Hadithi ya umslopagaas

Hadithi ya umslopagaas

SURA YA KUMI NA SABA


Basi sasa udhia ule ambao mpaka sasa ulikuwa kama wingu dogo tu! Ulianza kudhihirika kabisa, ndiyo pengo alilo nalo Sorais kwa Sir Henry.

Nyleptha alikuwa mwenye tabia ya wivu sana, alikua anaudhika mno kila mara Sorais alipomfanyia Sir Henry fadhili, lakini hata hivyo hakukubali Sir Henry amwambie Sorais ya kuwa anataka kumwoa dada yake.

Angalimruhusu labda mambo yangalitokea vingine. Tena, Sir Henry alijua kuwa Bwana Good anampenda Sorais, na kwa kweli alikuwa ameanza kudhoofu kwa ajili ya kumpenda.

Mambo yaliendelea hivyo, ikawa jinsi Sir Henry anavyojaribu kumwepuka Sorais, ndivyo Sorais, alivyozidi kumfuata nakumwonyesha jinsi gani anavyo mpenda, mpaka mambo yakawa mabaya sana.

Ilikuwa kama kwamba Sorais hana habari ya kuwa Sir Henry anampenda Nyleptha, nikaihofia sana siku atakayoamka na kuyatambua hayo.


Maana Sorais ni mwanamke mwenye tabia ya ukatili sana. Basi, wakati niliouhofia ukawadia kama nilivyojua kuwa lazima utafika.

Siku moja Bwana Good alikuwa anakwenda kuwinda, na Sir Henry na mimi tulikuwa tunazungumza, mara tarishi wa jumbani alileta barua kumwambia Sir Henry afuatane naye mpaka chumbani kwa Malkia Sorais.

Sir Henry aliguna, akasema, ‘’Je, wewe huwezi kwenda mahali pangu?’’ Nikamjibu, ‘’La, mimi siendi, afadhali kumkabili tembo aliyejeruhiwa kwa bunduki ya marisaa kuliko kumkabili Sorais.

Mimi simo! Kama wewe ni mzuri hata kuwafanya wanawake wakupapatikie, basi matokeo yake ni juu yako mwenyewe.’’

Mimi sikubali kuwa mahali pako hata kama utanipa ufalme.’’
Basi, aliondoka akamfuata Yule tarishi, na mimi nilibaki nikimngojea.

Baada ya kupita muda wa dakika arobaini na tano, alirudi amefadhaika sana. Nikamuuliza habari za huko, akasema na sauti yake ilipwaya , ‘’Habari ni mbaya! Kweli matata yapo karibu sasa.

Nilipomfuata Yule tarishi, alinichukua mpaka chumbani kwa Sorais, nika mkuta peke yake ameketi kitandani anapiga gambusi.

Nilisimama mbele yake, na kwa muda kidogo hakuniangalia ila aliendelea kupiga gambusi na kuimba tu, kisha alinitazama na kucheka. Akasema, Umekuja.

Nilifikiri labda umeenda kushughulika na mambo ya dada yangu Nyleptha. Maana siku zote unashughulika naye, nami naona bila shaka kuwa wewe ni mtumishi mwema na mwaminifu.

Basi, sikusema neno, ila nilikiinamisha kichwa tu. Akasema ‘’Nataka kusema nawe, basi keti ustarehe’’ akajijongeza kitandani afanye nafasi niketi. Nikasema ya kuwa sistahili kuketi pamoja na Malkia.

Akasema, ‘’Keti.’’

Basi, nikaketi, akaanza kinitazama sana kwa macho yake makubwa meusi, kisha akasema, ‘Inkubu, unapenda uwezo?’ Nikamjibu ya kuwa nadhani wanaume wote hupenda uwezo wa namna namna.

Akasema, ‘Utaupata. Unapenda utajiri?’ Nikamjibu ya kuwa napenda utajiri kwa ajili ya vitu vinavyoletwa nao.

Akasema, ‘Utaupata.unapenda uzuri?’ Nikajibu kuwa napenda kazi za sanaa na za ustadi na kadhalika.

Akaukunja uso wake. Basi,ikawa sasa nimefadhaika hata nilikuwa ninatetemeka, nikajua ya kuwa mambo mabaya yatatokea, maana nilikuwa kama nimeduwaa, wala sikujiweza.

Mwisho akasema, Inkubu, wataka kuwa mfalme ‘’Tazama u mgeni, mimi ninafikiri kukufanya mfalme wa Wazuvendi wote, na mume wake Sorais.

