Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,672
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 16
Mike alikuwa hoi kitandani, nyumbani kwake, akiamini kabisa kuwa angekufa baada ya siku si nyingi. Alikuwa katikati ya mateso makali na mawazo mengi na alimhurumia sana mke wake kwa sababu mateso aliyokuwa akiyapata hata mkewe pia yalikuwa yakimsubiri.
Ndani ya nafsi yake alijilaumu ni kwa nini alikubali kuacha matumizi ya kondomu kama walivyokuwa wamepanga.
"Mke wangu, UKIMWI si mchezo. Nakuhurumia sana nisingependa mateso haya yakupate lakini hakuna la kufanya, itabidi tu uyapitie haya yote. Mimi najua nitakufa lakini mali yote nitakuachia wewe na ninaagiza kuwa uitumie pesa hiyo kujali afya yako na kuwatunza wagonjwa wengine wa UKIMWI na hata yatima."
"Usiwe na wasiwasi, utapona tu Mike," Beatrice alimpa moyo.
"Mke wangu hali yangu si nzuri, naomba uende mjini haraka iwezekanavyo ukamwite Rwezaura nije nikuandikie hati ya urithi usije ukasumbuliwa baada ya mimi kuondoka."
"Mike lakini unajuaje kama unakufa? Tumwachie Mungu mume wangu!"
"Mimi najua tu Beatrice, ninaomba ufanye hivyo."
Beatrice alizidi kusimama pale bila kujua la kufanya, jambo lililomkera Mike ambaye aliangaza macho yake huku na kule na kumwona dada yake mdogo Violeth aliyeishi naye nyumbani.
"Violeth!" Mike aliita akiwa kakasirika. Violeth alikuja mbio chumbani.
"Nenda kwa Rwezaura upesi mwambie aje na mihuri yake yote nina kitu nataka kuandika sawa?”
Violeth aliitikia na kutoka hadi nje ambako aliondoka na gari la Mike, dakika kumi baadaye alirejea na wakili Rwezaura. Hali ya Mike ilikuwa dhaifu mno. Wakili aliandika hati ya urithi kuwa baada ya kifo cha Mike mali yote irithiwe na Beatrice na Beatrice akifa mali yote irithiwe na Violeth au watoto yatima.
Wakili aliondoka na nakala moja ya hati ya urithi kama kumbukumbu na nakala halisi alibaki nayo Beatrice.
"Mke wangu, najua nikifa wanaume wengi watakufuata na kutaka kukuoa sababu ya mali. Naomba usikubali, si kwamba sitaki mali yangu itumiwe na mtu mwingine, ila sitaki uue mtu mwingine tena; acha tufe wenyewe!" Mike alimwambia mkewe baada ya wakili kuondoka.
Baadaye Mike alimwomba Beatrice amsaidie kuandika barua kwa Chancellor Edmund kumjulisha juu ya hali mbaya aliyokuwa nayo kwani hapakuwa na mawasiliano yoyote kati yao. Beatrice hakutaka kufanya mzaha tena kwani hali ilishamtisha.
"Iweke hiyo barua kwenye bahasha kesho ukaitume Uingereza, pia hiyo hati iweke kwenye bahasha uitunze vizuri maana familia zetu za Kiafrika zina matatizo. Mara nyingi wake wa marehemu hunyanyaswa sana baada ya waume zao kufa!"
Beatrice alifanya kama alivyoambiwa, bahasha iliyokuwa na hati aliiweka katikati ya Biblia na kuifungia ndani ya kabati.
***
Mlango uligongwa, Beatrice akaufungua, alikuwa daktari Kalegeya kutoka kitengo cha kupambana na UKIMWI, pamoja na sista Fortunata aliyekuwa mhamasishaji wa mapambano dhidi ya UKIMWI kutoka Kanisa Katoliki jimbo la Mwanza.
"Ah! Karibuni sana dokta."
"Ahsante, tumekuja kumwona Mike maana siku nyingi sana zimepita bila kumtia machoni, anaendeleaje?"
"Yupo ndani, anaendelea hivyohivyo, tafadhali ingieni tu muongee naye."
Daktari Kalegeya na sista Fortunata waliingia ndani.
"Karibuni sana," Mike alimkabisha Dkt. Kalegeya.
Baada ya maongezi marefu na kupeana pole, daktari Kalegeya alikuwa na jambo.
“Kesho ni Siku ya UKIMWI Duniani, tungependa sana tuwakaribishe mshirikiane nasi katika kuadhimisha siku hiyo.”
"Zitafanyika wapi?" Mike aliuliza.
"Uwanja wa mpira wa Nyamagana."
"Nitapenda sana kuwepo...nina jambo la kuwaeleza vijana ambao bado wanauona UKIMWI kama kitu kidogo, ninataka wapate nafasi ya kuona labda itasaidia kidogo kuibadilisha jamii."
***
Maelfu ya watu walifurika katika Uwanja wa Nyamagana Barabara ya Posta mjini Mwanza, wakisikiliza hotuba za viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa juu ya ugonjwa wa UKIMWI.
Kila mtu alionekana kuwa na huzuni, yalikuwa ni maadhimisho mengine ambayo hufanyika katika viwanja hivyo. Kila kilichoongelewa kilionekana kuwagusa kwa uzito wote waliokuwepo uwanjani.
"Hivi sasa ni wakati wa kumkaribisha Mike Martin, kijana mwathirika wa UKIMWI ambaye ameamua kuongea nanyi siku ya leo ili mpate kuuona mfano hai wa mtu anayekufa kwa UKIMWI.
"Karibu Mike!" Mshereheshaji alimkaribisha.
Mike alinyanyuka kwa msaada wa mkewe na kusimama wima huku akiyumba, ilibidi Beatrice amshikilie vizuri. Uwanja wote ulikuwa kimya kabisa. Watu walipomwona jinsi alivyokuwa amekonda walisikitishwa sana.
"Jamani mnanionaaaa!" Mike alisema kwa sauti, umati wote wa watu ukaitikia.
"Ndiyoooooo!"
"Basi mimi ni mfano halisi wa mtu aneyekufa kwa UKIMWI, ndugu zangu! Leo hii nimeamua kujitokeza hadharani ili muelewe ugonjwa huu unatesa kiasi gani, mpate kubadilisha tabia zenu.”
Alisita kidogo, baadaye aliendelea: "Ndugu zangu ugonjwa huu ni mbaya nikisema mbaya, naomba nieleweke una mateso mengi mno na nisingependa mateso haya yampate mtu mwingine yoyote!
Ningependa mimi ndiye niwe mtu wa mwisho kufa kwa ugonjwa huu. Ndio maana nimesimama mbele yenu kuwaelezeni ninayoyasema.
Nimesikia vijana wengi wakisema UKIMWI ni kama mafua, UKIMWI ni kama malaria, UKIMWI ni kama taifodi lakini maneno hayo mnayasema kabla hamjaupata ugonjwa huu na kuyashuhudia mateso yake.
Ukishaupata utaomba atokee mtu autoe mwilini mwako lakini haitawezekana tena. Ni hapo ndipo utakapoanza kujuta na kuteseka."
Aliendelea, "Kama UKIMWI ungekuwa unaondolewa mwilini kwa pesa mimi ningepona, kwani nilibahatika kupata pesa nikiwa katika umri mdogo sana lakini pesa zangu zimeshindwa kunisaidia! Nimeshakwenda Kenya na Zaire nikatumia mamilioni ya fedha kwa dawa za Kemron na MMI bila mafanikio.
“Nimekwishakwenda Marekani kubadilisha damu mara mbili bila mafanikio, leo hii ninakufa pamoja na fedha nilizo nazo, naziacha pesa zangu!
"UKIMWI si jambo la kufanyia mzaha ndugu zangu..." Wakati Mike akitoa hotuba hii karibu nusu ya watu uwanjani hapo walikuwa wakilia.
"Msilie, chukueni tahadhari kabla mambo hayajawafika..." Alipofika hapo ghafla Mike alianguka chini na kugeuza macho, akaanza kutupa mikono.
Beatrice alianza kulia akimtingisha.
ANGELINA MOSHA 1962-1999 (2)
Mzee Martin, baba yake Mike, alizaliwa katika familia ya Mtemi Mchenya wa huko Dutwa, Bariadi. Alizaliwa akiitwa Longa na alikuwa mtoto wa mwisho katika familia yao iliyokuwa na watoto wengine saba waliotangulia. Ndugu zake wengine wote hawakujaliwa kwenda shule, walibaki nyumbani kumsaidia baba yao kazi na utawala wa ufugaji wa ng'ombe.
Longa akiwa na umri wa miaka mitano, baada ya kiongozi wa kikoloni DC William kumwona na kumpenda, alimwomba Mtemi Mchenya kumruhusu amchukue na kwenda kuishi naye Ikulu ili awe akicheza na mtoto wake aliyeitwa Smith mwenye umri sawa na Longa.
Kwa sababu aliombwa na DC, Mtemi Mchenya hakuwa na pingamizi, alikubali mtoto wake achukuliwe, Longa akawa amejiunga na familia ya DC Smith, Shinyanga mjini. Muda mfupi baadaye alibatizwa na kuitwa Martin Longa Mchenya.
Martin na Smith, kwa pamoja walifundishwa na mwalimu Mwingereza na katika muda mfupi Martin alijikuta akibadilika na kuwa kama Mwingereza. Ilikuwa sio rahisi kuamini alizaliwa katika familia ya Mtemi Mchenya, mara chache sana alikwenda nyumbani kwao Bariadi. Muda mwingi wa maisha yake alikuwa uzunguni, Shinyanga.
Martin akiwa na umri wa miaka kumi na mitano, DC William alitakiwa arudi nyumbani kwao Uingereza, kwa jinsi familia nzima ya DC huyo ilivyokuwa imemzoea Martin, ilishindwa kumuacha Tanganyika.
DC alimfuata Mtemi Longa kuomba ruhusa ili waondoke naye, lakini Mtemi alikataa na kusema mtoto wake asingeweza kuishi mbali na wazazi wake kiasi hicho. Alitaka Martin arudishwe nyumbani mara moja.
Hata hivyo, baadaye Martin alikwenda Bariadi kumbembeleza baba yake ambaye hatimaye alikubali na kutoa ruhusa mtoto wake aondoke na familia ya DC William kwenda Uingereza.
Martin hakurudi nchini mpaka mwaka 1961, ambapo alikuta utaratibu wa Utemi umefutwa lakini kwa elimu aliyokuwa nayo alipata kazi ya Ualimu katika shule ya msingi Mwika, huko Marangu, Kilimanjaro.
Ni shuleni hapo ndipo alipokutana na msichana wa Kichaga aliyeitwa Veridiana Mosha, yeye pia alikuwa mwalimu katika shule hiyo, na kujenga naye urafiki wa kimapenzi.
Matokeo ya urafiki wao yalisababisha ujauzito lakini mimba hiyo ikiwa na miezi sita mwalimu Martin aliomba uhamisho kwenda Mwanza ambako miaka mitatu baadaye alimwoa Cecilia Ndaki, mwanamke wa Kisukuma na miaka mitano baadaye mama huyo akawa mjamzito na kuzaa mtoto wao wa kwanza wa kiume ambaye walimwita jina la Mike!
Mike alikuwa ni mtoto mzuri mno, kila mtu alimpenda. Mama yake kila alipopanda basi na kusimama abiria walimgombania kumbeba mtoto huyo.
Je nini kitaendelea?
Mike alikuwa hoi kitandani, nyumbani kwake, akiamini kabisa kuwa angekufa baada ya siku si nyingi. Alikuwa katikati ya mateso makali na mawazo mengi na alimhurumia sana mke wake kwa sababu mateso aliyokuwa akiyapata hata mkewe pia yalikuwa yakimsubiri.
Ndani ya nafsi yake alijilaumu ni kwa nini alikubali kuacha matumizi ya kondomu kama walivyokuwa wamepanga.
"Mke wangu, UKIMWI si mchezo. Nakuhurumia sana nisingependa mateso haya yakupate lakini hakuna la kufanya, itabidi tu uyapitie haya yote. Mimi najua nitakufa lakini mali yote nitakuachia wewe na ninaagiza kuwa uitumie pesa hiyo kujali afya yako na kuwatunza wagonjwa wengine wa UKIMWI na hata yatima."
"Usiwe na wasiwasi, utapona tu Mike," Beatrice alimpa moyo.
"Mke wangu hali yangu si nzuri, naomba uende mjini haraka iwezekanavyo ukamwite Rwezaura nije nikuandikie hati ya urithi usije ukasumbuliwa baada ya mimi kuondoka."
"Mike lakini unajuaje kama unakufa? Tumwachie Mungu mume wangu!"
"Mimi najua tu Beatrice, ninaomba ufanye hivyo."
Beatrice alizidi kusimama pale bila kujua la kufanya, jambo lililomkera Mike ambaye aliangaza macho yake huku na kule na kumwona dada yake mdogo Violeth aliyeishi naye nyumbani.
"Violeth!" Mike aliita akiwa kakasirika. Violeth alikuja mbio chumbani.
"Nenda kwa Rwezaura upesi mwambie aje na mihuri yake yote nina kitu nataka kuandika sawa?”
Violeth aliitikia na kutoka hadi nje ambako aliondoka na gari la Mike, dakika kumi baadaye alirejea na wakili Rwezaura. Hali ya Mike ilikuwa dhaifu mno. Wakili aliandika hati ya urithi kuwa baada ya kifo cha Mike mali yote irithiwe na Beatrice na Beatrice akifa mali yote irithiwe na Violeth au watoto yatima.
Wakili aliondoka na nakala moja ya hati ya urithi kama kumbukumbu na nakala halisi alibaki nayo Beatrice.
"Mke wangu, najua nikifa wanaume wengi watakufuata na kutaka kukuoa sababu ya mali. Naomba usikubali, si kwamba sitaki mali yangu itumiwe na mtu mwingine, ila sitaki uue mtu mwingine tena; acha tufe wenyewe!" Mike alimwambia mkewe baada ya wakili kuondoka.
Baadaye Mike alimwomba Beatrice amsaidie kuandika barua kwa Chancellor Edmund kumjulisha juu ya hali mbaya aliyokuwa nayo kwani hapakuwa na mawasiliano yoyote kati yao. Beatrice hakutaka kufanya mzaha tena kwani hali ilishamtisha.
"Iweke hiyo barua kwenye bahasha kesho ukaitume Uingereza, pia hiyo hati iweke kwenye bahasha uitunze vizuri maana familia zetu za Kiafrika zina matatizo. Mara nyingi wake wa marehemu hunyanyaswa sana baada ya waume zao kufa!"
Beatrice alifanya kama alivyoambiwa, bahasha iliyokuwa na hati aliiweka katikati ya Biblia na kuifungia ndani ya kabati.
***
Mlango uligongwa, Beatrice akaufungua, alikuwa daktari Kalegeya kutoka kitengo cha kupambana na UKIMWI, pamoja na sista Fortunata aliyekuwa mhamasishaji wa mapambano dhidi ya UKIMWI kutoka Kanisa Katoliki jimbo la Mwanza.
"Ah! Karibuni sana dokta."
"Ahsante, tumekuja kumwona Mike maana siku nyingi sana zimepita bila kumtia machoni, anaendeleaje?"
"Yupo ndani, anaendelea hivyohivyo, tafadhali ingieni tu muongee naye."
Daktari Kalegeya na sista Fortunata waliingia ndani.
"Karibuni sana," Mike alimkabisha Dkt. Kalegeya.
Baada ya maongezi marefu na kupeana pole, daktari Kalegeya alikuwa na jambo.
“Kesho ni Siku ya UKIMWI Duniani, tungependa sana tuwakaribishe mshirikiane nasi katika kuadhimisha siku hiyo.”
"Zitafanyika wapi?" Mike aliuliza.
"Uwanja wa mpira wa Nyamagana."
"Nitapenda sana kuwepo...nina jambo la kuwaeleza vijana ambao bado wanauona UKIMWI kama kitu kidogo, ninataka wapate nafasi ya kuona labda itasaidia kidogo kuibadilisha jamii."
***
Maelfu ya watu walifurika katika Uwanja wa Nyamagana Barabara ya Posta mjini Mwanza, wakisikiliza hotuba za viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa juu ya ugonjwa wa UKIMWI.
Kila mtu alionekana kuwa na huzuni, yalikuwa ni maadhimisho mengine ambayo hufanyika katika viwanja hivyo. Kila kilichoongelewa kilionekana kuwagusa kwa uzito wote waliokuwepo uwanjani.
"Hivi sasa ni wakati wa kumkaribisha Mike Martin, kijana mwathirika wa UKIMWI ambaye ameamua kuongea nanyi siku ya leo ili mpate kuuona mfano hai wa mtu anayekufa kwa UKIMWI.
"Karibu Mike!" Mshereheshaji alimkaribisha.
Mike alinyanyuka kwa msaada wa mkewe na kusimama wima huku akiyumba, ilibidi Beatrice amshikilie vizuri. Uwanja wote ulikuwa kimya kabisa. Watu walipomwona jinsi alivyokuwa amekonda walisikitishwa sana.
"Jamani mnanionaaaa!" Mike alisema kwa sauti, umati wote wa watu ukaitikia.
"Ndiyoooooo!"
"Basi mimi ni mfano halisi wa mtu aneyekufa kwa UKIMWI, ndugu zangu! Leo hii nimeamua kujitokeza hadharani ili muelewe ugonjwa huu unatesa kiasi gani, mpate kubadilisha tabia zenu.”
Alisita kidogo, baadaye aliendelea: "Ndugu zangu ugonjwa huu ni mbaya nikisema mbaya, naomba nieleweke una mateso mengi mno na nisingependa mateso haya yampate mtu mwingine yoyote!
Ningependa mimi ndiye niwe mtu wa mwisho kufa kwa ugonjwa huu. Ndio maana nimesimama mbele yenu kuwaelezeni ninayoyasema.
Nimesikia vijana wengi wakisema UKIMWI ni kama mafua, UKIMWI ni kama malaria, UKIMWI ni kama taifodi lakini maneno hayo mnayasema kabla hamjaupata ugonjwa huu na kuyashuhudia mateso yake.
Ukishaupata utaomba atokee mtu autoe mwilini mwako lakini haitawezekana tena. Ni hapo ndipo utakapoanza kujuta na kuteseka."
Aliendelea, "Kama UKIMWI ungekuwa unaondolewa mwilini kwa pesa mimi ningepona, kwani nilibahatika kupata pesa nikiwa katika umri mdogo sana lakini pesa zangu zimeshindwa kunisaidia! Nimeshakwenda Kenya na Zaire nikatumia mamilioni ya fedha kwa dawa za Kemron na MMI bila mafanikio.
“Nimekwishakwenda Marekani kubadilisha damu mara mbili bila mafanikio, leo hii ninakufa pamoja na fedha nilizo nazo, naziacha pesa zangu!
"UKIMWI si jambo la kufanyia mzaha ndugu zangu..." Wakati Mike akitoa hotuba hii karibu nusu ya watu uwanjani hapo walikuwa wakilia.
"Msilie, chukueni tahadhari kabla mambo hayajawafika..." Alipofika hapo ghafla Mike alianguka chini na kugeuza macho, akaanza kutupa mikono.
Beatrice alianza kulia akimtingisha.
ANGELINA MOSHA 1962-1999 (2)
Mzee Martin, baba yake Mike, alizaliwa katika familia ya Mtemi Mchenya wa huko Dutwa, Bariadi. Alizaliwa akiitwa Longa na alikuwa mtoto wa mwisho katika familia yao iliyokuwa na watoto wengine saba waliotangulia. Ndugu zake wengine wote hawakujaliwa kwenda shule, walibaki nyumbani kumsaidia baba yao kazi na utawala wa ufugaji wa ng'ombe.
Longa akiwa na umri wa miaka mitano, baada ya kiongozi wa kikoloni DC William kumwona na kumpenda, alimwomba Mtemi Mchenya kumruhusu amchukue na kwenda kuishi naye Ikulu ili awe akicheza na mtoto wake aliyeitwa Smith mwenye umri sawa na Longa.
Kwa sababu aliombwa na DC, Mtemi Mchenya hakuwa na pingamizi, alikubali mtoto wake achukuliwe, Longa akawa amejiunga na familia ya DC Smith, Shinyanga mjini. Muda mfupi baadaye alibatizwa na kuitwa Martin Longa Mchenya.
Martin na Smith, kwa pamoja walifundishwa na mwalimu Mwingereza na katika muda mfupi Martin alijikuta akibadilika na kuwa kama Mwingereza. Ilikuwa sio rahisi kuamini alizaliwa katika familia ya Mtemi Mchenya, mara chache sana alikwenda nyumbani kwao Bariadi. Muda mwingi wa maisha yake alikuwa uzunguni, Shinyanga.
Martin akiwa na umri wa miaka kumi na mitano, DC William alitakiwa arudi nyumbani kwao Uingereza, kwa jinsi familia nzima ya DC huyo ilivyokuwa imemzoea Martin, ilishindwa kumuacha Tanganyika.
DC alimfuata Mtemi Longa kuomba ruhusa ili waondoke naye, lakini Mtemi alikataa na kusema mtoto wake asingeweza kuishi mbali na wazazi wake kiasi hicho. Alitaka Martin arudishwe nyumbani mara moja.
Hata hivyo, baadaye Martin alikwenda Bariadi kumbembeleza baba yake ambaye hatimaye alikubali na kutoa ruhusa mtoto wake aondoke na familia ya DC William kwenda Uingereza.
Martin hakurudi nchini mpaka mwaka 1961, ambapo alikuta utaratibu wa Utemi umefutwa lakini kwa elimu aliyokuwa nayo alipata kazi ya Ualimu katika shule ya msingi Mwika, huko Marangu, Kilimanjaro.
Ni shuleni hapo ndipo alipokutana na msichana wa Kichaga aliyeitwa Veridiana Mosha, yeye pia alikuwa mwalimu katika shule hiyo, na kujenga naye urafiki wa kimapenzi.
Matokeo ya urafiki wao yalisababisha ujauzito lakini mimba hiyo ikiwa na miezi sita mwalimu Martin aliomba uhamisho kwenda Mwanza ambako miaka mitatu baadaye alimwoa Cecilia Ndaki, mwanamke wa Kisukuma na miaka mitano baadaye mama huyo akawa mjamzito na kuzaa mtoto wao wa kwanza wa kiume ambaye walimwita jina la Mike!
Mike alikuwa ni mtoto mzuri mno, kila mtu alimpenda. Mama yake kila alipopanda basi na kusimama abiria walimgombania kumbeba mtoto huyo.
Je nini kitaendelea?