Hadithi ya Mapenzi: Nakufahamu vizuri

Hadithi ya Mapenzi: Nakufahamu vizuri

NAKUFAHAMU VIZURI

MTUNZI: KJM -0718274130

SEHEMU YA 07
★★★★★★★★

Nilielekea mlangoni na kumfungulia Amina. Kilichonishangaza juu yake baada ya kumuona ni namna alivyokuwa amevaa. Hakika ilikuwa sawa sawa na alivyovaa Lutfiya pale chumbani wakati ananiambia nikamfungulie Amina. Baibui jeusi lililobana kidogo, na mtandio wa rangi ya maziwa. Hapa pia nilipata kuona uwiano wa Amina na Lutfiya, nikagundua kuwa wanalingana hadi maumbo yao. Niliduwaa nikiwa nimesimama katikati ya mlango nashindwa kufanya maamuzi ya aidha nimruhusu Amina aingie ndani au Laa..!!.

“Wewe una matatizo gani? Mbona umeduwaa hapo mlangoni? Nipishe nipite”. Alisema Amina huku akinisukumia ndani. Niligoma kumruhusu na kumtunishia msuli ashindwe kunisukuma.

“Anhaaa, nimeshajua, una mwanamke wako ndani, sasa leo atanitambua huyo paka Zuwena”. Aliongea kwa hasira na kupandisha sauti Amina, watu wa karibu na nyumbani kwangu walishaanza kutukodolea macho, nikaamua kumruhusu ili tusije tukajaza watu.

Amina alielekea moja kwa moja chumbani kwangu huku mimi nikifuata nyuma. Baada ya kupiga hatua kadhaa nikakumbuka sijafunga mlango na funguo, nikarudi mlangoni na kufunga. Wakati napiga hatua sasa kuelekea chumbani, nilisikia Amina akiangua kilio huko chumbani. Nikachangamsha hatua zangu na kufika chumbani.

“Nini tena kinakuliza mpenzi?” Niliuliza huku nikimsogelea Amina karibu na pale kitandani alipokaa. Nilipitisha mkono wangu wa kushoto mgongoni mwake huku nikijaribu kuunyanyua uso wake aliokuwa ameinamia chini kwa kutumia mkono wangu wa kulia.

“Hiiv..ii Adaa..m ni li.ni uu..taa..cha umalaya..w.ee mwanaume?” aliniuliza swali kwa tabu kutokana na kwikwi za kilio, huku akinyanyua uso wake. Mkono wake wa kulia alikuwa ameshikilia chupi nyekundu. Nilipiga jicho la haraka haraka na kugundua ni chupi ya Lutfiya. Nilipigwa na butwaa na kukosa majibu.

“Au...kwa..ku.a na..k..upenda A..dam ndo unan..ifan..yi..a hivi??” Aliuliza tena Amina kwa kwikwi. Kiukweli sikuwa na cha kumjibu zaidi ya kumtazama tu na kujaribu kumsihi anyamaze nimuelezee. Licha ya kuwa sikuwa na cha kumueleza kwa wakati huo. Baada ya dakika kadhaa, Amina alinyamaza, akaelekea bafuni ambapo nako hakukaa hata dakika mbili, akarudi chumbani na kuchukua mkoba wake na kuelekea mlango wa nje wa kutokea. Niliongoza nyuma, nikamfungulia mlango kisha akatoka kwa hasira.

Nikafunga tena mlango na kurudi chumbani.
Nikajirusha kitandani huku nikiwa nimechoka sana na vitimbi vya siku ile. Ni kama nilipitiwa na usingizi hivi.
Nilishtuka baada ya mwanga mkali sana kupiga mle chumbani mwangu. Nikakurupuka na kukaa kitako kitandani. Nikapiga jicho saa yangu ya mkononi, ilikuwa ni majira ya saa tano kasoro dakika saba usiku.

Nilihisi moyo unaenda mbio sana, chumba kizima kikiwa kinaonesha kama mchana wa saa saba licha ya kuwa sio taa zilizokuwa zikimulika. Nilijiuliza maswali mengi sana, lakini mwisho nikajipa moyo kuwa vitakuwa ni vitimbi tu vya Lutfiya alivyoanza kuvionesha tangu asubuhi ya siku hii.

“Lutfiya, kwanini unanitesa hivi? Unataka nini?” niliamua kujisemea kwa sauti nikiamini hakuna muujiza mwengine wowote zaidi ya Lutfiya tu.

Nikaamua kushuka pale kitandani na kutoka nje ya chumba changu. Nikafungua mlango wa chumbani, lahaulaa..!! Nilikuta ule mwanga mkali ulikuwa umeenea nyumba nzima. Nikatembea kuelekea sebleni kwangu. Sikuamini macho yangu!! Nilikuta watu wamekaa sebleni, juu ya mkeka ambao sikuwahi kumiliki hapa nyumbani kwangu. Watu hawa, wote wanaume, waliovalia kanzu nyeupe na kofia nyeupe, vyote vikiwa vimefanana, sikuwa nawajua hata mmoja. Niliwahesabu haraka haraka na kukuta ni watu watano.

Tofauti na siku za nyuma ambapo mara nyingi nilikuwa nikipatwa na uoga hadi kuzimia ninapokutana na vitu kama hivi, lakini safari hii wala sikuwa na hofu yoyote.

“Karibu bwana Adam, ni wewe tu ndiye tunayekusubiri kuanza shughuli yetu”. Alisema mzee mmoja ambaye ndiye aliyeonekana mkubwa kiumri kati yao huku akinielekeza pa kukaa.

Itaendelea...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NAKUFAHAMU VIZURI

MTUNZI: KJM-0718274130

SEHEMU YA NANE

★★★★★★★★★★★★

Nilikaa nilipoelekezwa, nikiwa sijui kikao hiki kinahusiana na nini haswa.
“Bwana Adam, mimi naitwa Saidi Alhuram, ni baba mzazi wa Lutfiya. Na hawa unaowaona hapa ni baba zake wadogo bi Lutfiya”. Alisema yule mzee ambaye alionekana kuwa na umri mkubwa kuliko wote pale kikaoni. Sikuwa na la kusema zaidi ya kuitikia tu na kumuashiria yule mzee aendelee.

“Dhumuni hasa lililotuleta ni hii kadhia ya leo, kitendo ulichofanya cha kumzini binti yetu. Ni kitendo ambacho hakijawafurahisha wazee wake wote Lutfiya. Ni kitendo kibaya mno. Kitendo ambacho kwetu sisi majini hatukikubali”. Aliongea yule mzee huku akinikazia sura. Alionyesha kuchukizwa. Maneno yake yalifanya nihitimishe na kujiridhisha kuwa Lutfiya hakuwa binadamu wa kawaida, bali ni jini. Hisia ambazo nilikuwa nazo tangu asubuhi ya siku hii nilipokutana na Lutfiya.

“Najua kuwa umefanya bila kujitambua, na hii yote ni kutokana na hila za mtoto wetu Lutfiya, lakini ndio ushazini tayari. Ni juu yako kuepuka zinaa kwa mtu yeyote, si lazima Lutfiya. Ila kwakuwa hii ni tabia yako, tupo hapa kuikomesha”. Aliongeza yule mzee na kumuangalia mzee mwingine ambaye alikuwa muda mwingi akiniangalia machoni. Ni kama alimpa ishara ya kuongea hivi.

“Lutfiya amefanya jambo hili juu ya mapenzi yake kwako, hajitambui huyu mtoto. Amefanya hivyo akitaka kutupa shinikizo la sisi kumuozesha kwako, na anajua kuwa si jambo rahisi sana”. Aliongea yule mzee aliyeachiwa kijiti.
Mpaka wakati huu nilikuwa sijawaelewa kabisa wazee wale. Nilibaki nikijilaumu mwenyewe tu kwa kujiingiza katika janga hili zito. Sikutegemea kama ningepitia wakati mgumu kama huu katika siku ile. Pamoja na wazee wale kutangulia kuongea, bado shauku yangu nilitamani kujua zaidi hatma yangu.

“Kwahiyo wazee, mimi mnaniambiaje? Nini mlichoamua juu yangu?”. Niliamua kuvunja ukimya.
“Tumeamua kukuozesha Lutfiya”. Alisema mzee Said.
“Sasa hivi?” Niliuliza kwa sauti, hamu ya kulijua jambo hili kiundani ilikuwa kubwa.
“Hapana”. Aliongea Mzee Said na kunifanya nishushe presha kidogo.

“Tutakuozesha binti yetu baada ya taratibu zote kukamilika, tunajua tusipowaozesha huenda Lutfiya akafanya jambo baya zaidi. Ni mwaka mzima sasa amekua akilitaja hili jambo tunamkatalia. Lakini leo asubuhi tulipofanya makosa ya kiulinzi juu yake ndipo alipoitumia nafasi hiyo kukutana na wewe na akafanya mliyoyafanya, ni tukio linaloonesha kuwa amedhamiria kweli hili jambo, tukiendelea kumuacha huenda akafanya makubwa zaidi”.

Aliongeza Mzee Said na kunifanya nianze kupata picha kamili sasa. Ila nilijiuliza tu kama inawezekana kweli Lutfiya amenifuatilia mwaka mzima?.
“Kwahiyo ni taratibu gani ambazo zinatakiwa kukamilika ili uniozeshe?”. Niliuliza, kichwani nilikuwa sina nia ya kuoa, bali nilitaka tu kujua jambo hili kiundani ili nijue naliepuka vipi.

“Itabidi tuandae siku ya wewe kuja kwetu ujinini, upajue, uwaone na mama zake Lutfiya na ndugu wengine. Ni lazima pia tukuelekeze namna ya kufika huko, maana sisi tunaishi baharini”. Aliongea Mzee Said na kufanya nianze kutoka jasho jingi sana. Hali ya uoga ilianza kujirudia.

“Tutamtuma mwakilishi wetu kesho kuja kukupa maelekezo kamili, tafadhali nakuomba uwepo hapa nyumbani kesho saa 4:00 asubuhi. Sisi tunaondoka”. Alimalizia Mzee Said na kuniacha na butwaa. Kisha wote wakasimama na kushikana mikono. Nilipepesa macho na sikuwaona tena.

Nilijaribu kupiga kelele. Lakini nilijishangaa sana, sauti haikuwa ikitoka. Nikaamua kurudi kitandani na kuendelea na usingizi wangu. Lakini sikuweza kulala. Usingizi ulipaa. Nilitingwa na mawazo mazito mno. Nilianza kujutia vitendo vyangu vyote vya kimalaya nilivyovifanya huko nyuma. Saa chache za usiku huu zilizobaki, niliziona zaidi ya siku nzima. Nilibaki macho mpaka saa 12 asubuhi ambapo niliamua kutoka nje.

Nilienda moja kwa moja kwa muuza uji ambaye alikuwa akikaa nyumba kama tano kutoka nilipo. Mara nyingi nilikuwa nikipata uji asubuhi maeneo hayo, nilipenda sana uji wa ngano.
Zahara, dada aliyekuwa akiuza uji pale, alishanizoea sana. Alinipachika jina la "Fundi", hakumaanisha vingine bali ni fundi wa wanawake, mtaalamu wa kutengeneza wanawake.

“Karibu sana Fundi, nishakuwekea uji kabla hujafika, nilivyokuona tu nikasema ngoja nikutilie kabisa”. Alisema Zahara mara baada ya mimi kukaa pale na kumsalimia.

“Asante sana bi Zahara”. Niliitikia wakati napokea kikombe kikubwa cha nusu lita cha uji wa ngano.
“Jana nilishangaa kidogo, nilikuona ukiingia katika ile nyumba pale”. Alisema Zahara na kunifanya nishtuke kidogo.
“Kumbe uliniona? Enhee nambie, ina nini ile nyumba?”. Niliuliza kwa shauku.

“Nyumba ile ilikuwa ikiishi watu ambao walisemekana ni majini, baada ya wao kuondoka, hakuna aliyeweza kuishi ile nyumba, kila mtu alishindwa, ina vituko balaa..” Niliendelea kumsikiliza Zahara kwa umakini.
“Jana nilipokuona umeingia nimeshangaa sana, nikahisi labda na wewe ni mmojawapo kwakweli...” Aliongeza Zahara, bado nilikuwa nimeduwaa nikimsikiliza.

“Hebu nambie, ulienda kufanya nini mle ndani? Na ulipata wapi funguo za kuingia mle?”. Zahara aliuliza maswali ambayo sikuwa na majibu yake.

Itaendelea...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NAKUFAHAMU VIZURI

MTUNZI: KJM-0718274130

SEHEMU YA NANE

★★★★★★★★★★★★

Nilikaa nilipoelekezwa, nikiwa sijui kikao hiki kinahusiana na nini haswa.
“Bwana Adam, mimi naitwa Saidi Alhuram, ni baba mzazi wa Lutfiya. Na hawa unaowaona hapa ni baba zake wadogo bi Lutfiya”. Alisema yule mzee ambaye alionekana kuwa na umri mkubwa kuliko wote pale kikaoni. Sikuwa na la kusema zaidi ya kuitikia tu na kumuashiria yule mzee aendelee.
“Dhumuni hasa lililotuleta ni hii kadhia ya leo, kitendo ulichofanya cha kumzini binti yetu. Ni kitendo ambacho hakijawafurahisha wazee wake wote Lutfiya. Ni kitendo kibaya mno. Kitendo ambacho kwetu sisi majini hatukikubali”. Aliongea yule mzee huku akinikazia sura. Alionyesha kuchukizwa. Maneno yake yalifanya nihitimishe na kujiridhisha kuwa Lutfiya hakuwa binadamu wa kawaida, bali ni jini. Hisia ambazo nilikuwa nazo tangu asubuhi ya siku hii nilipokutana na Lutfiya.
“Najua kuwa umefanya bila kujitambua, na hii yote ni kutokana na hila za mtoto wetu Lutfiya, lakini ndio ushazini tayari. Ni juu yako kuepuka zinaa kwa mtu yeyote, si lazima Lutfiya. Ila kwakuwa hii ni tabia yako, tupo hapa kuikomesha”. Aliongeza yule mzee na kumuangalia mzee mwingine ambaye alikuwa muda mwingi akiniangalia machoni. Ni kama alimpa ishara ya kuongea hivi.
“Lutfiya amefanya jambo hili juu ya mapenzi yake kwako, hajitambui huyu mtoto. Amefanya hivyo akitaka kutupa shinikizo la sisi kumuozesha kwako, na anajua kuwa si jambo rahisi sana”. Aliongea yule mzee aliyeachiwa kijiti.
Mpaka wakati huu nilikuwa sijawaelewa kabisa wazee wale. Nilibaki nikijilaumu mwenyewe tu kwa kujiingiza katika janga hili zito. Sikutegemea kama ningepitia wakati mgumu kama huu katika siku ile. Pamoja na wazee wale kutangulia kuongea, bado shauku yangu nilitamani kujua zaidi hatma yangu.
“Kwahiyo wazee, mimi mnaniambiaje? Nini mlichoamua juu yangu?”. Niliamua kuvunja ukimya.
“Tumeamua kukuozesha Lutfiya”. Alisema mzee Said.
“Sasa hivi?” Niliuliza kwa sauti, hamu ya kulijua jambo hili kiundani ilikuwa kubwa.
“Hapana”. Aliongea Mzee Said na kunifanya nishushe presha kidogo.
“Tutakuozesha binti yetu baada ya taratibu zote kukamilika, tunajua tusipowaozesha huenda Lutfiya akafanya jambo baya zaidi. Ni mwaka mzima sasa amekua akilitaja hili jambo tunamkatalia. Lakini leo asubuhi tulipofanya makosa ya kiulinzi juu yake ndipo alipoitumia nafasi hiyo kukutana na wewe na akafanya mliyoyafanya, ni tukio linaloonesha kuwa amedhamiria kweli hili jambo, tukiendelea kumuacha huenda akafanya makubwa zaidi”. Aliongeza Mzee Said na kunifanya nianze kupata picha kamili sasa. Ila nilijiuliza tu kama inawezekana kweli Lutfiya amenifuatilia mwaka mzima?.
“Kwahiyo ni taratibu gani ambazo zinatakiwa kukamilika ili uniozeshe?”. Niliuliza, kichwani nilikuwa sina nia ya kuoa, bali nilitaka tu kujua jambo hili kiundani ili nijue naliepuka vipi.
“Itabidi tuandae siku ya wewe kuja kwetu ujinini, upajue, uwaone na mama zake Lutfiya na ndugu wengine. Ni lazima pia tukuelekeze namna ya kufika huko, maana sisi tunaishi baharini”. Aliongea Mzee Said na kufanya nianze kutoka jasho jingi sana. Hali ya uoga ilianza kujirudia.
“Tutamtuma mwakilishi wetu kesho kuja kukupa maelekezo kamili, tafadhali nakuomba uwepo hapa nyumbani kesho saa 4:00 asubuhi. Sisi tunaondoka”. Alimalizia Mzee Said na kuniacha na butwaa. Kisha wote wakasimama na kushikana mikono. Nilipepesa macho na sikuwaona tena. Nilijaribu kupiga kelele. Lakini nilijishangaa sana, sauti haikuwa ikitoka. Nikaamua kurudi kitandani na kuendelea na usingizi wangu. Lakini sikuweza kulala. Usingizi ulipaa. Nilitingwa na mawazo mazito mno. Nilianza kujutia vitendo vyangu vyote vya kimalaya nilivyovifanya huko nyuma. Saa chache za usiku huu zilizobaki, niliziona zaidi ya siku nzima. Nilibaki macho mpaka saa 12 asubuhi ambapo niliamua kutoka nje.
Nilienda moja kwa moja kwa muuza uji ambaye alikuwa akikaa nyumba kama tano kutoka nilipo. Mara nyingi nilikuwa nikipata uji asubuhi maeneo hayo, nilipenda sana uji wa ngano.
Zahara, dada aliyekuwa akiuza uji pale, alishanizoea sana. Alinipachika jina la "Fundi", hakumaanisha vingine bali ni fundi wa wanawake, mtaalamu wa kutengeneza wanawake.
“Karibu sana Fundi, nishakuwekea uji kabla hujafika, nilivyokuona tu nikasema ngoja nikutilie kabisa”. Alisema Zahara mara baada ya mimi kukaa pale na kumsalimia.
“Asante sana bi Zahara”. Niliitikia wakati napokea kikombe kikubwa cha nusu lita cha uji wa ngano.
“Jana nilishangaa kidogo, nilikuona ukiingia katika ile nyumba pale”. Alisema Zahara na kunifanya nishtuke kidogo.
“Kumbe uliniona? Enhee nambie, ina nini ile nyumba?”. Niliuliza kwa shauku.
“Nyumba ile ilikuwa ikiishi watu ambao walisemekana ni majini, baada ya wao kuondoka, hakuna aliyeweza kuishi ile nyumba, kila mtu alishindwa, ina vituko balaa..” Niliendelea kumsikiliza Zahara kwa umakini.
“Jana nilipokuona umeingia nimeshangaa sana, nikahisi labda na wewe ni mmojawapo kwakweli...” Aliongeza Zahara, bado nilikuwa nimeduwaa nikimsikiliza.
“Hebu nambie, ulienda kufanya nini mle ndani? Na ulipata wapi funguo za kuingia mle?”. Zahara aliuliza maswali ambayo sikuwa na majibu yake.

Itaendelea...

Sent using Jamii Forums mobile app
Tupe uzi huo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*NAKUFAHAMU VIZURI*
*MTUNZI: KJM-0718274130*

*SEHEMU YA TISA*

Sikuwa na majibu ya maana ya kumjibu Zahara, nilikatisha maongezi kwa kubadilisha mada. Nilimaliza kupata kikombe cha uji na kufikiria nini cha kufanya baada ya pale. Ahadi ya wale wazazi wa Lutfiya ilikuwa waje nyumbani saa 4 asubuhi. Nilifikiria kuwakimbia. Sikutaka wanikute nyumbani kwangu muda huo. Niliamua kutokomea na kwenda mbali zaidi. Lakini wakati sijafanya maamuzi ya wapi hasa pa kwenda, wazo jingine likanijia kichwani. Nikaamua kuelekea huko nilikofikiria. Nilikabidhi kikombe cha uji kwa Zahara kikiwa kitupu, nikamlipa na kuelekea nyumbani kwangu. Kwakuwa nilikua sijaoga, nikaingia bafuni na kuoga haraka haraka, kisha nikaingia chumbani kwangu, nikavaa na kutoka. Saa ya mkononi ilisomeka saa moja na robo asubuhi. "Bado mapema sana" nilijisemea moyoni na kupanda daladala nikiwa na begi langu (lenye vitu muhimu ikiwemo laptop) mgongoni.
Nilikuwa naelekea kwa babu yangu Mzee Mbogo-Para. Mtaalamu sana wa sayansi ya giza. Japo ni muda mrefu nilikuwa sijaonana nae wala kuwasiliana nae, niliamua kwenda moja kwa moja kijijini kwake pasi na kuwasiliana nae. Lengo ni kwenda kumueleza yanayonisibu na kuona jinsi gani atakavyonisaidia.
Mzee Mbogo-Para alikuwa akiishi mbali kidogo, ilinihitaji kupanda daladala za kuelekea mjini, huko ndipo ningepata gari za kuelekea kijijini kwa Mzee Mbogo-Para, safari ya zaidi ya masaa mawili hadi kufika sehemu ambayo ningepanda bodaboda na kunipandisha vilima na kushusha makorongo kwa zaidi ya nusu saa ndipo ningefika nyumbani kwa babu yangu huyu. Pamoja na kuyajua hayo yote, niliamua kwenda kwake kwakuwa sikuwa na namna ya kufanya. Mjini mambo yalishavurugika!!.
Baada ya kufika mjini nikatafuta gari zinazoelekea kijijini kwa babu. Zilikuwa za shida kidogo, hivyo nililazimika kusubiri. Tulikuwa tumesimama kituoni na abiria wengine ambao niliwatambua wanasubiri gari ninayoisubiri mimi. Nikapiga jicho la kitalii na kukutana uso kwa uso na dada mmoja mrembo akiwa amesimama sio mbali na nilipo. Kama ilivyokuwa kawaida yangu, tayari moyo wangu ulishaanza kwenda mbio. Nikaamua kumsogelea nikiamini huenda ningepata chochote.
“Za saa hizi dada..”. Nilimsalimia baada ya kufika alipokuwa amesimama.
“Nzuri tu, za kwako Adam?” Alijibu huku akiniangalia vizuri usoni, alikuwa anatabasamu. Nilishangaa kunijua jina langu. Akili yangu haraka haraka nikajua huyu atakuwa Lutfiya, ndiye mwenye tabia hizi. Nikaishiwa nguvu.
“Hapana, mimi sio Lutfiya, ni mdogo wake, naelekea huko unakoelekea wewe kuna jambo”. Alisema yule dada baada ya kuona nimekaa kimya nikiwaza. Sikuongeza neno lolote, nikaamua kuondoka na kusogea nilipokuwa mwanzo. Gari ilifika na nikapanda. Ila cha ajabu sikumuona yule dada mle ndani ya gari. Nikajiuliza maswali machache kichwani mwangu bila majibu. Ila nikaamua kupuuza.
Nikiwa njiani nilipitiwa na usingizi mzito, wala sikujua yanayoendelea. Hii ilitokana na kutolala karibu usiku mzima. Nilikuwa nimechoka sana.
“Kaka..tumefika” nilishtuka kutoka usingizini, konda alikuwa akinitikisa ili niamke. Niliangaza huku na huko na kugundua kweli nilishafika kijijini Mtakuja, kijiji cha babu yangu Mzee Mbogo-Para. Nilishuka, nikasimama na kupiga myayo mfululizo. Konda alikuwa amenisimamia pembeni akiniangalia kwa makini.
“Vipi bro, mbona kama tunashangaana?” nilimtupia swali konda nikianza kupiga hatua kuelekea zilipo bodaboda.
“Heshimu kazi za watu blazaa.. Heshima kitu cha bure bloo... Mimi nimetumwa hela kaka.. Wee vipi? Mi nkushangaeee?? weee vipi.. ?? Nitie changu nikisongeshe mbele kwa mbele..” Konda aling'aka kwa sauti ya juu. Nilikuwa nimesahau kuwa sijalipa nauli. Japo maneno ya konda huyu yalinichoma, lakini sikuamua kusema chochote zaidi ya kutoa pesa yake mfukoni na kumlipa. Alinipatia "change" yangu na kuiweka mfukoni. Nikasogea kwenye bodaboda na kupanda moja ya bodaboda ya kijana pale kituoni.
“Mbogo-Para” nilimwambia yule kijana baada ya kupanda.
“Elfu kumi bro..” alisema yule bodaboda huku akigeuka kunitazama.
“Fanya saba”. Nilimsihi.
“Utanipa nane, nitakusaidia...” aliongeza bodaboda na kupiga 'starter' kuanza safari. Mimi sikuongeza neno lolote, nilifikiria tu kufika salama. Njiani nikajiwa tena na mawazo ya yule binti niliyekutana nae pale kituoni. Aliniambia anakwenda ninapokwenda mimi. Anaenda kwa ajili ya 'jambo'. Ni jambo gani hilo? Na kwanini hakupanda gari ilipokuja? Nilijiuliza maswali mengi sana juu yake. Lakini nikajipa moyo kuwa leo ndio mwisho wao hawa majini. Babu yangu anakwenda kumaliza kila kitu. Bodaboda ilitembea dakika 33 na kunifikisha katika kiunga cha Mzee Mbogo-Para ndani ndani ya kijiji kile cha Mtakuja. Nikampa boda boda stahiki yake na kuniacha nikielekea mlango wa kijumba kile kidogo cha udongo kilichoezekwa kwa makuti ya kumba.
“Hodii..” nilibisha katika mlango ule wa kijumba cha makuti. Mlango wake ulikuwa wa makuti pia.
“Karibuu.." Sauti ambayo sikuifahamu, iliitikia huko ndani. Nikafungua mlango na kuingia katika kisebule cha kijumba kile ambacho kilikuwa katikati ya vyumba viwili.
“Karibu Adam, umefika muda muafaka sana, ni saa nne kasoro dakika tatu..” alinikaribisha Mzee Mbogo-Para, pembeni yake walikuwepo wale wazee watano wazazi wa Lutfiya, na pia alikuwepo yule binti ambaye nilikutana nae pale kituoni.


Itaendeleaa...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*NAKUFAHAMU VIZURI*
*MTUNZI: KJM-0718274130*

*SEHEMU YA TISA*

Sikuwa na majibu ya maana ya kumjibu Zahara, nilikatisha maongezi kwa kubadilisha mada. Nilimaliza kupata kikombe cha uji na kufikiria nini cha kufanya baada ya pale. Ahadi ya wale wazazi wa Lutfiya ilikuwa waje nyumbani saa 4 asubuhi. Nilifikiria kuwakimbia. Sikutaka wanikute nyumbani kwangu muda huo. Niliamua kutokomea na kwenda mbali zaidi. Lakini wakati sijafanya maamuzi ya wapi hasa pa kwenda, wazo jingine likanijia kichwani. Nikaamua kuelekea huko nilikofikiria. Nilikabidhi kikombe cha uji kwa Zahara kikiwa kitupu, nikamlipa na kuelekea nyumbani kwangu. Kwakuwa nilikua sijaoga, nikaingia bafuni na kuoga haraka haraka, kisha nikaingia chumbani kwangu, nikavaa na kutoka. Saa ya mkononi ilisomeka saa moja na robo asubuhi. "Bado mapema sana" nilijisemea moyoni na kupanda daladala nikiwa na begi langu (lenye vitu muhimu ikiwemo laptop) mgongoni.
Nilikuwa naelekea kwa babu yangu Mzee Mbogo-Para. Mtaalamu sana wa sayansi ya giza. Japo ni muda mrefu nilikuwa sijaonana nae wala kuwasiliana nae, niliamua kwenda moja kwa moja kijijini kwake pasi na kuwasiliana nae. Lengo ni kwenda kumueleza yanayonisibu na kuona jinsi gani atakavyonisaidia.
Mzee Mbogo-Para alikuwa akiishi mbali kidogo, ilinihitaji kupanda daladala za kuelekea mjini, huko ndipo ningepata gari za kuelekea kijijini kwa Mzee Mbogo-Para, safari ya zaidi ya masaa mawili hadi kufika sehemu ambayo ningepanda bodaboda na kunipandisha vilima na kushusha makorongo kwa zaidi ya nusu saa ndipo ningefika nyumbani kwa babu yangu huyu. Pamoja na kuyajua hayo yote, niliamua kwenda kwake kwakuwa sikuwa na namna ya kufanya. Mjini mambo yalishavurugika!!.
Baada ya kufika mjini nikatafuta gari zinazoelekea kijijini kwa babu. Zilikuwa za shida kidogo, hivyo nililazimika kusubiri. Tulikuwa tumesimama kituoni na abiria wengine ambao niliwatambua wanasubiri gari ninayoisubiri mimi. Nikapiga jicho la kitalii na kukutana uso kwa uso na dada mmoja mrembo akiwa amesimama sio mbali na nilipo. Kama ilivyokuwa kawaida yangu, tayari moyo wangu ulishaanza kwenda mbio. Nikaamua kumsogelea nikiamini huenda ningepata chochote.
“Za saa hizi dada..”. Nilimsalimia baada ya kufika alipokuwa amesimama.
“Nzuri tu, za kwako Adam?” Alijibu huku akiniangalia vizuri usoni, alikuwa anatabasamu. Nilishangaa kunijua jina langu. Akili yangu haraka haraka nikajua huyu atakuwa Lutfiya, ndiye mwenye tabia hizi. Nikaishiwa nguvu.
“Hapana, mimi sio Lutfiya, ni mdogo wake, naelekea huko unakoelekea wewe kuna jambo”. Alisema yule dada baada ya kuona nimekaa kimya nikiwaza. Sikuongeza neno lolote, nikaamua kuondoka na kusogea nilipokuwa mwanzo. Gari ilifika na nikapanda. Ila cha ajabu sikumuona yule dada mle ndani ya gari. Nikajiuliza maswali machache kichwani mwangu bila majibu. Ila nikaamua kupuuza.
Nikiwa njiani nilipitiwa na usingizi mzito, wala sikujua yanayoendelea. Hii ilitokana na kutolala karibu usiku mzima. Nilikuwa nimechoka sana.
“Kaka..tumefika” nilishtuka kutoka usingizini, konda alikuwa akinitikisa ili niamke. Niliangaza huku na huko na kugundua kweli nilishafika kijijini Mtakuja, kijiji cha babu yangu Mzee Mbogo-Para. Nilishuka, nikasimama na kupiga myayo mfululizo. Konda alikuwa amenisimamia pembeni akiniangalia kwa makini.
“Vipi bro, mbona kama tunashangaana?” nilimtupia swali konda nikianza kupiga hatua kuelekea zilipo bodaboda.
“Heshimu kazi za watu blazaa.. Heshima kitu cha bure bloo... Mimi nimetumwa hela kaka.. Wee vipi? Mi nkushangaeee?? weee vipi.. ?? Nitie changu nikisongeshe mbele kwa mbele..” Konda aling'aka kwa sauti ya juu. Nilikuwa nimesahau kuwa sijalipa nauli. Japo maneno ya konda huyu yalinichoma, lakini sikuamua kusema chochote zaidi ya kutoa pesa yake mfukoni na kumlipa. Alinipatia "change" yangu na kuiweka mfukoni. Nikasogea kwenye bodaboda na kupanda moja ya bodaboda ya kijana pale kituoni.
“Mbogo-Para” nilimwambia yule kijana baada ya kupanda.
“Elfu kumi bro..” alisema yule bodaboda huku akigeuka kunitazama.
“Fanya saba”. Nilimsihi.
“Utanipa nane, nitakusaidia...” aliongeza bodaboda na kupiga 'starter' kuanza safari. Mimi sikuongeza neno lolote, nilifikiria tu kufika salama. Njiani nikajiwa tena na mawazo ya yule binti niliyekutana nae pale kituoni. Aliniambia anakwenda ninapokwenda mimi. Anaenda kwa ajili ya 'jambo'. Ni jambo gani hilo? Na kwanini hakupanda gari ilipokuja? Nilijiuliza maswali mengi sana juu yake. Lakini nikajipa moyo kuwa leo ndio mwisho wao hawa majini. Babu yangu anakwenda kumaliza kila kitu. Bodaboda ilitembea dakika 33 na kunifikisha katika kiunga cha Mzee Mbogo-Para ndani ndani ya kijiji kile cha Mtakuja. Nikampa boda boda stahiki yake na kuniacha nikielekea mlango wa kijumba kile kidogo cha udongo kilichoezekwa kwa makuti ya kumba.
“Hodii..” nilibisha katika mlango ule wa kijumba cha makuti. Mlango wake ulikuwa wa makuti pia.
“Karibuu.." Sauti ambayo sikuifahamu, iliitikia huko ndani. Nikafungua mlango na kuingia katika kisebule cha kijumba kile ambacho kilikuwa katikati ya vyumba viwili.
“Karibu Adam, umefika muda muafaka sana, ni saa nne kasoro dakika tatu..” alinikaribisha Mzee Mbogo-Para, pembeni yake walikuwepo wale wazee watano wazazi wa Lutfiya, na pia alikuwepo yule binti ambaye nilikutana nae pale kituoni.


Itaendeleaa...

Sent using Jamii Forums mobile app
Huu wino balaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NAKUFAHAMU VIZURI
MTUNZI: KJM-0718274130

SEHEMU YA KUMI

Nilipigwa na butwaa, sikuamini kama Mzee Mbogo anaweza kuungana na kina Mzee Said kulazimisha mimi nimuoe Lutfiya. Niliwatupia jicho mmoja baada ya mwengine pale sebuleni, cha ajabu wote walikuwa wakionyesha nyuso za furaha sana. Nilifikiri cha kufanya kwa sekunde chache nilizosimama pale, nikaamua kugeuza na kutoka nje.
“Adaam...”. Mzee Mbogo aliita. Sikugeuka, nikatoka nje. Bahati nzuri nilimkuta yule bodaboda bado hajaondoka.
“Nirudishe kituoni”. Nilimwambia yule dereva wa ile bodaboda baada ya kupanda.
“Sawa boss”. Jamaa aliitikia na kujaribu kupiga "starter" bila mafanikio. Akajaribu tena na tena, haikuwaka. Akajaribu kupiga "kick" bado pia haikukubali.
“Adam.. ” sauti ya Mzee Mbogo iliita kutokea nyuma huku akinishika begani. Nikashuka kwenye pikipiki na kuanza kufuatana na Mzee Mbogo ambaye alisimama baada ya hatua chache tu.
“Huwezi kukimbia hapa wakati mimi ndiye niliyekuita, hakuna ubaya wowote.. Kama kungelikuwa na ubaya nisingeruhusu wewe uje hapa, wala pia nisingewapokea hawa wageni mjukuu wangu”. Mzee Mbogo-Para alinisihi. Nikaanza kumsikiliza.
“Kwani hujui babu kama hawa watu wananisumbua?”. Nilimuuliza Mzee Mbogo-Para.
“Najua, na ndio maana nikakuita uje hapa tumalizane nao”.
“Tumalizane nao kivipi?”
“Fanya wanavyotaka, tutaishi vizuri sana mjukuu wangu, hii ni nafasi ambayo hatupaswi kuipoteza”. Mzee Mbogo alijaribu kunisihi nikubali kuoa binti wa kijini kwa lazima ili tu mambo yetu yaende vizuri. Matumaini ya kupata msaada juu ya jambo langu ili niepukane na usumbufu nilioanza kuupata yalififia. Mzee Mbogo-Para, mtaalamu wa tiba asilia zinazohusisha Maruhani, babu yangu wa pekee aliyebaki hapa duniani, alishindwa kunisaidia. Mzee Mbogo-Para ni kaka wa babu yangu aliyenizalia babaangu. Babu yangu ambaye ni pacha wake akiwa mdogo (Dotto) na Mzee Mbogo yeye akiwa mkubwa (Kulwa). Babu yangu Dotto yeye alifariki mapema sana baada tu ya kupata watoto wawili. Baba yangu, na shangazi yangu ambaye naye hakuishi miaka mingi baada ya kufariki kaka yake. Baba yangu pamoja na mambo mengine aliyonisisitiza nayo, alinisihi niwe karibu sana na Mzee Mbogo-Para katika maisha yangu ya hapa duniani. Mara nyingi humfuata Mzee Mbogo mara ninapokwama na kukutana na zahma za hapa na pale kuhusiana na maisha yetu ya kila siku. Na mara zote amekua akinisaidia mno.
“Kwahiyo babu, unasisitiza mimi kuishi vizuri kupitia kuoa jini? Kweli?”. Nilimuuliza Mzee Mbogo baada ya kuona anamaanisha anachoongea.
“Ndio, unajua kama huna kazi kwa sasa Adam, unajua jinsi gani ilivyo ngumu kupata kazi kwa sasa, fursa hii si ya kuichezea”.
“Babu, unajua ni kama vile unataka kunifanya mjinga, lakini nakuapia kuwa najua kuna maslahi yako binafsi katika hili. Na nitayajua hivi karibuni, twende ndani”. Niliongea kwa kujiamini huku nikimtazama Mzee Mbogo machoni. Mzee Mbogo ni kama alishtushwa na maneno yangu yale, lakini aliamua kukaza. Tukaongozana na kuelekea ndani.
“Tuko tayari kwa jambo”. Mzee Mbogo-Para aliongea mara baada ya kukaa katika mkeka, akimtazama mzee Said. Mzee Said alitoa ishara kwa yule binti niliyekutana nae kituoni, ambaye mpaka sasa sikuwa namfahamu jina lake. Akanyanyuka na kuingia chumba ambacho huwa nakitumia nikiwa nimelala hapa. Kibanda hiki cha Mzee Mbogo kilikuwa na vyumba viwili tu, chake na hiki cha wageni ambacho pia hukitumia kwa shughuli za kazi zake zinazohitaji faragha kubwa. Ukimya ukatawala pale ndani, hakuna aliyeongea chochote zaidi ya kutazamana tu.
Dakika chache yule binti alirudi akiwa amemshika mkono Lutfiya, aliyeonekana kupendeza kuliko kawaida. Nilimtizama jinsi alivyopambwa na piko zilizochorwa maua yaliyopendeza miguuni, kifuani na mikononi. Mapigo ya moyo yalianza kwenda mbio. Nikahisi kumtamani upya.
“Sikubahatika kumfaidi akiwa katika muonekano huu, yule alikuwa Amina”. Nilijisemea moyoni nikimsindikiza kwa macho Lutfiya akikaa pembeni ya baba yake Mzee Said.
Ndoa hii ilipangwa kufungwa kiislamu, hivyo basi ilianza kwa dua. Baada ya dua ilifuata hotuba ya ndoa (maneno maalum yanayosomwa yakiwa na aya na hadithi za Mtume yanayohusiana na ndoa na umuhimu wake). Hotuba hii aliisoma babu yangu ambaye nilimuona kama msaliti kwa wakati huu, Mzee Mbogo-Para. Kisha ukafika wakati wa kuozeshwa.
“Naomba mkono wako bwana Adam nikuozeshe sasa”. Aliniambia Mzee Said huku akininyooshea mkono wake. Nilimuangalia vizuri kwa jicho la kishababi bila kumpa mkono, akahisi kuna tatizo. Akaurudisha mkono wake ulipokuwa.
“Naomba kuuliza swali moja kabla hamjaniozesha”. Nilijitutumua kidume kwa kujiamini.
“Bila shaka, endelea..” alinijibu Mzee Said.
“Ndoa hii inafungishwa kwa misingi ya dini gani?”. Nilimuelekezea swali Mzee Said.
“Kwa mujibu wa dini ya kiislamu”. Alijibu kwa haraka Mzee Said.
“Naomba unitajie masharti ya ndoa ya kiislam kutimia”. Nilimtupia swali bila kuogopa.
“Idhini ya wazazi wa anayeolewa, idhini ya anayeolewa, idhini ya muoaji...”
“Hapo hapo...” . Nilimkatisha Mzee Said.
“Hapo idhini ya muoaji haipo, sipo tayari kuoa jini sio leo wala kesho na katika maisha yangu yote. Kwahiyo hapa hakuna ndoa”. Nilimtolea macho Mzee Said na kumkazia sauti.
“Ni lazima uoe Adam..”. Sauti kali ya Mzee Mbogo-Para iliyosindikizwa na kofi zito lililotua vizuri katika shavu langu la kulia na kunifanya nione vinyotanyota.

Itaendelea...

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom