Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

Hadithi yako hinahu binafsi. Kwa nn washiliki wote ni waislam hina mahana sie ndio tuna majini na tunapenda zinaa hacha ukafiri wataje makafiri wezio .pili hakuna jini hayependa zinaa huyo hatakuwa jini kafiri kama ww

Povu jiingi bwana sheb! Hii ni hadithi kijana tuliza munkali.
Yaelekea unaijua sana elimu ya hawa viumbe majini ndiyo maana hujui kutumia silabi na maneno.
Nenda kaungane na Boko Haram!!
 
Hadithi yako hinahu binafsi. Kwa nn washiliki wote ni waislam hina mahana sie ndio tuna majini na tunapenda zinaa hacha ukafiri wataje makafiri wezio .pili hakuna jini hayependa zinaa huyo hatakuwa jini kafiri kama ww



Wewe si mzima halafu nadhani umepotea njia.
 
Leo episode imekuwa fupi sana mwe!big up sana!
 
Hadithi yako hinahu binafsi. Kwa nn washiliki wote ni waislam hina mahana sie ndio tuna majini na tunapenda zinaa hacha ukafiri wataje makafiri wezio .pili hakuna jini hayependa zinaa huyo hatakuwa jini kafiri kama ww

Jamani hii likizo haijaisha watoto warudi skuli wanatuletea nzi
 
We makato nn? Weka hadisi kama uanataka pesa tukichangie wacha kututesa hivi bana aahhhh
 
Kama mojawapo ya hadithi zilimo ndani ya Alf Lela U Lela. Big up sana mkuu.
 
Hadithi ya kusisimuwa mimba ya jini-26-

ILIPOISHIA:
Kwa vile mke wa Mustafa hakupakwa mafuta ya kumlaza, sauti ya kulalamika kimapenzi ilimshtua usingizini.
SASA ENDELEA...


Alipoangalia pembeni yake alimuona mumewe akifanya mapenzi na mwanamke mzuri wa Kiarabu, wote walikuwa katikati ya tendo. Alitulia kwa muda na kujiuliza alichokiona ni kweli au anaota.

Alikaa kitako na kupekecha macho yake kama kweli amelala au yupo macho, akili yake ilimweleza hakulala bali yupo macho na anachokiona ni kitu cha kweli wala si cha ndotoni.
Alijiuliza yule ni mwanamke gani asiye na woga aliyeingia ndani mwake bila hofu, alijiuliza tabia ile ya mumewe kuingia na mwanamke ndani na kufanya naye mapenzi kitanda wanacholala bila woga, imeanza lini?
Wakati akiwaza vile, Shehna alishtuka baada ya akili yake kutambua mke wa Mustafa ameamka na kuangalia kilichokuwa kikiendelea pembeni yake.
Alijibadili ghafla na kutoweka kitandani na kumuacha Mustafa akilalamika kwa kumwita jina lake.
“Shehna mpenzi unaenda wapi?”
Shehna hakujibu, alisogea pembeni ya mke wa Mustafa na kumpuliza usoni, usingizi mzito ulimchukua Husna na kurudi kitandani kulala.

Baada ya kulala, Shehna alimuuliza Mustafa aliyekuwa hajui nini kilichokuwa kikiendelea.
“Mustafa umefanya nini?”
“Kuhusu nini mpenzi?”
“Kwa nini hukumpaka mafuta mkeo?”
“Nilimpaka.”
“Muongo! Tutamwambia nini mkeo ikiwa ameona kila kitu?”
“Kwani aliamka?”
“Ameamka na ameona kila kitu.”
“Mungu wangu!” Mustafa alishika mikono kichwani.
“Basi mi naondoka na hutaniona tena katika maisha yako,” Shehna alisema kwa hasira huku akielekea alipoweka nguo zake.
“Usifanye hivyo mpenzi, nakuhitaji kuliko kitu chochote, inawezekana uchovu ulisababisha nipitiwe. Naomba unisamehe sana.”
“Mustafa nakupenda sana, lakini masharti yangu ya kuendelea kuwa na wewe yatakuwa magumu sana kuliko mwanzo na nina imani utayashindwa.”
“Nakuahidi kuyatekeleza yote.”
“Kweli?”
“Kweli kabisa.”
“Unajua nakupenda?”
“Tena sana.”
“Kesho mkeo lazima atakuuliza kuhusiana na alichokiona usiku huu kwa vile aliendelea na usingizi atataka ukweli kutoka kwako. Wewe kataa kwa vile hana uhakika kwa kile alichokiona kama ni kweli au ndoto.”
“Sawa nitafanya hivyo.”
“Kwa vile amelala tuendelee na dozi ya mwisho lakini kuanzia kesho tunabadili mfumo.”
“Sawa mpenzi nipo radhi kwa lolote.”
Walikwenda kuoga na kurudi kumalizia dozi ya mwisho kisha Shehna aliondoka na kumuacha Mustafa usingizini.
***
Husna alikuwa wa kwanza kuamka mumewe alikuwa bado amelala, alimuangalia na kujikuta akivuta kumbukumbu ya usiku na kujiuliza alichokiona usiku kilikuwa kweli au ndoto kwa vile toka aolewe na Mustafa, hakuwahi kutokewa na tukio kama lile kwa sababu alimuamini sana mumewe kwa uaminifu wa ndoa yao kwa kipindi chote pamoja na matatizo yote, hakuwahi kumdharau wala kumsaliti.
Kwa akili ya kawaida aliamini kabisa aliamka usiku na kukuta mumewe akifanya mapenzi na mwanamke wa kiarabu. Lakini kilichomshtua mbona ameamka asubuhi kutoka usingizini?
Kila lililokuja mbele yake lilimchanganya, ili apate jibu la kitendawili chake aliamua kumuamsha mumewe. Baada ya kumtikisa kwa muda huku akimwita kwa jina lake, Mustafa alishtuka usingizini na kumgeukia mkewe.
“Vipi?” alimuuliza huku akilazimisha macho kufumbuka.
“Mume wangu hebu amka.”
“Kuna nini?”
“Si uamke,” Husna alisema kwa sauti kali kidogo.
Mustafa aliamka na kukaa kitako ili amsikilize mkewe.
“Mume wangu,” alianza kwa kumwita.
“Naam.”
“Kuna kitu kimetokea sijui ni kweli au ndoto.”
“Kitu! Kitu gani?” Mustafa alijifanya kushtuka.
“Kuna kitu nimekiona usiku, kimenichanganya sana.”
“Kitu gani?” Mustafa alimuuliza huku akifikisha macho yake na kupiga miayo ya uchovu wa kulala.
Husna alimweleza mumewe kila kitu alichokiona ambacho yeye aliamini haikuwa ndoto. Kwa vile alielezwa na Shehna kilichotokea na nini ajibu, alimwambia mkewe.
“Kwa akili ya kawaida kitu hicho kinaweza kufanyika?”
“Hata mi nashangaa, lakini nakumbuka niliamka na kukaa kabisa.”


Je, nini kitafuatia hapo? Fuatilia baadae basi
 
Hadithi yako hinahu binafsi. Kwa nn washiliki wote ni waislam hina mahana sie ndio tuna majini na tunapenda zinaa hacha ukafiri wataje makafiri wezio .pili hakuna jini hayependa zinaa huyo hatakuwa jini kafiri kama ww
Sasa

wewe ulitaka Washiriki wawe akina nani wakristo au wayahudi? Acha kuleta Udini hapa mimi pia Muislam tena Maalim ninaitwa sasa

nimekuzidi hata wewe kielimu usilete Mambo ya Udini hapa kama huna kitu cha kuchangia bora usiandike kitu humu ndani tafadhali

Usiniharibie Hadithi yangu . Unajuwa ni nini maana ya neno hadithi? kama hujuwi nenda shule kwanza kamuulize Mwalimu wako ni nini

Maana ya neno Hadithi kisha ndio uje hapa kuleta ushindani wako wa mambo ya Udini nyamaza nina kuheshimu sana na wewe pia

niheshimu mimi asante.
 
Hadithi ya kusisimuwa mimba ya jini-27-

ILIPOISHIA:
Kwa vile alielezwa na Shehna kilichotokea na nini ajibu alimwambia mkewe.
"Kwa akili ya kawaida kitu hicho kinaweza kufanyika?"
"Hata mi nashangaa, lakini nakumbuka niliamka na kukaa kabisa."
SASA ENDELEA...


"Baada ya kukaa nini kiliendelea?"
"Sikumbuki zaidi ya kushtuka alfajiri na kujikuta nimelala."
"Sasa wasiwasi wako nini?"
"Ndipo hapo ninapo changanyikiwa kilikuwa nini."

"Hebu achana na ndoto, hivi kweli nilete mwanamke ndani na kufanya naye mapenzi kitanda tunacholala, imeanza lini?" Mustafa alizidi kujifanya kumshangaa mkewe.
"Hata mi namshangaa."
"Hebu achana na ndoto za kijinga."
"Basi samahani mume wangu kama nimekukwaza."

"Walaa, una haki ya kuniuliza chochote."
Wakiwa katikati ya mazungumzo simu ya Mustafa iliita, alipoangalia ilionesha inatokwa kwa Shehna. Aliipokea na kuzungumza naye.
"Haloo."
"Haloo, asalam aleykum."

"Waleykum salam."
"Vipi mmeamkaje?"
"Mmh! Salama."
"Kweli?" Shehna aliuliza.
"Kweli."
"Mbona kama mkeo ana tatizo?"
"Sijui ameota nini."

"Ameota nini?" Shehna alijifanya kushtuka.
"Sijui ameniona eti mimi nina fa...fa.."
"Hebu mpe mwenyewe azungumze, acha kung'ata maneno," Shehna alimkata kauli Mustafa.
Mustafa alimpa simu mkewe aliyekuwa bado amesimama pembeni ya kitanda. Husna aliipokea na kuzungumza.

"Asalam aleykum."
"Waleykum salam, eti mpenzi kuna nini?" Shehna alimuuliza kwa sauti ya upole.
Husna alimweleza kama alivyomweleza mumewe kilichotokea usiku. Baada ya kumsikia alisema:
"Mpenzi hizo ni ndoto ambazo huvunja ndoa nyingi kwa vile mtu huota ukiwa macho na kuweza kuamini ni jambo la kweli. Hizo ni ndoto tu, lakini mumeo akirudi kazini atakupatia dawa ya kujipaka wakati wa kulala haitakutokea tena."

"Nitashukuru kwa kweli ilinishtua sana."
"Pole mpenzi."
"Asante dada yangu, jamani nina hamu ya kukuona tutaonana lini?"
" Utaniona tu usiwe na wasiwasi hata mimi nina hamu na wewe, unasema uliyemuota akifanya mapenzi na mumeo uliiona sura yake?"
"Ndiyo."

"Kwa mfano akutokee mbele utamjua?"
"Nitamjua nilimuona vizuri sana japo nilikuwa naota."
"Basi mpenzi nikimaliza mizunguko yangu nitakuja utanichoka mwenyewe."
"Walaa labda unichoke wewe."
"Basi mpenzi usiendekeze ndoto."
"Nimekuelewa."

Shehna alimalizia kuzungumza na Husna na kumalizia kuzungumza na Mustafa kisha alikata simu. Mazungumzo yake yalirudisha imani moyoni kwa Husna na kuamini aliyosema Shehna yalikuwa na ukweli mkubwa. Baada ya moyo wake kuamini ile ilikuwa ndoto, alimtayarishia mumewe maji ya kuoga na kifungua kinywa huku moyo wake ukiwa mweupe.
Mustafa baada ya kufungua kinywa alimuaga mkewe na kuelekea kazini, kama kawaida alikuta ofisi imesafishwa. Akiwa ofisini Shehna alimtokea kabla hajaanza kazi na kuzungumza naye sakata la usiku.
"Mustafa nilitaka kukulaumu lakini umenilahisishia kazi, yale mafuta niliyokupa kumpaka mkeo mpe ajipake mwenyewe. Hakikisha unamkumbusha kujipaka kabla hajalala, itatusaidia kumteka bila kujijua."
"Yaani nashukuru sana sijui bila wewe ingekuwaje?"

"Ungekataa tu, lakini lazima angeuliza kwa watu na kutaka kuchimba na kuujua ukweli."
"Unafikiri angeujua ingekuaje?"
"Mmh! Tungejua tifanyeje japo ingetusumbua kidogo."
"Nashukuru sana mpenzi umenisaidia."

"Basi nikuache ufanye kazi."
"Nashukuru."
Shehna aliaga na kuondoka na kumuacha Mustafa akijiandaa kuanza kazi ya siku ile.


Itaendelea tena kesho wakati kama huu inshallah.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…