La! Nyamaza kwanza unisikilize vyema. Siwezi kudhubutu kumwambia hivyo hata mtu mmoja katika watu wangu hisia za moyo wangu. Lakini wewe ni mgeni na kwa hivi nimeweza kusema nawe bila kuona haya.

Tena nakumbuka yote ninayoweza kukupa, na kutambua jinsi ilivyo vigumu kwako kuniposa.

Tazama, ufalme umewekwa miguuni pako, Bwana wangu Inkubu, na pamoja na ufalme, mwanamke ambaye wengine wametamani kumposa. Na sasa nijibu, Ee mteule wangu, na maneno yako yatakuwa matamu masikioni mwangu.’’

‘’Nikasema, Ee Sorais, nakuomba usiseme namna hii, maana mambo hayo hayawezi kuwa. Nimekwisha mposa dada yako, nami nampenda yeye! Yeye tu.’’

Basi, nilipokuwa nikisema, Sorais aliuficha uso wake kwa mikono yake, na alipoyasikia maneno yangu, aliuinua uso wake pole pole, nilipouona uso wake nilifadhaika sana, maana uso wake ulikuwa mweupe kabisa na macho yake yaling’aa kama balbu.


Akaondoka, akasimama na kuvuta pumzi kama kwamba roho yake inataka kumtoka. Mara alikitazama kisu kilichokuwapo mezani, kisha akanitazama mimi kama kwamba anafikiri kuniua pale pale lakini hakukitwaa.

Mwishowe akasema neno moja tu, ‘Nenda!’ Nkaondoka, Nikashukuru kutoka chumbani humo salama.

Sasa je, nitafanya nini?’’ Nilikitikisa kichwa changu, maana mambo yamekwisha kuwa mabaya sana. Hata katika Jehanamu hakuna ukali kama wa mwanamke aliyekataliwa! Na hasa kama ni mwanamke kama Malkia Sorais. Nikahofia yale yatakayotokea, na pamoja nayo hatari ya maisha yetu.


Nikasema, ‘’Lazima Nyleptha aambiwe habari hizo haraka, nami naona afadhali nimwambie mimi; maana ukimwambie wewe haikosi atashuku neno. Nani mkubwa wa zamu usiku huu?’’

Akajibu Sir Henry ‘ni Kara’ Nikasema. ‘’Vyema, naona hapana anayeweza kumdhuru Nyleptha. Usishangae, maana mimi nadhani bila shaka Sorais atajaribu kumdhuru.

Je, tumwambie Bwana Good habari za mambo yaliyotokea?’’
Sir Henry akasema, ‘’Sijui, maana habari hizi ndizo zitamuumiza sana hasa kwa jinsi anavyompenda Sorais.’’


Nikasema, ‘’Kweli, na labda hapana haja kumwambia. Atapata habari mwenyewe upesi. Sasa, sikiliza maneno yangu! Bila shaka sasa Sorais atajipanga upande wa Nasta analiyenuna huko katika nchi yake ya kaskazini, na vita vitatokea ambavyo namna yake havijatokea katika nchi ya Zuvendi kwa miaka mingi.


Tazama! ‘’nikamwonyesha natarishi wawili wanaotoka mbio chumbani mwa Sorais. Nikasema, ‘’Nifuate,’’ nikapanda ngazi ya kufikia juu ya mnara wa kulinda zamu, nikachukua darubini nikatizama juu ya ukuta wa jumba.


Tukamwona tarishi anakwenda mbio Hekaluni. Hakosi anampelekea habari kuhani mkuu, Agon. Sikumwona Yule tarishi wa pili. Lakini halafu kidogo, niliona mpanda farasi anakwenda mbio sana kupita katika mlango wa bustanini wa mji, nikatambua ni Yule tarishi wa pili.


Nikasema, ‘’Ah! Ama Sorais ni mwanamke wa juhudi. Anafanya mambo upesi, tena kwa ustadi na kwa nguvu.

Umefanya kama kumtukana, na sasa damu ya watu itamwagika kama mito kabla jua halijafutika , na damu yako pia akiweza kukushika.

Basi, nakwenda kumwambia Nyleptha. Wewe kaa hapa hapa ujaribu kutulia tena.’’
Nikaondoka.

Nilipata ruhusa kuonana na Nyleptha upesi. Alikuwa akimtazamia Sir Henry, na aliponiona mimi alisema, ‘’Bwana wangu mgonjwa? Makumazanh! Hata haji kunitazama. Natumaini si mgonjwa.’’

Nikamwambia ya kuwa hajambo, ndipo nilipoanza kumwambia habari zile toka mwanzo mpaka mwisho.

Lo! Angalia basi jinsi alivyoghadhabika! Akasema,
‘’Umethubutuje kunijia na kuniambia hadithi ya uongo kama hii? Kusema kuwa Bwana wangu alikuwa akishughulika na dada yangu Sorais! Ni uongo kabisa.’’
Nikamjibu, ‘’Niwie radhi Malkia, nilisema kuwa Sorais ndiye aliyekuwa akishughulika na Bwana wako.’’

Akasema, ‘’Usinitandazie utando wa buibui wa maneno. Si mamoja pia? Mmoja hutoa, mwingine hupokea na zawadi hupitishwa, si haja kugundua mwenye hatia ni nani! Sorais! Ee jinsi ninavyomchukulia Sorais Malkia, tena ni dada yangu. Hakika hangalifanya mambo hayo kama asingalivutwa.’’

Nikajibu, ‘’Nyleptha, unajua kabisa kuwa maneno yako ni ya upuuzi mtupu, na wakati huu si wakati wa kufanya upuuzi.’’

Akaupiga mguu wake chini kwa hasira, akasema, ‘’Unathubutuje kusema maneno kama haya? Je, Bwana wangu mwongo amekutuma unitukane hata na mimi? Wewe ni nani? si mgeni! hata kuthubutu kusema na mimi Malkia, tena kwa maneno kama haya?’’
 
Nikajibu, ‘’Naam, nimethubutu. Sikiliza! Dakika hizi unazopoteza kwa ajili ya hasira zako za bure, zaweza kulipoteza taji lako, na maisha yetu pia.

Wapanda farasi wa Sorais wamekwisha kwenda kukusanya jeshi. Katika muda wa siku tatu. Nasta atajiamsha katika milima yake kama simba wakati wa jioni, na ngurumo zake zitasikika katika nchi ya kaskazini.

Sorais ana sauti tamu, naye hataitumia bure. Bendera yake itachukuliwa toka mlima mpaka mlima, na toka bonde mpaka bonde, na askari wataifuata kama mavumbi yanayofuata chamehela.

Nusu ya jeshi zima la nchi watamfuata na katika kila mji na kijiji makuhani watawasengenya wageni, nao watafanya vita hivi viwe vita vya kidini Nimesema Ee Malkia.’’

Nyleptha alikuwa ametulia sasa, hasira yake na wivu ulikuwa umitulia, akajibadili kabisa kwa haraka, na sasa si mwanamke Yule mwenye wivu tena ila ni Malkia mwenye kuweza kazi na matendo.

Akasema, ‘’Maneno yako, Ee Makumazahn, ni ya busara. Nisamehe upuuzi wangu mahaba ni kama umeme. Ni mzuri mno nao huunganisha dunia na mbingu, lakini ole wetu, namna unavyoyapofua macho. Nawe unafikiri kuwa dada yangu Sorais atafanya vita nami. Basi, na afanye.

Hatanishinda ng’o. mimi pia ninao rafiki zangu na wafuasi wangu. Wako wengi watakao ziinua sauti zao na kuita ‘Nyletpha’, bendera yangu itakapotwekwa, na mioto yangu itakapowashwa karibu milima usiku huu kuwajulisha habari za vita vyangu.

Nitazivunja nguvu zake na kuwatawanya askari zake, na sehemu ya Sorais, ‘bibi wa usiku’ itakuwa usiku wa milele. Nipe karatasi na wino.

Asante. Sasa mwite mkubwa wa zamu, najua ni mtu mwaminifu.’’
Nilifanya kama alivyo niambia, na mkubwa wa zamu, mzee mtulivu jina lake Kara aliingia, akajiinamisha kwa heshima.

Nyleptha akampa karatasi ile akamwambia, ‘’Twaa hati hii, ni nguvu zako, weka watu kulinda kila mahali pa kutokea na kuingilia vyumbani mwa dada yangu Sorais, ‘bibi wa usiku.’ Watu wasipewe ruhusa kutoka wala kuingia, au maisha yako yatatozwa.’’

Yule mtu alishangaa mno, lakini hakusema neno ila ‘’Neno la Malkia litimizwe .’’ Akaondoka. Kisha, Nyleptha akatuma mtu kumwita Sir Henry , akaja anaona haya nyingi. Nilifikiri labda Nyleptha ataanza tena maneno yake ya wivu, lakini hakumtaja.

Basi, halafu kidogo, Yule mkubwa wa zamu aliyetumwa, akarudi kupasha habari ya kuwa Sorais amekwisha ondoka. Alikuwa amekimbilia hekaluni. Basi, hapo tukaanza kufanya mashauri.

Majemadari waliojulikana kuwa ni waaminifu wakaitwa, wakaambiwa habari, si zote, ila zilizotosha kufahamu mambo jinsi yalivyo, wakaamrishwa kukusanya watu wa vikosi vyao kadiri walivyoweza.

Nyleptha akawaambia wakuu wengine alioweza kuwatumaini, na wengine wao walitoka siku ile ile kwenda mahali pa mbali kuwakusanya wafuasi wao na watu wa makabila yao.


Basi, mchana kutwa na jioni tulifanya kazi ya kutuma matarishi huko na huko, wala hatukurudi vyumbani mwetu mpaka saa mbili za usiku. Kabla ya kulala, Sir Henry akafikiri ni vizuri kumwambia Umslopogaas alinde zamu karibu na chumba cha Nyleptha.

Umslopogaas alikuwa anajuana na watu wote wa jumbani, na Malkia walikuwa wamekwisha toa amri aruhusiwe kwenda popote apendapo, akazoea kutembea tembea usiku, kwa hiyo, hata kama akionekana anatembea karibu na chumba cha Malkia, watu hawatashuku jambo.

Basi, alilitwaa shoka lake, akaondoka, na sisi tukalala.
Ilikuwa kama kwamba nimelala dakika chache tu, nikaamshwa kwa kuona kama mambo si sawasawa.

Niliona kama kwamba yumo mtu chumbani ananitazama, mara ile niliketi kitandani, nikastajabu kuona kumekwisha pambazuka, na karibu na kitanda changu, Umslopogaas amesimama kama kivuli.

Nikamuuliza, ‘’Je, umesimama hapa kwa muda gani?’’
Akajibu ‘’Kadiri ya nusu saa Makumazahn.. nataka kusema nawe.’’

Basi, mara ile nilikuwa macho kabisa, nikamwambia aseme maneno yake.

Akasema, ‘’Kama nilivyoambiwa usiku, nilikwenda kulinda zamu karibu na chumba cha Malkia, basi nilijificha nyuma ya nguzo katika chumba kilicho karibu na chumba cha kulala cha Malkia, nikangoja.

Bougwan (Bwana Good ) alikuwa peke yake katika chumba cha zamu, na nje ya chumba askari mmoja wa zamu alikuwa amesimama.

Nikataka kujua kama ninaweza kupita bila kuonekana, nikaweza, nikapita nyuma yao. Basi, hapo nilingoja saa kadha wa kadha, ndipo ghafla niliona mwanamke anakuja ameshika kisu mkonononi mwake.

Tena nilimwona Bougwan amevivua viatu vyake anamfuatia Yule mwanamke. Yule mwanamke alipita karibu nami, nikamwona alikuwa ‘Bibi wa Usiku,’ Basi, nikangoja, na Bougwan naye alinipita pia.

Basi, vivyo hivyo tuliendelea pole pole kimya kabisa. Wa kwanza Yule mwanamke, wa pili Bougwan na wa tatu mimi, ila Yule mwanamke hakumwona Bougwan, na Bougwan naye hakuniona mimi.

‘’Basi, ‘Bibi wa Usiku ‘ alifika mpaka katika pazia la chumba cha Malkia Nyleptha, akapita ndani na Bougwan alimfuatia, na mimi niliwafuatia.

Mwisho wa chumba ni kitanda cha malkia, na Malkia alikuwa amelala usingizi.

‘Bibi wa Usiku’ alijikunia hivi na huku ameshika kisu tayari, akanyemelea mpaka kitandani pa Malkia. Alipokikaribia sana, Bougwan akamgusa mkono, na mara ile aligeuka akampiga kisu.

Kwa bahati Bougwan alikuwa amevaa deraya chini ya nguo zake, ama sivyo angalimzuru. ndipo Bougwan alipomtambua Yule mwanamke yu nani, akarudi nyuma ameshangaa asiweze kusema neno.

‘Bibi wa Usiku’ naye alishangaa, asiseme neno ila alikiweka kidole chake midomoni pake, akarudi , akapita katika pazia, na Bougwan alimfuatia.

Basi, hivyo walipita, nikamsikia Yule mwanamke kama anamsihi, nayeye anajibu, Hapana! Hapana! Hapana.

Nikaona kuwa anataka kuwaita askari wa zamu, lakini Malkia Sorais aliacha kusema, akamkazia macho yake makubwa, nikaona ya kuwa Bougwan ameshindwa kujizuia kwa uzuri wake.

Kisha aliunyosha mkono wake na Boungwan aliubusu, nikajifanya tayari kumkamata, mara! Akatoweka.’

Nikasema, alitoweka?’’
Akajibu, ‘’Ndiyo, na Boungwan alisimama akimtizama ukutani kama kwamba ameshikwa na jinamizi la usingizi. Kisha, naye pia akaenda, na mimi nikaja hapa.’’

Nikamuuliza, ‘’Una hakika Umslopogaas ya kuwa hukua unaota ndoto ya mambo hayo?’’
Akaufumbua mkono wake, akanionyesha kipande cha chuma cha bapa la kisu, kadiri ya inchi tatu, akasema, ‘’Makumazahn, kama niliota ndoto, basi, tazama kitu nilichopewa kwenye hiyo ndoto.

Kisu kilivunjikia katika deraya za Bougwan, na nilipopita nilikiokota hiki katika chumba cha kulala cha Malkia Nyleptha.’’
 
Nikajibu, ‘’Naam, nimethubutu. Sikiliza! Dakika hizi unazopoteza kwa ajili ya hasira zako za bure, zaweza kulipoteza taji lako, na maisha yetu pia.

Wapanda farasi wa Sorais wamekwisha kwenda kukusanya jeshi. Katika muda wa siku tatu. Nasta atajiamsha katika milima yake kama simba wakati wa jioni, na ngurumo zake zitasikika katika nchi ya kaskazini.

Sorais ana sauti tamu, naye hataitumia bure. Bendera yake itachukuliwa toka mlima mpaka mlima, na toka bonde mpaka bonde, na askari wataifuata kama mavumbi yanayofuata chamehela.

Nusu ya jeshi zima la nchi watamfuata na katika kila mji na kijiji makuhani watawasengenya wageni, nao watafanya vita hivi viwe vita vya kidini Nimesema Ee Malkia.’’

Nyleptha alikuwa ametulia sasa, hasira yake na wivu ulikuwa umitulia, akajibadili kabisa kwa haraka, na sasa si mwanamke Yule mwenye wivu tena ila ni Malkia mwenye kuweza kazi na matendo.

Akasema, ‘’Maneno yako, Ee Makumazahn, ni ya busara. Nisamehe upuuzi wangu mahaba ni kama umeme. Ni mzuri mno nao huunganisha dunia na mbingu, lakini ole wetu, namna unavyoyapofua macho. Nawe unafikiri kuwa dada yangu Sorais atafanya vita nami. Basi, na afanye.

Hatanishinda ng’o. mimi pia ninao rafiki zangu na wafuasi wangu. Wako wengi watakao ziinua sauti zao na kuita ‘Nyletpha’, bendera yangu itakapotwekwa, na mioto yangu itakapowashwa karibu milima usiku huu kuwajulisha habari za vita vyangu.

Nitazivunja nguvu zake na kuwatawanya askari zake, na sehemu ya Sorais, ‘bibi wa usiku’ itakuwa usiku wa milele. Nipe karatasi na wino.

Asante. Sasa mwite mkubwa wa zamu, najua ni mtu mwaminifu.’’
Nilifanya kama alivyo niambia, na mkubwa wa zamu, mzee mtulivu jina lake Kara aliingia, akajiinamisha kwa heshima.

Nyleptha akampa karatasi ile akamwambia, ‘’Twaa hati hii, ni nguvu zako, weka watu kulinda kila mahali pa kutokea na kuingilia vyumbani mwa dada yangu Sorais, ‘bibi wa usiku.’ Watu wasipewe ruhusa kutoka wala kuingia, au maisha yako yatatozwa.’’

Yule mtu alishangaa mno, lakini hakusema neno ila ‘’Neno la Malkia litimizwe .’’ Akaondoka. Kisha, Nyleptha akatuma mtu kumwita Sir Henry , akaja anaona haya nyingi. Nilifikiri labda Nyleptha ataanza tena maneno yake ya wivu, lakini hakumtaja.

Basi, halafu kidogo, Yule mkubwa wa zamu aliyetumwa, akarudi kupasha habari ya kuwa Sorais amekwisha ondoka. Alikuwa amekimbilia hekaluni. Basi, hapo tukaanza kufanya mashauri.

Majemadari waliojulikana kuwa ni waaminifu wakaitwa, wakaambiwa habari, si zote, ila zilizotosha kufahamu mambo jinsi yalivyo, wakaamrishwa kukusanya watu wa vikosi vyao kadiri walivyoweza.

Nyleptha akawaambia wakuu wengine alioweza kuwatumaini, na wengine wao walitoka siku ile ile kwenda mahali pa mbali kuwakusanya wafuasi wao na watu wa makabila yao.


Basi, mchana kutwa na jioni tulifanya kazi ya kutuma matarishi huko na huko, wala hatukurudi vyumbani mwetu mpaka saa mbili za usiku. Kabla ya kulala, Sir Henry akafikiri ni vizuri kumwambia Umslopogaas alinde zamu karibu na chumba cha Nyleptha.

Umslopogaas alikuwa anajuana na watu wote wa jumbani, na Malkia walikuwa wamekwisha toa amri aruhusiwe kwenda popote apendapo, akazoea kutembea tembea usiku, kwa hiyo, hata kama akionekana anatembea karibu na chumba cha Malkia, watu hawatashuku jambo.

Basi, alilitwaa shoka lake, akaondoka, na sisi tukalala.
Ilikuwa kama kwamba nimelala dakika chache tu, nikaamshwa kwa kuona kama mambo si sawasawa.

Niliona kama kwamba yumo mtu chumbani ananitazama, mara ile niliketi kitandani, nikastajabu kuona kumekwisha pambazuka, na karibu na kitanda changu, Umslopogaas amesimama kama kivuli.

Nikamuuliza, ‘’Je, umesimama hapa kwa muda gani?’’
Akajibu ‘’Kadiri ya nusu saa Makumazahn.. nataka kusema nawe.’’

Basi, mara ile nilikuwa macho kabisa, nikamwambia aseme maneno yake.

Akasema, ‘’Kama nilivyoambiwa usiku, nilikwenda kulinda zamu karibu na chumba cha Malkia, basi nilijificha nyuma ya nguzo katika chumba kilicho karibu na chumba cha kulala cha Malkia, nikangoja.

Bougwan (Bwana Good ) alikuwa peke yake katika chumba cha zamu, na nje ya chumba askari mmoja wa zamu alikuwa amesimama.

Nikataka kujua kama ninaweza kupita bila kuonekana, nikaweza, nikapita nyuma yao. Basi, hapo nilingoja saa kadha wa kadha, ndipo ghafla niliona mwanamke anakuja ameshika kisu mkonononi mwake.

Tena nilimwona Bougwan amevivua viatu vyake anamfuatia Yule mwanamke. Yule mwanamke alipita karibu nami, nikamwona alikuwa ‘Bibi wa Usiku,’ Basi, nikangoja, na Bougwan naye alinipita pia.

Basi, vivyo hivyo tuliendelea pole pole kimya kabisa. Wa kwanza Yule mwanamke, wa pili Bougwan na wa tatu mimi, ila Yule mwanamke hakumwona Bougwan, na Bougwan naye hakuniona mimi.

‘’Basi, ‘Bibi wa Usiku ‘ alifika mpaka katika pazia la chumba cha Malkia Nyleptha, akapita ndani na Bougwan alimfuatia, na mimi niliwafuatia.

Mwisho wa chumba ni kitanda cha malkia, na Malkia alikuwa amelala usingizi.

‘Bibi wa Usiku’ alijikunia hivi na huku ameshika kisu tayari, akanyemelea mpaka kitandani pa Malkia. Alipokikaribia sana, Bougwan akamgusa mkono, na mara ile aligeuka akampiga kisu.

Kwa bahati Bougwan alikuwa amevaa deraya chini ya nguo zake, ama sivyo angalimzuru. ndipo Bougwan alipomtambua Yule mwanamke yu nani, akarudi nyuma ameshangaa asiweze kusema neno.

‘Bibi wa Usiku’ naye alishangaa, asiseme neno ila alikiweka kidole chake midomoni pake, akarudi , akapita katika pazia, na Bougwan alimfuatia.

Basi, hivyo walipita, nikamsikia Yule mwanamke kama anamsihi, nayeye anajibu, Hapana! Hapana! Hapana.

Nikaona kuwa anataka kuwaita askari wa zamu, lakini Malkia Sorais aliacha kusema, akamkazia macho yake makubwa, nikaona ya kuwa Bougwan ameshindwa kujizuia kwa uzuri wake.

Kisha aliunyosha mkono wake na Boungwan aliubusu, nikajifanya tayari kumkamata, mara! Akatoweka.’

Nikasema, alitoweka?’’
Akajibu, ‘’Ndiyo, na Boungwan alisimama akimtizama ukutani kama kwamba ameshikwa na jinamizi la usingizi. Kisha, naye pia akaenda, na mimi nikaja hapa.’’

Nikamuuliza, ‘’Una hakika Umslopogaas ya kuwa hukua unaota ndoto ya mambo hayo?’’
Akaufumbua mkono wake, akanionyesha kipande cha chuma cha bapa la kisu, kadiri ya inchi tatu, akasema, ‘’Makumazahn, kama niliota ndoto, basi, tazama kitu nilichopewa kwenye hiyo ndoto.

Kisu kilivunjikia katika deraya za Bougwan, na nilipopita nilikiokota hiki katika chumba cha kulala cha Malkia Nyleptha.’’
Barikiwa sana mkuu.
 
SURA YA KUMI NA NANE


Basi nilimwambia Umslopogaas aningojee, nikavaa nguo zangu kwa haraka nikamchukua mpaka chumbani mwa Sir Henry, akaisimulia tena ile hadithi yake.


Uso wa Sir Henry uligeuka rangi alipoisikia, akasema, ‘’Ole wangu na mimi nilikuwa nimelala usingizi na huku Nyleptha alitaka kuuawa tena kwa ajili yangu pia.


Lo, angalia jinsi Yule Sorais alivyo mwovu. Ingekuwa haki yake Umslopogaas angalimuua kwa shoka lake.’’

Umslopogaas akasema, ‘’Ndiyo usiwe na shaka; ningalimuua kabla hajamuua dada yake. Nilikuwa tayari nikingojea.’’

Basi, alipokwisha kuisimulia hadithi yake, Umslopogaas alikwenda kula chakula chake cha asubuhi kama kwamba hakuna jambo lililotokea, na Sir Henry na mimi tukakaa tunazungumza.

Kwanza aliona uchungu kwa sababu ya Bwana Good, akasema kuwa hawezi kutumainiwa tena, kwa kuwa amemwacha Sorais atoke kwa njia ya siri badala ya kumkamata na kumfunga kama ilivyokuwa wajibu wake.

Nikasema, ‘’Usisahau ya kuwa wewe ulikutana na mwanamke Yule, ukaona vigumu kujizuia usishindwe na uzuri wake.’’

Lakini ingawa nilisema haya, nilifikiri moyoni ya kuwa ingawa anampenda sana Sorais, Bwana Good amefanya jambo la aibu kumwacha aende zake. Maana alinuia kumuua dada yake, naye amemwacha huru.’

Halafu Bwana Good akaja na uso wake ulionyesha namna alivyokuwa akiona mashaka, na mara Umslopogaas alipomwona akasema,

‘’Ah Bougwan, salamu Mkuu! Kweli umechoka kwa kuwinda sana’’

Kisha, asingoje kujibiwa, akasema,

‘’Sikiliza Bougwan, nitakusimulia hadithi ni habari za mwanamke na kwa hiyo utazisikiliza sivyo.’’

‘’Palikuwa na ndugu wawili wanaume! Kaka mtu na mdogo wake, ikatokea mwanamke moja anampenda sana Yule ndugu mdogo, na Yule ndugu mkubwa naye pia anampenda sana Yule mwanamke.

Lakini Yule ndugu mdogo alikuwa na mke mwingine mpenzi wake, wala hakumpenda Yule mwanamke, akamfanyia dhihaka. Basi, Yule mwanamke kwa kuwa alikuwa mwerevu na mwenye moyo wa kutaka kisasi akafikiri moyoni, akamwambia Yule ndugu mkubwa, ‘Nakupenda, na ukifanya vita juu ya ndugu yako nitakusaidia.’

Na yule ndugu mkubwa alijua kuwa ni uongo, lakini kwa kuwa alimpenda sana Yule mwanamke aliyasikiliza maneno yake akafanya vita na ndugu yake.
Na baada ya kuuawa watu wengi, ndugu yake alimpelekea ujumbe kumuuliza’ mbona wataka kuniua?


Toka utoto wangu nimekupenda. Nimekudhuru namna gani? Ni ubaya gani niliokutendea kufikia kutaka kuniua? Ulipokuwa katika dhiki sikukuona hata nikakusaidia? Nasi hatukuenda pamoja kufanya vita! Tukagawanya mateka, mwanamke kwa mwanamke, ng’ombe kwa ng’ombe!

Basi, sasa mbona wataka kuniua ndugu yangu mpenzi?.

‘’Basi moyo wa Yule ndugu mkubwa uliingia simanzi, akajiutia matendo yake maovu, akamwepuka Yule mwanamke, akavikomesha vile vita, akakaa katika nyumba moja pamoja na ndugu yake.

Na baada ya muda kupita, Yule mwanamke akamjia tena Yule akasema, ‘’Na tuyasahau mambo yaliyopita, nitakuwa mke wako.’’ Na katika moyo wake alijua kuwa anasema uwongo, lakini kwa sababu alimpenda sana akamwoa.

‘’Na usiku ule ule waliooana, Yule mwanaume alipokuwa amelala usingizi, Yule mwanamke aliondoka kitandani akatwaa shoka lile analotumia mumewe, akanyemelea toka katika nyumba walimolala, akaingia chumbani mwa yule ndugu yake, akamuua pale pale alipokuwa usingizini.

Kisha akanyemelea akarudi chumbani tena kama simba aliyekwisha kula shibe yake, akaweka kitanzi cha kipini cha shoka lile lenye damu katika kiwiko cha mkono wa mume wake aliyekuwa bado amelala usingizi, akatoweka akaenda zake.’’

‘’Kulipo pambazuka, watu wa jumbani humo wakapiga ukelele ‘Lousta ameuawa usiku.’ Wakaja hata chumbani mwa Yule mwanaume kumpasha habari, wakamkuta bado amelala, na karibu naye lipo lile shoka lenye damu limelala.

Ndipo walipovikumbuka vile vita, wakasema, ‘’Tazama! Hakika amemuua ndugu yake,’ wakataka kumuua, lakini alikuwa mwepesi kuwa toroka basi akakimbia, na alipokuwa akikimbia alimuona Yule mwanamke akampitia na shoka lake na akamuua.’’

‘’Lakini mauti ya Yule mwanamke haikuweza kuyafuta maovu yake aliyoyafanya, na uzito wa ile dhambi yake ulimkalia Yule mwanaume. Kwa hivi ametupwa na watu wake, na jina lake ni twezo katikati ya watu wake maana mzigo wa dhambi aliyoitenda Yule mwanamke umetwikwa juu yake peke yake.

Basi, sasa Yule aliyekuwa mkuu hutembea tembea huko na huko mbali na kwao, hana nyumba wala mke, na kwa hiyo atakufa kama mnyama aliyepigwa , na jina lake limelaaniwa toka vizazi hata vizazi, kwa kuwa watu husema alimuua ndugu yake, Lousta, kwa hila wakati wa usiku.’’

Basi, Yule mzee Mzulu akanyamaza kidogo, nikaona jinsi hadithi yake inavyomhuzunisha. Halafu alikiinua kichwa chake tena, akaendelea.

‘’Mimi ndiye huyo mtu, Bougwan. Ndiyo Mimi ni mtu Yule, na wewe unisikilize! Kama mimi nilivyo, hata na wewe ndivyo utakavyokuwa chombo,kitu cha kuchezea, ng’ombe achukuaye mzigo wa maovu ya mtu mwingine.


Sikiliza. Wewe uliponyemelea kumfuata, ‘Bibi wa Usiku’ mimi nilikuwa nikikufuatia wewe. Alipokupiga kisu katika chumba cha kulala cha Malkia Nyleptha, mimi nilikuwamo pia, ulipomwacha aende zake kama nyoka katika miamba, mimi nilikuona , nikajua ya kuwa amekuloga, naya kuwa mtu mwaminifu ametoka katika uaminifu wake, na yeye ambaye alipenda njia iliyonyooka, amechagua njia iliyopotoka.


Nisamehe baba yangu, kama maneno yangu ni makali, lakini yanatoka katika moyo uliojaa.

Usionane naye tena, na hivyo utashuka katika kaburi lako kwa heshima ama sivyo, labda wewe utakuwa kama mimi nilivyo, tena kwa haki kuliko mimi! Tena wengi wameangushwa kwa ajili ya uzuri wa mwanamke unaochakaa kama vazi lililokwisha valiwa,ujiepushe usizidishe hesabu yao. Nimesema!’’

Basi, wakati Umslopogaas alipokuwa akisema maneno hayo Bwana Good alisimama kimya kabisa, lakini hadithi ilipoanza kufanana na hali yake ilivyo, aligeuka rangi, na alipojua ya kuwa habari zile. Za yeye na Sorais zimebainika, alifadhaika sana.
 
Back
Top Bottom