Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

Hadithi yako hinahu binafsi. Kwa nn washiliki wote ni waislam hina mahana sie ndio tuna majini na tunapenda zinaa hacha ukafiri wataje makafiri wezio .pili hakuna jini hayependa zinaa huyo hatakuwa jini kafiri kama ww

Povu jiingi bwana sheb! Hii ni hadithi kijana tuliza munkali.
Yaelekea unaijua sana elimu ya hawa viumbe majini ndiyo maana hujui kutumia silabi na maneno.
Nenda kaungane na Boko Haram!!
 
Hadithi yako hinahu binafsi. Kwa nn washiliki wote ni waislam hina mahana sie ndio tuna majini na tunapenda zinaa hacha ukafiri wataje makafiri wezio .pili hakuna jini hayependa zinaa huyo hatakuwa jini kafiri kama ww



Wewe si mzima halafu nadhani umepotea njia.
 
Hadithi ya kusisimuwa mimba ya jini-25-

ILIPOISHIAJANA :
Vijakazi na watwana waliingia katika kazi ya usafi iliyochukua dakika tano kila kitu kilikuwa safi ndani. Kilibadilishwa kila kitu na kuwekwa pazia nzuri la halili na kuifanya ofisi ipendeze mara dufu. Baada ya kufanya usafi walipiga magoti mbele ya Shehna na kusema.
SASA ENDELEA…


“Mtukufu mwana wa Mfalme wa jini la bahari ya dhahabu tumemaliza kazi, kama kuna kasoro tupo tayari kwa adhabu yoyote kutoka kwako.”

“Hapana nawamini.”
“Asante mwana wa mfalme.”
Shehna hakuwa na shida ya kukagua kwa kuamini majini walikuwa wakijua usafi kuliko mwanadamu.
“Nimefurahi kwa yenu nzuri, mnaweza kuondoka.”

Kufumba na kufumbua vijakazi na watwana walitoweka na kumuacha Shehna alifurahia hali nzuri ya kupendeza ya ofisi. Alitoka nje na kumwita Mustafa aliyekuwa akizungumza na mlinzi. Alikwenda ndani na kuishangaa ofisi ilivyopendeza tofauti na siku zote.
“Duh! Kazi hii imeifanya peke yako?”
“Umemuona nani akinisaidia?”

“Hongera sana.”
“Asante, ila kama Sara hatatokea na kesho funguo iache mlangoni, nitakuwa nawahi mapema kufanya usafi kabla hujafika mpaka atakaporudi kazini .”
“Nitafanya hivyo.”

“Mustafa mimi si mkaaji ilikuja kukushukuru wa mapenzi yako matamu, hakika leo nimefaidi usichana wangu kwa kupata penzi lililokamilika. Nakuahidi baada ya kushika ujauzito nitakupatia zawadi kubwa sana.”
“Wala usihofu, lakini nina wasiwasi wa kuharibu masharti yako.”
“Wala usiwe na wasiwasi, asubuhi umenilaisishia kufanya mambo yetu bila mkeo kukusumbua. La muhimu kufanya yote kama niliyokuelekeza.”

“Nitafanya hivyo.”
“Basi nikuache uendelee na kazi.”
“Nashukuru.”
Walikumbatiana kisha Shehna aliondoka na kumuacha Mustafa alimsindiza kwa macho.
***
Wiki nzima ilikatika bila kuonekana kwa Sara huku Shehna akiendelea kufanya usafi kila siku na kuifanya ofisi izidi kupendeza. Kwa hali ile ilifikia hatua ya Mustafa kuomba Sara isirudi tena kutokana na usafi uliokuwa ukifanywa na Shehna uliifanya ofisi yake isifikiwe kwa kila aliyeingia na kutaka kupatiwa mtu mwenye uwezo wa kufanya usafi kama wa ofisini kwake.

Wakati wote huo kila siku Shehna alikwenda nyumbani kwa Mustafa na kufanya naye mapenzi kitandani kwake huku mkewe akiwa amepitiwa usingizi. Siku zote alifuata masharti aliyopewa kuyafanya kabla ya kulala. Zoezi kubwa kwake lilikuwa kumpaka mafuta mkewe ambayo humfanya alale mpaka asubuhi bila kugeuka na kuacha wafanye mambo yao bila yeye kujua kinachoendelea.
Mustafa alifanya vitu vyake siku zote kwa umakini mkubwa kwa vile mkewe hakuweza kukutana naye tena kimwili baada ya kuelezwa na Shehna ili aweze kupata mtoto huku akiendelea kutumia dawa alizopewa. Hata kulala sehemu ya ukutani hakulazimishwa kwa vile lilikuwa moja ya masharti ya dawa.
Siku zote alifanya kama alivyoelekezwa, lakini siku moja alirudi nyumbani akiwa amechoka sana na kusahau kumpaka mafuta mkewe kwa kuamini aliisha mpaka. Usiku kama kawaida Shehna aliingia ndani na kunyanyua Mustafa na kwenda naye bafuni kuoga baada ya kuoga alirudi kitandani na kuanza kuandaana kisha waliingia kwenye tendo.
Hatua ya awali iliisha kila mmoja alifurahia penzi la mwenzake kisha walipumzika kwa muda ili kujiandaa kwa hatua nyingine. Shehna kama kawaida alimpa Mustafa maji ya kunywa yaliyomrudishia nguvu na kurudi tena bafuni kuoga na kuingia hatua ya pili. Mapenzi yalipopamba moto Shehna aligugumia kimapenzi kwa kuusifia uwezo wa Mustafa kimapenzi.
Kwa vile mke wa Mustafa hakupakwa mafuta ya kumlaza, sauti ya kulalamika kimapenzi ilimshtuka usingizini.


Itaendelea Kesho Wakati kama huu
Leo episode imekuwa fupi sana mwe!big up sana!
 
Hadithi yako hinahu binafsi. Kwa nn washiliki wote ni waislam hina mahana sie ndio tuna majini na tunapenda zinaa hacha ukafiri wataje makafiri wezio .pili hakuna jini hayependa zinaa huyo hatakuwa jini kafiri kama ww

Jamani hii likizo haijaisha watoto warudi skuli wanatuletea nzi
 
We makato nn? Weka hadisi kama uanataka pesa tukichangie wacha kututesa hivi bana aahhhh
 
Hadithi ya kusisimuwa mimba ya jini-26-

ILIPOISHIA:
Kwa vile mke wa Mustafa hakupakwa mafuta ya kumlaza, sauti ya kulalamika kimapenzi ilimshtua usingizini.
SASA ENDELEA...


Alipoangalia pembeni yake alimuona mumewe akifanya mapenzi na mwanamke mzuri wa Kiarabu, wote walikuwa katikati ya tendo. Alitulia kwa muda na kujiuliza alichokiona ni kweli au anaota.

Alikaa kitako na kupekecha macho yake kama kweli amelala au yupo macho, akili yake ilimweleza hakulala bali yupo macho na anachokiona ni kitu cha kweli wala si cha ndotoni.
Alijiuliza yule ni mwanamke gani asiye na woga aliyeingia ndani mwake bila hofu, alijiuliza tabia ile ya mumewe kuingia na mwanamke ndani na kufanya naye mapenzi kitanda wanacholala bila woga, imeanza lini?
Wakati akiwaza vile, Shehna alishtuka baada ya akili yake kutambua mke wa Mustafa ameamka na kuangalia kilichokuwa kikiendelea pembeni yake.
Alijibadili ghafla na kutoweka kitandani na kumuacha Mustafa akilalamika kwa kumwita jina lake.
“Shehna mpenzi unaenda wapi?”
Shehna hakujibu, alisogea pembeni ya mke wa Mustafa na kumpuliza usoni, usingizi mzito ulimchukua Husna na kurudi kitandani kulala.

Baada ya kulala, Shehna alimuuliza Mustafa aliyekuwa hajui nini kilichokuwa kikiendelea.
“Mustafa umefanya nini?”
“Kuhusu nini mpenzi?”
“Kwa nini hukumpaka mafuta mkeo?”
“Nilimpaka.”
“Muongo! Tutamwambia nini mkeo ikiwa ameona kila kitu?”
“Kwani aliamka?”
“Ameamka na ameona kila kitu.”
“Mungu wangu!” Mustafa alishika mikono kichwani.
“Basi mi naondoka na hutaniona tena katika maisha yako,” Shehna alisema kwa hasira huku akielekea alipoweka nguo zake.
“Usifanye hivyo mpenzi, nakuhitaji kuliko kitu chochote, inawezekana uchovu ulisababisha nipitiwe. Naomba unisamehe sana.”
“Mustafa nakupenda sana, lakini masharti yangu ya kuendelea kuwa na wewe yatakuwa magumu sana kuliko mwanzo na nina imani utayashindwa.”
“Nakuahidi kuyatekeleza yote.”
“Kweli?”
“Kweli kabisa.”
“Unajua nakupenda?”
“Tena sana.”
“Kesho mkeo lazima atakuuliza kuhusiana na alichokiona usiku huu kwa vile aliendelea na usingizi atataka ukweli kutoka kwako. Wewe kataa kwa vile hana uhakika kwa kile alichokiona kama ni kweli au ndoto.”
“Sawa nitafanya hivyo.”
“Kwa vile amelala tuendelee na dozi ya mwisho lakini kuanzia kesho tunabadili mfumo.”
“Sawa mpenzi nipo radhi kwa lolote.”
Walikwenda kuoga na kurudi kumalizia dozi ya mwisho kisha Shehna aliondoka na kumuacha Mustafa usingizini.
***
Husna alikuwa wa kwanza kuamka mumewe alikuwa bado amelala, alimuangalia na kujikuta akivuta kumbukumbu ya usiku na kujiuliza alichokiona usiku kilikuwa kweli au ndoto kwa vile toka aolewe na Mustafa, hakuwahi kutokewa na tukio kama lile kwa sababu alimuamini sana mumewe kwa uaminifu wa ndoa yao kwa kipindi chote pamoja na matatizo yote, hakuwahi kumdharau wala kumsaliti.
Kwa akili ya kawaida aliamini kabisa aliamka usiku na kukuta mumewe akifanya mapenzi na mwanamke wa kiarabu. Lakini kilichomshtua mbona ameamka asubuhi kutoka usingizini?
Kila lililokuja mbele yake lilimchanganya, ili apate jibu la kitendawili chake aliamua kumuamsha mumewe. Baada ya kumtikisa kwa muda huku akimwita kwa jina lake, Mustafa alishtuka usingizini na kumgeukia mkewe.
“Vipi?” alimuuliza huku akilazimisha macho kufumbuka.
“Mume wangu hebu amka.”
“Kuna nini?”
“Si uamke,” Husna alisema kwa sauti kali kidogo.
Mustafa aliamka na kukaa kitako ili amsikilize mkewe.
“Mume wangu,” alianza kwa kumwita.
“Naam.”
“Kuna kitu kimetokea sijui ni kweli au ndoto.”
“Kitu! Kitu gani?” Mustafa alijifanya kushtuka.
“Kuna kitu nimekiona usiku, kimenichanganya sana.”
“Kitu gani?” Mustafa alimuuliza huku akifikisha macho yake na kupiga miayo ya uchovu wa kulala.
Husna alimweleza mumewe kila kitu alichokiona ambacho yeye aliamini haikuwa ndoto. Kwa vile alielezwa na Shehna kilichotokea na nini ajibu, alimwambia mkewe.
“Kwa akili ya kawaida kitu hicho kinaweza kufanyika?”
“Hata mi nashangaa, lakini nakumbuka niliamka na kukaa kabisa.”


Je, nini kitafuatia hapo? Fuatilia baadae basi
 
Hadithi yako hinahu binafsi. Kwa nn washiliki wote ni waislam hina mahana sie ndio tuna majini na tunapenda zinaa hacha ukafiri wataje makafiri wezio .pili hakuna jini hayependa zinaa huyo hatakuwa jini kafiri kama ww
Sasa

wewe ulitaka Washiriki wawe akina nani wakristo au wayahudi? Acha kuleta Udini hapa mimi pia Muislam tena Maalim ninaitwa sasa

nimekuzidi hata wewe kielimu usilete Mambo ya Udini hapa kama huna kitu cha kuchangia bora usiandike kitu humu ndani tafadhali

Usiniharibie Hadithi yangu . Unajuwa ni nini maana ya neno hadithi? kama hujuwi nenda shule kwanza kamuulize Mwalimu wako ni nini

Maana ya neno Hadithi kisha ndio uje hapa kuleta ushindani wako wa mambo ya Udini nyamaza nina kuheshimu sana na wewe pia

niheshimu mimi asante.
 
Hadithi ya kusisimuwa mimba ya jini-27-

ILIPOISHIA:
Kwa vile alielezwa na Shehna kilichotokea na nini ajibu alimwambia mkewe.
"Kwa akili ya kawaida kitu hicho kinaweza kufanyika?"
"Hata mi nashangaa, lakini nakumbuka niliamka na kukaa kabisa."
SASA ENDELEA...


"Baada ya kukaa nini kiliendelea?"
"Sikumbuki zaidi ya kushtuka alfajiri na kujikuta nimelala."
"Sasa wasiwasi wako nini?"
"Ndipo hapo ninapo changanyikiwa kilikuwa nini."

"Hebu achana na ndoto, hivi kweli nilete mwanamke ndani na kufanya naye mapenzi kitanda tunacholala, imeanza lini?" Mustafa alizidi kujifanya kumshangaa mkewe.
"Hata mi namshangaa."
"Hebu achana na ndoto za kijinga."
"Basi samahani mume wangu kama nimekukwaza."

"Walaa, una haki ya kuniuliza chochote."
Wakiwa katikati ya mazungumzo simu ya Mustafa iliita, alipoangalia ilionesha inatokwa kwa Shehna. Aliipokea na kuzungumza naye.
"Haloo."
"Haloo, asalam aleykum."

"Waleykum salam."
"Vipi mmeamkaje?"
"Mmh! Salama."
"Kweli?" Shehna aliuliza.
"Kweli."
"Mbona kama mkeo ana tatizo?"
"Sijui ameota nini."

"Ameota nini?" Shehna alijifanya kushtuka.
"Sijui ameniona eti mimi nina fa...fa.."
"Hebu mpe mwenyewe azungumze, acha kung'ata maneno," Shehna alimkata kauli Mustafa.
Mustafa alimpa simu mkewe aliyekuwa bado amesimama pembeni ya kitanda. Husna aliipokea na kuzungumza.

"Asalam aleykum."
"Waleykum salam, eti mpenzi kuna nini?" Shehna alimuuliza kwa sauti ya upole.
Husna alimweleza kama alivyomweleza mumewe kilichotokea usiku. Baada ya kumsikia alisema:
"Mpenzi hizo ni ndoto ambazo huvunja ndoa nyingi kwa vile mtu huota ukiwa macho na kuweza kuamini ni jambo la kweli. Hizo ni ndoto tu, lakini mumeo akirudi kazini atakupatia dawa ya kujipaka wakati wa kulala haitakutokea tena."

"Nitashukuru kwa kweli ilinishtua sana."
"Pole mpenzi."
"Asante dada yangu, jamani nina hamu ya kukuona tutaonana lini?"
" Utaniona tu usiwe na wasiwasi hata mimi nina hamu na wewe, unasema uliyemuota akifanya mapenzi na mumeo uliiona sura yake?"
"Ndiyo."

"Kwa mfano akutokee mbele utamjua?"
"Nitamjua nilimuona vizuri sana japo nilikuwa naota."
"Basi mpenzi nikimaliza mizunguko yangu nitakuja utanichoka mwenyewe."
"Walaa labda unichoke wewe."
"Basi mpenzi usiendekeze ndoto."
"Nimekuelewa."

Shehna alimalizia kuzungumza na Husna na kumalizia kuzungumza na Mustafa kisha alikata simu. Mazungumzo yake yalirudisha imani moyoni kwa Husna na kuamini aliyosema Shehna yalikuwa na ukweli mkubwa. Baada ya moyo wake kuamini ile ilikuwa ndoto, alimtayarishia mumewe maji ya kuoga na kifungua kinywa huku moyo wake ukiwa mweupe.
Mustafa baada ya kufungua kinywa alimuaga mkewe na kuelekea kazini, kama kawaida alikuta ofisi imesafishwa. Akiwa ofisini Shehna alimtokea kabla hajaanza kazi na kuzungumza naye sakata la usiku.
"Mustafa nilitaka kukulaumu lakini umenilahisishia kazi, yale mafuta niliyokupa kumpaka mkeo mpe ajipake mwenyewe. Hakikisha unamkumbusha kujipaka kabla hajalala, itatusaidia kumteka bila kujijua."
"Yaani nashukuru sana sijui bila wewe ingekuwaje?"

"Ungekataa tu, lakini lazima angeuliza kwa watu na kutaka kuchimba na kuujua ukweli."
"Unafikiri angeujua ingekuaje?"
"Mmh! Tungejua tifanyeje japo ingetusumbua kidogo."
"Nashukuru sana mpenzi umenisaidia."

"Basi nikuache ufanye kazi."
"Nashukuru."
Shehna aliaga na kuondoka na kumuacha Mustafa akijiandaa kuanza kazi ya siku ile.


Itaendelea tena kesho wakati kama huu inshallah.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom