Hadithi ya Mapenzi: Nakufahamu vizuri

Hadithi ya Mapenzi: Nakufahamu vizuri

NAKUFAHAMU VIZURI

MTUNZI: KJM-0718274130


SEHEMU YA 13


Lutfiya alitii na kuanza kusogea taratibu kuelekea mikono yangu ili anikumbatie. Nilijaa ujasiri na kujikuta nikijisikia poa sana moyoni mwangu licha ya kujua uzito wa jambo nililokaribia kulifanya. Lutfiya alishachanganyikiwa kwa nguvu ya ile dawa, nilishazima nguvu zake zote za kijini alizokuwa nazo na asingeweza kung'amua chochote. Aliendelea kusogea huku machozi yakiendelea kumwagika machoni mwake. Nilimtazama lakini sikuwa na hata chembe ya huruma juu yake. Nilijua kuwa endapo wangefanikiwa kupata mkoba wangu ule na dhamira yao mbaya ambayo hawakutaka kuiweka wazi, ni dhahiri mimi wangeniua tu hapo baadae, kwahiyo nikaamua niwajeruhi wao kwanza ili nitume salamu.

“Lutfiyaaaa achaaaaa” ni sauti kali sana iliyosikika mle chumbani na kumfanya Lutfiya awe kama mtu aliyeshituka hivi kutoka usingizini. Lutfiya alikua amebakisha hatua moja tu kugusa mikono yangu. Akaniangalia akionekana mwenye hasira sana, nami nilimkazia macho bila kuongea chochote, akatoweka. Nilibaki nimeduwaa pale chumbani nikiendelea kusimama nilipokuwa. Nilijaribu kutafakari nimekosea wapi, nikagundua kuwa kutokana na kutojihusisha na mambo haya tangu nikabidhiwe, nilisahau vitu vingi. Hatua ya kwanza kabisa ilikua ni kuilinda nyumba ili mtu wala jini asione kinachoendelea ndani, kisha ndio nifanye mambo yangu. Mimi sikufanya hatua hiyo muhimu ambayo sasa itasababisha hasira kubwa mno kwa majini baada ya kugundua ninataka kumuua binti yao. Nikiwa nimesimama pale, nikapata wazo la haraka la kujikinga mimi mwenyewe kabla hawajanirudia na kunidhuru. Nikaamua niende tena katika kile chumba kidogo chenye ule mkoba nikashughulike kidogo kujiweka sawa.

Nilipogeuka, nilikutana uso kwa uso na Mzee Said, sura yake ikionekana kuchukizwa mno.

“Umeamua kutaka kuidhuru familia yangu, lakini nakuambia tu kuwa umeanzisha vita kubwa sana ambayo hutaiweza, huu ndio mwanzo mbaya wa mahusiano yetu sisi na wewe”. Aliongea Mzee Said bila salamu, na pasi na kuongeza neno lolote wala kusubiri majibu yangu, Mzee Said alitoweka.

Wakati naelekea katika chumba kile kidogo, nilisikia kicheko nyuma yangu. Nikageuka, sikuona mtu. Kwakuwa kicheko kile kilitokea pale sebuleni, niliamua kwenda sebuleni ambako nako sikuona mtu zaidi ya kukisikia kicheko kingine kikitokea chumbani kwangu. Niliamua kwenda chumbani kwangu, sikuona mtu, nikasikia vicheko vinaongezeka na kuwa vingi kila sehemu. Hatimaye nyumba nzima, kila kona kulikua na kicheko. Nilihisi kuchanganyikiwa, niliamua kuelekea pale kwenye kile chumba kidogo. Nikapiga hatua za haraka haraka lakini wakati nimekaribia nikahisi kama miguu inaishiwa nguvu, nikajikaza na kuendelea kutembea kuelekea mbele, nikanyong'onyea zaidi na kushindwa kabisa, hatimaye nikakaa chini. Nikajaribu kujinyanyua, lakini kila mara nilipojaribu kunyanyua nilishindwa. Hatimaye mwili wote uliishiwa nguvu na kujikuta siwezi hata kukaa, nikaamua kulala chali. Kuna dua ambayo nilitakiwa kusoma ninapokutana na zahma kama hizi, lakini sikuikumbuka tena. Macho yangu nayo yalianza kuingia giza, nikawa naona kwa mbali sana..

Nilishangaa kuona nimezungukwa na kikundi cha watu wamevalia nguo nyeupe wote. Wengi wao sikuwatambua, lakini nilifanikiwa kuwaona Mzee Mbogo na Mzee Said kuwa ni miongoni mwa watu walionizunguka. Wakati nikitafakari cha kufanya, nikakumbuka kuwa bado mkononi mwangu nilikuwa na dawa niliyokusudia kumpaka Lutfiya, nilijua kutokana na nguvu ya dawa ile, bado ilikuwa inafanya kazi. Nikawatazama vizuri wale walionizunguka pale, nikajitahidi kunyoosha mkono wangu na kukamata mmoja kati ya mguu uliokuwa karibu, nikafanikiwa.

“Lahaulaaa...” nilisikia sauti kali ikiongea hilo neno huku yule niliyemkamata mguu akianguka chini kama mzoga. Nilijaribu kujinyanyua, nikajikuta nina nguvu zangu kama awali, nikasimama. Nikawatazama vizuri watu wote waliokuwepo pale, ni kama walikua wamepigwa na butwaa hivi wakimkodolea macho mwenzao aliyekuwa ameanguka. Nami nikapata fursa ya kumuangalia yule mtu, ndipo nilipogundua alikuwa babu yangu Mzee Mbogo-Para.


Itaendeleaa...




Sent using Jamii Forums mobile app
 
NAKUFAHAMU VIZURI
MTUNZI: KJM-0718274130

SEHEMU YA 14

Huo ndio ulikua mwisho wa Mzee Mbogo, alishafariki. Sikupenda kifo cha babu yangu huyu kipenzi nikisababishe mimi, lakini nani wa kulaumiwa kati yangu mimi na yeye? Tamaa zilimponza. Licha ya kuwa ni moja kati ya vifo vilivyonihuzunisha sana, lakini sikujutia hata kidogo. Sababu kuu ya kutokujuatia ni madhara ambayo yangenikuta endapo Mzee Mbogo angefanikisha mpango wake wa kidhalimu na wenzake dhidi yangu.
Wale kina Mzee Said walibaki kama waliopigwa shoti ya umeme, wameduwaa tu na hawajui cha kufanya. Nikautumia mwanya huu kumshika mmoja kati ya wale wazee, yeye alikua pembeni yangu kabisa, nilimshika bega, akaanguka chini na kupoteza maisha. Hapo ndipo wale kina Mzee Said na wenzake waliposhituka na kuamua kutoweka, wakiwaacha Mzee Mbogo na yule Mzee mwengine ambaye nilikuja kugundua kuwa ni babaake mdogo Lutfiya akiitwa Mahmoud Noor.
Baada ya kina Mzee Said kutokomea, niliingia katika kile chumba na kuchukua dawa ya kuifunga ile nyumba sasa. Nilifanikiwa kuifunga ile nyumba, na asingeweza kuingia mchawi au jini wa aina yeyote mle ndani pasi na idhini yangu. Kisha nikaingia chumbani kwangu kuumalizia usingizi wangu. Nililala mpaka asubuhi, nikaamka na kuingia bafuni kuoga, kisha nikavaa na kurudi pale sebuleni kuangalia zile maiti. Cha ajabu, sikuikuta maiti ya Mzee Mbogo pale nilipowaacha, alikuwepo Mzee Mahmoud peke yake. Nilipigwa na butwaa. Nilijiuliza sana atakua amechukuliwa na nani Mzee Mbogo? Kwanini maiti yake haipo? Kwanini imebaki ya yule jini pale? Sikupata jibu!!. Wakati nikiwa bado katika mshangao, mlango wa nyumba yangu uligongwa.
“Nanii??” Niliuliza wakati nikielekea kufungua mlango.
“Naitwa Mubarak Said Mansour”. Ilisema sauti iliyokuwa nyuma ya mlango huko nje.
Nilifungua, na kukutana na mzee mmoja wa kiarabu, amevalia kanzu na kofia ya kutunga na uzi. Miguuni alivalia kobadhi nyeusi, mkononi ameshika bakora ya chuma iliyonakshiwa vizuri.
“Karibu sana, naweza kukusaidia”. Nilimwambia yule mzee huku nikisindika mlango, sote tukiwa nje. Nilimnyooshea mkono kama ishara ya kusalimiana, lakini hakupokea mkono wangu.
“Sina maongezi marefu, mimi ni baba mzazi wa huyo maiti humo ndani, nimekuja kukuomba nimchukue mwanangu nikamzike”. Aliongea yule Mzee akiwa amenikazia macho. Sikutaka kubishana nae, nikamfungulia mlango na kumuonyesha ishara ya kumkaribisha ndani.
“Naomba unitolee hapa nje, siwezi kunasa katika mitego midogo kiasi hicho mimi ni mtu mzima kuliko marehemu baba yako”. Aliongea Mzee Mahmoud, na kunifanya nikakumbuka nilivyoifunga hii nyumba, nikaingia ndani na kumburuza yule marehemu nikamleta mpaka nje. Mzee Mahmoud alimbeba mgongoni na kitendo cha kupepesa macho, sikuwaona walishatokomea.
Sikurudi ndani, nikaelekea kwa Zahara muuza uji, akanikaribisha huku akiniwekea uji.
“Mbona kama nilikuona unaburuza kiroba? Ni mzigo gani mzito ulikua unauleta nje? Au sio wewe?”. Aliniuliza Zahara na kufanya nihamaki. Kumbe yule marehemu alionekana kama kiroba huku nje? Daah.. Sikuamini. Nilizama katika dimbwi la mawazo kutafakari mengi juu ya maisha ninayopitia sasa, maisha ya ulimwengu wa pili. Yakaja pia mawazo juu ya babu yangu Mzee Mbogo, sikupata majibu kamili.
“Vipi Adam? Uko sawa?”. Aliniuliza Zahara baada ya kuona niko mbali, hapo ndipo nliposhtuka kutoka katika dimbwi la mawazo na kumjibu niko sawa. Nikanywa uji wangu, nikamlipa kisha nikarudi nyumbani.
Nikiwa pale nyumbani, nilipata wazo la kwenda nyumbani kwa Mzee Mbogo, nikaangalie kinachoendelea. Niliamini huenda Mzee Mbogo amechukuliwa kutumia nguvu zake za kichawi na wameenda kumzika huko kwake.
Nilienda kituoni kupanda daladala mpaka mjini, ambapo nilipanda magari yanayoenda Mtakuja. Nilifanikiwa kupata gari mapema wala sikusubiri. Wakati tuko njiani, mvua kubwa sana ikaanza kunyesha, na kila tulivyokaribia ndivyo mvua ilivyozidi. Kwakuwa haukuwa msimu wa mvua, nilishangaa sana, nikajaribu kulihusisha tukio la mvua na safari yangu, lakini nikajipa moyo.
Tulifika, mvua bado ikiwa inanyesha, nikakaa katika moja ya baraza za nyumba pale kituoni, nikisubiri mvua ipungue. Hatimaye ilikata. Nikamuomba boda boda anipeleke kwa Mzee Mbogo.
“Bro, huko hakwendeki, mvua imeharibu njia, labda uuchape kwa mguu kaka”. Majibu ya bodaboda yalinivunja moyo. Ila niliamua kuukanyaga kwa mguu hadi nikashuhudie kinachoendelea huko Mtakuja. Nilitembea kwa masaa matatu mpaka nilipoiona nyumba ya Mzee Mbogo kwa mbali. Niliwaona watu wengi sana wamekusanyika nje ya nyumba ile. Machozi yakaanza kunitoka kwa kujua ukweli wa kuwa kifo cha Mzee Mbogo nimekisababisha mimi. Nilijutia sana, pamoja na aliyoyakusudia kuyafanya Mzee Mbogo kwangu, bado nilitamani sana isingekuwa vile, nilitamani afe kifo ambacho sitakibeba mimi kama mhusika mkuu.
Kadri nilivyosogea, ndivyo majuto yangu juu ya niliyoyatenda yalivyozidi. Sikutakiwa kuamua kumkamata mtu yeyote pale ilihali nikijua yupo babu yangu kipenzi Mzee Mbogo. Nilifika hadi nje kwa Mzee Mbogo, niliwakuta kina mama wengi zaidi kuliko wanaume. Vilio vilitawala kila kona ya uwanja wa nyumba ile ya Mzee Mbogo. Nikazama moja kwa moja pale katika kisebule kidogo cha Mzee Mbogo, nikawakuta wazee wa familia wote wapo pale, akiwemo Mzee Mbogo-Para mwenyewe. Nilinyong'onyea..


Itaendelea...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NAKUFAHAMU VIZURI


MTUNZI: KJM-0718274130


SEHEMU YA 15


BAADA ya macho yangu kugongana na Mzee Mbogo, alinyanyuka akanishika mkono na kunitoa nje!. Akanizungusha mpaka nyuma ya kile kibanda ambako hakukua na mtu yeyote, alionekana kutaka kuniambia jambo fulani ambalo nilishalihisi.

“Bibi yako amefariki”. Ndicho alichoniambia, na ni kitu nilichokitegemea.

“Kwanini umefanya hivi?”. Nilimuuliza Mzee mbogo kwa hasira.

“Bibi yangu ana hatia gani mpaka umfanyie hivi?”. Niliendelea kumuuliza maswali.

“Mimi ni mtu muhimu, nisingeweza kufa abaki yeye, ndio maana nikaona ni bora atangulie yeye”. Alijitetea Mzee Mbogo na kunipandisha hasira ambazo sikuwahi kuzihisi tangu nizaliwe. Nilijikuta nikinyanyua mkono wangu na kumchapa kofi zito sana Mzee Mbogo, kofi lililomfanya ayumbe na kuweweseka karibu ya kuanguka. Nilijawa na hasira sana, sikuamini kama Mzee Mbogo anaweza kuwa na roho mbaya kiasi cha kubadilisha dawa kuwa kafara na kuamua kumuua bibi yule asiyekuwa na hatia. Mzee Mbogo alipiga magoti akiniomba nimsamehe, nilihisi kama naota. Nilianza kupatwa na hali fulani ambayo sikuielewa kabisa, kizunguzungu, mwili kukosa nguvu na hatimaye nilianguka chini na kupoteza fahamu.

Nilizinduka ikiwa jioni sana, watu wamekwishazika. Bado sikuwa na nguvu kabisa, nilijilaumu kwa kitendo kilichosababisha bibi yangu kuuawa, lakini sikuwa na mtu wa kumwambia. Nilijihisi mnyonge sana, sikuona msiba ule kama wa kawaida, niliona nilihusika kwa namna moja ama nyingine juu ya kifo cha bibi yangu. Nilijikongoja na mtu wa kwanza kumuulizia ni Mzee Mbogo, nikaelekezwa alipo. Cha kushangaza ni kuwa, waliniambia kuwa tangu mimi nipoteze fahamu nikiwa na Mzee Mbogo, mpaka wakati huo Mzee Mbogo analia bila kunyamaza. Nilionana nae, japo hasira zilikuwa bado zipo juu yake, lakini hali yake ilinifanya nirudi nyuma kidogo. Ni mzee wangu, amekosea anastahili kusamehewa. Kilio cha Mzee Mbogo kilinifanya nihisi kuwa anajua amekosea. Lakini kilio chake kilikua na siri ambayo watu wote pale msibani hawakuijua zaidi yangu. Nilimnyanyua na kumkumbatia, nikimnong'oneza kuwa asijali mimi niko pamoja nae. Kidogo alipata faraja na kurudi kuungana na ndugu wengine msibani. Watu wengi pale msibani waliomuonea huruma Mzee Mbogo juu ya kifo cha mkewe. Wengi wakidai kuwa huzuni ile ilitokana na Mzee Mbogo kumpenda sana mkewe kuliko kawaida. Mimi nilikua najisemea moyoni tu kuwa usilolijua ni sawa na usiku wa giza.

Nilikaa pale msibani kwa siku tatu, ni siku ngumu zaidi ambazo sijawahi kuziishi katika maisha yangu. Lakini baadae nikaona kawaida. Siku ya nne niliaga na kuondoka kurudi mjini. Ila niliapa kutorudi tena pale kwa Mzee Mbogo, labda anitafute yeye. Nilitaka kusahau kabisa kuhusu bibi (mkewe Mzee Mbogo) na nilihisi njia pekee ya kumsahau ni kutokufika pale. Maisha yaliendelea kwa siku kadhaa bila rapsha rapsha zozote. Mtu aliyekuwa akinisumbua sana ni Amina ambaye mara zote alionekana kutaka 'huduma' yangu, nami sikuwa tayari kufanya hivyo. Akili yangu kwa kipindi hiki ilikua haijatulia kwa kiasi hicho. Nilijikita zaidi katika harakati za kutafuta kazi.

Asubuhi ya Jumatano moja nilipigiwa simu ya kuitwa katika usaili katika kampuni moja. Simu ilipigwa na dada aliyejitambulisha kwa jina la Mariam. Nilitakiwa kufika kwenye usaili kesho yake saa 2:00 asubuhi, nilifurahi sana kuona sasa naenda kupata kazi mpya itakayonifanya nitengeneze kipato upya kama zamani. Wazo la kufanya biashara kwangu lilikuwa gumu sana, kwa sababu sikuzoea. Niliona kuajiriwa ndio rahisi zaidi kwangu. Kwakuwa nilikuwa sijui tumeitwa watu wangapi kwenye usaili, nilijipanga kwa ajili ya maswali mawili matatu nitakayoulizwa niweze kuyajibu kwa ufasaha wa hali ya juu. Nilijiandaa mpaka saa 7 usiku nilipopitiwa na usingizi. Asubuhi niliamka na kujiandaa harakaharaka kidogo, maana nilikuwa nyuma ya muda kidogo. Mpaka nafika eneo la tukio tayari ilishakuwa saa 2 kasoro dakika mbilu tu. Nikashusha pumzi nzito na kutoa kitambaa kuanza kufuta jasho. Nilipoelekezwa kukaa sikukuta mtu mwengine yeyote kwa ajili ya usaili, lakini wala sikujisumbua kujiuliza maswali mengi. Hamu yangu ni kutamani kufanyiwa usaili na hatimaye kupata kazi.

Ilipofika saa 2:03, dada mmoja alifungua mlango uliokuwa unanielekea alikua mrefu mwembamba sana, alivalia sketi nyeusi aliyochomekea katika shati jeupe lenye mistari ya kijani. Chini alivaa viatu vyenye visigino virefu.

“Habari yako?”

“Nzuri tu”

“Adam, right?”

“Yes”

“Please nifuate”.

Nikanyanyuka na kumfuata dada yule ambaye aligeuza na kurudi kule ndani. Ilikuwa ni ofisi nzuri sana, iliyopambwa na meza nzuri sana na viti vya thamani. Kiyoyozi kilipuliza vizuri na kusababisha nisahau shida za joto la nilipotoka. Mbele yangu nilimuona dada wa saizi yangu ambaye ndiye alionekana bosi katika ofisi ile. Alikaa nyuma ya meza moja kubwa akiwa katika kiti cha kuzunguka. Pembeni ya ile meza palikuwa na kompyuta na printer.

“Karibu bwana Adam Ahmad Ngudu, karibu ukae”. Alinikaribisha yule dada huku akinielekeza kukaa wakati huohuo akimpa ishara yule dada aliyenileta pale ndani kutoka nje.

“Bwana Adam, sisi tumevutiwa mno na CV yako pamoja na uzoefu wako, hatuna shaka wewe ni mfanyakazi mzuri sana. Hatukuona haja ya kuwa na watu wengi hapa kwa ajili ya usaili, tumeona tukuajiri wewe moja kwa moja kama utakuwa tayari uanze kazi leoleo”. Maelezo ya moja kwa moja ya huyu bosi yalinifanya nisahau shida zangu zote na kuanza kufurahi moyoni. Nikanyoosha mikono juu kumshukuru Mungu kwa kujibu maombi yangu ya muda mrefu.

“Nashkuru sana bosi, sina la kusema, naamini mnalipa vizuri, nafurahi sana kwa kuniamini”.

“Usijali kuhusu malipo, utapokea 'package' nzuri kuliko huko ulikokuwa ukifanya kazi awali.

Baada ya hapo bosi akasimama, akanielekeza kutoka nje ili akanitambulishe kwa wafanyakazi wengine tayari kwa kuanza kazi. Wakati nimetangulia mbele, bosi akiwa nyuma nilianza kupata wasiwasi juu ya ile kazi, nikiwa nimekaribia kabisa mlango wa kutokea pale ofisini, niligeuka na kumtazama vizuri usoni yule bosi, nilimuona akitabasamu. Nilimuangalia kwa umakini kuanzia juu hadi chini, na yeye akawa kama ananishangaa na kujiuliza maswali.

“Najua wewe ni Lutfiya, lakini nakuhakikishia kuwa huwezi kunipata kirahisi kiasi hiki, kwa leo tena hesabu hasara, nenda kajipange upya mwanaharamu mkubwa wewe...”. Nilimwambia kwa kujiamini huku nikimkodolea macho, akabaki ameduwaa, nikafungua mlango nikatoka na kuubamiza kwa nguvu nikitokomea kurudi nyumbani.



Itaendelea...




Sent using Jamii Forums mobile app
 
NAKUFAHAMU VIZURI

MTUNZI: KJM-0718274130


SEHEMU YA 16


Baada ya kutembea hatua chache tu nje ya ofisi ile huku nikisonya sana kutokana na ujinga wa Lutfiya, mbele yangu alisimama Mzee Mahmoud. Akanifanya nigeuze uelekeo wa safari yangu na kukunja kulia, akaniita. Nikageuka na kutaka kumsikiliza, akatembea na kuja nilipo.

“Adam, Lutfiya anaonekana kukupenda sana, jaribu kumsikiliza”. Alisema Mzee Mahmoud mara baada ya kufika nilipokuwa nimesimama.

“Kitu cha ajabu ni kuona mtu mzima kama wewe unageuka kuwa kuwadi wa Lutfiya, nitaendelea kuwashawishi watu wote wanaoogopa majini kuwa waache tabia hiyo, majini kama ndio nyie, ni wapuuzi sana hampaswi kuogopwa kwa kiasi hicho”. Niliongea kwa kujiamini nikimkazia macho Mzee Mahmoud, nahisi hakuamini aliyokuwa anayasikia, akageuza na kutokomea. Mimi nikarudi kwenye uelekeo wangu ule ule wa mwanzo unaoelekea kituo cha daladala. Mbele kidogo alisimama Lutfiya, nilipomtazama machoni niliona machozi yakimwagika.

“Adam, naomba unisikilize angalau kwa dakika moja tu”. Lutfiya aliomba. Nilimtazama vizuri machoni, nikaona ukweli wa nafsi yake.

“Twende tukaliongelee nyumbani”. Nilitamka na kumshika mkono, yeye hakuwa na la kusema, alitii.

Tukapanda daladala mpaka nyumbani kwangu, nikafungua mlango wa nje na kumkaribisha ndani.

“Adam, unataka kuniua?”. Aliniuliza Lutfiya akiwa bado amesimama pale mlangoni, nikakumbuka kuhusu ile dawa. Nikasoma dua maalum kisha nikamshika mkono na kumuingiza ndani, haoo moja kwa moja hadi chumbani. Baada tu ya kufunga mlango wa chumbani, nilimrukia Lutfiya na kumkumbatia, mwili wake ulikuwa na joto lisilo la kawaida. Chuchu zake zilizosimama mithili ya msumari ziligusa katika kifua changu, muda huu Lutfiya alikuwa analia kwa kwikwi. Nikajichomoa na kumuangalia usoni, nikamuona ana sura ya kutaka kutabasamu huku analia. Nikagusanisha lips zangu na zake, alitii. Tukaanza kupata mate, mkono wangu mmoja ukiwa unatalii nyuma kubinyabinya na kupapasa tako zake laini kabisa. Hatimaye nikaona kama baibui lake linanizonga, nikalivuta juu na kulitupa pembeni. Wakati huu kichwa cha chini kilishakolea moto, kichwa cha juu kilikuwa hakifanyi kazi tena. Sasa Lutfiya alibaki na gauni jepesi, nalo nikalivuta juu na kulitupa chini, hapa ndipo nilipofaidi muonekano wake maridhawa, naam.. Lutfiya aliumbika hasa, shepu yke mithili ile ya kuchora kwa msanii maarufu, rangi yake moja mwili mzima iliupamba vizuri sana mwili wake. Wakati huu Lutfiya akiwa amebaki na pichu tu na sidiria. Nikapeleka vidole vyangu nyuma ya mgongo wake na kuifyatua sidiria ambayo iliachia taratibu, nikaichomoa na kuitupa ambapo sikupajua. Bahati nzuri alikuwa na pichu ya kisasa, kwahiyo nikafungua mkanda tu na kuiacha ianguke yenyewe. Kisha nikambeba na kumtupia kitandani, nikasaula haraka haraka na kujitupa kitandani nikiwa mtupu kabisa. Nilianzia chini kabisa katika unyayo wake, nikiuramba taratibu kwa kutumia ulimi wangu, Lutfiya ni kama mtu aliyehisi kutekenywa hivi, akawa kama anashtuka shtuka na kujisogeza juu. Wakati nikiendelea na zoezi hili, mikono yangu ilikua ikipapasa mapaja laini yanayovutia ya Lutfiya, kwa mbaali nilisikia akigumia. Nikapanda juu taratibu nikiendelea kuyanyonya mapaja yake mpaka nikafika chumvini. Nikazama uvinza na kuanza kuipiga brash 'starter' yake. Hapo ndipo nilipomsikia Lutfiya akitoa kilio cha burudani.

“Aa..adaa...mm..aiiis..iii...taaammmm". Mimi niliendelea kuzungusha ulimi taratibu katika eneo la tukio, dakika moja tu nikamuona Lutfiya akitetemeka sana na kuanza kurusha miguu kama ng'ombe aliyepigwa kisu, naam.. Barabara kabisa alikuwa amefika kilele cha burudani, mimi sikujali, niliendelea na zoezi langu hilo huku mkono mmoja nikiuzungusha katika kiuno chake, nikamuona akiitika tena na tena mpaka ikafika idadi nisizozikumbuka. Nikaacha na kuhamia katika matiti yake yaliyochongoka, muda wote huu alikuwa akitoa sauti za miguno tu, hakuweza hata kunyanyua mkono. Nikaanza kupitisha ulimi katika chuchu ya ziwa lake la kulia..

“Adaa..m iii..na..tosshaa banaa.. I..na..toosh..aa". Sauti hii ya Lutfiya ilinifanya niache ninachokifanya, nikijivuta chini na kumchomeka taratiib mheshimiwa spika bungeni kwake. Hali ya hewa ya umande ilimfanya Mheshimiwa spika kuingia vizuri pale bungeni pasi na mikwaruzano.. Hapo nilimsikia Lutfiya akipiga kelele za kama mtu anayekata roho.. Nikaanza kupiga misere ya nje ndani taratib hadi spidi ilipokolea. Lutfiya alinishika kiuno huku akinikandamiza, nikajua tayari kwa mara nyingine.

“Nakupenda saanaa.. adam.." Nilimsikia akiongea kwa sauti ya kupagawa. Mimi kwa mbaali nikaanza kuwasikia wachina wakiomba ruhusa ya kuingia bungeni, nikaona niwaruhusu hata kama kuna Corona, sikujali. Wakati huu wa kuwakaribisha wachina bungeni ndipo spidi yangy ilipokuwa kali zaidi. Ndipo ghafla Lutfiya akanisukuma na kunichomoa pale huku akitweta.

“Adaamm ukimwaga ndani leo napata mimba”. Aliongea kwa sauti ya kuhamaki. Mimi sikumwelewa kabisa, sikujua hata anazungumzia kitu gani kwakweli. Nikamvuta karibu na kuchomeka tena. Nikapiga tako mbili tatu mara wachina haoo... Nilimsikia tu Lutfiya akisema "ayaaaa ushantia mimbaa".


Itaendelea..




Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom