Nzi Chuma
JF-Expert Member
- Jun 21, 2015
- 475
- 1,176
NAKUFAHAMU VIZURI
MTUNZI: KJM (0718274130)
SEHEMU YA KWANZA
Niliamka mapema kidogo kuliko kawaida yangu. Nikaingia bafuni na kuoga kisha nikarudi chumbani kwangu. Nikavaa nguo harakaharaka kisha nikatoka. Ni mtu ambaye kama hunijui ungedhani nawahi sehemu ya maana kidogo na yenye "dili" la uhakika. Ila haikua hivyo, niliamua tu kuwafurahisha majirani.
Nilipokua nakwenda wala sikuwa nikipajua. Ilikuwa ilimradi nitoke tu. Nikakaa kituoni kusubiri daladala nikiwa na begi langu lenye "laptop" ndani yake. Usafiri ulikuwa wa shida kidogo asubuhi hii, magari mengi yakigeuzia juu kwa juu baada ya kujaza mapema. Ukizingatia mimi nilikua nikiishi ndani kidogo, ilihitaji subira ya hali ya juu kupata gari kwa wakati ule ambao wengi walikua wakigombania kuwahi makazini mwao.
Mbali na mimi, na abiria wengi pale kituoni, pembeni yangu alikuepo dada mmoja mrefu mweupe, mwenye umbo lilichongoka vizuri. Macho yake yaliyokoleza wanja yalishabihiana sana na sura yake ya upole akikutazama. Mkono wa kulia alishika mkoba wake mdogo mweusi, na wa kushoto alikamata simu ya bei mbaya. Alivalia baibui jeusi lililombana kidogo kiasi cha kukupa uhuru wa kung'amua shepu yake. Manukato yake yalizagaa kituo kizima cha daladala. Baada ya kumthaminisha vizuri, niliona nimsalimie japo mwanzo sikufanya hivyo.
“Habari yako dada?”
Alinitazama, pasi na kujibu chochote. Nilijisikia vibaya sana, kwani abiria kadhaa walinigeukia kutazama nani aliyesalimia pasi na kupewa jibu. Nilifadhaika.
“Assalam alykum...” Nilisema tena kumuelekea yule dada, safari hii nikimtazama machoni.
“Waalykum Salaam..” Alijibu huku akitabasamu. Akanifanya nikashangaa zaidi.
“Unaonaje tukatembea tu hadi pale barabara kubwa ambapo magari ni ya uhakika? Unajua sio mbali kutokea hapa”. Niliona nitumie fursa ya lile tabasamu.
“Sawa, twende”. Alinijibu na kunifanya nishangae zaidi. Licha ya kumpa hilo wazo, lakini sikutegemea alikubali bila kusema chochote, nikijaribu kuangalia na alivyoanza na mimi. Ila nikaungana nae na kuondoka mdogo mdogo kuelekea barabara kuu ambapo ni mwendo za zaidi ya dakika 15 ukitembea kwa miguu.
“Adam, kwanini unapenda sana wanawake?” Aliniuliza swali hili hatua kumi tu toka tulipoanza safari. Nilikua sijaongea chochote, na nilipanga swali langu la kwanza liwe kuulizana majina, lakini yeye alionekana kunifahamu vizuri. Maswali kichwani mwangu yakawa mengi sana kuliko kawaida.
Ni kweli naitwa Adam, na ni kweli sifa ya kupenda wanawake ninayo, tena sana tu. Na hata yeye niliamua kumuongelesha kwa sababu hiyo. Ila cha kushangaza ni kuwa yeye simjui, kwanini mimi ananijua vizuri namna hiyo?.
“Hivi unanifahamu kumbe?” nilimuuliza kabla ya kumjibu swali lake.
“Adam Ahmad Ngudu, una miaka 29 tu na ni mtoto wa nne katika familia ya Marehemu Mzee Ahmad Ngudu, mtoto wa mke wake wa pili baada ya yule wa kwanza bi Maryam Suleiman Kijiko kufariki kwa ajali ya meli mwaka 1984, mtoto pekee wa kiume kwa mama yako. Hujafanikiwa kuoa, lakini una watoto wanne, Rukia, Kulthum, Safia na Latifa.
Mungu amekupa watoto wote wa kike ili aje akuonyeshe vizuri uchungu wa unayoyafanya ukifanyiwa wewe. Na naijua dhamira yako juu yangu, naijua vizuri tu, tena sana. Ila niseme tu, sitaki kuchezewa. Ukiamua kunipenda kweli, niko tayari”. Sikuwa na nguvu ya kusema chochote baada ya hapo. Nilihisi kama naanguka chini na sikujua tena kinachoendelea.
Itaendelea...
Mawasiliano: 0718274130
Sent using Jamii Forums mobile app
MTUNZI: KJM (0718274130)
SEHEMU YA KWANZA
Niliamka mapema kidogo kuliko kawaida yangu. Nikaingia bafuni na kuoga kisha nikarudi chumbani kwangu. Nikavaa nguo harakaharaka kisha nikatoka. Ni mtu ambaye kama hunijui ungedhani nawahi sehemu ya maana kidogo na yenye "dili" la uhakika. Ila haikua hivyo, niliamua tu kuwafurahisha majirani.
Nilipokua nakwenda wala sikuwa nikipajua. Ilikuwa ilimradi nitoke tu. Nikakaa kituoni kusubiri daladala nikiwa na begi langu lenye "laptop" ndani yake. Usafiri ulikuwa wa shida kidogo asubuhi hii, magari mengi yakigeuzia juu kwa juu baada ya kujaza mapema. Ukizingatia mimi nilikua nikiishi ndani kidogo, ilihitaji subira ya hali ya juu kupata gari kwa wakati ule ambao wengi walikua wakigombania kuwahi makazini mwao.
Mbali na mimi, na abiria wengi pale kituoni, pembeni yangu alikuepo dada mmoja mrefu mweupe, mwenye umbo lilichongoka vizuri. Macho yake yaliyokoleza wanja yalishabihiana sana na sura yake ya upole akikutazama. Mkono wa kulia alishika mkoba wake mdogo mweusi, na wa kushoto alikamata simu ya bei mbaya. Alivalia baibui jeusi lililombana kidogo kiasi cha kukupa uhuru wa kung'amua shepu yake. Manukato yake yalizagaa kituo kizima cha daladala. Baada ya kumthaminisha vizuri, niliona nimsalimie japo mwanzo sikufanya hivyo.
“Habari yako dada?”
Alinitazama, pasi na kujibu chochote. Nilijisikia vibaya sana, kwani abiria kadhaa walinigeukia kutazama nani aliyesalimia pasi na kupewa jibu. Nilifadhaika.
“Assalam alykum...” Nilisema tena kumuelekea yule dada, safari hii nikimtazama machoni.
“Waalykum Salaam..” Alijibu huku akitabasamu. Akanifanya nikashangaa zaidi.
“Unaonaje tukatembea tu hadi pale barabara kubwa ambapo magari ni ya uhakika? Unajua sio mbali kutokea hapa”. Niliona nitumie fursa ya lile tabasamu.
“Sawa, twende”. Alinijibu na kunifanya nishangae zaidi. Licha ya kumpa hilo wazo, lakini sikutegemea alikubali bila kusema chochote, nikijaribu kuangalia na alivyoanza na mimi. Ila nikaungana nae na kuondoka mdogo mdogo kuelekea barabara kuu ambapo ni mwendo za zaidi ya dakika 15 ukitembea kwa miguu.
“Adam, kwanini unapenda sana wanawake?” Aliniuliza swali hili hatua kumi tu toka tulipoanza safari. Nilikua sijaongea chochote, na nilipanga swali langu la kwanza liwe kuulizana majina, lakini yeye alionekana kunifahamu vizuri. Maswali kichwani mwangu yakawa mengi sana kuliko kawaida.
Ni kweli naitwa Adam, na ni kweli sifa ya kupenda wanawake ninayo, tena sana tu. Na hata yeye niliamua kumuongelesha kwa sababu hiyo. Ila cha kushangaza ni kuwa yeye simjui, kwanini mimi ananijua vizuri namna hiyo?.
“Hivi unanifahamu kumbe?” nilimuuliza kabla ya kumjibu swali lake.
“Adam Ahmad Ngudu, una miaka 29 tu na ni mtoto wa nne katika familia ya Marehemu Mzee Ahmad Ngudu, mtoto wa mke wake wa pili baada ya yule wa kwanza bi Maryam Suleiman Kijiko kufariki kwa ajali ya meli mwaka 1984, mtoto pekee wa kiume kwa mama yako. Hujafanikiwa kuoa, lakini una watoto wanne, Rukia, Kulthum, Safia na Latifa.
Mungu amekupa watoto wote wa kike ili aje akuonyeshe vizuri uchungu wa unayoyafanya ukifanyiwa wewe. Na naijua dhamira yako juu yangu, naijua vizuri tu, tena sana. Ila niseme tu, sitaki kuchezewa. Ukiamua kunipenda kweli, niko tayari”. Sikuwa na nguvu ya kusema chochote baada ya hapo. Nilihisi kama naanguka chini na sikujua tena kinachoendelea.
Itaendelea...
Mawasiliano: 0718274130
Sent using Jamii Forums mobile app