blackstarline
JF-Expert Member
- Sep 19, 2016
- 3,517
- 8,872
- Thread starter
- #321
Basi mwishowe niliacha kutakafari juu ya mambo hayo nikayaacha yale yatakayotokea kesho katika mikono ya Mungu Mwenyenzi.
Basi mwishowe jua jekundu lilichomoza, na majeshi yaliamka kwa kishindo kikubwa na ngurumo yakajikusanya kufanya vita. Matengenezo yote yalikuwa mazuri ya kutisha, na Umslopogaas alikuwa ameliinamia shoka lake na kuyatazama na huku anachekelea kwa furaha.
Akasema, ‘’Makumazahn, sijaona namna yake, hata mara moja. Vita vya watu wangu vilikuwa kama michezo ya watoto vikilinganishwa na vita hivi namna vitakavyo kuwa. Je, waonaje watapigana hata mwisho?’’
Nikajibu kwa huzuni, ‘’Ndiyo, mpaka kufa. Uwe radhi Inkosikazi atakula shibe yake leo. Basi, wakati ulipita bila kuwapo dalili ya shambulio.
Kundi dogo la wapanda farasi lilipita mbele yetu polepole, na kwa dhahiri lilikuwa likichungulia namna tulivyopangwa na hesabu ya askari zetu, lakini hatukulishambulia, maana tulikuwa tumekwisha kusudia kukaa na kujitetea tu wala si kupoteza hata mtu mmoja.
Askari wetu walikula chakula chao cha asubuhi, wakasimama na silaha zao tayari, na saa zikapita. Saa sita watu walipokuwa wakila chakula cha mchana, maana tulifikiri wataweza kupigana vizuri zaidi kama hawana njaa, tulisikia kelele, ‘’Sorais! Sorais!’’ ilikuwa kama ngurumo ikitokea upande wa kuume wa adui zetu, nikatwaa darubini nikatazama, nikaweza kumwona Sorais mwenyewe anapita polepole mbele ya majeshi yake amezungukwa na wakuu waliokuwa wamevaa vizuri sana.
Na alipokuwa akipita, askari walimpigia ukelele wa shangwe kama ngurumo ya magari elfu kumi, au kama mvumo wa mawimbi ya bahari upepo ugeukapo na kuchukua sauti yake ghafla masikioni mwa mtu anayesikiliza, mpaka ardhi ilitikisika na hewa ilijaa wingi wa sauti.
Basi, tulisikia kuwa hii ndiyo alama ya kuanzisha vita, tukakaa kimya tukijiweka tayari. Wala hatukuwekwa sana. Mara, kama ndimi za moto zitokazo katika mdomo wa mzinga, vikosi viwili vya wapanda farasi vilitoka mbio, wakateremka mwinuko kutujia, kwanza pole pole kidogo, na kuongeza mbio walipokuwa wakija.
Lakini kabla hawajaufikia mto ule mdogo uliokuwa bondeni, Sir Henry aliipeleka amri kupeleka askari elfu tano wapanda farasi wenye panga kuwapiga, maana aliogopa kuwa wakiachiwa kuwashambulia askari wa miguu wa katikati kwa nguvu zao zote, hawataweza kustahimili. Basi nilipeleka askari wale, nikabaki nyuma pamoja na watu wangu waliosalia.
Basi, askari wale wapanda farasi elfu tano walikwenda wamepangwa mfano wa kabari na kuongozwa vizuri.
Na mkuu wao. Kwanza walikwenda taratibu muda wa yadi mia tatu, wakielekea sawasawa mbele, ndipo Yule mkuu wao alipowapeleka ghafla upande wakazidi kupiga mbio, nikaona kabari ile inapinda, na kabla kikosi cha adui hakijaweza kwenda upande au kujizuia, ilikipiga katikati kwa kishindo kikubwa mno.
Kabari ile ya wapanda farasi iliingia mpaka katika moyo wa kikosi, na wapanda farasi adui, walitupwa upande huu na huu kama udongo unavyotupwa jembe linapovutwa na ng’ombe likipita katika shamba, au kama maji ya bahari yanavyotupwa huko na huko kwa omo la merikebu inapokwenda mbio.
Ndani ndani zaidi, na kikosi cha adui kilipinda kama nyoka anavyojipinda aumizwapo ili ailinde sehemu yake ya katikati ndani zaidi. Kumbe watu wetu wemepita na kutokeza upande wa pili, waka geuka wakashambulia tena adui waliotawanyika kama povu mbele ya upepo wenye nguvu, na huku askari zetu wote wanatazama na kupiga kelele za shangwe.
Hata mwishowe, kikosi kile cha adui kilivunjika, kikageuka kikarudi mbio katikati ya farasi wengi wasio na askari, na miali ya panga zinazopungwa huko na huko, na kelele za shangwe za askari waliokuwa wakiwafukuza. Kikarudi mbio kutafuta salama nyuma ya askari wenzao.
Basi, jeshi lililokuwa likija mbele lilifunguka kukipa nafasi ya kuingia, na askari zangu walirud, wamepata hasara ya watu kadiri ya mia tano nami nilifikiri si wengi kwa kadiri ya ukali wa vita vilivyokuwa.
Basi, sasa vikosi vya upande wa kushoto wa adui vilivyokuwa karibu vyote ni vya watu wa Nasta, vilikuwa vikitujia, na huku tukasikia kelele ‘’Nasta’’ na ‘’Sorais’’ tukaona bendera zinapepea, na panga zinapungwa, vikatujia kama makundi ya siafu.
Nilipewa amri tena nijaribu kuwapinga kwa kupeleka vikosi vya wapanda farasi, nikafanya kadiri nilivyoweza kupeleka vikosi vya watu elfu moja.
Vikosi hivyo viliwatia adui kama kisu kinachong’aa na kuingia katika moyo wao, lakini tulipata hasara ya watu wengi, maana sasa askari wa adui hawakushikamana kama katika shambulio la kwanza, ila walifunguka wakaacha nafasi ili wapanda farasi wapite katikati, kisha walijitupa chini wakawakata miguu farasi walipokuwa wakipita.
Basi kadiri tulivyoweza kufanya, adui walizidi kutukaribia, mpaka wakakishambulia kwa nguvu kikosi cha Bwana Good. Tena, wakati huo huo nikasikia kishindo kilichonifaamisha kuwa adui wameshambulia katikati na kwa upande wa kushoto pia.
Nilijiinua katika vikuku vya miguu juu ya farasi wangu nikatazama upande wa kushoto, nikaona mng’aro wa panga zinazopungwa na wa ncha za mikuki inayosukumwa upeo wa macho yangu.
Basi, hapo majeshi yalitikisika huku na huku yakishindana, pengine yakirudi nyuma, pengine yakisukumwa mbele, katika fujo ya kushambulia na kujitetea. Basi, vivyo hivyo vita viliendelea kwa muda wa saa nne bila kituo, na mwisho wa wakati huo tulikuwa haujaendelea mbele wala kurudi nyuma.
Mwishowe mashambulio yalififia na jeshi la Sorais lilirudi, nikaanza kufikiri askari zao wamechoka. Lakini sivyo, sasa Sorais aliwapanga wapanda farasi vikosi vidogo vidogo wakatushambulia kwa nguvu kila mahali, ndipo wakati huo, huo alipopeleka mbele tena jeshi kubwa.
Sorais mwenyewe alikuwa akiamrisha. Basi, wakaja mbele kama mawimbi makubwa yenye nguvu nyingi mno, wakapambana na askari wa katikati ya kidari cha jeshi letu. Basi, askari wa sehemu ya katikati ya jeshi letu walipinda kama upinde, wakafunguka, na kama askari wale elfu kumi wasingalikuwa wamewekwa nyuma kuwategemeza, wangaliangamia kabisa.
Kikosi cha Bwana Good pia kilisukumwa nyuma na sehemu moja ilivunjika, na nusu ya askari wakapotea. Lakini shambulio lilikuwa lenye nguvu mno na nguvu zake hazikuweza kuendelea hivyo. Mara ikawa kama vita vinageuka, na kwa muda mfupi ilikuwa kama pande zote mbili zimesimama tu.
Ndipo vita vilipoanza kuiendea kambi ya Sorais. Tena, wakati huo huo kikosi cha Nasta kikarudi nyuma, sijui kama askari zake walikata tamaa kwa ajili ya hasara waliyoipata, au kama ni hila waliyofanya.
Lakini hapo, kikosi cha Bwana Good kilipaacha mahali pake kikashambulia na huku kinapiga kelele.
Na mara ilea dui waligeuka wakashambulia tena kwa nguvu. Basi, adui walikizunguka kile kikosi kikaangamia kabisa, nikaona kuwa Bwana Good amepanda farasi mkubwa yu katika hatari ya kuuwa.
Baada ya dakika chache kikosi kizima kilitawanyika nami sikuweza kumwona Bwana Good katika mauaji ya kutisha yaliyofuata.
Halafu nikaona farasi mweupe anatoka mbio katika fujo, akanipita mbio hana mtu mgongoni, nikamtambua ni farasi wa Bwana Good. Basi, hapo sikusita zaidi, wala sikungoja kupewa amri, ila niliwaamrisha watu wangu kadiri ya elfu nne au tano, tukawashambulia wale watu wa Nasta wenye panga.
Walituona tunakuja, tena, walionywa kwa vishindo vya miguu ya farasi zetu, wakageuka wakatungojea. Wala hawakukubali kurudi nyuma hata kidogo, tukajaribu kuwakanyaga, tukawapigapiga, tukawatenga lakini walionekana kama wainukao tena, wakawashambulia farasi wetu kwa panga zao kali, wakaikata miguu yao, kisha wakawashambulia askari walipoanguka chini wakawakata vipande vipande.
Farasi wangu akauawa, lakini kwa bahati nilikuwa na mwingine aliyewekwa pamoja na askari nyuma, ikawa sina budi kufanya niwezavyo. Baadaye kidogo nilijiona katikati ya askari wa Bwana Good waliosalia ambao walikuwa wamemzunguka na sasa wanapigana kuyaokoa maisha yao.
Ndipo nilipojikwaa nikatazama chini nikaona rodi ya Bwana Good, alikuwa ameangushwa kigotigoti, na mtu mkubwa sana alikuwa amesimama anapunga upanga mkubwa tayari kumpiga. Sijui namna nilivyoweza, lakini niliwahi kumuua Yule mtu kwa sime ya Kijivuni niliyokuwa nayo.
Lakini nilipokuwa nikifanya hivyo alinipiga dharuba moja upande wa kushoto wa kifua, na ingawa nilikuwa nimevaa deraya chini ya nguo zangu, lakini nilitambua ameniumiza vibaya sana.
Kwa dakika moja niliangukia mikono na magoti katikati ya maiti na watu waliokuwa wakifa, na moyo wangu ulielea nikataka kuzirai.
Nilipokuja juu tena, niliona ya kuwa askari wa Nasta, au wale waliosalia, wanarudi nyuma ya mto, na Bwana Good amesimama karibu na huku anachechemea, akasema, ‘’Lo! Tulikuwa karibu kufa, lakini asante tumepona.’’
Nikakubali, lakini nilijua ya kuwa nimeumia vibaya. Basi, hapo tuliona vikosi vyetu vya wapanda farasi wenye panga vya upande wa kuume na vya kushoto vilivyo wekwa nyuma, vikitoka mahali pao kama mishale na kuwangukia askari wa Sorais waliokuwa sasa wametawanyika, na shambulio hilo ndilo lililovimaliza vita.
Baada ya kupita dakika mbili tatu, adui walikuwa wakirudi nyuma kuuvuka ule mto mdogo, wakajipanga huko tena. Kisha, kukawa kimya kidogo, nikawahi kumpata farasi wangu wa pili. Aliyekuwa nyuma, nikapewa amri na Sir Henry kushambuliwa mbele. Basi hapo tulifanya kelele moja kwa moja, tukazipepea bendera zetu, tukapunga panga na mikuki, tukawafutia adui tukawafukuza.
Tulipokuwa tukipita juu ya chungu za maiti na watu waliokuwa wakikata roho nilimwona mtu mmoja ananijia mbio sana amepanda farasi, akaniita kwa sauti ya hofu! Nikasimama, nikamuuliza ana habari gani.
Akaniambia kuwa ana habari ya haraka sana! akaniambia, ya kuwa Malkia Nyleptha atauawa kwa hila katika jumba la Milosis mara kutakapopambazuka kesho. Aliniambia kuwa askari wa zamu watapaacha mahali pao, na makuhani watamuua Malkia. Nikashtuka kwa ushangao, nikamuuliza, ‘’ Unasemaje?’’
Akasema, ‘’Ni kweli, Yule shetani Nasta aliondoka usiku akafanya shauri na Agon. Askari wa zamu wataufungua mlango, na Nasta na makuhani wa Agon wataingia na kumuua Malkia.’’
Basi, nilimchukua Yule mtu nikaenda naye mbio mbio mpaka nilipomwona Sir Henry katikati ya wakuu wengine. Mara nilipomwona, askari walikuwa wanaanza kuendelea mbele tena.
Kichwa chake kilifungwa kwa kitambaa chenye damu, lakini niliona ya kuwa macho yake na kama desturi yake, na karibu naye Umslopogaas alikuwa amesimama amelishika shoka lake, jekundu kwa damu, lakini yeye alionekana mzima kabisa.
Sir Henry akauliza, ‘’Kuna nini Quatermain?’’
Nikajibu, ‘’Wanafanya hila kumuua Malkia mara kutakapo pambazuka kesho. Mtu huyu aliyetoroka toka upande wa Sorais alisikia habari za hila wanazotaka kuzifanya.’’
Rangi ya uso wa Sir Henry ilibadilika, akawa mweupe sana, akasema, ‘’Kutakapo pambazuka, na sasa jua linashuka kunapambazuka saa kumi, na toka hapa mpaka huko ni mwendo wa maili mia moja. Tutafanya nini?’’
Basi, nilifikiri shauri, nikamuuliza, ‘’Je farasi wako amechoka?’’ akajibu, ‘’La, ndiyo kwanza nimpande, tena amekwisha kula.’’
Nikasema, ‘’Na farasi wangu pia hajafanya kazi leo. Basi, shuka chini umwache Umslopogaas ampande, tutafika Milosis kabla hakujapambazuka, na kama hatuwahi kufika, basi tumeshindwa.
Sir Henry akataka kwenda pamoja nasi, Nikamwambia! Hapana, hapana, wewe huwezi kuacha vita sasa. Watu wasipokuona watakufa moyo na vita vitapotea. Askari wangefikiri umekimbia. Basi, upesi, upesi.’’
Basi mara ile alishuka, na Umslopogaas alipanda mahali pake. Nikasema, ‘’Kwa heri. Peleka wapanda farasi elfu moja watufuatie baada ya saa moja ikiwezekana tena peleka mkuu apashike mahali pangu umweleze sababu niliyotoka.’’
Akasema, ‘’Utafanya uwezavyo kumwokoa Nyleptha, Quatermain?’’
Nikajibu, ‘’Ndiyo, kadiri ninavyoweza kufanya. Sasa nenda, unaachwa nyuma.’’
Basi, alitutazama mara moja tu, kisha akageuka akawafuata watu wake akaenda upesi kujiunga na askari zake.
Na Umslopogaas na mimi tukatoka mahali pale kama mishale inavyotoka katika upinde, na baada ya kupita dakika chache, tulikuwa tumetoka kabisa mahali pale pa mauaji na harufu ya damu, na sauti za vita zikawa kama mvumo wa bahari ya mbali katika masikio yetu.
Basi mwishowe jua jekundu lilichomoza, na majeshi yaliamka kwa kishindo kikubwa na ngurumo yakajikusanya kufanya vita. Matengenezo yote yalikuwa mazuri ya kutisha, na Umslopogaas alikuwa ameliinamia shoka lake na kuyatazama na huku anachekelea kwa furaha.
Akasema, ‘’Makumazahn, sijaona namna yake, hata mara moja. Vita vya watu wangu vilikuwa kama michezo ya watoto vikilinganishwa na vita hivi namna vitakavyo kuwa. Je, waonaje watapigana hata mwisho?’’
Nikajibu kwa huzuni, ‘’Ndiyo, mpaka kufa. Uwe radhi Inkosikazi atakula shibe yake leo. Basi, wakati ulipita bila kuwapo dalili ya shambulio.
Kundi dogo la wapanda farasi lilipita mbele yetu polepole, na kwa dhahiri lilikuwa likichungulia namna tulivyopangwa na hesabu ya askari zetu, lakini hatukulishambulia, maana tulikuwa tumekwisha kusudia kukaa na kujitetea tu wala si kupoteza hata mtu mmoja.
Askari wetu walikula chakula chao cha asubuhi, wakasimama na silaha zao tayari, na saa zikapita. Saa sita watu walipokuwa wakila chakula cha mchana, maana tulifikiri wataweza kupigana vizuri zaidi kama hawana njaa, tulisikia kelele, ‘’Sorais! Sorais!’’ ilikuwa kama ngurumo ikitokea upande wa kuume wa adui zetu, nikatwaa darubini nikatazama, nikaweza kumwona Sorais mwenyewe anapita polepole mbele ya majeshi yake amezungukwa na wakuu waliokuwa wamevaa vizuri sana.
Na alipokuwa akipita, askari walimpigia ukelele wa shangwe kama ngurumo ya magari elfu kumi, au kama mvumo wa mawimbi ya bahari upepo ugeukapo na kuchukua sauti yake ghafla masikioni mwa mtu anayesikiliza, mpaka ardhi ilitikisika na hewa ilijaa wingi wa sauti.
Basi, tulisikia kuwa hii ndiyo alama ya kuanzisha vita, tukakaa kimya tukijiweka tayari. Wala hatukuwekwa sana. Mara, kama ndimi za moto zitokazo katika mdomo wa mzinga, vikosi viwili vya wapanda farasi vilitoka mbio, wakateremka mwinuko kutujia, kwanza pole pole kidogo, na kuongeza mbio walipokuwa wakija.
Lakini kabla hawajaufikia mto ule mdogo uliokuwa bondeni, Sir Henry aliipeleka amri kupeleka askari elfu tano wapanda farasi wenye panga kuwapiga, maana aliogopa kuwa wakiachiwa kuwashambulia askari wa miguu wa katikati kwa nguvu zao zote, hawataweza kustahimili. Basi nilipeleka askari wale, nikabaki nyuma pamoja na watu wangu waliosalia.
Basi, askari wale wapanda farasi elfu tano walikwenda wamepangwa mfano wa kabari na kuongozwa vizuri.
Na mkuu wao. Kwanza walikwenda taratibu muda wa yadi mia tatu, wakielekea sawasawa mbele, ndipo Yule mkuu wao alipowapeleka ghafla upande wakazidi kupiga mbio, nikaona kabari ile inapinda, na kabla kikosi cha adui hakijaweza kwenda upande au kujizuia, ilikipiga katikati kwa kishindo kikubwa mno.
Kabari ile ya wapanda farasi iliingia mpaka katika moyo wa kikosi, na wapanda farasi adui, walitupwa upande huu na huu kama udongo unavyotupwa jembe linapovutwa na ng’ombe likipita katika shamba, au kama maji ya bahari yanavyotupwa huko na huko kwa omo la merikebu inapokwenda mbio.
Ndani ndani zaidi, na kikosi cha adui kilipinda kama nyoka anavyojipinda aumizwapo ili ailinde sehemu yake ya katikati ndani zaidi. Kumbe watu wetu wemepita na kutokeza upande wa pili, waka geuka wakashambulia tena adui waliotawanyika kama povu mbele ya upepo wenye nguvu, na huku askari zetu wote wanatazama na kupiga kelele za shangwe.
Hata mwishowe, kikosi kile cha adui kilivunjika, kikageuka kikarudi mbio katikati ya farasi wengi wasio na askari, na miali ya panga zinazopungwa huko na huko, na kelele za shangwe za askari waliokuwa wakiwafukuza. Kikarudi mbio kutafuta salama nyuma ya askari wenzao.
Basi, jeshi lililokuwa likija mbele lilifunguka kukipa nafasi ya kuingia, na askari zangu walirud, wamepata hasara ya watu kadiri ya mia tano nami nilifikiri si wengi kwa kadiri ya ukali wa vita vilivyokuwa.
Basi, sasa vikosi vya upande wa kushoto wa adui vilivyokuwa karibu vyote ni vya watu wa Nasta, vilikuwa vikitujia, na huku tukasikia kelele ‘’Nasta’’ na ‘’Sorais’’ tukaona bendera zinapepea, na panga zinapungwa, vikatujia kama makundi ya siafu.
Nilipewa amri tena nijaribu kuwapinga kwa kupeleka vikosi vya wapanda farasi, nikafanya kadiri nilivyoweza kupeleka vikosi vya watu elfu moja.
Vikosi hivyo viliwatia adui kama kisu kinachong’aa na kuingia katika moyo wao, lakini tulipata hasara ya watu wengi, maana sasa askari wa adui hawakushikamana kama katika shambulio la kwanza, ila walifunguka wakaacha nafasi ili wapanda farasi wapite katikati, kisha walijitupa chini wakawakata miguu farasi walipokuwa wakipita.
Basi kadiri tulivyoweza kufanya, adui walizidi kutukaribia, mpaka wakakishambulia kwa nguvu kikosi cha Bwana Good. Tena, wakati huo huo nikasikia kishindo kilichonifaamisha kuwa adui wameshambulia katikati na kwa upande wa kushoto pia.
Nilijiinua katika vikuku vya miguu juu ya farasi wangu nikatazama upande wa kushoto, nikaona mng’aro wa panga zinazopungwa na wa ncha za mikuki inayosukumwa upeo wa macho yangu.
Basi, hapo majeshi yalitikisika huku na huku yakishindana, pengine yakirudi nyuma, pengine yakisukumwa mbele, katika fujo ya kushambulia na kujitetea. Basi, vivyo hivyo vita viliendelea kwa muda wa saa nne bila kituo, na mwisho wa wakati huo tulikuwa haujaendelea mbele wala kurudi nyuma.
Mwishowe mashambulio yalififia na jeshi la Sorais lilirudi, nikaanza kufikiri askari zao wamechoka. Lakini sivyo, sasa Sorais aliwapanga wapanda farasi vikosi vidogo vidogo wakatushambulia kwa nguvu kila mahali, ndipo wakati huo, huo alipopeleka mbele tena jeshi kubwa.
Sorais mwenyewe alikuwa akiamrisha. Basi, wakaja mbele kama mawimbi makubwa yenye nguvu nyingi mno, wakapambana na askari wa katikati ya kidari cha jeshi letu. Basi, askari wa sehemu ya katikati ya jeshi letu walipinda kama upinde, wakafunguka, na kama askari wale elfu kumi wasingalikuwa wamewekwa nyuma kuwategemeza, wangaliangamia kabisa.
Kikosi cha Bwana Good pia kilisukumwa nyuma na sehemu moja ilivunjika, na nusu ya askari wakapotea. Lakini shambulio lilikuwa lenye nguvu mno na nguvu zake hazikuweza kuendelea hivyo. Mara ikawa kama vita vinageuka, na kwa muda mfupi ilikuwa kama pande zote mbili zimesimama tu.
Ndipo vita vilipoanza kuiendea kambi ya Sorais. Tena, wakati huo huo kikosi cha Nasta kikarudi nyuma, sijui kama askari zake walikata tamaa kwa ajili ya hasara waliyoipata, au kama ni hila waliyofanya.
Lakini hapo, kikosi cha Bwana Good kilipaacha mahali pake kikashambulia na huku kinapiga kelele.
Na mara ilea dui waligeuka wakashambulia tena kwa nguvu. Basi, adui walikizunguka kile kikosi kikaangamia kabisa, nikaona kuwa Bwana Good amepanda farasi mkubwa yu katika hatari ya kuuwa.
Baada ya dakika chache kikosi kizima kilitawanyika nami sikuweza kumwona Bwana Good katika mauaji ya kutisha yaliyofuata.
Halafu nikaona farasi mweupe anatoka mbio katika fujo, akanipita mbio hana mtu mgongoni, nikamtambua ni farasi wa Bwana Good. Basi, hapo sikusita zaidi, wala sikungoja kupewa amri, ila niliwaamrisha watu wangu kadiri ya elfu nne au tano, tukawashambulia wale watu wa Nasta wenye panga.
Walituona tunakuja, tena, walionywa kwa vishindo vya miguu ya farasi zetu, wakageuka wakatungojea. Wala hawakukubali kurudi nyuma hata kidogo, tukajaribu kuwakanyaga, tukawapigapiga, tukawatenga lakini walionekana kama wainukao tena, wakawashambulia farasi wetu kwa panga zao kali, wakaikata miguu yao, kisha wakawashambulia askari walipoanguka chini wakawakata vipande vipande.
Farasi wangu akauawa, lakini kwa bahati nilikuwa na mwingine aliyewekwa pamoja na askari nyuma, ikawa sina budi kufanya niwezavyo. Baadaye kidogo nilijiona katikati ya askari wa Bwana Good waliosalia ambao walikuwa wamemzunguka na sasa wanapigana kuyaokoa maisha yao.
Ndipo nilipojikwaa nikatazama chini nikaona rodi ya Bwana Good, alikuwa ameangushwa kigotigoti, na mtu mkubwa sana alikuwa amesimama anapunga upanga mkubwa tayari kumpiga. Sijui namna nilivyoweza, lakini niliwahi kumuua Yule mtu kwa sime ya Kijivuni niliyokuwa nayo.
Lakini nilipokuwa nikifanya hivyo alinipiga dharuba moja upande wa kushoto wa kifua, na ingawa nilikuwa nimevaa deraya chini ya nguo zangu, lakini nilitambua ameniumiza vibaya sana.
Kwa dakika moja niliangukia mikono na magoti katikati ya maiti na watu waliokuwa wakifa, na moyo wangu ulielea nikataka kuzirai.
Nilipokuja juu tena, niliona ya kuwa askari wa Nasta, au wale waliosalia, wanarudi nyuma ya mto, na Bwana Good amesimama karibu na huku anachechemea, akasema, ‘’Lo! Tulikuwa karibu kufa, lakini asante tumepona.’’
Nikakubali, lakini nilijua ya kuwa nimeumia vibaya. Basi, hapo tuliona vikosi vyetu vya wapanda farasi wenye panga vya upande wa kuume na vya kushoto vilivyo wekwa nyuma, vikitoka mahali pao kama mishale na kuwangukia askari wa Sorais waliokuwa sasa wametawanyika, na shambulio hilo ndilo lililovimaliza vita.
Baada ya kupita dakika mbili tatu, adui walikuwa wakirudi nyuma kuuvuka ule mto mdogo, wakajipanga huko tena. Kisha, kukawa kimya kidogo, nikawahi kumpata farasi wangu wa pili. Aliyekuwa nyuma, nikapewa amri na Sir Henry kushambuliwa mbele. Basi hapo tulifanya kelele moja kwa moja, tukazipepea bendera zetu, tukapunga panga na mikuki, tukawafutia adui tukawafukuza.
Tulipokuwa tukipita juu ya chungu za maiti na watu waliokuwa wakikata roho nilimwona mtu mmoja ananijia mbio sana amepanda farasi, akaniita kwa sauti ya hofu! Nikasimama, nikamuuliza ana habari gani.
Akaniambia kuwa ana habari ya haraka sana! akaniambia, ya kuwa Malkia Nyleptha atauawa kwa hila katika jumba la Milosis mara kutakapopambazuka kesho. Aliniambia kuwa askari wa zamu watapaacha mahali pao, na makuhani watamuua Malkia. Nikashtuka kwa ushangao, nikamuuliza, ‘’ Unasemaje?’’
Akasema, ‘’Ni kweli, Yule shetani Nasta aliondoka usiku akafanya shauri na Agon. Askari wa zamu wataufungua mlango, na Nasta na makuhani wa Agon wataingia na kumuua Malkia.’’
Basi, nilimchukua Yule mtu nikaenda naye mbio mbio mpaka nilipomwona Sir Henry katikati ya wakuu wengine. Mara nilipomwona, askari walikuwa wanaanza kuendelea mbele tena.
Kichwa chake kilifungwa kwa kitambaa chenye damu, lakini niliona ya kuwa macho yake na kama desturi yake, na karibu naye Umslopogaas alikuwa amesimama amelishika shoka lake, jekundu kwa damu, lakini yeye alionekana mzima kabisa.
Sir Henry akauliza, ‘’Kuna nini Quatermain?’’
Nikajibu, ‘’Wanafanya hila kumuua Malkia mara kutakapo pambazuka kesho. Mtu huyu aliyetoroka toka upande wa Sorais alisikia habari za hila wanazotaka kuzifanya.’’
Rangi ya uso wa Sir Henry ilibadilika, akawa mweupe sana, akasema, ‘’Kutakapo pambazuka, na sasa jua linashuka kunapambazuka saa kumi, na toka hapa mpaka huko ni mwendo wa maili mia moja. Tutafanya nini?’’
Basi, nilifikiri shauri, nikamuuliza, ‘’Je farasi wako amechoka?’’ akajibu, ‘’La, ndiyo kwanza nimpande, tena amekwisha kula.’’
Nikasema, ‘’Na farasi wangu pia hajafanya kazi leo. Basi, shuka chini umwache Umslopogaas ampande, tutafika Milosis kabla hakujapambazuka, na kama hatuwahi kufika, basi tumeshindwa.
Sir Henry akataka kwenda pamoja nasi, Nikamwambia! Hapana, hapana, wewe huwezi kuacha vita sasa. Watu wasipokuona watakufa moyo na vita vitapotea. Askari wangefikiri umekimbia. Basi, upesi, upesi.’’
Basi mara ile alishuka, na Umslopogaas alipanda mahali pake. Nikasema, ‘’Kwa heri. Peleka wapanda farasi elfu moja watufuatie baada ya saa moja ikiwezekana tena peleka mkuu apashike mahali pangu umweleze sababu niliyotoka.’’
Akasema, ‘’Utafanya uwezavyo kumwokoa Nyleptha, Quatermain?’’
Nikajibu, ‘’Ndiyo, kadiri ninavyoweza kufanya. Sasa nenda, unaachwa nyuma.’’
Basi, alitutazama mara moja tu, kisha akageuka akawafuata watu wake akaenda upesi kujiunga na askari zake.
Na Umslopogaas na mimi tukatoka mahali pale kama mishale inavyotoka katika upinde, na baada ya kupita dakika chache, tulikuwa tumetoka kabisa mahali pale pa mauaji na harufu ya damu, na sauti za vita zikawa kama mvumo wa bahari ya mbali katika masikio yetu.