Hadithi ya kusisimua: Jini mauti

Hadithi ya kusisimua: Jini mauti

Hadithi ya kusisimua: Jini Mauti-17

ILIPOISHIA

ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:


“Tulikubaliana vipi?”
“Nimezidiwa mpenzi, naomba unionee huruma.”
Wakati akiniambia hayo, hakuwa ameacha kufanya alichokuwa akikifanya, aliendelea kuudadisi mwili wangu.

Hali iliyoniweka katika hali mbaya na mimi kuanza kutoa miguno.Nilishindwa kumzuia, alionekana kuwa na nguvu, baada ya dakika chache, wote wawili tulikuwa watupu na yeye kuanza kufanya alichotaka kukifanya. Nikaanza kuyasikia maumivu makali chini ya kitovu, mchezo ule sikuuzoea, lakini ghafla huku akiendelea kufanya mchezo huo, nikaanza kumuona akianza kutetemeka huku akigugumia kwa maumivu makali.
“Mudi…” niliita.

Hakunijibu, aliendelea kutetemeka na kugugumia kwa maumivu, mara nikaanza kuyaona macho yake yakibadilika na kuwa mekundu, kwa kweli nilishtuka, sikuamini kile kilichokuwa kikiendelea.

Nikamsukuma pembeni, alizidi kutetemeka zaidi. Niliogopa kile kilichokuwa kimetokea, nikamshika na kuanza kumuita lakini hakuitikia zaidi ya kutetemeka kama mtu aliyekuwa na kifafa, hapohapo akaanza kutokwa na mapovu yaliyochanganyikana na damu mdomoni.

“Mudi…Mudi….” nilimuita lakini hakuitikia, macho yake yakabadilika, yakatoka katika rangi nyekundu na kuwa meupe kabisa, mwili ukakakamaa na wala hakuchukua muda mrefu, akatulia tuli, akawa amekwishafariki dunia.

Nilichanganyikiwa mno, kile kilichokuwa kimetokea kwa Mudi ndicho kilichotokea kwa Thomas kipindi cha nyuma. Sikujua ningefanya nini, nje ya chumba kile kulikuwa na watu wengine, kulikuwa na ndugu zake ambao waliniona wakati nikiingia naye.

Sikujua ningetoka vipi pasipo kugundulika. Kiukweli nilichanganyikiwa kupita kawaida. Nilichokifanya ni kuvaa nguo zangu, ndani hakukuonekana kuwa salama tena, ili niweze kuepuka kesi ya mauaji ilikuwa ni lazima niondokemle chumbani.

Sikutaka kujiuliza sana, nilichokifanya ni kutoka chumbani humo. Kitu kilichonishangaza, niliwaangalia ndugu zake wale, hawakuonekana kama watu waliokuwa wakiniona, nilisogea mpaka pale walipokuwa, nikawaaga lakini wakawa kama watu wasionisikia au kuniona kabisa, nilichokifanya ni kuondoka, tena nikikimbia kwa mwendo wa kasi.

“Nimeua,” nilisema huku nikikimbia, jasho lilikuwa likinitoka.
Nilipofika nyumbani, nikaingia moja kwa moja ndani. Nilikuwa nikilia mno, mama ambaye alikuwa nje akaingia ndani na kunijulia hali kwani alishangazwa na kile kilichokuwa kimetokea, kufika nyumbani usiku tena huku nikikimbia, hakika aliogopa.
“Davina…kuna nini?” aliniuliza huku akionekana kushangaa.

“Niache mama, niache…”
“Niambie kuna nini.”
Sikutaka kumjibu, nililia mno, sikuamini kile kilichokuwa kimetokea kwamba Mudi alikuwa mtu wa pili kufa katika mikono yangu. Hapo ndipo nilipopata picha kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea.

Haikuwezekana watu wawili wafe kipindi walichokuwa wakifanya mapenzi na mimi, nilihisi kulikuwa na kitu ambacho bibi yangu alikuwa akikifahamu.
Usiku wa siku hiyo sikulala, nilibaki nikilia tu. Sikutaka kwenda uwanjani kukutana na wachawi wenzangu zaidi ya kukaa tu nyumbani. Ilipofika usiku bibi na wachawi wengine wawili wakafika chumbani kwangu.

Kitu cha kwanza kabisa kukifanya ni kuviinamisha vichwa vyao mbele yangu kisha kunipongeza kwa kazi niliyokuwa nimeifanya ya kumchukua mtu wa pili na kumpeleka kule kulipokuwa na kundi kubwa la misukule.

“Kwa nini mimi?” niliuliza huku nikilia.
“Wewe ni kiongozi wetu.”
“Ndiyo niue? Sitaki kuua.”

Nilisema huku nikilia mno. Hawakuniambia kitu chochote kile zaidi ya kuondoka. Katika kipindi chote hicho sikuwa nikijua kwamba bibi yangu aliniwekea jini mauti mwilini mwangu.
Je, kilifuatia nini? Usikose mwendelezo wake wiki ijayo.
 
Hadithi ya kusisimua: Jini Mauti-13

ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:

Nyumbani kwao alikuwa yeye na mfanyakazi wa ndani tu, hakukuwa na mtu mwingine. Kweli nikaenda. Akanipokea kwa furaha, mabusu mfululizo, kilichofuata ni kwenda chumbani kwake. Mapigo ya moyo yalinidunda kwa nguvu, niliogopa mno. SASA
ENDELEA?
Sikuwahi kufanya kitendo kile alichotaka tukifanye, kila alipokuwa akiugusa mwili wangu, nilitetemeka sana.
Thomas.
Naam.
Naomba tufanye siku nyingine.?
Kwa nini isiwe leo??
Sijajiandaa.
Hapana! Linaloweza kufanyika leo, lisingoje kesho mpenzi,? aliniambia. Tayari tulibaki kama tulivyozaliwa.
Thomas.
Unasemaje??
Naogopa!
Usiogope, hautakufa.
Ila nitaumia, naomba tufanye siku nyingine.

Siwezi kuvumilia mpenzi! Hata mimi sijawahi, leo ndiyo kwanza siku ya kwanza, aliniambia.
Alionekana kuchanganyikiwa mno, hakutaka kuniacha hivihivi, alichokifanya ni kunilalia kwa juu. Kweli nilianza kusikia maumivu makali chini ya kitovu, maumivu ambayo sikuwahi kuyasikia kabla.

Nilipiga kelele na kuhisi damu ilianza kutoka, Thomas hakuacha, aliendelea kufanya vilevile. Kila nilipomwambia kwamba naumia, aliniambia ningezoea tu, hivyo aliendelea kama kawaida.
Thomas nilimwita jina lake, tayari chozi lilinitoka.
Subiriiii aliniambia huku akiendelea kufanya alichotaka tufanye.
Ghafla, akiwa kwenye hali hiyo nikaanza kumuona akibadilika, akaanza kutetemeka, mwili ukaanza kukakamaa na macho yake kuanza kubadilika rangi na kuwa mekundu.

iliogopa, Thomas alianza kutisha pale kifuani mwangu, nilipoona hivyo, nikamuweka pembeni, mapovu yakaanza kumtoka mdomoni, macho yakabadilika rangi, mboni nyeusi ikatoka na kubaki nyeupe tu.
Aliendelea kutetemeka, akawa kama mtu anayeumwa degedege. Nilimshika na kuliita jina lake lakini aliendelea kuwa vilevile, mapovu yaliongezeka, damu zikaanza kumtoka masikioni, puani na hata kwenye kucha zake.

Kiukweli nilichanganyikiwa mno, sikujua ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea. Nikaanza kuliita jina lake huku nikilia, sikuamini kilichokuwa kikiendelea. Wala hazikupita dakika nyingi, hapohapo Thomas akatulia, akafariki dunia kitu kilichonichanganya mno.
Nilibaki nikitetemeka tu, sikuamini kile kilichokuwa kimetokea, kufariki dunia kwa Thomas, mbele ya macho yangu tena juu ya kifua changu

kulinichanganya mno. Nilibaki kuwa na hofu kubwa, nilijaribu kumwamsha Thomas mahali pale lakini hakutingishika na nilipoyasikiliza mapigo yake ya moyo, yalikuwa yametulia kabisa.

Nikasimama, sikujua kipi nilitakiwa kufanya, nilibaki nikilia lakini nilichokifanya ni kuupiga moyo konde, huo haukuwa muda wa kulia tena, nilitakiwa nifanye kitu ili niweze kuondoka hata kabla wazazi wake hawajafika.

Nikaufungua mlango na kuelekea sebuleni, nilipofika, sikutaka kutulia, nikaondoka zangu kuelekea nyumbani. Njiani, ndipo nilipoanza kulia sana, nilichechemea kwa maumivu makali chini ya kitovu, nilitembea kwa mwendo wa kasi mpaka nilipofika nyumbani.

Vipi tena?? aliniuliza mama.
Hakuna kitu, nilijibu na kuanza kuelekea chumbani.
Wewe Davina!?
Abee mama.
Kuna nini??
Hakuna kitu mama.
Mbona unalia.?
Nani mimi?? niliuliza, sikulijibu swali hilo, nikaingia chumbani.

Nilipofika chumbani, nikakifuata kitanda na kuendelea kulia. Moyo wangu uliniuma mno, sikuamini kama mvulana niliyempenda kwa mapenzi ya dhati, Thomas alikuwa amefariki dunia tena juu ya kifua changu.
Sikujua tatizo lilikuwa ni nini, sikujua kwa nini Mungu aliamua kufanya jambo lile tena juu ya kifua changu, kila nilipojifikiria, nikaona kwamba Mungu alifanya makosa.

Hata usiku wa siku hiyo tulipokutana kwenye uwanja wa wachawi, sikuonekana kuwa na furaha, nilionekana kuwa mnyonge sana, bibi alifahamu kila kitu kilichotokea, akaamua kunifuata.


Je, kilifuatia nini? Usikose mwendelezo wake wiki ijayo.
maskin handsome thomas........kwisha habar yake
 
Hadithi ya kusisimua: Jini Mauti-18

ILIPOISHIA

ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:


Nilisema huku nikilia mno. Hawakuniambia kitu chochote kile zaidi ya kuondoka. Katika kipindi chote hicho sikuwa nikijua kwamba bibi yangu aliniwekea jini mauti mwilini mwangu na kwamba kwa kila mwanaume ambaye ningefanya naye mapenzi ilikuwa ni lazima afariki dunia. Endelea….

Siku iliyofuata, nilikwenda shuleni kama kawaida, nilipofika, nikaanza kusikia vilio kutoka kwa wanafunzi mbalimbali, moyoni niliumia mno, nilijua fika kwamba kile kilichokuwa kikiwaliza ni kuhusu kifo cha Mudi aliyefariki dunia mbele ya macho yangu.

Nikashindwa kuvumilia, machozi yakaanza kunibubujika, nilihisi moyo wangu kuwa na maumivu makali mno. Sikuamini kama nilikabidhiwa umalkia ambao ulinifanya kumuua mwanaume yeyote ambaye ningelala naye.

Moyo wangu ukakosa amani kabisa, nilipokuwa nikiwaangalia walimu na wanafunzi waliokuwa wakilia, moyo wangu ulijisikia hukumu sana. Wengi walijua kwamba nilikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mudi lakini hakukuwa na aliyefahamu kama jana usiku tulikuwa wote hivyo kuona kwamba nisingeweza kugundulika.

Kitu kilichonishangaza ni wanafunzi wengi kuanza kuninyooshea vidole. Kwanza nikashangaa, haikuwa kawaida hata kidogo, kwa nini sasa waninyooshee vidole? Niliwafanya nini mpaka kunifanyia kitu kama hicho, kila nilichojiuliza, nikakosa majibu kabisa.

Sikutaka kujali sana, nikazidi kuendelea mbele mpaka nilipoingia darasani, huko nako kila mwanafunzi aliogopa kunisogelea ni marafiki zangu wawili tu ndiyo walionifuata, alikuwa Anita na Maria.

“Mbona watu wananikimbia na kuninyooshea vidole?” niliwauliza huku nikilia.
“Wanasema wewe ndiye umemuua Mudi,” alinijibu Anita.
“Mimi nimuue Mudi?”

“Ndiyo! Wanasema haukuanza kuua hapo, hata ulipokuwa na Thomas, ilikuwa hivyohivyo, alikufa kifo kama hiki, tena chumbani kwake,” alisema Maria, maneno yale yakaniongezea uchungu.

“Yaani mimi nimuue Mudi?” niliuliza kwa sauti ya juu na kuanza kulia.
Ndiyo nilimuua lakini sikujua nilimuua vipi. Wanafunzi waliniogopa sana na wengi wakayaamini maneno aliyokuwa akiyapakaza Agape kwamba nilikuwa mchawi. Kuanzia siku hiyo sikuwa na amani na hata nilipotaka kwenda mazishini na wanafunzi wengine, wote wakanitenga.

Niliachwa shuleni nikilia peke yangu, kilio changu kilikuwa ni kumlilia bibi yangu kwa kile alichokuwa amenifanyia. Sikutaka kabisa kuua, watu wote waliokuwa wamefariki dunia walikuwa wale niliowapenda kwa moyo wa dhati.

Hakukuwa na wa kunibembeleza tena, kila mtu alinikimbia na hawakutaka hata kunisogelea. Nilijisikia aibu kubwa, shule ikawa chungu, kuanzia siku hiyo nikajuta kuwa mchawi, sikuwa na uhuru hata kidogo, sikuwa na uhuru wa kuwa na mwanaume yeyote.

Wakati nikikaa hapo darasani huku nikilia tena shule nzima kukiwa hakuna mtu yeyote zaidi ya mlinzi, ghafla nikaanza kusikia kizunguzungu kikali, nikajikaza lakini ikashindikana kabisa, kizunguzungu kile kikanipelekesha mno, nikajaribu kusimama, nikashindwa, nikaangukia viti na hapohapo nikaanza kuona giza, sikujua tena ni kitu gani kiliendelea.
***
Nilikuja kupata fahamu na kujikuta nikiwa kitandani, dripu ilikuwa ikining’inia juu yangu na maji yalikuwa yakiingia taratibu katika mshipa wangu. Macho yangu yalikuwa mazito, kitendo cha kuiona dripu ile tu nikajua kwamba mahali nilipokuwa palikuwa ni hospitalini.

Nikaanza kuangalia huku na kule mle chumbani nilimokuwa peke yangu. Nikaanza kuvuta kumbukumbu ilikuwaje mpaka nikafika hapo pale.


Je, kilifuatia nini? Usikose mwendelezo wake wiki ijayo.
 
Mkavu buana wiki episode moja ndugu yangu fanya Hata tatu ama
 
SEHEMU YA 19
Nikaanza kuangalia huku na kule mle chumbani nilimokuwa peke yangu. Nikaanza kuvuta kumbukumbu ilikuwaje mpaka nikafika pale. Endelea…

kwani nilichokikumbuka ni kwamba ulipita mwaka wa nne sikuwa nimeumwa ugonjwa wowote.
Hapo ndipo kumbukumbu zangu zilipoanza kurudi nyuma kabisa, nikaanza kukumbuka kipindi kile nilichofika shuleni ambapo wanafunzi wenzangu walikuwa wakilia, baada ya hapo wote wakaanza kuninyooshea vidole, kilichoendelea ni kwenda darasani, baada ya hapo, sikujua kitu gani kiliendelea.

Wakati nikifikiria hayo ndipo mlango ulipofunguliwa, mwanamke mmoja, alikuwa mtu mzima akaingia ndani ya chumba kile, alivalia koti jeupe, lilikuwa kubwa na hapa kifuani, upande wa kushoto kulikuwa na kibati kidogo kilichoandikwa Dk. Lucy.
“Umerudiwa na fahamu, kweli Mungu mkubwa,” aliniambia daktari yule huku akiachia tabasamu pana usoni mwake.

“Nipo hospitali gani?”
“Mtakatifu Tabitha,” alinijibu.
“Ipo wapi?”

“Hapa Manzese,” alinijibu tena.
Nilikaa hospitalini hapo nikimsubiri mama aje, wala haikuchukua saa nyingi mama akafika hospitalini hapo, aliponiona, alionekana kufurahi sana na ndipo aliponiuliza ni kitu gani kilitokea mpaka kuwa kwenye hali hiyo.

Sikumficha, nikaanza kumuhadithia kila kitu kilichotokea, alisikitika mno, kila nilipomwangalia, nilijisemea kwamba muda wowote ule angeweza kumwaga machozi yake kitu ambacho kingeniuma sana kwani sikutegemea kuyaona machozi ya mama.
“Pole sana Davina…” aliniambia.

“Asante mama. Baba yupo wapi?” nilimuuliza.
“Amekwenda kazini, tukirudi utamuona,” aliniambia.
Hakukuwa na mwanafunzi yeyote aliyekuja kuniona, nilijisikia mpweke sana hata marafiki zangu wawili niliowategemea, Maria na Anita hawakuweza kufika hospitalini hapo. Moyo wangu uliniuma mno, sikuamini kama mimi ndiye niliyekuwa nikipitia yale au mtu mwingine. Wakati mwingine nilitamani kila kitu kilichokuwa kinaendelea kiwe ndoto na baada ya dakika kadhaa niamke kutoka usingizini.

Ilipofika saa sita mchana nikaruhusiwa kurudi nyumbani. Njiani nilitembea kwa unyonge, kila mtu niliyekuwa nikimuona niliamini kwamba na yeye aliambiwa juu ya kile kilichokuwa kimetokea hivyo watu wote kuniona mchawi.
“Mama….” nilimuita.

“Abee mwanangu.”
“Mudi amekufa?” niliuliza huku nikionekana kutokuamini.
“Ndiyo! Kazi ya Mungu haina makosa,” aliniambia mama, nikaanza kulia.

Ukweli ni kwamba nilimpenda sana Mudi, baada ya Thomas kufariki dunia, mtu ambaye aliuteka moyo wangu vilivyo alikuwa Mudi tu. Sikuamini kilichokuwa kimetokea, kitendo cha kumpoteza Mudi muda mchache baada ya kuanza kufanya mapenzi hakika iliniuma sana.

Wanafunzi na walimu hawakutaka kuwa nami, hawakutaka kunifariji kwani walijua ni kwa jinsi gani nilikuwa karibu na Mudi, matokeo yake, badala ya kunifariji ndiyo kwanza wakanitenga na kuniacha shuleni nikiwa peke yangu.

Baada ya kufika nyumbani, saa moja baadaye mzee Abdallah, baba wa kambo alipokuja mama alimwambia kile kilichotokea. Baba hakuamini kama kweli walimu na wanafunzi, pamoja na elimu yao walikubaliana na maneno kwamba nilikuwa mchawi. Waliona kwamba ninasingiziwa na hata hao watu waliokufa ni kwamba siku zao zilifika.

“Hawa walimu ni wapumbavu sana,” alisema baba huku akionekana kukasirika.
“Tena sana, yaani umtenge mtoto kisa tu mnasema yeye ni mchawi,” alisema mama, wote kwa pamoja walionekana kuwa na hasira mno.

Japokuwa mama alionekana kunitetea sana lakini alikuwa na wasiwasi mno, kila nilipomuona akiwa peke yake, mawazo yalimsonga na alionekana kufikiria mambo mengi sana. Ukweli ni kwamba mama alikuwa na wasiwasi mwingi, kila kitu kilichokuwa kikitokea kilimfanya kuwa na mawazo mno.
“Davina…” aliniita.
“Abee mama.”
Itaendelea .......
 
hii hadithi inapatikana global publisher, kwahiyo mpaka wao watoe ndio inaletwa hapa
Hadithi ya kusisimua: Jini Mauti-19

ILIPOISHIA

ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:


Nikaanza kuangalia huku na kule mle chumbani nilimokuwa peke yangu. Nikaanza kuvuta kumbukumbu ilikuwaje mpaka nikafika pale. Endelea…

kwani nilichokikumbuka ni kwamba ulipita mwaka wa nne sikuwa nimeumwa ugonjwa wowote.
Hapo ndipo kumbukumbu zangu zilipoanza kurudi nyuma kabisa, nikaanza kukumbuka kipindi kile nilichofika shuleni ambapo wanafunzi wenzangu walikuwa wakilia, baada ya hapo wote wakaanza kuninyooshea vidole, kilichoendelea ni kwenda darasani, baada ya hapo, sikujua kitu gani kiliendelea.


Wakati nikifikiria hayo ndipo mlango ulipofunguliwa, mwanamke mmoja, alikuwa mtu mzima akaingia ndani ya chumba kile, alivalia koti jeupe, lilikuwa kubwa na hapa kifuani, upande wa kushoto kulikuwa na kibati kidogo kilichoandikwa Dk. Lucy.
“Umerudiwa na fahamu, kweli Mungu mkubwa,” aliniambia daktari yule huku akiachia tabasamu pana usoni mwake.


“Nipo hospitali gani?”
“Mtakatifu Tabitha,” alinijibu.
“Ipo wapi?”


“Hapa Manzese,” alinijibu tena.
Nilikaa hospitalini hapo nikimsubiri mama aje, wala haikuchukua saa nyingi mama akafika hospitalini hapo, aliponiona, alionekana kufurahi sana na ndipo aliponiuliza ni kitu gani kilitokea mpaka kuwa kwenye hali hiyo.


Sikumficha, nikaanza kumuhadithia kila kitu kilichotokea, alisikitika mno, kila nilipomwangalia, nilijisemea kwamba muda wowote ule angeweza kumwaga machozi yake kitu ambacho kingeniuma sana kwani sikutegemea kuyaona machozi ya mama.
“Pole sana Davina…” aliniambia.


“Asante mama. Baba yupo wapi?” nilimuuliza.
“Amekwenda kazini, tukirudi utamuona,” aliniambia.
Hakukuwa na mwanafunzi yeyote aliyekuja kuniona, nilijisikia mpweke sana hata marafiki zangu wawili niliowategemea, Maria na Anita hawakuweza kufika hospitalini hapo. Moyo wangu uliniuma mno, sikuamini kama mimi ndiye niliyekuwa nikipitia yale au mtu mwingine. Wakati mwingine nilitamani kila kitu kilichokuwa kinaendelea kiwe ndoto na baada ya dakika kadhaa niamke kutoka usingizini.


Ilipofika saa sita mchana nikaruhusiwa kurudi nyumbani. Njiani nilitembea kwa unyonge, kila mtu niliyekuwa nikimuona niliamini kwamba na yeye aliambiwa juu ya kile kilichokuwa kimetokea hivyo watu wote kuniona mchawi.
“Mama….” nilimuita.


“Abee mwanangu.”
“Mudi amekufa?” niliuliza huku nikionekana kutokuamini.
“Ndiyo! Kazi ya Mungu haina makosa,” aliniambia mama, nikaanza kulia.


Ukweli ni kwamba nilimpenda sana Mudi, baada ya Thomas kufariki dunia, mtu ambaye aliuteka moyo wangu vilivyo alikuwa Mudi tu. Sikuamini kilichokuwa kimetokea, kitendo cha kumpoteza Mudi muda mchache baada ya kuanza kufanya mapenzi hakika iliniuma sana.

Wanafunzi na walimu hawakutaka kuwa nami, hawakutaka kunifariji kwani walijua ni kwa jinsi gani nilikuwa karibu na Mudi, matokeo yake, badala ya kunifariji ndiyo kwanza wakanitenga na kuniacha shuleni nikiwa peke yangu.

Baada ya kufika nyumbani, saa moja baadaye mzee Abdallah, baba wa kambo alipokuja mama alimwambia kile kilichotokea. Baba hakuamini kama kweli walimu na wanafunzi, pamoja na elimu yao walikubaliana na maneno kwamba nilikuwa mchawi. Waliona kwamba ninasingiziwa na hata hao watu waliokufa ni kwamba siku zao zilifika.

“Hawa walimu ni wapumbavu sana,” alisema baba huku akionekana kukasirika.
“Tena sana, yaani umtenge mtoto kisa tu mnasema yeye ni mchawi,” alisema mama, wote kwa pamoja walionekana kuwa na hasira mno.


Japokuwa mama alionekana kunitetea sana lakini alikuwa na wasiwasi mno, kila nilipomuona akiwa peke yake, mawazo yalimsonga na alionekana kufikiria mambo mengi sana. Ukweli ni kwamba mama alikuwa na wasiwasi mwingi, kila kitu kilichokuwa kikitokea kilimfanya kuwa na mawazo mno.
“Davina…” aliniita.
“Abee mama.”


Itaendelea wiki ijayo.
 
Hadithi ya kusisimua: Jini Mauti-20

ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:

Japokuwa mama alionekana kunitetea sana lakini alikuwa na wasiwasi mno, kila nilipomuona akiwa peke yake, mawazo yalimsonga na alionekana kufikiria mambo mengi sana. Ukweli ni kwamba mama alikuwa na wasiwasi mwingi, kila kitu kilichokuwa kikitokea kilimfanya kuwa na mawazo mno. Endelea…

“Davina…” aliniita.
“Abee mama.”
“Hebu niambie ukweli, wewe ni mchawi?” aliniuliza, alinikazia macho.
“Mimi?”

“Si ndiyo naongea nawe.”
“Hapana mama! Mimi si mchawi.”
“Kweli?”
“Ndiyo mama!”

“Na mbona kila unayefanya naye mapenzi anakufa?” aliniuliza.
“Mama! Mimi sijui.”
“Hapana! Lazima kuna kitu. Utakuwa umepewa mkoba wa uchawi ni lazima nikupeleke kanisani kuombewa,” aliniambia.
“Kwenda kanisani?”

“Ndiyo!”
“Sitaki, siwezi kwenda kanisani.”
“Kwa nini?”
“Basi tu.”

Sikutaka kwenda kanisani, nilikuwa na hofu kubwa kwani nilijua mambo ya kanisani yalikuwa vipi. Nilimkatalia mama, sikuwa radhi kuona nikienda kanisani kwani maisha yangu hayakuwa mazuri hata kidogo.

Sikwenda tena shule, nilimuomba baba anichukulie uhamisho na kweli akafanya hivyo, nikahamia katika Shule ya Sekondari ya Mbezi. Shule hiyo ilikuwa tofauti na Manzese, pale Manzese ilikuwa ni shule ya serikali lakini hii ilikuwa ya mtu binafsi.

Hapo kulikuwa na wasichana warembo walioonekana kuwa na maisha mazuri. Kuna wengine waliokuwa wakijiita majina mazuri ya Kizungu ilimradi kuwaonesha watu ni jinsi gani walikuwa warembo.
Mimi sikuwa msichana mrembo ila Mungu alinibariki kwa kunipa umbo zuri kwa nyuma, nilikuwa nimeumbika na kila nilipopita mbele ya wanaume ilikuwa ni lazima kunitazama kwa nyuma na kama ukinitazama ilikuwa ni lazima unitamani.

Nilipoingia shuleni hapo ilikuwa gumzo, wanaume wengi walinizungumzia, wengine wakawaambia wasichana wawaunganishie kwangu lakini sikuweza kukubaliana nao.

Bado nilikumbuka kilichotokea kwa Thomas na Mudi, sikutaka kitokee kwa mtu mwingine. Wanaume wengi walikuwa wakinifuata kila siku lakini sikutaka kukubaliana nao. Kidogo hapo Mbezi nilionekana kuwa na amani, hakukuwa na mtu aliyenisimanga kwa kuwa nilikuwa mchawi.

Kati ya wanaume wote waliokuwa wakinifuata, kulikuwa na watatu ambao walionesha uhitaji mkubwa wa kuwa nami, wa kwanza aliitwa Michael, huyu alikuwa mwanafunzi wa kidato cha nne, wa pili alikuwa Sifael, mwanafunzi wa kidato cha tatu kama mimi na mwingine alikuwa dereva bodaboda ambaye alikuwa akiegesha pikipiki yake katika eneo ambalo halikuwa mbali na shuleni hapo, huyo aliitwa Hemed.

Kama msichana nilionesha msimamo wangu, halikuwa jambo jepesi kunilaghai, mbali na hiyo nilikuwa na wasiwasi kwamba kama ningemkubali mwanaume yeyote basi ingekuwa ni lazima afe wakati wa kufanya mapenzi.

Kuroga sikuacha, bado niliendelea kama kawaida. Tulisafiri usiku na ungo, tulikwenda sehemu mbalimbali huku nikisimama kama kiongozi. Nilipata nafasi ya kula nyama za watu na kunywa damu zao na mambo mengine ya kishirikina.

Katika maisha yangu yote ya uchawi nilikuwa naogopa kwenda kwa watu wa makanisani ambao walisimama imara na Mungu. Wakati mwingine nilitoa hofu na kwenda kuwaroga watu hao majumbani mwao.

Huko, tulikuwa tukikutana na mambo ya ajabu mno ambayo yalitushangaza. Nakumbuka kuna siku tulipanga kwenda kumroga mchungaji wa kanisa moja la Praise And Worship la pale Mwenge, tulitaka tumpe uchovu wa kufika kanisani kwake kwani alikuwa akitusumbua sana.

Tulipofika katika eneo la nyumba yake, hatukukuta nyumba yoyote ile zaidi ya bahari iliyokuwa ikipiga mawimbi makubwa.

Itaendelea wiki ijayo.
 
Hadithi ya kusisimua: Jini Mauti-21

ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:

Tulipofika katika eneo la nyumba yake, hatukukuta nyumba yoyote ile zaidi ya bahari iliyokuwa ikipiga mawimbi makubwa. Endelea…

Tulishangaa sana, tulihisi labda tulikuwa tumekosea njia, tuliondoka na kurudi tena usiku huohuo, tena kwa kuangalia vizuri njia, tulichokiona mara ya kwanza ndicho tulichokiona tena, bahari kubwa iliyokuwa ikipiga mawimbi makubwa.

Haikuwa hivyo tu, wakati mwingine tulipokuwa tukija, hatukukuta kitu chochote zaidi ya jangwa kubwa lililokuwa na mchanga wa moto. Matukio hayo yalitushangaza mno hivyo tukaachana na mambo ya kumfuatilia mchungaji huyo.

Sikutaka kuona mtu mwingine akifa tena kwa ajili yangu na ndiyo maana kila mwanaume aliyeniambia ukweli hakuweza kunipata. Hemed ndiye aliyeonekana kuwa msumbufu sana kwangu, kila nilipotoka shule ilikuwa ni lazima kunifuata na pikipiki yake, akinichukua na kunirudisha nyumbani, aliponifikisha, hakuwa akiondoka, alikuwa akizungumza na mimi kwanza ndiyo aondoke.

Alinisumbua sana. Simu yangu ya kwanza kutumia nilinunuliwa na yeye. Sikutaka kuichukua kwa mara ya kwanza lakini baada ya kunibembeleza sana, nikajikuta nikiichukua. Tulikuwa tukizungumza usiku, kuchati kama kawaida na aliendelea kuniambia kwamba alinipenda sana.

“Ninakupenda Davina,” aliniambia mara kwa mara simuni.
“Lakini bado nasoma.”
“Hakuna tatizo. Kwani nitakatisha masomo yako?”
“Hapana. Ila naogopa mimba.”

“Kwani si kuna kinga jamani, kuwa wangu Davina,” aliniambia kwa sauti ya kubembeleza.

“Hemedi.”
“Naam.”
“Najua unanipenda lakini naomba unipe muda jamani,” nilimwambia.
Hapo ndipo nilipoamini kwamba mwanaume anapoamua kumtafuta mwanamke huamua kwa nguvu zote. Sikupumua vizuri, Hemedi anapiga, sikutulia vizuri, Hemedi anatuma meseji, yaani alifanya mambo yote kuonyesha kwamba alikuwa akinipenda mno. Pamoja na hayo yote, wasiwasi wangu ulikuwa mmoja tu kwamba sikutaka kufanya naye mapenzi kwa kuwa sikutaka kuona akifariki dunia.
“Hemedi…”

“Naaam!”
“Sitaki ufe…”
“Hutaki nife?”

“Ndiyo! Nataka uishi mpaka kifo cha kawaida kitakapokukuta.”
“Unamaanisha nini?”
“Ukifanya mapenzi na mimi, utakufa.”
“Hahaha! Davina acha kunipiga saundi, au ndiyo unaninyima kijanja?” aliniuliza Hemedi huku akicheka kwenye simu.

“Hemedi! Sitaki ufe, naomba unielewe.”
“Na kama nikitaka kufa kwa ajili yako, kuna tatizo kwani?”
“Hemedi! Mbona wewe mwanaume unakuwa mbishi?”
“Nakuwa mbishi kwa sababu nakupenda. Davina, kwanza hebu naomba tukutane sehemu tuongee,” aliniambia.

“Wapi?”
“Popote pale.”
“Sema wewe.”
“Tukutane Sinza.”

“Sinza gani?”
“White Inn kwenye Bar ya Shika More.”
“Sawa.”
Kilichofuata ni kupanga mikakati ya kuonana. Tulipanga kuonana majira ya saa kumi na moja. Nilikuwa na mawazo mengi, nilijitahidi kwa nguvu zote kumkataa Hemedi lakini hakutaka kunielewa kabisa, kila wakati alikuwa akinisumbua.

Nilimwambia kwamba endapo angefanya mapenzi na mimi ilikuwa ni lazima afariki dunia lakini hakutaka kusikia kabisa na ndiyo kwanza aliniambia maneno mengi ya kimahaba kwamba alikuwa tayari kufa kwa ajili yangu.

Siku hiyo nilikubali kuonana naye lakini sikutaka kufanya naye mapenzi kabisa, yaani ilikuwa ni kukutana, kupiga stori kisha kila mtu kuondoka zake. Nilipofika katika Baa ya Shika More, nilimuona akiwa ametulia kwenye meza moja iliyokusanya viti vinne, aliponiona, akaanza kutoa tabasamu pana.

“Karibu mrembo,” alinikaribisha na kutulia kitini.

Itaendelea wiki ijayo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom