Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

Hadithi ya kusisimuwa mimba ya jini-30-

ILIPOISHIA:
"Zile sauti za kutisha zilizidi kunisogelea nikaona kama nitazubaa basi nitakufa. Nilijilazimisha kukimbia huku nimeshika mkono kwenye mbavu. Nilikwenda hivyo kwa kuchechemea mpaka nilipotokea kwenye mti mkubwa.
SASA ENDELEA...


"Kwa vile nilikuwa nimechoka sana, nilijiegemeza kwenye mti mkubwa pembeni ya barabara, pamoja na alfajiri ile kuwa na baridi kali lakini usingizi ulinichukua.
"Mpaka nilipoamshwa na wanakijiji, sikuamini waliponiambia pale ni Kongwa Dodoma na muda ule ni saa nane mchana, kingine kilichonishangaza kuelezwa siku ile ni Jumapili wakati niliondoka nyumbani Jumatatu.

"Yani bado siamini kutembea kwa mguu kwa wiki nzima, kibaya zaidi nakumbuka nilitembea usiku mmoja lakini imeonekana nilitembea wiki nzima. Kama nilitembea wiki nzima, mbona sikuuona mchana zaidi ya usiku tu?" Sara alihoji huku machozi ya uchungu yakimtoka.
"Dada hiki ni kituko yani lazima uende kanisani ukaombewe, lazima watakuwa ni wachawi tu walikuchukua."

"Na..na..kwe...," Sara alisita kuzungumza baada ya kumuona nguruwe amekaa kwenye kiti alichokaa Happy, alipiga kelele za uoga.
"Mamaa nakufa nguruwe."
"Sara nguruwe yupo wapi?" Happy alimshangaa rafiki yake.
"Si..si...," alituliza macho na kushangaa kumuona aliyekaa mbele yake ni Happy na si nguruwe kama alivyoona..

"Sara upo sawa?" Happy aliamini rafiki yake hayupo sawa.
"Ni..ni..hapana..hapana," Sara alituliza macho yake baada ya kumuona tena nguruwe kwenye kochi hakupiga kelele, alitulia na kufikicha macho ili kupata uhakika kama kweli kilichopo mbele yake ni nguruwe au anaona maruweruwe. Baada ya macho kutulia alimuona tena shoga yake Happy wala si nguruwe.
"Happy naomba nipumzike, siko vizuri sijielewi kabisa."

"Sawa dada lakini kwanza nenda ukaoge ili kuufanya mwili upumue."
"Sawa," Sara alisema huku akivua nguo alizokuja nazo na kuchukua taulo ili aende bafuni.
Alichukua sabuni na mswaki kisha alitoka nje na kumuacha shoga yake akimfanya usafi wa chumba. Sara alielekea nje alipofika mlangoni alisita kutoka baada ya kuona nguruwe wamejaa uani. Alizidi kushangaa na kumwita Happy kwa sauti.
"Happy njoo."
Happy aliacha kufanya usafi na kusogea mlangoni.
‘Vipi?"
"Eti nje unaona nini?"
"Kawaida, kwani umeona nini?"
"Nguruwe."
"Nguruwe?" Happy alishtuka.

"Hebu ngoja," Sara alisema huku akipekecha macho na kuona wapo wapangaji wenzake na si nguruwe.
"Mmh! Mbona mwaka huu wangu."
"Shoga kuna umuhimu twende kanisani ukaombewe."
"Ngoja nikaoge."
Sara alikwenda hadi bafuni na kuoga kisha alirudi ndani bila hali ile kumtokea tena. Kwa vile alikuwa amechoka sana, alipanda kitandani na usingizi mzito ulimchukua.
****
Siku ya pili Sara alidamka mapema na kuoga kisha alitoka kwenda kazini kwa kumuaga shoga yake Happy. Happy alimuuliza alivyolala.
"Vipi umelala salama?"
"Namshukuru Mungu nimelala salama, wacha niwahi kazini japo sijui bosi wangu kama atanielewa."
"Atakuelewa tu kwani kilichotokea si cha kawaida."
"Mmh! Ngoja niwahi."
"Mi nilikuwa na wazo."
"Wazo gani?"
"Nilikuwa na wazo la kwenda kwanza kanisani ukaombewe pepo mchafu."
"Wazo zuri lakini lazima nifike kwanza ofisini nijue hatima yangu ndipo twende huko kanisani."
"Basi ukirudi jioni tutapanga."
"Sawa."
Sara aliagana na shoga yake na kuwahi kazini kama kawaida kwa kuwahi ili afanye usafi kabla bosi wake hajafika.


Je, nini kitatokea? Kesho wakati kama huu itaendelea....
 

Ndugu mzizimkavu umerudia hii sehemu...cross check tena kwenye server yako!!!
 

we jamaa ni kumazan
 
Hadithi ya kusisimuwa: Mimba ya jini-31-


ILIPOISHIA:
"Wazo zuri lakini lazima nifike kwanza ofisini nijue hatima yangu ndipo twende huko kanisani."
"Basi ukirudi jioni tutapanga."
"Sawa."
Sara aliagana na shoga yake na kuwahi kazini kama kawaida ili afanye usafi kabla bosi wake hajafika.
SASA ENDELEA...

Mlinzi alimpa ufunguo kama kawaida, alifungua ofisi na kushtuka kuikuta safi imeisha safishwa. Hali ile ilimshtua na kumfanya atoke nje mpaka kwa mlinzi na kumuuliza;

"Eti nani kafanya usafi?"
"Wapi?"
"Ndani ya ofisi?"
"Wewe ndo wa kwanza kuja sijamuona mtu yeyote."

"Kwa...kwa niiii toka nilipoondoka nani alikuwa akifanya usafi?"
"Kwani da Sara ulienda wapi?"
"John si muhimu kujua, nijibu swali langu."

"Toka uondoke sijawahi kumuona mtu akifanya usafi, nakumbuka siku ambayo wewe hukuja bila taarifa nilitaka kwenda kufanya usafi lakini bosi alinikataza, tokea siku hiyo sijamuona mtu akifanya usafi."
"Ina maana toka niondoke hakuna mtu uliyemuona anafanya usafi?"
"Sijawahi kumuona."

"Mbona ofisi inaonesha imefanyiwa usafi muda si mrefu tena wa hali ya juu?"
"Basi majini ndiyo yamefanya usafi," mlinzi alisema kwa utani.
"John na wewe umeligundua hilo?"
"Lipi?"

"La kuwepo na jini ofisini?"
"Mi nimesema tu, hilo jini lifanye usafi kwa ajili gani?"
"Kama mimi nilikuwa sifanyi usafi, basi nani amefanya?"
"Mmh! Labda bosi."

"Nataka kukuambia hapa kuna mchezo, unamjua yule mwanamke?"
"Mwanamke gani?"
"Yule mrembo anayekujaga ofisini."
"Ndiyo."

"Yule nina wasiwasi siyo mtu wa kawaida."
"Una maanisha nini?"
"Mimi simwelewi huenda ni jini!"
"Jini? We acha mambo ya ajabu angekuwa jini tungemuona?"
"Nakwambia ipo siku utakubaliana na mimi."

"Kwa hiyo bosi wateja wake wengine ni majini?"
"Hebu kwanza nikuulize?"
"Uliza."
"Tangu niondoke yule mwanamke kaja mara ngapi?"
"Kwa kweli sijamuona."

"Muongo!"
"Kweli."
"Basi we subiri kama ni yeye nitakomeshana...na...na,"Sara alinyamaza baada ya kuliona gari la bosi wake likisimama getini.

Hakutaka kuongeza neno alichepua mwendo kuwahi ofisini, alijisikia vibaya bosi wake kumkuta eneo lile badala ya ofisini. Lakini alipanga kujitetea alikuwa akimuuliza kitu mlinzi.
Mustafa toka akiwa ndani ya gari alishtuka kumuona Sara, baada ya kupaki gari alielekea ofisini na kupokewa na Sara kama ilivyokuwa kawaida na kupeleka vitu ndani.

Wakati wa kupokelewa alitaka kukataa lakini hakuona sababu ya kukataa, alimuacha apokee lakini alitaka maelezo ya kina atakapomuuliza ili aendelee na kazi lakini kinyume na hapo alipanga kumfukuza kazi kwani tangu aondoke hakukuwa na pengo lolote.
Baada ya kutulia kwa muda Sara aliingia ofisini kwa bosi wake akiwa hajiamini na kufika kusimama mbele ya bosi wake. Mustafa aliacha kusoma gazeti la siku ile na kunyanyua uso wake kumtazama.
"Shikamoo," Sara alimuamkia kwa kupiga magoti.

Ilikuwa mara ya kwanza Sara kumuamkia kwa heshima vile jambo ambalo hakuwahi kulifanya siku za nyuma. Mustafa alijikuta akimshangaa Sara kwa kitendo kile, wakati huo Sara alishtuka kuona aliyekaa mbele yake si bosi bali nguruwe. Alituliza macho ili kupata uhakika.
Hakukuwa na mabadiliko zaidi ya kuona nguruwe amesimama kwenye kiti cha bosi wake akichezesha pua. Alikaza macho kuangalia kama alichokiona ni kweli au maruweruwe. Bado hali ilibakia ileile ya kumuona nguruwe mbele yake, alipekecha macho ili kuikataa hali ile kwa kuamini yale yalikuwa maruweruwe kama yaliyomtokea jana yake.

Itaendelea kesho wakati kama huu....
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…