo hili.’’

Basi, Agon alikuwa ameitwa mapema asubuhi wala hakupata nafasi ya kula chakula, na hata hapo anaona. Njaa kwa hivi baadaye kidogo akaghairi akasema ya kuwa atawaoza, lakini asichukue daraka lolote katika mambo hayo.

Basi, baadaye Nyleptha alikuja amefuatana na mabibi wawili, akaja mpaka aliposimama Sir Henry, akamshika mkono akamwongoza mpaka mbele ya madhabahu, na baada ya kitambo Agon akaja akawaoza.

Walipokwisha ozwa na Agon, mimi nilisimama mbele nimeshika kitabu cha sala mkononi mwangu, maana kila niendapo huchukua kitabu changu cha sala, nikasema:

‘’Sir Henry, mimi si kasisi, wala sina habari kuwa yale ninayoyataka kuyafanya ni mazuri najua si sheria lakini kama wewe na Malkia mtakubali nitapenda kusoma ibada ya Ndoa Takatifu ya Kanisa la Kiingereza.

Mambo unayoyafanya ni makuu, nami naona ya kuwa kwa kadiri inavyowezekana, yataka idhini ya dini yako wewe pia.’’

Sir Henry akajibu ‘’Mimi pia nimeyafikiri hayo, na nitapenda sana ufanye hivyo, maana nusu naona kama sijaoa bado.’’

Nyleptha hakukaidi, akafahamu kuwa mume wake anataka ndoa ifungwe kama desturi ya nchi yake, basi nilianza kusoma ibada ya Ndoa Takatifu toka mwanzo hata mwisho.


Huku nyuma Agon alijizuia kwa shida, maana alifahamu upesi ya kuwa wanaozwa kwa kawaida ya dini nyingine, na kwa kweli anafikiri kuwa mimi ni kuhani mkuu, kwa hiyo ni adui yake.

Basi, mambo haya yalipokwisha, Bwana Good na Umslopogaas na mimi tuliondoka tukawaacha Sir Henry na Nyleptha mume na mke. Good na mimi tulikula peke yetu siku ile, tukaona kama kwamba ndiyo kwanza tumemzika rafiki yetu badala ya kumwoza, na asubuhi yake kazi yetu ilianza kwa kweli.


Sasa makundi ya watu wenye silaha walianza kuhudhuria mjini kuitikia barua na matarishi aliopeleka Nyleptha.


Hatukumwona Nyleptha mara nyingi, wala Sir Henry, lakini Bwana Good na mimi tulikaa tukafanya mashauri pamoja na majemedari na wakuu tukitunga mashauri ya vita, tukitengeneza habari za zana za vita, na kutoa amri na kuangalia mambo kadha wa kadha yanayopasa vita.

Watu wengi walifika, na njia ya kufika Milosis ilitapakaa bendera za wakuu wanaofika pamoja na wafuasi wao kumsaidia Nyleptha.


Baada ya siku mbili ilikuwa dhahiri ya kuwa tutaweza kuanza vita tuna askari wa miguu kadiri ya arobaini elfu, na askari wapanda farasi kadiri ya ishirini elfu, lakini kwa habari tulizozipata, jeshi la Sorais.

Lilikuwa kubwa zaidi. Alikuwa amefanya kambi yake kuu katika mji uitwao Marstuna upande wa kaskazini wa Milosis, na watu wote wa pande za huko walikuwa wakienda kwake kumsaidia, Bwana mkuu Nasta alikuwa ametoka kwake amefuatana na wafuasi wake kadiri ya ishirini na tano elfu, walio askari wakali kupita wote wa Zuvendi.


Mkuu mwingine jina lake Belusha aliyekaa katika nchi walikofuga farasi, alikuwa amefika pamoja na wafuasi wake wapanda farasi kadiri ya kumi na mbili elfu, vivyo hivyo.


Ikaonekana kwamba jumla ya askari wa Sorais hawatapungua kadiri mia elfu.
Ndipo tulipopata habari kuwa Sorais anakusudia kutoka kambini na kujia mji wa Milosis na kuingangamiza nchi yote apitamo. Basi, sasa tulifikiri shauri moja, kama ni afadhali kukaa Milosis mpaka atakapokuja, ama kutoka na kupigana naye njiani.


Tulipoulizwa shauri, Bwana Good na mimi tulisema afadhali tutoke tupigane njiani. Kama tukikaa mjini na kungoja, watu watafikiri tunaogopa.


Tena ni jambo kuu katika shauri kama hili ambalo jambo dogo huweza kugeuza mioyo ya watu, kuanza kushughulika wala si kukaa tu.


Sir Henry naye alikubali shauri letu, na Nyleptha pia. Kadiri ya maili thelathini toka Marstuna, na maili tisini toka Milosis, palikuwa na mahali ambapo njia ilipinda kidogo ikapita katikati ya milima milima yenye misitu minene na upana wa kipito cha katikati kilikuwa kadiri ya maili mbili na nusu tu, basi, ilikuwa dhahiri ya kuwa kipito hicho kikizibwa, jeshi lenye mizigo mingi ya zana za vita halitaweza kupita.


Nyleptha alifikiri sana, kisha alikitaja kipito kile, akageuka kumtazama mume wake, akasema. ‘’Ni hapa utakapokutana na jeshi la Sorais. Napajua mahali hapo, na hapo utakutana nao na kuwafukuza mbele yako kama mavumbi mbele ya dhoruba.’’
Sir Henry alitazama tu asiseme neno.
 
SURA YA ISHIRINI


Siku ya tatu asubuhi Sir Henry na mimi tuliondoka. Jeshi lote lilikuwa limekwisha toka usiku isipokuwa kundi dogo tu, na mji wa Milosis ulikuwa hauna watu, tena kimya kabisa.


Hatukuweza kuacha askari mjini isipokuwa wachache tu kumlinda Nyleptha, na wale waliozuiwa wasiende vitani kwa sababu ya ungonjwa au sababu nyinginezo. Lakini hatukuona hofu kwa ajili ya mji, maana kwa namna ulivyojengwa haufikiki ila kwa shida, tena, adui wako mbele yetu wala si nyuma.


Bwana Good na Umslopogaas walikuwa wamefuatana na jeshi, lakini Nyleptha alifuatana na Sir Henry na mimi mpaka mlangoni pa mji, amepanda farasi mweupe mzuri sana jina lake Nuru, aliyesifiwa kuwa mwepesi kuliko farasi wote wa Zuvendi. Uso wake ulionyesha dalili ya machozi ya huzuni, lakini alijikaza kwa uvumilie wa uchungu pale tulipokuwa tuna agana.


Tulipofika mlangoni, alimsimamisha farasi wake akatuaga. Jana yake alikuwa amewakagua askari na wakubwa, akawatolea hotuba ya maneno ya ushujaa akiwaambia kwamba anawatumaini kabisa ya kuwa kwa ujasiri na uhodari wao hawakosi watashinda, wakatiwa moyo, wakaondoka na huku wanapiga ukulele wa kumshangilia, mpaka ardhi ikatikisika, na leo ikawa kama anafikiri vivyo hivyo, akasema, ‘’Kwa heri Makumazahn! Kumbuka kuwa naitumainia busara yako kutuokoa na Sorais. Najua utafanya wajibu wako.


Kwa heri Bwana wangu! Rudi na hali umeshinda, ama sivyo, uchukuliwe juu ya mikuki ya askari zako’’ (maana ni desturi kuchukua maiti ya mkuu aliyeuawa vitani juu ya namna ya kitanda kilichofanywa kwa mikuki).


Sir Henry hakusema neno, ila alimgeuza farasi wake aende mbele, labda roho yake ilimpanda kooni asiweze kusema. Nyleptha akasema, ‘’Nitasimama hapa hapa kuwapokea mtakaporudi hali mmeshinda. Na sasa Bwana zangu, kwa herini!’’


Basi, tuliondoka, lakini tulipokuwa tumekwenda kadiri ya yadi hamsini hivi, tuligeuka tukamwona amesimama pale pale, anatutazama, ndipo tulipoondoka kabisa.


Tulipokwenda kadiri ya maili moja, tulisikia vishindo vya askari mpanda farasi anatufuata; tukageuka tukamwona mtu anatujia anamwongoza Yule farasi bora Nuru.


Akasema, ‘’Malkia amenituma nimletee zawadi Bwana Inkubu, naye aliniambia niseme kuwa ana mbio na juhudi ya kuendelea kuliko farasi wote wa nchi.’’


Kwanza Sir Henry hakutaka kumpokea, akasema kuwa, si vizuri kumtumia farasi bora kwa kazi iliyo mbele yetu, lakini nilimshauri ampokee, nikijua kuwa Nyleptha ataudhika akimrudisha. Basi alimpokea naku mwambia Yule mtu ampe asante Malkia, tuliendelea katika safari yetu.


Ilipopata saa sita tuliwafikia askari wa nyumba ya jeshi letu, na Sir Henry akachukua daraka la kuwa mkuu wa jeshi zima. Tuliendelea bila kupigwa, na kwa kweli bila kuonekana na watu ila wachache, maana wenyeji wote wa miji na vijiji walikuwa wamekimbia wameogopa kuwa watatengwa katikati ya majeshi yanayopigana, na kusagwa kama ngano inavyosagwa katikati ya jiwe la juu na la chini ya kinu cha kusagia.


Siku ya nne jioni, maana mwendo wa jeshi kubwa ni wa pole pole, tulipiga kambi kadiri ya maili mbili upande huu wa kipito nilichotaja, na wapelelezi wetu walituletea habari kuwa Sorais na jeshi lake wanatujia, wamepiga kambi kadiri ya maili kumi upande mwingine wa kipito. Basi, kabla hakujapambazuka, tuliwatanguliza wapanda farasi elfu moja na mia tano ili wakishike kipito.


Mara walipofika, walishambuliwa na kikosi cha wapanda farasi wa Sorais, na vita vikali vikapiganwa. Sisi tulipata hasara ya watu kadiri ya thelathini waliouawa, lakini askari wengine wa upande wetu walipokifikia kikosi cha Sorais, kilirudi nyuma kikiwachukuwa wafu na majeruhi wao pamoja nao.


Jeshi letu kubwa lilifika kipito kwenye saa sita, na lazima nikiri ya kuwa shauri la Nyleptha lilikuwa zuri, maana kipito kile kilikuwa mahali pazuri sana pa kupigania, na hasa kwa sababu jeshi la adui ni kubwa kuliko letu.


Njia ilipanda kadiri ya maili moja mpaka kufika juu ya mwinuko, kisha iliteremka taratibu mpaka kwenye mto mdogo, kisha ilipanda tena mpaka kufika uwandani. Urefu wa njia toka juu ya mwinuko mpaka mtoni ulikuwa kadiri ya nusu maili, na wa toka mto mpaka juu ya mwinuko upande wa pili, ulikuwa karibuni kupata nusu maili.


Urefu wa mwinuko wa juu ulikuwa kadiri ya maili mbili na robo, ndiyo sawasawa na upana wa kipito ambacho kilipita katikati ya milima yenye misitu minene, na upande huu na huu wa kipito kuna miamba na vichaka vinavyofaa sana kufichia askari.


Basi, Sir Henry alilipanga jeshi lake juu ya mwinuko wa upande huu. Jeshi letu ambalo lilikuwa na askari kadiri ya sitini elfu, Ilipangwa hivi: katikati askari elfu ishirini wa miguu, wenye mikuki, panga na ngao za ngozi ya kiboko walipangwa. Kwa mfano, hao walikuwa kidari cha askari, nao walisaidiwa na askari wa miguu elfu tano na wapanda farasi elfu tatu waliowekwa nyuma yao wawe mfano wa akiba.


Pande zote mbili za kidari hicho, askari wapanda farasi elfu saba walipangwa na pande zao ila kwa mbele kidogo, vikosi viwili, kila kikosi chenye askari wenye mikuki, saba elfu mia tano walipangwa; kikosi kimoja upande huu na kimoja upande huu, na wapanda farasi elfu moja mia tano kila upande. ‘Basi, jumla ni sitini elfu.


Sir Henry alikuwa mkuu wa jeshi zima, mimi nilikuwa mkuu wa askari wapanda farasi elfu saba waliokuwa katikati ya kidari na wale wa upande wa kuume, ambao walikuwa chini ya amri ya Bwana Good, na vikosi vingine vilikuwa chini ya amri ya majemadari wa Zuvendi.
Mara tulipojipanga tu! jeshi la Sorais lilianza kujipanga juu ya mwinuko wa upande ule kadiri ya maili moja mbele yetu, mpaka mahali pote palifunikwa kwa ncha za mikuki, na ardhi ilitikisika kwa vishindo vya miguu ya askari zake.


Ilikuwa dhahiri wapelelezi wetu walituambia kweli, maana jeshi lake ni kubwa kuliko letu. Kwanza tulifikiri kuwa Sorais anataka kutushambulia papo hapo kwa jinsi wapanda farasi walivyoshughulika huko na huko, lakini vita havikutokea siku hii.


Mchana kutwa tulitazamana tukingojea, lakini hapana jambo lililotokea, na giza lilishuka, na mioto mingi sana iliwaka kila mahali kasha ikafifia tena. Saa zikapita, kukawa kimya sana kati majeshi ya pande zote mbili.

Usiku ule ulichosha sana, maana mambo mengi lazima yatengenezwe, tena hali ya kungojeshwa hivyo ilituudhi mno.


Nilifikiri juu ya vita vya kesho yake jinsi vitakavyo kuwa vikubwa mno, na mauaji yatakavyokuwa ya kutisha, nilipotafakari juu ya mambo yanayotegemea vita hivi, niliona shaka nyingi. Tena, ilihuzunisha sana kufikiri kuwa majeshi haya mawili yamekutanika kuangamizana kwa ajili ya wivu na hasira ya mwanamke.


Hii ndiyo nguvu iliyofichika, nayo ndiyo itakayopeleka majeshi ya wapanda farasi wapambane kama umeme ulio hai kupitia lile bonde lililo katikati, na kuyapindua pindua majeshi kama mawingu dhoruba inapopambana na dhoruba nyingine.


Fikira hii ilikuwa ya kutisha mno, nayo iliingiza mawazo moyoni juu ya madaraka ya wakuu wa dunia. Tulikaa hivi tukishauriana usiku, wenye nyuso nyeupe na mioyo mizito, huku walinda zamu wakipita pita huku na huko, na majemedari waliovalia wakaja na kuenda, wakaja na kuenda, kimya kama kivuli.


Basi, wakati ulipita hivyo mpaka kila jambo lilipokuwa tayari kwa mauaji yanayokuja; nikalala na mawazo mengi, nikajaribu kupata usingizi nisiweze kuupata kwa hofu ya kesho maana nani anayeweza kutabiri jambo litakalotokea kesho! Majonzi na mauti ni hakika; ni zaidi ya hayo hatuna habari nazo, na lazima nikiri kuwa niliona hofu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom