Hadithi nzuri za kusisimua

Hadithi nzuri za kusisimua

Elly official

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2018
Posts
767
Reaction score
1,029
NILIOLEWA NA JINI BILA YA KUTARAJIA 1:
Ilikuwa kwenye mida ya saa mbili usiku wakati tumekaaa kwaajili ya chakula cha usiku.
Wakati nakula simu yangu ikaita kuangalia mpigaji ni mpenzi wangu Sam ila nikashindwa kunyanyuka kwenda kupokea kwani mama alikuwa ananiangalia sana ikabidi nibonyeze kitufye cha kimya (silence).
Mama kumbe alisikia wakati inaita akauliza,
"Nani anakupigia wakati wa kula?"
"Hakuna mtu mama, ni alarm tu"
"Unadhani sijasikia wakati inaita? Umeanza uongo eeh!!"
"Hapana mama ni Sam"
"Nilijua tu, anakupigia wakati wa kula amekununulia hiyo simu? Anaijua bei yake?"
Ikabidi nikae kimya, mama yangu alikuwa anamchukia sana Sam. Hakupenda kabisa mahusiano ya mimi na Sam ingawa tulipendana sana.
Tulipomaliza kula tulikuwa tumekaa sebleni, nikatamani kuinuka kwenda chumbani nikazungumze kidogo na Sam na kumwambia kuwa muda aliokuwa anapiga nilikuwa nakula.
Nikawa nainuka, mama akaanza kuongea kabla hata sijaanza kutembea.
"Unaenda wapi Sabrina?"
"Naenda chumbani mara moja mama"
"Kuongea na simu eeh!! Amekupa nini huyo Sam jamani? Yani unashindwa kukaa hapa kuzungumza na mama yako na chakula kitulie, wewe macho juu juu kukimbilia ndani kuongea na Sam. Amekuwa mzazi wako huyo? Sipendi hiyo tabia, haya kaa tuzungumze ya maana hapa"
Ikabidi nikae ila mawazo yangu yote yalikuwa ni kwa Sam tu hata maneno ambayo mama alizungumza sikumuelewa hata kidogo, nikaona anapiga kelele tu.
Nadhani pale aliyekuwa anamsikiliza ni dada yangu Penina tu maana ndio waliokuwa wakijibishana.
Mama akaniomba simu yangu na kupigia ndugu zake, akaongea wee hadi muda wa maongezi ulipokata ndio akanirudishia. Nikabakiwa na ujumbe mfupi tu bila ya muda wa maongezi.
Mama aliponyanyuka nami nikanyanyuka kuelekea chumbani, kisha nikamtumia ujumbe mfupi Sam kuwa anipigia. Naye hakusita kunipigia ila alinipa lawama mwanzo mwisho.
"Sabrina una dharau sana, yani simu yangu hupokei. Nangoja kidogo kupiga namba inatumika yani kuna watu unawaona wanathamani sana kushinda mimi. Poa tu Sabrina"
"Jamani Sam mpenzi wangu, tafadhari nisamehe"
"Umefanya makusudi wewe, poa tu mi nalala saivi"
Halafu akakata simu, nikajisikia vibaya sana ikabidi nimtumie ujumbe wa kumuomba msamaha ila Sam hakupiga wala kujibu ujumbe wangu.
Sikuweza kumwambia Sam kama mama yangu anamchukia kwani nilijua wazi kuwa akijua tu lazima atajisikha vibaya ukizingatia kwao mama yake ananipenda sana mimi.
Asubuhi na mapema nikapata ujumbe toka kwa Sam.
"Yani wewe Sabrina una dharau sana, sijui kwavile umejua nakupenda sana. Yani umeshindwa hata kunipigia simu upooze mawazo yangu umekazana na ujumbe tu!! Najua muda wote wa maongezi umemaliza kwa watu wako ila poa tu. Mimi nitaendelea kukupenda Sabrina"
Nikaamua kuamka na kwenda kununua vocha ili nipate kuzungumza na Sam.
Ila maduka yalikuwa bado hayajafunguliwa, nikaamua kuanza kufanya kazi mbalimbali za pale nyumbani ili niwahi kumaliza na niweze kwenda kwa Sam kwani nililuwa nimemkumbuka na pia nilitaka nikamweleweshe ya jana.
Baada ya kazi nikamuaga mama kuwa naenda kumtembelea rafiki yangu Suzy, mama hakuwa na pingamizi akaniruhusu niende nami nikaenda moja kwa moja kwa Sam ila sikumkuta na mlango wake ulikuwa na kufuri.
Ikabidi niende duka la karibu kununua vocha kisha nikampigia ila hakupokea nikajua tu kisirani kimempanda.
Nikaamua kuondoka na kwenda kweli kwa kina Suzy ili badae nipate kurudi tena kumuangalia.
Nilikaa sana kwa kina Suzy ila sikumueleza Suzy jambo lolote lile kuhusu Sam, badae nikaaga na kwenda tena kwa Sam nikawa namngoja kuwa pengine ameenda kazini ila ilikuwa ni mwisho wa wiki ndiomana nilijiamini na kwenda.
Nilimngoja sana Sam bila ya kutokea, nilikata tamaa na moyo kuniuma sana kuwa kwanini Sam amenifanyia vile kwa kosa dogo kiasi kile.
Nikajaribu kuwauliza na majirani ambao walisema kuwa Sam ameondoka asubuhi sana, nikajiuliza kuwa labda ameenda kwao ila kwanini asipokee simu? Nikaona kuwa Sam ananifanyia kusudi, hisia mbaya zikanitawala kuwa Sam atakuwa kwa mwanamke mwingine tu hapo roho ikaniuma sana.
Muda ulizidi kwenda, ikabidi nirudi nyumbani.
Nilifika nyumbani kwenye mida ya saa tatu usiku, nikamkuta mama na dada wakifanya maongezi ya hapa na pale.
Nikawasalimia na kwenda kuoga kisha kula chakula.
Dada akaanza kuzungumza,
"Halafu wewe Sabrina, kupenda kwako huko kutembea usiku usiku ipo siku utakumbana na majini huko njiani"
Nikashtuka sana na kumuuliza dada,
"Majini? Una maana gani dada?"
"Usiku ni mida ya majini, yakikukumba huko usituletee balaa hapa"
"Kwani majini yakoje?"
"Ukikutana nayo lazima nywele zisisimke, halafu ni marefu sana mara nyingine huwezi ona mwisho wa urefu wao"
"Mbona unanitisha dada?"
"Sikutishi ila huo ndio ukweli, unatakiwa kuwa makini sana. Majini hayana masikhara, likikuvaa ndio limekuvaa utakula nalo, kulala nalo na kuamka nalo bila ya kutarajia"
Nikaanza kuingiwa na uoga, mama nae akaanza kuchangia hoja zake.
"Unakumbuka kule makaburini wakati wanamzika yule dada mwenye mashetani kilichotokea?"
Dada akajibu,
"Ndio nakumbuka mama, yani majini hayataki mchezo"
Ikabidi niulize tena,
"Kwani majini yanafanana na kitu gani"
"Majini yanatisha mdogo wangu usiombe ukutane nayo njiani unaweza usilale siku mbili unaweweseka tu."
"Inamaana yanaweza kutokea wakati mtu amelala?"
"Ndio, unaweza ukashangaa umelala na jini pembeni yako"
Niliogopa sana na kuwaza kwanini nimesikiliza habari za majini usiku.
Mama akaongezea kitu kingine ambacho kilifanya niende chumbani kumtafuta Sam.
"Ila leo umenifurahisha kitu kimoja, kwenda kweli kwa Suzy maana huyo Sam wako amekuwa hapa siku nzima kukungoja"
Nikagundua kuwa, wakati mimi namngoja Sam kule kwake kumbe na yeye alikuwa kwetu kuningoja ila kwanini hakutaka kupokea simu yangu.
Nikaenda zangu chumbani kwa lengo la kumpigia tena Sam simu.
Ila nikasita kwani nikaona Sam nae ananifanyia kusudi, kama kweli alikuwa kwetu kuningoja kitu gani kimemfanya asipokee simu yangu. Mara dada akaniita na kufanya yale mawazo yangu juu ya Sam yakatike.
"Vipi Sabrina ndio unataka kulala muda huu?"
"Ndio dada, nataka kulala"
"Njoo mara moja, kuna kitu nataka unisaidie huku chumbani kwangu"
Nikatoka na kufatana na dada hadi chumbani kwake.
"Kuna kitu kinanichanganya hapa kwenye computer yangu, naomba uniondolee hii picha"
Mimi nikaitazama ile picha, ilikuwa ni ya mwanaume mzuri sana. Nikamuuliza dada kuwa kwanini anataka kuifuta,
"Kwanini uifute dada? Mbona picha yenyewe ni nzuri?"
"Hata sielewi nimeidownload vipi hiyo picha hadi imekaa hapo, nitolee bhana mipicha mingine inaweza kuwa ya majini"
"Mbona unapenda sana story za majini dada?"
"Yapo na ndiomana nayaongelea, usishangae siku ukitokewa na jini"
"Basi yaishe, mi sitaki tena hizo habari nisije kushindwa kulala bure"
Nikafanya ninachojua kuifuta ile picha kisha nikamuaga dada usiku mwema na kuondoka.
Nikarudi chumbani na kuendelea kuwaza kuhusu Sam wangu. Wakati nikiwaza juu ya Sam, wazo la majini likanijia tena kichwani nikajikuta naanza kuogopa chumbani halafu ile picha ambayo dada aliniomba kuwa nimsaidie kufuta ikawa inatembea kichwani mwangu.
Niliona chumba kimekuwa kikubwa sana, nilipokaa kitandani nilihisi kama vile kuna mtu pembeni yangu nikaanza kuogopa zaidi huku nikijilaumu kuwa kwanini nimesikiliza stori za kutisha muda wa kulala.
Nikachukua tena simu na kuamua kumpigia Sam ili kujiliwaza kidogo ila kabla sijapiga nikapitiwa na usingizi.
Mwanaume mzuri sana na mtanashati alikuwa mbele yangu, asili yake kama mwarabu hivi au muhindi.
Alikuwa anatabasamu na kusogea taratibu kuja mahali ambako mimi nipo.
Nilikuwa namwangalia kwa jicho la mshangao tu.
Alipofika karibu yangu, akanivuta mkono kisha akatoa kitu cha ajabu kilichofanya nishtuke.
 
NILIOLEWA NA JINI BILA YA KUTARAJIA 1:
Ilikuwa kwenye mida ya saa mbili usiku wakati tumekaaa kwaajili ya chakula cha usiku.
Wakati nakula simu yangu ikaita kuangalia mpigaji ni mpenzi wangu Sam ila nikashindwa kunyanyuka kwenda kupokea kwani mama alikuwa ananiangalia sana ikabidi nibonyeze kitufye cha kimya (silence).
Mama kumbe alisikia wakati inaita akauliza,
"Nani anakupigia wakati wa kula?"
"Hakuna mtu mama, ni alarm tu"
"Unadhani sijasikia wakati inaita? Umeanza uongo eeh!!"
"Hapana mama ni Sam"
"Nilijua tu, anakupigia wakati wa kula amekununulia hiyo simu? Anaijua bei yake?"
Ikabidi nikae kimya, mama yangu alikuwa anamchukia sana Sam. Hakupenda kabisa mahusiano ya mimi na Sam ingawa tulipendana sana.
Tulipomaliza kula tulikuwa tumekaa sebleni, nikatamani kuinuka kwenda chumbani nikazungumze kidogo na Sam na kumwambia kuwa muda aliokuwa anapiga nilikuwa nakula.
Nikawa nainuka, mama akaanza kuongea kabla hata sijaanza kutembea.
"Unaenda wapi Sabrina?"
"Naenda chumbani mara moja mama"
"Kuongea na simu eeh!! Amekupa nini huyo Sam jamani? Yani unashindwa kukaa hapa kuzungumza na mama yako na chakula kitulie, wewe macho juu juu kukimbilia ndani kuongea na Sam. Amekuwa mzazi wako huyo? Sipendi hiyo tabia, haya kaa tuzungumze ya maana hapa"
Ikabidi nikae ila mawazo yangu yote yalikuwa ni kwa Sam tu hata maneno ambayo mama alizungumza sikumuelewa hata kidogo, nikaona anapiga kelele tu.
Nadhani pale aliyekuwa anamsikiliza ni dada yangu Penina tu maana ndio waliokuwa wakijibishana.
Mama akaniomba simu yangu na kupigia ndugu zake, akaongea wee hadi muda wa maongezi ulipokata ndio akanirudishia. Nikabakiwa na ujumbe mfupi tu bila ya muda wa maongezi.
Mama aliponyanyuka nami nikanyanyuka kuelekea chumbani, kisha nikamtumia ujumbe mfupi Sam kuwa anipigia. Naye hakusita kunipigia ila alinipa lawama mwanzo mwisho.
"Sabrina una dharau sana, yani simu yangu hupokei. Nangoja kidogo kupiga namba inatumika yani kuna watu unawaona wanathamani sana kushinda mimi. Poa tu Sabrina"
"Jamani Sam mpenzi wangu, tafadhari nisamehe"
"Umefanya makusudi wewe, poa tu mi nalala saivi"
Halafu akakata simu, nikajisikia vibaya sana ikabidi nimtumie ujumbe wa kumuomba msamaha ila Sam hakupiga wala kujibu ujumbe wangu.
Sikuweza kumwambia Sam kama mama yangu anamchukia kwani nilijua wazi kuwa akijua tu lazima atajisikha vibaya ukizingatia kwao mama yake ananipenda sana mimi.
Asubuhi na mapema nikapata ujumbe toka kwa Sam.
"Yani wewe Sabrina una dharau sana, sijui kwavile umejua nakupenda sana. Yani umeshindwa hata kunipigia simu upooze mawazo yangu umekazana na ujumbe tu!! Najua muda wote wa maongezi umemaliza kwa watu wako ila poa tu. Mimi nitaendelea kukupenda Sabrina"
Nikaamua kuamka na kwenda kununua vocha ili nipate kuzungumza na Sam.
Ila maduka yalikuwa bado hayajafunguliwa, nikaamua kuanza kufanya kazi mbalimbali za pale nyumbani ili niwahi kumaliza na niweze kwenda kwa Sam kwani nililuwa nimemkumbuka na pia nilitaka nikamweleweshe ya jana.
Baada ya kazi nikamuaga mama kuwa naenda kumtembelea rafiki yangu Suzy, mama hakuwa na pingamizi akaniruhusu niende nami nikaenda moja kwa moja kwa Sam ila sikumkuta na mlango wake ulikuwa na kufuri.
Ikabidi niende duka la karibu kununua vocha kisha nikampigia ila hakupokea nikajua tu kisirani kimempanda.
Nikaamua kuondoka na kwenda kweli kwa kina Suzy ili badae nipate kurudi tena kumuangalia.
Nilikaa sana kwa kina Suzy ila sikumueleza Suzy jambo lolote lile kuhusu Sam, badae nikaaga na kwenda tena kwa Sam nikawa namngoja kuwa pengine ameenda kazini ila ilikuwa ni mwisho wa wiki ndiomana nilijiamini na kwenda.
Nilimngoja sana Sam bila ya kutokea, nilikata tamaa na moyo kuniuma sana kuwa kwanini Sam amenifanyia vile kwa kosa dogo kiasi kile.
Nikajaribu kuwauliza na majirani ambao walisema kuwa Sam ameondoka asubuhi sana, nikajiuliza kuwa labda ameenda kwao ila kwanini asipokee simu? Nikaona kuwa Sam ananifanyia kusudi, hisia mbaya zikanitawala kuwa Sam atakuwa kwa mwanamke mwingine tu hapo roho ikaniuma sana.
Muda ulizidi kwenda, ikabidi nirudi nyumbani.
Nilifika nyumbani kwenye mida ya saa tatu usiku, nikamkuta mama na dada wakifanya maongezi ya hapa na pale.
Nikawasalimia na kwenda kuoga kisha kula chakula.
Dada akaanza kuzungumza,
"Halafu wewe Sabrina, kupenda kwako huko kutembea usiku usiku ipo siku utakumbana na majini huko njiani"
Nikashtuka sana na kumuuliza dada,
"Majini? Una maana gani dada?"
"Usiku ni mida ya majini, yakikukumba huko usituletee balaa hapa"
"Kwani majini yakoje?"
"Ukikutana nayo lazima nywele zisisimke, halafu ni marefu sana mara nyingine huwezi ona mwisho wa urefu wao"
"Mbona unanitisha dada?"
"Sikutishi ila huo ndio ukweli, unatakiwa kuwa makini sana. Majini hayana masikhara, likikuvaa ndio limekuvaa utakula nalo, kulala nalo na kuamka nalo bila ya kutarajia"
Nikaanza kuingiwa na uoga, mama nae akaanza kuchangia hoja zake.
"Unakumbuka kule makaburini wakati wanamzika yule dada mwenye mashetani kilichotokea?"
Dada akajibu,
"Ndio nakumbuka mama, yani majini hayataki mchezo"
Ikabidi niulize tena,
"Kwani majini yanafanana na kitu gani"
"Majini yanatisha mdogo wangu usiombe ukutane nayo njiani unaweza usilale siku mbili unaweweseka tu."
"Inamaana yanaweza kutokea wakati mtu amelala?"
"Ndio, unaweza ukashangaa umelala na jini pembeni yako"
Niliogopa sana na kuwaza kwanini nimesikiliza habari za majini usiku.
Mama akaongezea kitu kingine ambacho kilifanya niende chumbani kumtafuta Sam.
"Ila leo umenifurahisha kitu kimoja, kwenda kweli kwa Suzy maana huyo Sam wako amekuwa hapa siku nzima kukungoja"
Nikagundua kuwa, wakati mimi namngoja Sam kule kwake kumbe na yeye alikuwa kwetu kuningoja ila kwanini hakutaka kupokea simu yangu.
Nikaenda zangu chumbani kwa lengo la kumpigia tena Sam simu.
Ila nikasita kwani nikaona Sam nae ananifanyia kusudi, kama kweli alikuwa kwetu kuningoja kitu gani kimemfanya asipokee simu yangu. Mara dada akaniita na kufanya yale mawazo yangu juu ya Sam yakatike.
"Vipi Sabrina ndio unataka kulala muda huu?"
"Ndio dada, nataka kulala"
"Njoo mara moja, kuna kitu nataka unisaidie huku chumbani kwangu"
Nikatoka na kufatana na dada hadi chumbani kwake.
"Kuna kitu kinanichanganya hapa kwenye computer yangu, naomba uniondolee hii picha"
Mimi nikaitazama ile picha, ilikuwa ni ya mwanaume mzuri sana. Nikamuuliza dada kuwa kwanini anataka kuifuta,
"Kwanini uifute dada? Mbona picha yenyewe ni nzuri?"
"Hata sielewi nimeidownload vipi hiyo picha hadi imekaa hapo, nitolee bhana mipicha mingine inaweza kuwa ya majini"
"Mbona unapenda sana story za majini dada?"
"Yapo na ndiomana nayaongelea, usishangae siku ukitokewa na jini"
"Basi yaishe, mi sitaki tena hizo habari nisije kushindwa kulala bure"
Nikafanya ninachojua kuifuta ile picha kisha nikamuaga dada usiku mwema na kuondoka.
Nikarudi chumbani na kuendelea kuwaza kuhusu Sam wangu. Wakati nikiwaza juu ya Sam, wazo la majini likanijia tena kichwani nikajikuta naanza kuogopa chumbani halafu ile picha ambayo dada aliniomba kuwa nimsaidie kufuta ikawa inatembea kichwani mwangu.
Niliona chumba kimekuwa kikubwa sana, nilipokaa kitandani nilihisi kama vile kuna mtu pembeni yangu nikaanza kuogopa zaidi huku nikijilaumu kuwa kwanini nimesikiliza stori za kutisha muda wa kulala.
Nikachukua tena simu na kuamua kumpigia Sam ili kujiliwaza kidogo ila kabla sijapiga nikapitiwa na usingizi.
Mwanaume mzuri sana na mtanashati alikuwa mbele yangu, asili yake kama mwarabu hivi au muhindi.
Alikuwa anatabasamu na kusogea taratibu kuja mahali ambako mimi nipo.
Nilikuwa namwangalia kwa jicho la mshangao tu.
Alipofika karibu yangu, akanivuta mkono kisha akatoa kitu cha ajabu kilichofanya nishtuke.
Inaendelea...........
 
NILIOLEWA NA JINI BILA YA KUTARAJIA 2:
Akanivuta mkono kisha akatoa kitu cha ajabu kilichofanya nishtuke.
Nikajikuta jasho jingi likinitoka pale kitandani, nikawa najiuliza kuwa ni ndoto ya aina gani na inamaanisha kitu gani? Je huyo mwanaume mzuri sana kushinda Sam wangu ni nani?
Hapo ndio nikakumbuka kuwa natakiwa kumpigia Sam simu.
Nikaangalia simu yangu na kuichukua kisha nikaibonyeza, nikakuta simu ambazo hazijapokelewa kumi (10 missed call), kuangalia zote ni kutoka kwa Sam na ujumbe mfupi tano (5 messages).
Kila ujumbe ulikuwa ni wa lawama tu kutoka kwa Sam, nikaona haya majanga sasa.
Nikabonyeza simu na kuanza kupiga nikasikia,
"Salio lako halitoshi kupiga simu, tafadhari ongeza........."
Nikaishusha ile simu na kuikata, kuangalia kweli nimebakiwa na sifuri nikaanza kujiuliza kuwa nimeitumiaje ndipo nikakumbuka kuwa nilinunua salio na kusahau kujiunga na huduma za bure na wakati narudi nyumbani nilimpigia Suzy na kuongea nae sana tu nikijua nimejiunga kumbe sikujiunga, vocha yangu yote ya elfu mbili imekwenda bure bure bila hata ya faida sikujua cha kufanya kwa wakati huo.
Nikatamani niende chumbani kwa mama nikachukue simu yake na kuhamishia salio lake kwangu kama ana salio.
Nikainuka pale kitandani na kusogelea mlango kisha nikafungua, wazo la stori za majini likanijia tena kichwani na kujikuta nikiubamiza ule mlango kwa kuufunga na kurudi tena kitandani, nikajiuliza kuwa kwanini ile stori ya majini imenikaa sana kichwani mwangu? Nikaanza tena kufikiria ile ndoto kuwa ilikuwa na maana gani kwangu.
Sikuweza kulala tena kwa uoga na pia bado nilikuwa na mawazo juu ya Sam.
Asubuhi yake, mimi ndio nilikuwa wa kwanza tena kuamka, nikafanya usafi na kazi za hapa na pale nyumbani huku nikingoja pakuche vizuri nikanunue vocha ya kuweza kumpigia Sam.
Nilipomaliza usafi nilirudi tena chumbani, nikajilaza kitandani na usingizi ukanichukua hapohapo.
Yule mkaka mtanashati akaanza kunionyesha mali zake, zilikuwa nyingi sana. Kumbe yule mkaka alikuwa tajiri, akanionyesha magari ya aina nne halafu akaniambia kuwa nichague moja liwe langu naye atanipa lotelote, nikawa natabasamu kwani magari yalikuwa mazuri sana na ndoto zangu siku zote ni kuwa na gari ila gafla nikakumbuka kuwa nina Sam wangu ambaye hawezi kunipa vyote vile ila anaweza kunipa mapenzi ya dhati, nikajikuta nikishtuka na kupiga kelele.
"Saaaaaaaaaammmmmm....."
Mama akaja chumbani na kusema.
"Wee Sabrina wewe, usiniletee uchuro nyumbani kwangu. Yani wewe kuamka tu na kumtaja Sam! Amekuwa Mungu huyo Sam?"
"Hapana mama, ila nimeota vibaya"
Jasho nalo lilikuwa lanitoka.
"Umeota vibaya kivipi? Umeota Sam anachinjwa au?"
"Hapana mama."
"Haya inuka hapo, kuna mboga ya kukata kata huku"
Nikainuka tena pale kitandani na kumfata mama jikoni, kisha kukiendea kisu na kukata kata ile mboga.
Mawazo yalikuwa ni juu ya ile ndoto na yale magari, kisha nikakumbuka tena kuwa nilitakiwa kununua vocha na kumpigia Sam.
Nilikata mboga haraka haraka na kuibandika jikoni kisha nikajitanda vizuri ili niende dukani kwanza.
Kabla sijatoka mama akauliza,
"Unaenda wapi Sabrina?"
"Naenda dukani mama."
"Kufanya nini?"
"Kununua vocha mama"
"Ili umpigie Sam eeh!! Sijui huyo mwanaume amekupa nini mwanangu unakuwa kama chizi"
Sikutaka kumsikiliza zaidi kwani nilijua kuwa lazima atanizuia tu.
Nilinunua vocha na kurudi nyumbani. Nikamkuta mama sebleni,
"Huna adabu mwanangu Sabrina, yani umeona vocha ya maana kuliko maneno yangu? Vocha ambayo pesa nakupa mimi!!"
Nilibaki kumuangalia tu mama na maneno yake kwani nilijua yote sababu hataki niwasiliane na Sam.
"Haya lete hiyo vocha haraka"
Nilimpa ile vocha mama kwa shingo upande kwani moyo uliniuma sana, nikatamani hata kuwa na maisha ya kwangu. Nikatamani kutoa machozi mbele yake ila nikajizuia kwa kufumba macho ili mama asinione mzembe, ingawa na kujizuia kule bado machozi yalipenya na kudondoka mashavuni mwangu.
"Kaone kalivyo kajinga, eti kanamlilia mwanaume. Hebu niondolee uchizi wako mbele yangu haraka"
Nikaondoka na kukimbilia chumbani, huko nililia nitakavyo katika kupooza uchungu wangu.
Nilipotazama tena simu nikaona ujumbe wa Sam tena wa kutosha, sikuweza kujibu hata jumbe moja kwa kukosa vocha. Nikajikuta nikiulaumu mtandao ninaotumia pia kwa kushindwa kutuma tafadhari nipigie.
Nilizidi kutokwa na machozi tu mule ndani.
Wakati nalia nikasikia mtu akigonga mlango wa chumba changu, nikashtuka na kujiuliza ni nani maana dada na mama hawanaga hodi, huwa wanaingia tu chumbani.
Nikamuitikia kuwa aingie ndani, huku nikimaliza kujikausha machozi yangu. Kumbe alikuwa ni rafiki yangu mpenzi Lucy, nilifurahi kumuona nikainuka pale kitandani na kumkumbatia, nikamkaribisha vizuri sana.
Kumbe Lucy naye alishangazwa na hali aliyonikuta nayo,
"Nimekungoja sana hapo sebleni kwenu ndipo mama yako aliposema nikufate chumbani eti umechukia sababu ya mwanaume. Mmh! Mwanaume gani tena huyo Sabrina?"
Nikamueleza kwa kifupi kuhusu Sam kwani Lucy alikuwa hajui chochote kuhusu Sam.
"Inamaana kushindwa kuwasiliana nae ndio kunakuliza jamani shoga yangu? Chukua basi simu yangu uwasiliane nae maana ina muda wa kutosha"
Nikachukua simu ya Lucy na kumpigia simu ambapo alishangaa kuona namba ngeni.
"Mbona namba mpya hii, ni ya nani?"
"Ni ya rafiki yangu mmoja anaitwa Lucy ila wewe humjui, ipo siku utamjua"
Wakati nazungumza na Sam, Lucy nae akaniomba simu ili amsalimie shemeji yake huyo, nami nikamkabidhi.
Baada ya salamu tukazungumza na Sam kisha tukapatana tena na kusameheana kwa yote yaliyopita halafu Sam akanitumia vocha ili niache kumpigia kwa namba mpya.
Kilichobaki ilikuwa ni stori na vicheko baina yangu na Lucy.
"Mmh shemeji ana sauti ya kuvutia huyo, yaonyesha atakuwa handsome sana"
"Mmh Lucy ushaanza maneno yako, hukui wewe?"
"Kwani nikimsifia shem wangu kuna ubaya Sabrina?"
"Hakuna ubaya"
"Ila ningependa kumfahamu zaidi, natumaini ipo siku utanikutanisha nae"
Niliongea mengi sana na Lucy ila alikazana sana kumsifia Sam hadi akawa ananipa mashaka ila sikuyatilia maanani sana.
Lucy alipoaga, nilimsindikiza akaondoka.
Jioni ilipoingia kama kawaida ya siku hizi za karibuni, wakaanza tena stori zao za majini na aliyeanzisha alikuwa ni dada yangu Penina.
"Jamani Posta kuna mambo, yani mtu niliyepishana nae ni dhahiri kabisa alikuwa jini maana nywele zote zilinisimama"
Mama nae akadakia,
"Ulikuwa hujui mwanangu? Yani Posta na Kariakoo hakuwezi kukosa majini kule, unadhani unaopishana nao huko wote ni watu basi! Nusu yao ni majini"
Nikaanza kuogopa tena kwa yale maneno na hata sikujua kwanini mimi yaliniogopesha wakati wao walioyaongea hawakuogopa.
"Hivi jamani, kwanini ikifika usiku ndio mnaanza hizo stori za majini? Hakuna stori zingine?"
Dada akaanza kunicheka kuwa kwanini naogopa wakati ni kitu cha kawaida tu.
"Sasa wewe Sabrina unaogopa nini? Unadhani yatakutokea?"
"Naogopa tu jamani"
Mara mama akanitisha,
"Haya, huyo nyuma yako"
Nilipiga kelele na kurukaruka, huku wote wakiwa wananicheka.
"Hutakiwi kuogopa mwanangu, haya ni mambo ya kawaida na wengi yanawapata ndiomana tunayaongelea. Na ukitaka kutokuogopa kitu basi wewe kizoee"
"Ndio kuzoea majini mama?"
"Hapana si kuzoea majini, ila stori hizi uzione kama kawaida na hautapata shida tena"
Wakaendelea kusimuliana mambo ya watu wanaofufuka na majini.
Ikabidi nimuulize dada kuhusu ile picha aliyoniomba niifute jana yake.
"Dada, nakumbuka uliniambia kuwa majini ni mabaya na sura zao zina tisha. Mbona yule mkaka mzuri ulisema tufute picha yake kuwa huenda akawa jini?"
"Nilikuwa najisemea tu ila hata hivyo majini yanamtindo wa kubadilika kama kinyonga"
Mama akaingilia mazungumzo yetu.
"Kumbe na wewe Sabrina unawajua wakaka wazuri? Mbona ukampenda Sam basi?"
Dada akanisaidia kujibu,
"Ila Sam sio mbaya jamani mama, humpendi tu sababu ya kipato ila usisingizie uzuri"
Nikawaacha na kwenda chumbani kwangu. Nikaenda kuoga kisha kujiandaa kulala.
Usiku wa leo ulikuwa na uoga kiasi kwangu na furaha pia kwani vocha nilikuwa nayo na Sam nilishapatana naye.
Nilipokuwa tu kitandani nikampigia Sam simu ili kupotezea yale mawazo ya stori ambazo mama na dada walikuwa wakisimuliana.
Niliongea sana na Sam kwenye simu hadi saa saba usiku kisha nikapitiwa na usingizi huku simu ikiwa sikioni.
Nilikuwa ufukweni (beach) na Sam tukifurahia upepo na kuchezea maji. Sam alivaa nguo nyeupe na mimi nilivaa gauni la pinki, tulifanya mambo mengi sana ambayo wapendanao huwa wanafanya.
Tukaanza mchezo wa kufunikana macho kwa nyuma na wakati huo Sam alikuwa nyuma yangu na mikono yake imepita juu ya mabega yangu kisha viganja vyake vilifunika macho yangu, akaanza kunitembeza na kunipeleka nisipopajua.
Kufika mbele akaniuliza,
"Nikufumbue macho nisikufumbue?"
Nami nikamjibu kwa sauti ya taratibu tena ile ya kudeka,
"Nifumbue bwana"
Basi Sam akaachia vile viganja vya mikono yake nami nikapata kuona kilichopo mbele yangu, nikamuona yule mkaka wa kwenye ndoto akiwa mbele yangu na alivaa nguo nyeupe tupu kuanzia kiatu, suruali hadi shati.
Nikajikuta nikitetemeka ila yeye alikuwa akitabasamu, nikaangalia nyuma yangu kama yupo Sam ila hakuwepo na sikujua ameelekea wapi, nikaanza kukimbia huku yule mkaka akinifata nyuma alipokaribia kunishika nikashtuka kumbe nilikuwa naota.
Jasho jingi lilinitoka, kutazama nje kulikuwa kumekucha kabisa yani kama sio saa mbili basi ni saa tatu.
Kabla sijafanya chochote, simu yangu ikawa inaita kuangalia ni Sam anapiga basi nikaipokea, baada ya salamu nikamsikia.
"Uwahi kujiandaa mpenzi ili badae twende beach, sawa Sabrina. Halafu uvae lile gauni lako la pinki"
Niliendelea kuweka ile simu sikioni bila ya kujua cha kujibu.
 
Mkuu kabla hujapost kitu uwe unaandika unachopost kwnye sehem ya kusearch alafu urudi tena kuandika.....Hii hadithi unayoipost ipo humu muda mrefu sana
 
Ukianzisha hadithi za vita vita ama za kijasusi nitag Mkuu, naona huku nimechochola
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom