Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

nina miaka miwili JF naingia kwa simu na sijawahi kumpa mtu like shauri ya uwezo wa simu yangu.
unavyosema mtumiane pm ma likers huoni kuwa unatuonea?

Ooooops m so sorry i was just kiddin' trust me i ddnt mean it,samahani tena km nimekukwaza.
 
Hadithi ya kusisimuwa mimba ya jini-13-

ILIPOISHIA:

Aliushangaa uwezo wa Shehna wa kuelewa vitu vingi vinavyoonekana na vilivyojificha. Alikuwa

amefanya siri ambayo hata mkewe na watu wengi hawakuijua kama ana nyumba ndogo. Lakini

yeye aliijua bila kumwambia, alijiuliza ni nani kwenye uganga hayupo kwa vile alionekana

mwanamke mrembo tena mwenye kujipenda.


SASA ENDELEA...


Tofauti na waganga wengi ambao wengi wao huwa hawajipendi, mavazi yao huwa ya kujiachia wala hawajui mapambo na manukato.
"Sasa Shehna ni nani...au jini? Ha...hapana huko nimefika mbali," Mustafa alijiuliza na kukataa mwenyewe.
"Mbona jana niliota nimelala naye sehemu nzuri lakini nilipoamka nilijikuta nipo nyumbani kwangu? Na Shehna alirudi saa ngapi na kwa nini hakuniamsha mpaka niliposhtuka asubuhi na kujikuta nimetumika kutokana na kufanya naye mapenzi ya ndotoni.

"Mmh! Shehna mbona anataka kunipa mtihani mzito, anataka nizae naye kwa ahadi ya kumpatia mtoto kupitia kwa mke wangu. Sasa mbona ametaka azae yeye kwanza? Mmh! Kazi ipo."
Alijikuta amefika hospitali bila kupata jibu kitu kinachomtatiza kuhusu Shehna. Aliingia hospitali na kwenda chumba alicholala mkewe, alimkuta akiwa amejiandaa kutoka baada ya kupewa ruhusa mapema.

"Yaani mume wangu unajua naumwa unaniacha mpaka saa hizi?" Husna alimuuliza kwa hasira.
"Tabia hii imeanza lini, hata salamu unafikia kunilaumu, ningekufa ungefurahi?" Mustafa alijibu kwa hasira.
"Ufe na nini?"
"Kwa vile hukutaka kujua haina muhimu, unaendeleaje?" Mustafa naye alikuwa mkali kwa mkewe.

"Nisamehe mume wangu nilichanganyikiwa baada ya kuchelewa kukuona wivu uliniingia, ulipatwa na nini mume wangu?"
"Ilitakiwa tusalimiane tujuliane hali kisha tuzungumze mambo mengine."
"Ni kweli, nisamehe mume wangu nimekosa wivu wakati mwingine ugonjwa."
"Nimekukataza mara ngapi sipendi wivu wa kijinga, kila siku umekuwa ukiniona akili yangu unawaza ujinga."

Mustafa alimjia juu mkewe kwa vile alikuwa amepata nafasi, naye alikuwa amechoka na wivu wa kijinga wa mkewe ambao uligeuka kero kitu kilichosababisha kuanzisha uhusiano na mwanamke ambaye mkewe alimshtumu anatembea naye. Mwanamke huyo ilitokana na kushtumiwa na mkewe kwa hisia bila ukweli.
Kwa hasira alifanya kweli kwa kutembea na yule mwanamke ambaye baadaye alimfanya nyumba ndogo na kumuhamisha mtaa ule na kwenda kumpangia sehemu nyingine na kuendeleza mapenzi kwa siri.
Siri ile aliijua peke yake hata rafiki yake hakujua kama ana nyumba ndogo, lakini alishangaa Shehna kuijua.
"Mume wangu huna dogo, nimekosa nisamehe."

"Sawa, vipi unaendeleaje?"
"Namshukuru Mungu sijambo japokuwa mwili hauna nguvu."
"Pole mke wangu, wakati nakuja kuna mwendesha pikipiki alijigonga kwenye gari langu, watu wakajua nimemgonga wakataka kunipiga lakini askari wa barabarani alifika na kuniokoa," Mustafa alitengeneza uongo ili kumpoza mkewe.
"Jamani pole mume wangu!" Husna alisema kwa sauti ya huruma.

"Asante."
Mustafa alimchukua mkewe na kurudi naye nyumbani, alipofika alijikuta akitaka kujua kipi kilimfanya akaidi amri ya Shehna. Baada ya kutulia kwa muda alimsemesha mkewe.
"Mke wangu."
"Abee, mume wangu."
"Kipi kilichokufanya umuue mtoto wangu?"

"Mume wangu kupima ujauzito ni kumuua mtoto?" Husna alishtuka.
"Shehna alituambia nini?"
"Mume wangu utaamini vipi una ujauzito bila kupima?" Husna alijitetea.
"Si alitukataza?"

"Ndiyo! Lakini bado nilishindwa kumuamini, mume wangu kwanza Shehna ni nani mbona masharti yake ya ajabuajabu?"
"Mke wangu tumehangaika sehemu ngapi tumepewa masharti mangapi tuliyoyatekeleza, yaani hili ndilo umeliona gumu?"
"Mi nimechoka kila siku masharti magumu."
"Ha! Mke wangu umeweza kulala makaburini kutafuta mtoto, umeona kazi kutotumia dawa za kizungu ikiwa hali yako ilikuwa nzuri?"



Itaendelea kesho Wakati kama huu ..................
 
Hadithi ya kusisimuwa mimba ya jini-14-

ILIPOISHIA...JANA
"Mke wangu tumehangaika sehemu ngapi tumepewa masharti mangapi tuliyoyatekeleza, yaani hili ndilo umeliona gumu?"
"Mi nimechoka kila siku masharti magumu."
"Ha! Mke wangu umeweza kulala makaburini kutafuta mtoto, umeone kazi kutotumia dawa za kizungu ikiwa hali yako ilikuwa nzuri?"
SASA ENDELEA...


"Mume wangu mimi nina wasiwasi huyu mwanamke si mwanadamu!"

"Mke wangu shida yetu mtoto au kujua Shehna ni mtu au jini?"
"Mi simuelewielewi."
"Mke wangu Shehna si jini ni mwanadamu pia si mganga."
"Ni nani?"
"Nimekuambia mtu."
"Kama si jini wala mganga ni nani mbona unataka kutusaidia?"
"Yule dada alipatwa na tatizo kama letu kuna siku nilimsikia akizungumza na mtu jinsi alivyohangaika kutafuta mtoto na kufanikiwa kupata. Nilivutiwa na habari zake na kumuomba anisaidie. Aliahidi kunisaidia na ndicho alichotusaidia, sasa mke wangu kipi kilichokutuma kuniulia mwanangu?" Mustafa alimuuliza akiwa amemkazia macho mkewe.
"Mume wangu sikujua," Husna alikuwa mpole.
"Sasa tutafanya nini? Lazima Shehna tumemuudhi tutafanyaje, kumbuka mke wangu tumehangaika sehemu ngapi hatukuona dalili za mimba hata siku moja. Lakini dawa ya Shehna siku moja na mimba juu."
"Dah! Sijui itakuwaje ukimuona naomba uniombee msamaha, nipo radhi kufuata masharti yoyote atakayonipa."
"Mmh! Sijui!"
"Mume wangu tusitake kujihukumu, najua lazima atapiga simu, naomba umweleze aje nyumbani ili nimuombe msamaha au nimfuate popote."
"Sawa nikimuona au kunipigia simu nitafanya hivyo."
Mustafa alimuaga Husna na kwenda kazini kwa vile alichelewa kutokana na kumfuata mkewe hospitali.
***
Mustafa baada ya kufika ofisini, alijawa na mawazo kuhusiana na matukio yote yaliyokuwa yakimtokea. Bado alikuwa njia panda kutokana na Shehna mwanamke mrembo aliyeonesha mapenzi mazito kwake. Lakini mambo yake yalionekana kama yana muujiza yaliyokuwa kila siku yanamstaajabisha.
Alijiuliza alimjulia wapi mpaka kumpenda kiasi kile, kutokana na mavazi na vito vyote alivyovaa vilikuwa vya thamani kubwa sana. Ilionesha anatoka katika familia yenye uwezo mkubwa sana. Alipanga akikutana naye amuulize vizuri ajue alimuonea wapi na kipi kilichomfanya ampende na kupelekea kutaka kuzaa naye na si mwanaume mwingine.
Sara akiwa bado yupo katika dimbwi la mawazo, sekretari wake aliingia ofisini na kushangaa kumkuta bosi wake amezama kwenye mawazo. Toka aingie ilikuwa ilimeta saa moja bila kugusa kitu zaidi ya kuzama kwenye mawazo. Alimwita na kumfanya ashtuke.
"Vipi bosi mbona upo mbali kimawazo?"
"Wee acha tu, vipi unasemaje?" alijibu huku akifuta mikono usoni na kujinyoosha kama mtu mwenye usingizi au aliyechoka sana.
"Nimekupigia simu ya mezani nashangaa inaita bila kupokelewa, naingia ndani naona upo kwenye dimbwi la mawazo. Unajua bosi siku hizi sikuelewi kabisa inaonekana hapo sawa."
"Nipo sawa, ulikuwa unasemaje?" Mustafa alijibu huku akijiweka sawa kitini na kuiweka sawa Laptop iliyokuwa juu ya meza.
"Kuna mgeni wako."
"Duh! Akili yangu haijakaa sawa mwambie arudi baadaye," alijibu huku akifungua kazi kwenye desktop.
"Lakini mgeni unamjua?"
"Kwani nani?"
"Yule dada mrembo."
"Ooh! Kumbe Shehna mwambie apite."
"Unaona!" Sara alisema huku akitabasamu na kutoka nje.
Mustafa alishtuka na kushangaa kumfuata ofisini ikiwa walilala pamoja na kuachana muda mfupi. Akiwa ameinama alishtuliwa na harufu ya manukato na sauti tamu ya Shehna.
"Asalamu aleykum Mustafa."
"Waleykum salam Shehna."
Alinyanyua uso na kukutana na Shehna akiwa katika vazi la hijabu iliyomziba mwili mzima. Baada ya kuketi aliiondoa nikabu iliyomziba uso na kufanya aonekane vizuri kisha alitikisa nywele zake nyingi nyeusi na kufanya zichanue kama ua huku tabasamu mwanana akilichanua na kumfanya Mustafa kujiona kama yupo ndotoni.
Alitulia na kumtazama Mustafa aliyekuwa ametulia kama mtu aliyekuwa akitazama picha nzuri na kuitikia kama ameitwa.
"Abee mpenzi," Shehna aliitikia bila kuitwa kitu kilichomshtua Mustafa na kumuuliza:
"Shehna mbona unaitikia? Sijakuita."
"Mustafa uniite mara ngapi?"Shehna alimtazama Mustafa usomi huku macho yake makubwa kidogo ya kusinzia yaliyopakwa wanja na kufanya azidi kupendeza. Hakika Shehna alikuwa mrembo wa warembo.
"Haki ya nani Shehna sijakuita," Mustafa alijitetea kwa kuamini toka aachane naye hajapiga simu wala kuonana naye.
"Huna kitu unachotaka kuniuliza?" Shehna alimuuliza huku amemkazia macho ambayo yalizidisha uzuri wake.

Itaendelea Kesho Wakati kama huu
 
Alhaji mzimi hakuna hadithi uliyoileta vizuri kama ile jini wa daraja la selenda ilikwenda faster, lakini hizi nyengine mateso kaka. Kama unatugawia dozi ya malaria!
 
Back
Top Bottom