Stephen Ngalya Chelu
JF-Expert Member
- Oct 31, 2017
- 8,288
- 18,571
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI.
SEHEMU YA KWANZA.
Mtunzi & Mwandishi: Stephen Chelu
Utangulizi:
Simulizi hii imejengwa kwa kutumia matukio halisi na ya kufikirika ili kuleta mvuto zaidi kwa msomaji.
Hadithi hii inajengwa katika maisha ya kawaida ya mtaani, hivyo kunaweza kuwa na matumizi ya lugha isiyo na tafsida, lengo si kuvunja kanuni za maadili bali kuonyesha uhalisia wa matukio yenyewe.
=======================
SASISHO
Naona mods wamehariri content kwa kuondoa/kubadili maneno yenye ukakasi kwa maana ya kuwa hakuna njia tunaweza kuyatumia tena katika sehemu zijazo. Hivyo kuanzia sasa nitaweka simulizi ambayo tayari itakuwa imehaririwa kwa kuwaondoa maneno hayo yasiyo na tafsida ili kuwapunguzia mods kazi.
Itakuwa inakuja mara moja kwa wiki.
========================
SASISHO
Kuna mdau kaoma iwe inakuja mara mbili kwa wiki, hivyo kuanzia sasa itakuwa inakuja mara mbili kwa wiki. (Jumamosi na jumatano).
Tuanze sasa....
“Karibu sana kijana, jisikie huru. Nadhani umeshaelekezwa mahali pa kupata huduma zote muhimu kama bomba la maji, choo na bafu” Yalikuwa ni maneno ya mwenye nyumba baada ya kumaliza kusaini mkataba wa pango la nyumba.
“Usijali mzee nipo sawa, Mama alinielekeza” Nilimjibu kwa mkato nikitamani aondoke ili aniache nipumzike. Muda huo rafiki yangu na mwenyeji wangu, Denis alikuwa amekaa pembeni akiwa kimya akifuatilia mazungumzo yangu na mwenye nyumba.
“Ok, sawa. Ngoja nikuacheni mpumzike.” alisema baba mwenye nyumba huku akinyanyuka akielekea nje. Ni Kama alikuwa akijua ni nini nilikuwa nawaza.
“Asante mzee, nashukuru sana.”
“usijali kijana, unakaribishwa.”
Alifungua mlango na akatoka nje na kutuacha mimi na Denis tukiwa ndani ya chumba ambacho kwa muda huo mimi ndiye niliyekuwa mpangaji rasmi au naweza sema mmliki wa muda. Nilimwangalia Denis ambaye alikuwa ananiangalia Mimi, tukatabasamu huku nikitikisa kichwa juu chini.
“Sasa dogo maisha ndo yameanza hivo” alisema Denis
“daaah aise kweli mzee baba” nilimjibu
“sasa we si bado unapumzika nini, ngoja mi niingie geto nikakorofishe, si unajua shemeji yako ni mtoro mtoro, anakwepa majukumu.”
“hahahaha poa bhana, ngoja mi nijipumzishe, then midamida ntakustua”
“poa, kwani unalala masaa mangapi mzee wa kazi?”
“si muda mrefu, natoa uchovu tu”
“ok poa, mi ntakuja mida saa 12 twende tukatembee kidogo”
“ok fresh tutasomana mjuba”
“Poa” Alisema Denis akinyanyuka na kuondoka.
Denis hakuwa akiishi mbali na pale nilipokuwa naishi mimi, ilikuwa ni umbali wa mwendo wa dakika kama saba au nane hivi kwa miguu. Denis ndiye aliyefanya mpango wa kunitafutia chumba baada ya kumwambia kuwa nina mpango wa kuja mjini. Ni rafiki yangu wa karibu na urafiki wetu si wa kukutana barabarani bali tulikuwa tukifahamiana vizuri tangu tukiwa wadogo. Tulisoma shule ya msingi pamoja na pia shule ya upili tulisoma pamoja pia hadi pale nilipofika kidato cha tatu ambapo nililazimika kuacha shule.
Pia Denis ndiye aliyefanya mpango wa mimi kupata dili la kuuza nyama kwenye moja ya bucha hapa mjini. Ndiyo, nilikuwa nategemea kuanza kufanya kazi buchani ili kujaribu kutafuta maisha. Siku iliyokuwa inafuata ndiyo siku ilikuwa natakiwa kwenda kuripoti kazini kwa mara ya kwanza. Denis alikuwa ni moja ya marafiki wazuri ambao niliwahi kuwa nao.
Nilijikusanya na kujilaza kwenye godoro lililokuwa limetandikwa sakafuni nikalala. Ndiyo, sakafuni, sikiwa na kitanda, nikitolee wapi? Mara kidogo usingizi ukanipitia.
Nilikuja kuamka baada ya masaa manne hivi, muda huo ilikuwa yapata kama saa kumi na moja. Niliamka na kuanza kupanga baadhi ya vitu ndani ya chumba angalau kukiweka katika mpangilio mzuri japokuwa sikuwa na vitu vingi. Nilikuwa na godoro, begi la nguo, ndoo mbili, jiko la gesi na vyombo vichache vya kupikia. Baaada ya kumaliza kuyafanya hayo nilifungua begi langu la nguo ili kuzitoa baadhi ya nguo na kuzitundika kwenye hang’a. Baada ya kumaliza zoezi hilo nilifungua zipu ya juu ya begi ili nichukue chaja ya simu, wakati nafanya hili niliona kitu ambacho kilifanya moyo wangu ushituke. Si ni kwa sababu kilikuwa na kitu cha kutisha, bali nilikuwa nimesahau kuwa nilikuwa na kitu cha aina ile.
Kitu hiki kilinikumbusha mbali, japokuwa haikuwa mbali sana. Hadi kufikia muda huo ilikuwa imepita kama miaka minne hivi. Kilinikumbusha tukio lililobadili dira nzima ya maisha yangu. Tukio lililofanya niamue kuacha shule nikiwa kidato cha tatu. Tukio lililofanya nipoteze marafiki wengi.
Tukio lililofanya wazazi wangu wapunguze upendo wao kwangu, japokuwa hali ya hewa ilikuja kutulia baadae, lakini haukuwa upendo ule ambao nilikuwa nikiupokea tangu utoto hadi siku ya kabla ya tukio hilo. Tukio lililonifanya nikawa na msongo wa mawazo kwa muda mrefu. Tukio ambalo huwa nashindwa kujizuia kumwaga machozi kila nikilikumbuka.
Kitu chenyewe kilichonirudisna miaka minne nyuma kilikuwa ni bahasha. Ndiyo, bahasha tu. Niliishika mkononi huku nikiiangalia macho yakilengwa na machozi. Sikutaka kuifungua, maana nilikuwa najua ni nini hasa kilikuwa ndani ya bahasha hiyo, nilikijua fika.
Mawazo yangu yalikuja kukatizwa na mtu aliyegonga mlango. Kabla ya kumjibu alisikika akisema “vipi bado umelala tu?”. Alikuwa ni Denis
Nikanyanyuka kwenda kufungua mlango. Alipoingia akaniangalia, akaonyesa sura ya kuwa na wasiwasi na mimi huenda kuna kitu hakipo sawa ila kwa sababu nilikiuwa nimetoka kulala, huenda alidhani ni usingizi tu. Akapita ndani, akakaa kwenye godoro, kwa bahati iliyo mbaya, alikalia ile bahasha.
“Oooh…ni nini hiki nimekalia, ni vyeti amah?’ alisema huku akinyanyuka kuangalia ilikuwa na nini. Alipoiona ile bahasha alishtuka.
Alishtuka kwa sababu alikuwa anaifahamu vizuri hiyo bahasha. Alijua kila kitu kilichosababisha hiyo bahasha ikawepo. Ni kwa sababu wakati hayo yote yalipokuwa yakitokea, yeye alikuwani mtu wangu wa karibu hivyo alikuwa akifahamu kila kitu.
Alinitazama kwa muda kisha akauliza “ni lini utaacha kufikiri kuhusu hili jambo?’
“Wewe unadhani ni rahisi kiasi gani?’ nilimjibu
“Ni miaka minne sasa, bado unakumbuka na linakutesa kama limetokea jana, tupa hii kitu mbali, wewe ni mwanaume”
“Tatizo huwa tunadhani kuwa ukiwa mwanaume unakuwa si binadamu wa kawaida, mimi ni binadamu mwenye hisia na pia hii ni sehemu ya maisha yangu, siwezi tupa”
“Ona ulivyokaa kihuzuni, yalishatokea yakapita, hata ukitumia miaka mia kufikiria kulihusu, huwezi badilisha hata sekunde moja ya tukio lenyewe”
“Sijawahi kufikiria kubadilisha chochote katika tukio hilo lakini kama siwezi kulibadilisha si vibaya nikiruhusu linibadilishe ”
“huko aliko hakukumbuki, hana uwezo na nafasi ya kufanya hivyo, unalijua vizuri hili”
“Hilo si tatizo kwangu, mimi kumkumbuka yeye inatosha sana” nilisema huku nikiibeba ile bahasha na kwenda kuiweka kwenye begi.
“anyway……tuachane na hilo, vipi umejiandaaje hiyo kesho?’
“Aaah kuna cha kujiandaa tena hapo!” nilisema nikifunga zipu ya begi
“Kwa hiyo, wewe ni mzoefu sio!”
“Kutoka wapi? uzoefu unaupatia huko huko”
“ila kuwa makini tu jembe, maana hapa mjini usipoangalia unapotea hivihivi, cha msingi ni kuangalia hasa wewe unahitaji nini katika maisha yako.”
“Yaaap……ni kweli, nalifahamu hilo, cha msingi ni kuweka mkazo tu.”
“ok poa……….tunasepa au?’ aliuliza
“Au” nilimjibu
“hujaacha ujinga wako bado.” Alisema Denis huku akicheka.
“Kwani wewe ulishaacha?” nilisema huku nikinyanyuka nikiashiria kuwa tuondoke.
“siwezi kuacha kwa sababu sikuwahi kuwa. Ila wewe ulikuwa mi msumbufu sana japo ulikuwa na wa chini chini”
“amna aiseee…..sema mimi sikuwa na ule utukutu kivile but sikuwa na aibu, labda hicho tu”
“aah wapi…wewe ulikuwa hatari , hivi unakumbuka ile siku ulimla denda Nancy mbele ya darasa?”
Nilijikuta nacheka kwa sauti kubwa, lilikuwa ni tukio moja la kuvutia sana. Nakumbuka ilikuwa ni katika kipindi cha fema club. Ikuwa katika igizo lililokuwa linahusu kuonyesha ni jinsi gani msichana anaweza kushawishiwa a kujikuta kujiingiza katika masuala ya mapenzi ilhali bado yupo shuleni. Sasa mimi nilikuwa katika nafasi ya kajana anayemshawishi huyo msichana. Sasa wakati tunaendelea na igizo, ambalo muda huo nilikuwa namtongoza nikajikuta napandwa na mzuka, si nakamkamata mtoto nikampiga denda mbele ya kadamnasi….acha watu walipuke na shangwe. Ilikuwa ni kumbukumbu nzuri sana.
Tuliendelea kukumbushana mambo baadhi tuliyoyafanya wakati tukiwa shule. Ilinisaidia kuondoa mawazo niliyokuwa nayo kuhusu ile bahasha.
Itaendelea...
SEHEMU YA KWANZA.
Mtunzi & Mwandishi: Stephen Chelu
Utangulizi:
Simulizi hii imejengwa kwa kutumia matukio halisi na ya kufikirika ili kuleta mvuto zaidi kwa msomaji.
Hadithi hii inajengwa katika maisha ya kawaida ya mtaani, hivyo kunaweza kuwa na matumizi ya lugha isiyo na tafsida, lengo si kuvunja kanuni za maadili bali kuonyesha uhalisia wa matukio yenyewe.
=======================
SASISHO
Naona mods wamehariri content kwa kuondoa/kubadili maneno yenye ukakasi kwa maana ya kuwa hakuna njia tunaweza kuyatumia tena katika sehemu zijazo. Hivyo kuanzia sasa nitaweka simulizi ambayo tayari itakuwa imehaririwa kwa kuwaondoa maneno hayo yasiyo na tafsida ili kuwapunguzia mods kazi.
Itakuwa inakuja mara moja kwa wiki.
========================
SASISHO
Kuna mdau kaoma iwe inakuja mara mbili kwa wiki, hivyo kuanzia sasa itakuwa inakuja mara mbili kwa wiki. (Jumamosi na jumatano).
Tuanze sasa....
“Karibu sana kijana, jisikie huru. Nadhani umeshaelekezwa mahali pa kupata huduma zote muhimu kama bomba la maji, choo na bafu” Yalikuwa ni maneno ya mwenye nyumba baada ya kumaliza kusaini mkataba wa pango la nyumba.
“Usijali mzee nipo sawa, Mama alinielekeza” Nilimjibu kwa mkato nikitamani aondoke ili aniache nipumzike. Muda huo rafiki yangu na mwenyeji wangu, Denis alikuwa amekaa pembeni akiwa kimya akifuatilia mazungumzo yangu na mwenye nyumba.
“Ok, sawa. Ngoja nikuacheni mpumzike.” alisema baba mwenye nyumba huku akinyanyuka akielekea nje. Ni Kama alikuwa akijua ni nini nilikuwa nawaza.
“Asante mzee, nashukuru sana.”
“usijali kijana, unakaribishwa.”
Alifungua mlango na akatoka nje na kutuacha mimi na Denis tukiwa ndani ya chumba ambacho kwa muda huo mimi ndiye niliyekuwa mpangaji rasmi au naweza sema mmliki wa muda. Nilimwangalia Denis ambaye alikuwa ananiangalia Mimi, tukatabasamu huku nikitikisa kichwa juu chini.
“Sasa dogo maisha ndo yameanza hivo” alisema Denis
“daaah aise kweli mzee baba” nilimjibu
“sasa we si bado unapumzika nini, ngoja mi niingie geto nikakorofishe, si unajua shemeji yako ni mtoro mtoro, anakwepa majukumu.”
“hahahaha poa bhana, ngoja mi nijipumzishe, then midamida ntakustua”
“poa, kwani unalala masaa mangapi mzee wa kazi?”
“si muda mrefu, natoa uchovu tu”
“ok poa, mi ntakuja mida saa 12 twende tukatembee kidogo”
“ok fresh tutasomana mjuba”
“Poa” Alisema Denis akinyanyuka na kuondoka.
Denis hakuwa akiishi mbali na pale nilipokuwa naishi mimi, ilikuwa ni umbali wa mwendo wa dakika kama saba au nane hivi kwa miguu. Denis ndiye aliyefanya mpango wa kunitafutia chumba baada ya kumwambia kuwa nina mpango wa kuja mjini. Ni rafiki yangu wa karibu na urafiki wetu si wa kukutana barabarani bali tulikuwa tukifahamiana vizuri tangu tukiwa wadogo. Tulisoma shule ya msingi pamoja na pia shule ya upili tulisoma pamoja pia hadi pale nilipofika kidato cha tatu ambapo nililazimika kuacha shule.
Pia Denis ndiye aliyefanya mpango wa mimi kupata dili la kuuza nyama kwenye moja ya bucha hapa mjini. Ndiyo, nilikuwa nategemea kuanza kufanya kazi buchani ili kujaribu kutafuta maisha. Siku iliyokuwa inafuata ndiyo siku ilikuwa natakiwa kwenda kuripoti kazini kwa mara ya kwanza. Denis alikuwa ni moja ya marafiki wazuri ambao niliwahi kuwa nao.
Nilijikusanya na kujilaza kwenye godoro lililokuwa limetandikwa sakafuni nikalala. Ndiyo, sakafuni, sikiwa na kitanda, nikitolee wapi? Mara kidogo usingizi ukanipitia.
Nilikuja kuamka baada ya masaa manne hivi, muda huo ilikuwa yapata kama saa kumi na moja. Niliamka na kuanza kupanga baadhi ya vitu ndani ya chumba angalau kukiweka katika mpangilio mzuri japokuwa sikuwa na vitu vingi. Nilikuwa na godoro, begi la nguo, ndoo mbili, jiko la gesi na vyombo vichache vya kupikia. Baaada ya kumaliza kuyafanya hayo nilifungua begi langu la nguo ili kuzitoa baadhi ya nguo na kuzitundika kwenye hang’a. Baada ya kumaliza zoezi hilo nilifungua zipu ya juu ya begi ili nichukue chaja ya simu, wakati nafanya hili niliona kitu ambacho kilifanya moyo wangu ushituke. Si ni kwa sababu kilikuwa na kitu cha kutisha, bali nilikuwa nimesahau kuwa nilikuwa na kitu cha aina ile.
Kitu hiki kilinikumbusha mbali, japokuwa haikuwa mbali sana. Hadi kufikia muda huo ilikuwa imepita kama miaka minne hivi. Kilinikumbusha tukio lililobadili dira nzima ya maisha yangu. Tukio lililofanya niamue kuacha shule nikiwa kidato cha tatu. Tukio lililofanya nipoteze marafiki wengi.
Tukio lililofanya wazazi wangu wapunguze upendo wao kwangu, japokuwa hali ya hewa ilikuja kutulia baadae, lakini haukuwa upendo ule ambao nilikuwa nikiupokea tangu utoto hadi siku ya kabla ya tukio hilo. Tukio lililonifanya nikawa na msongo wa mawazo kwa muda mrefu. Tukio ambalo huwa nashindwa kujizuia kumwaga machozi kila nikilikumbuka.
Kitu chenyewe kilichonirudisna miaka minne nyuma kilikuwa ni bahasha. Ndiyo, bahasha tu. Niliishika mkononi huku nikiiangalia macho yakilengwa na machozi. Sikutaka kuifungua, maana nilikuwa najua ni nini hasa kilikuwa ndani ya bahasha hiyo, nilikijua fika.
Mawazo yangu yalikuja kukatizwa na mtu aliyegonga mlango. Kabla ya kumjibu alisikika akisema “vipi bado umelala tu?”. Alikuwa ni Denis
Nikanyanyuka kwenda kufungua mlango. Alipoingia akaniangalia, akaonyesa sura ya kuwa na wasiwasi na mimi huenda kuna kitu hakipo sawa ila kwa sababu nilikiuwa nimetoka kulala, huenda alidhani ni usingizi tu. Akapita ndani, akakaa kwenye godoro, kwa bahati iliyo mbaya, alikalia ile bahasha.
“Oooh…ni nini hiki nimekalia, ni vyeti amah?’ alisema huku akinyanyuka kuangalia ilikuwa na nini. Alipoiona ile bahasha alishtuka.
Alishtuka kwa sababu alikuwa anaifahamu vizuri hiyo bahasha. Alijua kila kitu kilichosababisha hiyo bahasha ikawepo. Ni kwa sababu wakati hayo yote yalipokuwa yakitokea, yeye alikuwani mtu wangu wa karibu hivyo alikuwa akifahamu kila kitu.
Alinitazama kwa muda kisha akauliza “ni lini utaacha kufikiri kuhusu hili jambo?’
“Wewe unadhani ni rahisi kiasi gani?’ nilimjibu
“Ni miaka minne sasa, bado unakumbuka na linakutesa kama limetokea jana, tupa hii kitu mbali, wewe ni mwanaume”
“Tatizo huwa tunadhani kuwa ukiwa mwanaume unakuwa si binadamu wa kawaida, mimi ni binadamu mwenye hisia na pia hii ni sehemu ya maisha yangu, siwezi tupa”
“Ona ulivyokaa kihuzuni, yalishatokea yakapita, hata ukitumia miaka mia kufikiria kulihusu, huwezi badilisha hata sekunde moja ya tukio lenyewe”
“Sijawahi kufikiria kubadilisha chochote katika tukio hilo lakini kama siwezi kulibadilisha si vibaya nikiruhusu linibadilishe ”
“huko aliko hakukumbuki, hana uwezo na nafasi ya kufanya hivyo, unalijua vizuri hili”
“Hilo si tatizo kwangu, mimi kumkumbuka yeye inatosha sana” nilisema huku nikiibeba ile bahasha na kwenda kuiweka kwenye begi.
“anyway……tuachane na hilo, vipi umejiandaaje hiyo kesho?’
“Aaah kuna cha kujiandaa tena hapo!” nilisema nikifunga zipu ya begi
“Kwa hiyo, wewe ni mzoefu sio!”
“Kutoka wapi? uzoefu unaupatia huko huko”
“ila kuwa makini tu jembe, maana hapa mjini usipoangalia unapotea hivihivi, cha msingi ni kuangalia hasa wewe unahitaji nini katika maisha yako.”
“Yaaap……ni kweli, nalifahamu hilo, cha msingi ni kuweka mkazo tu.”
“ok poa……….tunasepa au?’ aliuliza
“Au” nilimjibu
“hujaacha ujinga wako bado.” Alisema Denis huku akicheka.
“Kwani wewe ulishaacha?” nilisema huku nikinyanyuka nikiashiria kuwa tuondoke.
“siwezi kuacha kwa sababu sikuwahi kuwa. Ila wewe ulikuwa mi msumbufu sana japo ulikuwa na wa chini chini”
“amna aiseee…..sema mimi sikuwa na ule utukutu kivile but sikuwa na aibu, labda hicho tu”
“aah wapi…wewe ulikuwa hatari , hivi unakumbuka ile siku ulimla denda Nancy mbele ya darasa?”
Nilijikuta nacheka kwa sauti kubwa, lilikuwa ni tukio moja la kuvutia sana. Nakumbuka ilikuwa ni katika kipindi cha fema club. Ikuwa katika igizo lililokuwa linahusu kuonyesha ni jinsi gani msichana anaweza kushawishiwa a kujikuta kujiingiza katika masuala ya mapenzi ilhali bado yupo shuleni. Sasa mimi nilikuwa katika nafasi ya kajana anayemshawishi huyo msichana. Sasa wakati tunaendelea na igizo, ambalo muda huo nilikuwa namtongoza nikajikuta napandwa na mzuka, si nakamkamata mtoto nikampiga denda mbele ya kadamnasi….acha watu walipuke na shangwe. Ilikuwa ni kumbukumbu nzuri sana.
Tuliendelea kukumbushana mambo baadhi tuliyoyafanya wakati tukiwa shule. Ilinisaidia kuondoa mawazo niliyokuwa nayo kuhusu ile bahasha.
Itaendelea...