Hadithi: Maisha yangu nyuma ya pazia jeusi

Hadithi: Maisha yangu nyuma ya pazia jeusi

Stephen Ngalya Chelu

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2017
Posts
8,288
Reaction score
18,571
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI.
SEHEMU YA KWANZA.
Mtunzi & Mwandishi: Stephen Chelu

Utangulizi:
Simulizi hii imejengwa kwa kutumia matukio halisi na ya kufikirika ili kuleta mvuto zaidi kwa msomaji.
Hadithi hii inajengwa katika maisha ya kawaida ya mtaani, hivyo kunaweza kuwa na matumizi ya lugha isiyo na tafsida, lengo si kuvunja kanuni za maadili bali kuonyesha uhalisia wa matukio yenyewe.
=======================
SASISHO
Naona mods wamehariri content kwa kuondoa/kubadili maneno yenye ukakasi kwa maana ya kuwa hakuna njia tunaweza kuyatumia tena katika sehemu zijazo. Hivyo kuanzia sasa nitaweka simulizi ambayo tayari itakuwa imehaririwa kwa kuwaondoa maneno hayo yasiyo na tafsida ili kuwapunguzia mods kazi.

Itakuwa inakuja mara moja kwa wiki.
========================
SASISHO
Kuna mdau kaoma iwe inakuja mara mbili kwa wiki, hivyo kuanzia sasa itakuwa inakuja mara mbili kwa wiki. (Jumamosi na jumatano).

Tuanze sasa....
“Karibu sana kijana, jisikie huru. Nadhani umeshaelekezwa mahali pa kupata huduma zote muhimu kama bomba la maji, choo na bafu” Yalikuwa ni maneno ya mwenye nyumba baada ya kumaliza kusaini mkataba wa pango la nyumba.

“Usijali mzee nipo sawa, Mama alinielekeza” Nilimjibu kwa mkato nikitamani aondoke ili aniache nipumzike. Muda huo rafiki yangu na mwenyeji wangu, Denis alikuwa amekaa pembeni akiwa kimya akifuatilia mazungumzo yangu na mwenye nyumba.

“Ok, sawa. Ngoja nikuacheni mpumzike.” alisema baba mwenye nyumba huku akinyanyuka akielekea nje. Ni Kama alikuwa akijua ni nini nilikuwa nawaza.
“Asante mzee, nashukuru sana.”
“usijali kijana, unakaribishwa.”
Alifungua mlango na akatoka nje na kutuacha mimi na Denis tukiwa ndani ya chumba ambacho kwa muda huo mimi ndiye niliyekuwa mpangaji rasmi au naweza sema mmliki wa muda. Nilimwangalia Denis ambaye alikuwa ananiangalia Mimi, tukatabasamu huku nikitikisa kichwa juu chini.
“Sasa dogo maisha ndo yameanza hivo” alisema Denis
“daaah aise kweli mzee baba” nilimjibu
“sasa we si bado unapumzika nini, ngoja mi niingie geto nikakorofishe, si unajua shemeji yako ni mtoro mtoro, anakwepa majukumu.”
“hahahaha poa bhana, ngoja mi nijipumzishe, then midamida ntakustua”
“poa, kwani unalala masaa mangapi mzee wa kazi?”
“si muda mrefu, natoa uchovu tu”
“ok poa, mi ntakuja mida saa 12 twende tukatembee kidogo”
“ok fresh tutasomana mjuba”
“Poa” Alisema Denis akinyanyuka na kuondoka.

Denis hakuwa akiishi mbali na pale nilipokuwa naishi mimi, ilikuwa ni umbali wa mwendo wa dakika kama saba au nane hivi kwa miguu. Denis ndiye aliyefanya mpango wa kunitafutia chumba baada ya kumwambia kuwa nina mpango wa kuja mjini. Ni rafiki yangu wa karibu na urafiki wetu si wa kukutana barabarani bali tulikuwa tukifahamiana vizuri tangu tukiwa wadogo. Tulisoma shule ya msingi pamoja na pia shule ya upili tulisoma pamoja pia hadi pale nilipofika kidato cha tatu ambapo nililazimika kuacha shule.

Pia Denis ndiye aliyefanya mpango wa mimi kupata dili la kuuza nyama kwenye moja ya bucha hapa mjini. Ndiyo, nilikuwa nategemea kuanza kufanya kazi buchani ili kujaribu kutafuta maisha. Siku iliyokuwa inafuata ndiyo siku ilikuwa natakiwa kwenda kuripoti kazini kwa mara ya kwanza. Denis alikuwa ni moja ya marafiki wazuri ambao niliwahi kuwa nao.

Nilijikusanya na kujilaza kwenye godoro lililokuwa limetandikwa sakafuni nikalala. Ndiyo, sakafuni, sikiwa na kitanda, nikitolee wapi? Mara kidogo usingizi ukanipitia.

Nilikuja kuamka baada ya masaa manne hivi, muda huo ilikuwa yapata kama saa kumi na moja. Niliamka na kuanza kupanga baadhi ya vitu ndani ya chumba angalau kukiweka katika mpangilio mzuri japokuwa sikuwa na vitu vingi. Nilikuwa na godoro, begi la nguo, ndoo mbili, jiko la gesi na vyombo vichache vya kupikia. Baaada ya kumaliza kuyafanya hayo nilifungua begi langu la nguo ili kuzitoa baadhi ya nguo na kuzitundika kwenye hang’a. Baada ya kumaliza zoezi hilo nilifungua zipu ya juu ya begi ili nichukue chaja ya simu, wakati nafanya hili niliona kitu ambacho kilifanya moyo wangu ushituke. Si ni kwa sababu kilikuwa na kitu cha kutisha, bali nilikuwa nimesahau kuwa nilikuwa na kitu cha aina ile.

Kitu hiki kilinikumbusha mbali, japokuwa haikuwa mbali sana. Hadi kufikia muda huo ilikuwa imepita kama miaka minne hivi. Kilinikumbusha tukio lililobadili dira nzima ya maisha yangu. Tukio lililofanya niamue kuacha shule nikiwa kidato cha tatu. Tukio lililofanya nipoteze marafiki wengi.

Tukio lililofanya wazazi wangu wapunguze upendo wao kwangu, japokuwa hali ya hewa ilikuja kutulia baadae, lakini haukuwa upendo ule ambao nilikuwa nikiupokea tangu utoto hadi siku ya kabla ya tukio hilo. Tukio lililonifanya nikawa na msongo wa mawazo kwa muda mrefu. Tukio ambalo huwa nashindwa kujizuia kumwaga machozi kila nikilikumbuka.

Kitu chenyewe kilichonirudisna miaka minne nyuma kilikuwa ni bahasha. Ndiyo, bahasha tu. Niliishika mkononi huku nikiiangalia macho yakilengwa na machozi. Sikutaka kuifungua, maana nilikuwa najua ni nini hasa kilikuwa ndani ya bahasha hiyo, nilikijua fika.

Mawazo yangu yalikuja kukatizwa na mtu aliyegonga mlango. Kabla ya kumjibu alisikika akisema “vipi bado umelala tu?”. Alikuwa ni Denis

Nikanyanyuka kwenda kufungua mlango. Alipoingia akaniangalia, akaonyesa sura ya kuwa na wasiwasi na mimi huenda kuna kitu hakipo sawa ila kwa sababu nilikiuwa nimetoka kulala, huenda alidhani ni usingizi tu. Akapita ndani, akakaa kwenye godoro, kwa bahati iliyo mbaya, alikalia ile bahasha.

“Oooh…ni nini hiki nimekalia, ni vyeti amah?’ alisema huku akinyanyuka kuangalia ilikuwa na nini. Alipoiona ile bahasha alishtuka.

Alishtuka kwa sababu alikuwa anaifahamu vizuri hiyo bahasha. Alijua kila kitu kilichosababisha hiyo bahasha ikawepo. Ni kwa sababu wakati hayo yote yalipokuwa yakitokea, yeye alikuwani mtu wangu wa karibu hivyo alikuwa akifahamu kila kitu.
Alinitazama kwa muda kisha akauliza “ni lini utaacha kufikiri kuhusu hili jambo?’

“Wewe unadhani ni rahisi kiasi gani?’ nilimjibu
“Ni miaka minne sasa, bado unakumbuka na linakutesa kama limetokea jana, tupa hii kitu mbali, wewe ni mwanaume”
“Tatizo huwa tunadhani kuwa ukiwa mwanaume unakuwa si binadamu wa kawaida, mimi ni binadamu mwenye hisia na pia hii ni sehemu ya maisha yangu, siwezi tupa”
“Ona ulivyokaa kihuzuni, yalishatokea yakapita, hata ukitumia miaka mia kufikiria kulihusu, huwezi badilisha hata sekunde moja ya tukio lenyewe”
“Sijawahi kufikiria kubadilisha chochote katika tukio hilo lakini kama siwezi kulibadilisha si vibaya nikiruhusu linibadilishe ”
“huko aliko hakukumbuki, hana uwezo na nafasi ya kufanya hivyo, unalijua vizuri hili”
“Hilo si tatizo kwangu, mimi kumkumbuka yeye inatosha sana” nilisema huku nikiibeba ile bahasha na kwenda kuiweka kwenye begi.
“anyway……tuachane na hilo, vipi umejiandaaje hiyo kesho?’
“Aaah kuna cha kujiandaa tena hapo!” nilisema nikifunga zipu ya begi
“Kwa hiyo, wewe ni mzoefu sio!”
“Kutoka wapi? uzoefu unaupatia huko huko”
“ila kuwa makini tu jembe, maana hapa mjini usipoangalia unapotea hivihivi, cha msingi ni kuangalia hasa wewe unahitaji nini katika maisha yako.”
“Yaaap……ni kweli, nalifahamu hilo, cha msingi ni kuweka mkazo tu.”
“ok poa……….tunasepa au?’ aliuliza
“Au” nilimjibu
“hujaacha ujinga wako bado.” Alisema Denis huku akicheka.
“Kwani wewe ulishaacha?” nilisema huku nikinyanyuka nikiashiria kuwa tuondoke.
“siwezi kuacha kwa sababu sikuwahi kuwa. Ila wewe ulikuwa mi msumbufu sana japo ulikuwa na wa chini chini”
“amna aiseee…..sema mimi sikuwa na ule utukutu kivile but sikuwa na aibu, labda hicho tu”
“aah wapi…wewe ulikuwa hatari , hivi unakumbuka ile siku ulimla denda Nancy mbele ya darasa?”

Nilijikuta nacheka kwa sauti kubwa, lilikuwa ni tukio moja la kuvutia sana. Nakumbuka ilikuwa ni katika kipindi cha fema club. Ikuwa katika igizo lililokuwa linahusu kuonyesha ni jinsi gani msichana anaweza kushawishiwa a kujikuta kujiingiza katika masuala ya mapenzi ilhali bado yupo shuleni. Sasa mimi nilikuwa katika nafasi ya kajana anayemshawishi huyo msichana. Sasa wakati tunaendelea na igizo, ambalo muda huo nilikuwa namtongoza nikajikuta napandwa na mzuka, si nakamkamata mtoto nikampiga denda mbele ya kadamnasi….acha watu walipuke na shangwe. Ilikuwa ni kumbukumbu nzuri sana.

Tuliendelea kukumbushana mambo baadhi tuliyoyafanya wakati tukiwa shule. Ilinisaidia kuondoa mawazo niliyokuwa nayo kuhusu ile bahasha.

Itaendelea...
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI.
SEHEMU YA KWANZA.
Mtunzi & Mwandishi: Stephen Chelu

Utangulizi:
Hadithi hii imejengwa kwa kutumia matukio halisi na ya kufikirika ili kuleta mvuto zaidi kwa msomaji.
Hadithi hii inajengwa katika maisha ya kawaida ya mtaani, hivyo kunaweza kuwa na matumizi ya lugha isiyo na tafsida, lengo si kuvunja kanuni za maadili bali kuonyesha uhalisia wa matukio yenyewe.

Itakuwa inakuja mara moja kwa wiki.

Tuanze sasa....
“Karibu sana kijana, jisikie huru. Nadhani umeshaelekezwa mahali pa kupata huduma zote muhimu kama bomba la maji, choo na bafu” Yalikuwa ni maneno ya mwenye nyumba baada ya kumaliza kusaini mkataba wa pango la nyumba.

“Usijali mzee nipo sawa, Mama alinielekeza” Nilimjibu kwa mkato nikitamani aondoke ili aniache nipumzike. Muda huo rafiki yangu na mwenyeji wangu, Denis alikuwa amekaa pembeni akiwa kimya akifuatilia mazungumzo yangu na mwenye nyumba.

“Ok, sawa. Ngoja nikuacheni mpumzike.” alisema baba mwenye nyumba huku akinyanyuka akielekea nje. Ni Kama alikuwa akijua ni nini nilikuwa nawaza.
“Asante mzee, nashukuru sana.”
“usijali kijana, unakaribishwa.”
Alifungua mlango na akatoka nje na kutuacha mimi na Denis tukiwa ndani ya chumba ambacho kwa muda huo mimi ndiye niliyekuwa mpangaji rasmi au naweza sema mmliki wa muda. Nilimwangalia Denis ambaye alikuwa ananiangalia Mimi, tukatabasamu huku nikitikisa kichwa juu chini.
“Sasa dogo maisha ndo yameanza hivo” alisema Denis
“daaah aise kweli mzee baba” nilimjibu
“sasa we si bado unapumzika nini, ngoja mi niingie geto nikakorofishe, si unajua shemeji yako ni mtoro mtoro, anakwepa majukumu.”
“hahahaha poa bhana, ngoja mi nijipumzishe, then midamida ntakustua”
“poa, kwani unalala masaa mangapi mzee wa kazi?”
“si muda mrefu, natoa uchovu tu”
“ok poa, mi ntakuja mida saa 12 twende tukatembee kidogo”
“ok fresh tutasomana mjuba”
“Poa” Alisema Denis akinyanyuka na kuondoka.

Denis hakuwa akiishi mbali na pale nilipokuwa naishi mimi, ilikuwa ni umbali wa mwendo wa dakika kama saba au nane hivi kwa miguu. Denis ndiye aliyefanya mpango wa kunitafutia chumba baada ya kumwambia kuwa nina mpango wa kuja mjini. Ni rafiki yangu wa karibu na urafiki wetu si wa kukutana barabarani bali tulikuwa tukifahamiana vizuri tangu tukiwa wadogo. Tulisoma shule ya msingi pamoja na pia shule ya upili tulisoma pamoja pia hadi pale nilipofika kidato cha tatu ambapo nililazimika kuacha shule.

Pia Denis ndiye aliyefanya mpango wa mimi kupata dili la kuuza nyama kwenye moja ya bucha hapa mjini. Ndiyo, nilikuwa nategemea kuanza kufanya kazi buchani ili kujaribu kutafuta maisha. Siku iliyokuwa inafuata ndiyo siku ilikuwa natakiwa kwenda kuripoti kazini kwa mara ya kwanza. Denis alikuwa ni moja ya marafiki wazuri ambao niliwahi kuwa nao.

Nilijikusanya na kujilaza kwenye godoro lililokuwa limetandikwa sakafuni nikalala. Ndiyo, sakafuni, sikiwa na kitanda, nikitolee wapi? Mara kidogo usingizi ukanipitia.

Nilikuja kuamka baada ya masaa manne hivi, muda huo ilikuwa yapata kama saa kumi na moja. Niliamka na kuanza kupanga baadhi ya vitu ndani ya chumba angalau kukiweka katika mpangilio mzuri japokuwa sikuwa na vitu vingi. Nilikuwa na godoro, begi la nguo, ndoo mbili, jiko la gesi na vyombo vichache vya kupikia. Baaada ya kumaliza kuyafanya hayo nilifungua begi langu la nguo ili kuzitoa baadhi ya nguo na kuzitundika kwenye hang’a. Baada ya kumaliza zoezi hilo nilifungua zipu ya juu ya begi ili nichukue chaja ya simu, wakati nafanya hili niliona kitu ambacho kilifanya moyo wangu ushituke. Si ni kwa sababu kilikuwa na kitu cha kutisha, bali nilikuwa nimesahau kuwa nilikuwa na kitu cha aina ile.

Kitu hiki kilinikumbusha mbali, japokuwa haikuwa mbali sana. Hadi kufikia muda huo ilikuwa imepita kama miaka minne hivi. Kilinikumbusha tukio lililobadili dira nzima ya maisha yangu. Tukio lililofanya niamue kuacha shule nikiwa kidato cha tatu. Tukio lililofanya nipoteze marafiki wengi.

Tukio lililofanya wazazi wangu wapunguze upendo wao kwangu, japokuwa hali ya hewa ilikuja kutulia baadae, lakini haukuwa upendo ule ambao nilikuwa nikiupokea tangu utoto hadi siku ya kabla ya tukio hilo. Tukio lililonifanya nikawa na msongo wa mawazo kwa muda mrefu. Tukio ambalo huwa nashindwa kujizuia kumwaga machozi kila nikilikumbuka.

Kitu chenyewe kilichonirudisna miaka minne nyuma kilikuwa ni bahasha. Ndiyo, bahasha tu. Niliishika mkononi huku nikiiangalia macho yakilengwa na machozi. Sikutaka kuifungua, maana nilikuwa najua ni nini hasa kilikuwa ndani ya bahasha hiyo, nilikijua fika.

Mawazo yangu yalikuja kukatizwa na mtu aliyegonga mlango. Kabla ya kumjibu alisikika akisema “vipi bado umelala tu?”. Alikuwa ni Denis

Nikanyanyuka kwenda kufungua mlango. Alipoingia akaniangalia, akaonyesa sura ya kuwa na wasiwasi na mimi huenda kuna kitu hakipo sawa ila kwa sababu nilikiuwa nimetoka kulala, huenda alidhani ni usingizi tu. Akapita ndani, akakaa kwenye godoro, kwa bahati iliyo mbaya, alikalia ile bahasha.

“Oooh…ni nini hiki nimekalia, ni vyeti amah?’ alisema huku akinyanyuka kuangalia ilikuwa na nini. Alipoiona ile bahasha alishtuka.

Alishtuka kwa sababu alikuwa anaifahamu vizuri hiyo bahasha. Alijua kila kitu kilichosababisha hiyo bahasha ikawepo. Ni kwa sababu wakati hayo yote yalipokuwa yakitokea, yeye alikuwani mtu wangu wa karibu hivyo alikuwa akifahamu kila kitu.
Alinitazama kwa muda kisha akauliza “ni lini utaacha kufikiri kuhusu hili jambo?’

“Wewe unadhani ni rahisi kiasi gani?’ nilimjibu
“Ni miaka minne sasa, bado unakumbuka na linakutesa kama limetokea jana, tupa hii kitu mbali, wewe ni mwanaume”
“Tatizo huwa tunadhani kuwa ukiwa mwanaume unakuwa si binadamu wa kawaida, mimi ni binadamu mwenye hisia na pia hii ni sehemu ya maisha yangu, siwezi tupa”
“Ona ulivyokaa kihuzuni, yalishatokea yakapita, hata ukitumia miaka mia kufikiria kulihusu, huwezi badilisha hata sekunde moja ya tukio lenyewe”
“Sijawahi kufikiria kubadilisha chochote katika tukio hilo lakini kama siwezi kulibadilisha si vibaya nikiruhusu linibadilishe ”
“huko aliko hakukumbuki, hana uwezo na nafasi ya kufanya hivyo, unalijua vizuri hili”
“Hilo si tatizo kwangu, mimi kumkumbuka yeye inatosha sana” nilisema huku nikiibeba ile bahasha na kwenda kuiweka kwenye begi.
“anyway……tuachane na hilo, vipi umejiandaaje hiyo kesho?’
“Aaah kuna cha kujiandaa tena hapo!” nilisema nikifunga zipu ya begi
“Kwa hiyo, wewe ni mzoefu sio!”
“Kutoka wapi? uzoefu unaupatia huko huko”
“ila kuwa makini tu jembe, maana hapa mjini usipoangalia unapotea hivihivi, cha msingi ni kuangalia hasa wewe unahitaji nini katika maisha yako.”
“Yaaap……ni kweli, nalifahamu hilo, cha msingi ni kuweka mkazo tu.”
“ok poa……….tunasepa au?’ aliuliza
“Au” nilimjibu
“hujaacha ujinga wako bado.” Alisema Denis huku akicheka.
“Kwani wewe ulishaacha?” nilisema huku nikinyanyuka nikiashiria kuwa tuondoke.
“siwezi kuacha kwa sababu sikuwahi kuwa. Ila wewe ulikuwa mi msumbufu sana japo ulikuwa na wa chini chini”
“amna aiseee…..sema mimi sikuwa na ule utukutu kivile but sikuwa na aibu, labda hicho tu”
“aah wapi…wewe ulikuwa hatari , hivi unakumbuka ile siku ulimla denda Nancy mbele ya darasa?”

Nilijikuta nacheka kwa sauti kubwa, lilikuwa ni tukio moja la kuvutia sana. Nakumbuka ilikuwa ni katika kipindi cha fema club. Ikuwa katika igizo lililokuwa linahusu kuonyesha ni jinsi gani msichana anaweza kushawishiwa a kujikuta kujiingiza katika masuala ya mapenzi ilhali bado yupo shuleni. Sasa mimi nilikuwa katika nafasi ya kajana anayemshawishi huyo msichana. Sasa wakati tunaendelea na igizo, ambalo muda huo nilikuwa namtongoza nikajikuta napandwa na mzuka, si nakamkamata mtoto nikampiga denda mbele ya kadamnasi….acha watu walipuke na shangwe. Ilikuwa ni kumbukumbu nzuri sana.

Tuliendelea kukumbushana mambo baadhi tuliyoyafanya wakati tukiwa shule. Ilinisaidia kuondoa mawazo niliyokuwa nayo kuhusu ile bahasha.

Itaendelea...
Tuko pamoja mkuu.
Unaweza ukatufikiria angalau mara mbili kwa wiki mkuu?
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI
SEHEMUJ YA PILI
Ilipoishia…
“aah wapi…wewe ulikuwa hatari , hivi unakumbuka ile siku ulimla denda Nancy mbele ya darasa?”

Nilijikuta nacheka kwa sauti kubwa, lilikuwa ni tukio moja la kuvutia sana. Nakumbuka ilikuwa ni katika kipindi cha fema club. Ikuwa katika igizo lililokuwa linahusu kuonyesha ni jinsi gani msichana anaweza kushawishiwa a kujikuta kujiingiza katika masuala ya mapenzi ilhali bado yupo shuleni. Sasa mimi nilikuwa katika nafasi ya kajana anayemshawishi huyo msichana. Sasa wakati tunaendelea na igizo, ambalo muda huo nilikuwa namtongoza nikajikuta napandwa na mzuka, si nakamkamata mtoto nikampiga denda mbele ya kadamnasi….acha watu walipuke na shangwe. Ilikuwa ni kumbukumbu nzuri sana.

Tuliendelea kukumbushana mambo baadhi tuliyoyafanya wakati tukiwa shule. Ilinisaidia kuondoa mawazo niliyokuwa nayo kuhusu ile bahasha.
Sasa endelea….
Wiki kadhaa zilipita tangu nianze kufanya kazi ya kuuza nyama katika bucha ambalo nilitengenezewa mchongo na Denis. Mambo yalikuwa yanaenda vizuri tu, na kwa asili ya kazi niliyokuwa naifanya ilikuwa ni kawaida mimi kula nyama angalau kila siku. Nilikuwa ni mmoja kati ya watu wachache ambao walikuwa wanapata nafasi ya kupata kitoweo hicho adimu kwa wakazi wengi wa mji huu.

Japokuwa nilikuwa nafanya kazi ya kuuza nyama, lakini malengo yangu ya kimaisha yalikuwa na mbali na hicho nilichokuwa nakifanya. Mimi nilikuwa nikiishi kutamani kuwa mwanamuziki. Nilipenda sana kusikiliza muziki wa hip hop. Simu yangu ilijaa nyimbo za hip hop za wasanii kutoka marekani na wasanii wa hapa nchini kwetu. Nilipenda sana hip hop kwa sababu niliamini kuwa ndio mziki pekee ambao ulikuwa unagusa maisha ya wananchi wa kawaida pia nilikuwa Napata hamasa ya kupambana na maisha kila niliposikiliza. Hata hivyo pia nilikuwa nasikiliza aina nyingine za muziki kama pop, reage na slow jams. kwa ufupi muziki ulikuwa na sehemu ya damu yangu. Na niliamua kwenda mjini kufanya kazi kuuza nyama buchani lakini ilikuwa ni njia ya kukusanya pesa ili kuanza harakati zangu za kimuziki. Na nilijipa imani sana kuwa ni lazima ningetoka tu.

Pia muda ule nilikuwa ni mtu niliyependa kusali, nilijizoesha hivyo tangu zamani. Japokuwa nilikuwa naamini kuwa kwenda kanisani si njia pekee ya kujiweka safi mbele ya Mungu, lakini nilikuwa naamini kuwa kufika maeneo ya kanisani kulikuwa kunatosha sana kunitoa mawazo ya ajabu ambayo yalikuwa yananitawala kwa muda wote wa wiki husika. Na kwa kuwa mmiliki wa bucha nililokuwa nafanya kazi alikuwa mkristo kindakindaki, siku ya jumapili ilikuwa siku ya mapumziko kwa hiyo niliitumia kwenda kanisani kuabudu.

Tabia hii ya kupenda kwenda kanisani ilinifanya niwe tofauti na wapangaji wenzangu wengi kwa sababu wengi wao walikuwa si watu waliokuwa wakipenda kwenda kanisani. Katika ile nyumba watu pekee tuliokuwa ni wahudhuriaji wazuri wa kanisani tulikuwa mimi na familia ya mwenye nyumba iliyokuwa ikijumuisha mkewe na mfanyakazi wao wa ndani. Kwa kuwa wote tulikuwa wakatoliki mara kadhaa nilikuwa naambatana nao kwenda kanisani kwa kutumia gari lao binafsi japokuwa nilikuwa najitahidi kukwepa ofa hiyo maana nilikuwa nahisi kuwa nakuwa siko huru. Tabia ya mimi kupenda kwenda kanisani ilinifanya nianze kuaminika na baba mwenye nyumba jambo ambalo lilikuwa linanipa faraja pia.

Jumapili moja wakati nilipofika nyumbani kutoka kanisani nilikutana na sura mpya kwenye nyumba ile niliyokuwa nimepanga. Alikuwa ni msichana wa kadiri ya miaka kumi na saba hivi. Na ilionekana huenda alikuwa na mtoto au ndugu wa mwenye nyumba. Japokuwa kwa kiasi kikubwa niliamini atakuwa ni mtoto wa mwenye nyumba kwa kuwa alionekana kufanana na mke wa mwenye nyumba. Sikutaka kujipa udadisi sana, niliingia ndani ya chumba changu na kuendelea na mambo yangu binafsi.

Kwa kuwa nilikuwa na njaa kiasi chake, nilianza kuandaa mazingira ili niweze kupika. Nilichukua nyama nakakatakata kisha nikaiosha, nikaitia ndani ya sufuria nakaweka maji kiasi kisha nikabandika jikoni kisha nikawasha gesi. Baadeye nilikuja kugundua kuwa chumvi ilikuwa ilmeisha hivyo nikajihimu kwenda kununua chumvi hapo nje jirani na nilipokuwa naishi.

Wakati nikiwa naelekea dukani kununua chumvi, nilisikia kelele za mwizi. Nimekuwa nikiichukia hii tabia ya watu kujichukulia sheria mkononi kwa kuwa naamini si mara zote watu wanaouliwa kwa kuchomwa moto ama kupigwa na vitu vizito kwa tuhuma za wizi huwa wameiba. Nawachukia wezi ila nawachukia zaidi wale wanaojichukulia sheria mikononi dhidi yao bila ya kuwa na ushahidi wa kutosha. Na hata kama kweli mtu huyo ameiba, hakuna sheria inayoruhusu kumuadhibu mwizi kwa namna hiyo.

Kuna kesi nyingi ambazo watu walituhumiwa kuwa ni wezi wakapigwa wakauwawa na baadae ikaja kugundulika kuwa hawakuwa wezi. Na mara nyingi huja kugundulika wakati tayari mtuhumiwa ameshajeruhiwa vibaya au amekwisha fariki tayari.

Hata hivyo na mimi niliamua kusogea mahali kelele zilipokuwa zinatokea ili nione ni nini hatma ya mtu huyo ambaye kwa muda huo uhai wake ulikuwa mashakani. Nilifanikiwa kufika eneo hilo baaba ya mwendo wa kama dakika moja hivi na kukuta mtuhumiwa aliyetapakaa damu amelala na juu yake kukiwa na mawe matofali na kila aina ya silaha zisizo rasmi. Japo nilikuwa nimesimama kwa mbali kidogo kwa sababu za kulinda usalama wangu lakini niliweza kuona mtuhumiwa akijinyoosha nyoosha. Ni wazi alikiwa anapigania uhai wake ambao ulikuwa unadhulumiwa na wananchi wanaojiita 'raia wenye hasira kali'. Lilikuwa ni moja ya matukio mabaya kuyashuhudia.

Hakuna aliyejali, kila mtu alikuwa anaondoka kama hakuwa mhusika wa tukio hilo kwa namna yoyote ile. Nami niliamua kuondoka haraka eneo hilo huku nikiwa na chuki kubwa moyoni juu ya hao wanaojiita raia wenye hasira kali. Wakati nikiwa natembea nilisikia maongezi ya baadhi ya watu kuhusu tukio hili. Wapo waliosema eti alikuwa ameiba viatu vya machinga. Hebu fikiri, viatu tu watu wanaamua kumtoa mtu uhai, ukatili ulioje.

Niliondoka eneo la tukio nikiwa na mawazo lukuki juu ya tukio nililoliona. Nilielekea kwenye duka la rejareja nikanunua chumvi kisha nikaanza safari ya kwenda geto kwangu. Niliongeza kasi na urefu wa hatua zangu ili niweze kufika haraka maana nilihisi nimechelewa. Nilifika geto na kuingia ndani, nilishtuka kwa nilichokikuta. Kulikuwa na harufu ya mboga kuungulia, sufuria ilikuwa chini, na jiko lilikuwa limezimwa. Nikiwa bado natafakari ni nani alishusha sufuria na kuzima gesi na pia ni nini nifanye nakasikia sauti ya kike ikipiga hodi mlangoni kwangu. Nikaitikia kisha nikaenda kumwangalia. Alikuwa na Yule binti ambaye nilimwona saa chache zilizopita.

“Mambo” alinisalimia

“Fresh” nilimjibu huku nikimwangalia usoni hali iliyomfanya aone aibu kidogo akaangalia pembeni.

“Samahani mkaka, hivi wewe ndiye unayekaa kwenye chumba hiki?” aliuliza

“Ndio”

“Sawa, samahani kwa kuingia kwako bila ruhusa, nilisikia harufu ya kama kitu kinaungulia kwa muda mrefu na nikaona kama hakuna mtu hivyo nikaamua kuja kuona ni nini kinaungulia. Ndiyo maana umekuta hivyo vitu hivyo jinsi vilivyo”

“haina shida dada’angu, umenisaidia sana, asante sana maana isingekuwa wewe hiki chumba kingekuwa kama tanuru”

“hahahaha….usijali” aliongea huku akicheka kicheko chenye aibu ndani yake.

“sasa ngoja nianze upya maana nina njaa hatari” nilisema hivyo ili kumuondoa japokuwa alikuwa amenisaidia sana.

“kwa hiyo unaanza kupika tena?”

“ndiyo, sasa unadhani nitafanya nini? Siwezi kuahirisha kula” niliongea huku nikiujaza uso wangu kwa tabasamu.

“kweli, lakini ngoja nikaangalie kama kuna uwezekano wa kitu kingine kufanyika.” alisema kisha akaondoka kuelekea ndani kwa mwenye nyumba.

'kitu! Kitu gani?'niliwaza.

Nilisimama mlangoni kidogo kisha nikaenda ndani kuona ni nini naweza fanya ili kurekebisha mambo. Nikiwa bado sijafanya chochote nikaisikia sauti iliyokuja kubisha hodi mwanzo ikibisha hodi tena. Nikanyanyuka haraka kwenda mlangoni, nikamkuta msichana Yule akiwa amesimama akiwa na ma’hotpot’ mawili, moja dogo na moja kubwa. Nikayatolea macho, nikajua humo kulikuwa na chakula na si vimginevyo.

Aliniangalia akionyesha ishara kuwa nichukue.

“dada, lakini ni kwa nini haya yote? Naweza kujiandalia chakula changu mwenyewe. Nimekuwa nikifanya hivyo siku zote.” Nilimwambia.

“lakini ona leo hauko katika nafasi nzuri ya kufanya hivyo, sivyo?”

Nilitulia kwa muda nikiwaza. Lakini nikaona ya nini kujisumbua, nilihitaji kula na chakula kimeletwa. Nikaangalia huku na huko ili kuona kama kuna mtu yeyote alikuwa anashuhudia tukio lile. Maana kwa mazingira yale ilikuwa ni rahisi kuzuka umbea kitu ambacho nilikuwa sikitaki kabisa kitokee. Kwa bahati, hakukuwa na mpangaji yeyote nje. Nikanyoosha mikono yangu na kuchukua yale mahotpot.


“asante” nilimwanbia, akaitikia kwa kichwa kisha akaondoka.


Nikaingia ndani, nilijikuta nikiwa na shauku ya hali ya juu, nikafungua ili nione kulikuwa na nini. Nikaanza na lile dogo, nikakuta ni samaki, na mchuzi mwekunduu, mchuzi uliokozwa nyanya haswa…mate yakanijaa si mchezo. Nikafungua hotpot kubwa, nkakuta ugali, nikatabasamu. Nikachukua maji nikanawa ili nianze kuushambulia. Cha kwanza niling’oa macho Yule samaki, huwa sipendi kula samaki huku akiwa ananitizama. Nikakata tonge la kwanza, bila kulirembaremba wala kulitengeneza vizuri nikalitumbukiza ndani ya mboga kisha hilooo mdomoni. Kilikuwa ni chakula kitamu. Sikujua ni yeye au mfanyakazi au mke wa mwenye nyumba au ni nani alikipika, lakini huyo aliyekipika kile chakula, alikuwa ni mtaalamu wa mapishi.

Nikakumbuka bibi yangu aliwahi kusema kuwa, mwanamke asiyejua kupika au asiyependa kupika ni sawa na kuku asiye na manyoya. Lakini siku hizi wanawake wengi wamekuwa ama hawajui kupika au wanajua kupika lakini hawataki kupika. Wanawake wa zamani walikuwa wanapika kama mama zao lakini wa siku hizi wanalewa kama baba zao, kweli zama zinabadilika. Niliendelea kula huku nikiliwaza tukio nililolishuhudia la mwizi kuuliwa na hii ilinifanya spidi ya yangu ya kula iwe ndogo. Baada ya kumaliza kula nilichukua maji na kuviosha vyombo ili akija kuvichukua avikute ni visafi.

Baada yakumaliza nililala ili kuweza kupumzisha mwili na tumbo huku picha ya yule mtu aliyeuliwa ikisumbua fikra zangu. Baada ya kuona kuwa tukio hilo litanivuruga ikabidi nihamishe mawazo yangu kwa huyu msichana aliyeniletea chakula. Nilijiuliza ni kwa nini dada huyu alikujwa mkarimu sana kwangu katika siku yangu ya kwanza kumuona? Bado sikuweza kupata jibu.

Wakati nikiwa katikati ya dimbwi la tafakari, nilisikia mlango ukigongwa tena. Nikajizoazoa na kwenda kumwona ni nani aliyekuwa anagonga japo nilikuwa aghalabu najua ni nani alikuwa anagonga. Ndiyo, alikuwa yuleyule ambaye nilikuwa namdhani, Yule msichana mgeni.

“umeshamaliza kula?” aliuliza

“ndiyo, asante sana dada. Ngoja nikuletee vyombo” nilimjibu.
“sawa”

Niliingia ndani na kuvibeba vyombo hivyo kisha kumpelekea huyo msichana.

“Asante sana dada angu, ubarikiwe sana. Chakula kilikuwa kitamu na nimeshiba.” nilisema huku nikimpa yule msichana vyombo vya chakula.

“umeviosha kabisa.!” Aliuliza kwa mshangao huku akiwa anatabasamu

“kwani ni uhalifu?”

“hapana, nashukuru kwa kunisaidia”

“Samahani dada, naweza kukufahamu jina?”

“naitwa Ingrid”

“anhaa, ni ndugu yake mzee mwenye nyumba eeh..?”

“mimi ni mtoto wake” alijibu akicheka huku akionyesha hali ya aibu

“oooh kumbe..! Mimi naitwa Barry” niliamua kujitambulisha pia.

"Nashukuru kukufahamu, haya siku njema” alisema kisha akageuka na kuanza kuonduka.

“Ingrid” nilimwita, akageuka. Aliniagalia akiwa ana uso wa mshangao kiasi Fulani. Pengine alikuwa anajiuliza ni nini kingine nilikuwa nataka kumwambia. “Ingrid, wewe…..wewe ni mkarimu sana” niliongea kwa kusitasita kama vile sikuwa na uhakika na kile nilichokuwa nakitamka. Ingrid aliangalia chini kwa aibu flani za kike , kisha akaniangalia akiwa anatabasabu.

“asante” alijibu kwa sauti ya chini kisha akageuka na kuanza kuondoka. Mara hii mwendo wake ulikuwa ni wa haraka zaidi kuliko awali.

Sikujizuia kumwangalia. Alikuwa ni mzuri haswa. Nilibaki kumwangalia upande wake nyuma uliokuwa unaonekana wakati akienda.

“aiseee” nilisema kwa sauti ya chini huku nikitikisa kichwa nikiwa bado nimesimama mlangoni.

Itaendelea…..
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI

SEHEMU YA 3
Ilipoishia....

“asante” alijibu kwa sauti ya chini kisha akageuka na kuanza kuondoka. Mara hii mwendo wake ulikuwa ni wa haraka zaidi kuliko awali.



Sikujizuia kumwangalia. Alikuwa ni mzuri haswa. Nilibaki kumwangalia upande wake nyuma uliokuwa unaonekana wakati akienda.



“aiseee” nilisema kwa sauti ya chini huku nikitikisa kichwa nikiwa bado nimesimama mlangoni.

Endelea......

Sikutaka kujipa kazi ya kudadisi ni kwa nini Yule msichana alikuwa mwema kwangu japo nilionana naye muda mfupi uliopita tu, kwa sababu sikuwa na historia nzuri wasichaa. Mara nyingi urafiki na ukaribu wangu kwa na wasichana ulikuwa ni wa mashaka sana. Sikuwahi kujua ni nini kilisababisha hali hiyo japo mara nyingi nilikuwa nahisi kuwa labda wasichana walikuwa hawaielewi misimamo na mitazamo yangu.

Siku zikapita, nikaendelea na maisha kama kawaida. Hatimaye ikafika jumapili nyingine. Nikiwa njiani kuelekea kanisani kama ilivyo kawaida yangu, nilisikia sauti ambayo aghalabu nilikuwa naifahamu. Niligeuka na kuangalia ni nani alikuwa ananiita ili kujiridhisha kama ni kweli Yule ambaye nilikuwa nadhani ndiye. Ni kweli, alikuwa ni Ingrid, akiniomba nimsubiri ili twende wote kanisani, nikamsubiri. Ingrid alianza kukimbia kwa mwendo wa wastani, hatimaje akanifikia.

“Mambo” alinisalimia baada ya kunifikia huku akihema kwa sauti kutokana na kukimbia.

“Safi vipi, inrid”

“Nani?” aliniuliza kwa hamaki huku akiendelea kuhema japo alijaribu kujibana ili nisione kama anahema sana.

“Inrid. Au nimekosea?”

"Ndiyo, naitwa Ingrid na sio inrid. Yaani mara hii ushasahau jina langu?”aliniuliza huku akiniangalia machoni huku akitabasamu kwa mbali.

“kumbe…! Samahani madame,hayo majina ya kizungu yanatupa tabu sana sisi tuliokulia chamwino ndani ndani huko” nilitania.

“mhh, mbona jina rahisi tu hilo jamani..!”


“binafsi sijawahi kukutana na msichana mwenye jina kama lako, ndo maana linanipiga chenga”


“mmh, yaani wewe” aliongea huku akiambatanisha na kicheko kwa mbali. Ni wazi utani wangu wa hapa na pale uliikosha nafsi yake.


“ vipi mzee hayupo nini?!” nilimuuliza swali hili ili kubadili mada.

“kwa nini?”

“naona unaenda kanisani kwa mguu, au wewe hutumiagi usafiri wa mzee wako?”

“aaaah, mi sipendagi kwenda kanisani kwa gari”

“kwa nini?”

“basi tuu, lakini hata hivyo nimekuja juzijuzi, so Napata wasaa wa kuangalia mazingira pia.”

“ok”

Tuliendelea kupiga hatua kuelekea kanisani. Kulikuwa na umbali kidogo kutoka kule tulipokuwa tukiishi hadi kanisani, ulikuwa ni mwendo wa dakika ishirini hivi kwa miguu. Muda huo kimya kilitawala kati yetu, ni sauti za hatua na watu pembeni waliokuwa wakiendelea na shughuli zao zilisikika.

Tulipita mahali tukakuta ugomvi uliokuwa ni kati ya watu ambao huenda walikuwa ni wapenzi au wanandoa. Mwanamke alionekana kulia huku akitoa maneno machafu kwa mwanaume. Ilivyoonekana ni kama mwanamke alikuwa amemfumania mwanaume wake na mwanamke mwingine. Watu walikuwa wametapakaa kushuhudia tukio hilo kama ilivyo kawaida ya watu wa mji huu.

Hata Ingrid pia alionekana kuvutwa a tukio hilo kwa maaa nilimuona akiwa anatembea huku shingo akiwa ameielekeza upande ambapo tukio lilipokuwa linatokea. Na mimi nilimwacha aendelee kupata kile ambacho alikuwa anataka kukipata. Aliendelea kulifuatilia tukio hilo hadi pale tulipovuka kabisa eneo hilo.

“wanaume bwana” alisema Ingrid hali iliyofanya kuvunjika kwa ukimya uliotawala kati yetu.

“tumefanyaje tena?”niliuliza nikigeuka kumwangalia.

“huwa nashindwa kuwaelewa kabisa”

“kwa nini?”

“hivi inakuwaje mtu anakupenda but wewe huthamini upendo wake?”

“ kipi kimekufanya uwaze hivyo?”

“we huoni huyo mwanamke analalamika nini?”

“una uhakika gani kuwa madai yake ni ya kweli, kuwa hakuna kitu kipo nyuma ya hapo?”

“usimtetee huyo mwanaume mwenzio, hamtabiriki ninyi”

“vipi kuhusu nyinyi wanawake, huwa mnatabirika?”

“sisi huwa tuko vile vile wakati wote, hivyo hakuna hitaji la kututabiri”

“si kweli…”

“unabisha bila sababu, kusema ule ukweli wanaume wa siku hizi sijui nani kawaroga. Yaani hamridhiki na mwanamke mmoja.”

“hilo ndo tatizo kubwa kwenu ninyi wanawake. Mara zote mmekuwa mkitaka kuwahodhi wanaume katika mahusiano pasipo kujua kuwa tangu dunia iumbwe, hajawahi kuumbwa mwanaume mwenye uwezo wa kuridhika na mwanamke mmoja..hayupo mwanaume wa hivyo. Mbinguni hakuna udongo wa kumuumba mwaname wa kurindika na mwanamke mmoja. Mwanaume ameumbwa kuwa na wanawake kadiri ya matamanio yake. Na tatizo linalowasumbua nyinyi wanawake ni kuwa hampendani nyinyi kwa nyinyi, hivi kwani mimi nikiwa na wewe halafu nikawa na rafiki yako kwani kuna ubaya gani?. Wewe utakuwa unapata share yako na yeye atapata share yake. Kwanza wanaume tuko wachache duniani kwa hiyo mkitaka kila mwanaume awe na mwanamke mmoja kuna wengine wataingiliwa na ukame mkali. Acheni roho ya ubinafsi. Sisi wanaume ni raslimali adimu, hivyo mnapaswa kugawana kidogo kidogo kila mwanamke apate.” niliongea nikiwa naonyesha kabisa kuwa sikuwa natania.

“wewe barry, unakisikia unachokiongea na unaelekea kanisani?” hili swali lilinishtua si kidogo. Ni kweli sikufaa kutamka maneno yale wakati muda huo nelekea kanisani, japo huo ndiyo ulikuwa msimamo wangu. Binafsi niliamini kuwa ni rahisi zaidi mwanaume kukaa bila kuwa na mahusiano kuliko mwanaume kuwa na mahusiano na mwanamke mmoja tu. Ila kwa kuwa Ingrid alistuka sana ikanibidi kubadili uelekeo. Na sikushagaa kwa sababu wanawake wako hivyo, huwa hawapendi kusikia ukweli ambao ni mchungu kwao, ila wanapenda uongo mtamu ambao unaburudisha mioyo yao.

“usishituke Ingrid, nilikuwa natania tu. Lakini mimi naona wote tuna kasoro zetu” nikahamisha magoli huku nikijitetea kimtindo ili kumridhisha yeye.

“kivipi?” aliuliza

“hata nyinyi si waaminifu pia”

"Sisi na nani?, labda wengine”

“kwa hiyo wewe ni mwaminifu?”


“a hundred percent” alijibu kwa kujiamini.


“hongera kama ni kweli” niliongea huku nikimshika begani, akageuka, akaniangalia, akatabasamu kisha akaitikia kwa kichwa. Mweeee. Nikaona stori yaweza kwenda ndani sana nikaamua kubadili upepo. “hivi ulikuwaga wapi?”

“nilikuwa shule” alijibu.

“oooh, wapi huko?”

“Kilimanjaro”

“ok, kwa hiyo mmefunga sio”

“Hapana, mi nishamaliza nasubiri tu matokeo mwezi wa saba nione ni nini kitaendelea”

“Mmmmh, mmemaliza mwezi wa tano, ulikuwa unasoma nini kwani, mtihani si huwa unafanyika mwezi wa kumi na moja au ndo wamebadilisha?” niliuliza kwa mshangao kidogo.

“Wanaomalizaga mwezi wa kumi na moja ni form four, mimi nilikuwa nipo form six”

“Ooh kumbe, utafaulu tu ndugu yangu, au sio”

“Yeah, tuombe Mungu iwe hivyo” alinijibu

Kutokana na kutojihusisha na mambo ya shule kwa muda mrefu ilifika wakati nikawa nimesahau utaratibu wa shule ulivyo. Ni kwa sababu shule hakikuwa ni kitu kilichokuwa kinanihusu kwa muda huo, japokuwa nilikuwa natamani sana siku moja ningekuwa na nafasi ambayo alikuwa nayo Ingrid lakini haikuwezekana. Nilipata maumivu kiasi lakini nilizuia yasinitawale.

Tuliendelea kupiga stori za hapa na pale, tukafika kanisani, tukasali na takarudi huku tukipiga story za hapa na pale. Ingrid alionyesha kunizoea sana. Na mimi pia nilipenda ucheshi wake na nikaamua kujitahidi kumfanya kuwa rafiki yangu japo sikuwa a uwezo wa kufanya urafiki kati yangu na wasichana udumu kwa muda mrefu.

Ulifika wakati wa usiku . Usiku ulikuwa ni muda wa mimi kupumzika na kuwaza mambo ya hapa na pale. Mara nyingine huwa natumia kusikiliza mziki, mara nyingine kuimba, mara nyingine kucheza mziki. Ndiyo, nikijifungia ndani peke yangu hakuna atakayejua ni nini nafanya.

Lakini usiku ule ulikiwa wa tofauti kidogo, nilijikuta namuwaza Ingrid. Nilijiuliza ni kwa jinsi gani aliweza kunizoea kwa haraka kiasi kile. Nilijikuta naanza kutumia muda wangu kuwaza kumhusu. Alikuwa ni msichana mrembo kiasi chake. Japokuwa sikuwa nahisi kumtamani kimapenzi, lakini nilijikuta namuwaza tu. Nikakumbuka kicheko chake, tabasamu lake na pia ile siku ya kwanza kabisa aliponiletea chakula “ni msichana wa aina yake” nilijisemea moyoni. Lakini niliamua kujizuia kuyaruhusu mawazo kumhusu Ingrid yanitawale, nikaamua kuchukua daftari nililokuwa nimeandika nyimbo zangu, nilitaka kuongeza mashairi kidogo kwenye baadhi ya nyimbo.

Nilianza kulifunua daftari huku macho yakipita kwenye majina ya nyimbo ambazo nilikuwa nimeziandika ili nione ni ipi ilifaa kujaziwa mashairi. ‘nimevurugwa’, hapana… ‘all words on me’,hapana….’love or fear’, hapana….’dear x’……macho yakaganda kwenye huu wimbo. Nikaanza kuyasoma mashairi yake, yalikuwa yananigusa mimi moja kwa moja. Niliuandika maalum kwa ajili yangu. Nikakumbuka tukio lililopelekea niandike huu wimbo. Nikatikisa kichwa kwa kusikitika, nilikuwa nikijaribu mara nyingi kadri ya uwezo wangu kusahau matukio yaliyoniumiza katika kipiindi kile kifupi cha maisha yangu lakini nilikuwa nashindwa. Ndipo nikaja kuamini kuwa kumbukumbu huwa haifutiki iwe nzuri au mbaya kumbukumbu ni kumbukumbu tu.

Nilichukua peni kisha nikaanza kuandika mistari kadhaa ambayo ilinijia kichwani..

“Nilikuumiza kihisia pia kimwili/
Licha ya upendo wako nilikulipa ukatili/
Nilifurahi kuona machozi yako/
Ni kama niliichukia furaha yako/
Kwa nguvu ya pendo lako ulivumilia yote/
Ukiamini kuwa…”


Nilishindwa kupata maneno ya kujazia ili kukamilisha mstari, nikaweka peni katikati ya daftari kisha nikalifukika na kuliweka lilipokuwa kisha nikajilaza kwenye godoro nikisubiri usingizi unipitie.

Itaendelea…
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI


SEHEMU YA 4

lipoishia..
nilichukua peni kisha nikaanza kuandika mistari kadhaa ambayo ilinijia kichwani..

“Nilikuumiza kihisia pia kimwili/
Licha ya upendo wako nilikulipa ukatili/
Nilifurahi kuona machozi yako/
Ni kama niliichukia furaha yako/
Kwa nguvu ya pendo lako ulivumilia yote/
Ukiamini kuwa…”


Nilishindwa kupata maneno ya kujazia ili kukamilisha mstari, nikaweka pei katikati ya daftari kisha nikalifukika na kuliweka lilipokuwa kisha nikajilaza kwenye godoro nikisubiri usingizi unipitie.

Endelea..
Miezi miwili ilikatika, maisha yakazidi kusonga mbele, nikaanza kuzoeleka kwa watu hasa wateja wa bidhaa niliyokuwa nauza. Niliendelea kupiga kazi kwa kujituma, japokuwa pia sikuwa nyuma kufuatilia mipango yangu ya kutoka kimuziki japokuwa sikuwa nafanya kwa nguvu sana. Nilikuwa nasubiri nikusanye angalau pesa za kunitosha ili nikianza harakati zangu, ziwe ni harakati kweli. Ingrid naye hakuwa nyuma, alinizoea hasa, tukawa kama marafiki wakubwa sana kwa kipindi kile kifupi nilichofahamiana naye. Na nilikuwa nafurahia uwepo wake kila wakati. Alikuwa ni mwanye kujali sana, alikuwa mwema sana kwangu. Ni kama alikuja kubadili mtizamo wangu juu ya uhusiano wangu na wasichana.

Siku moja wakati nikiwa naandaa chakula changu cha usiku nilisikia sauti ya ujumbe kutoka whatsapp kwenye simu yangu. Sikuwa na haraka kujua ni nani aliyekuwa amenitumia ujumbe kwa muda huo. Niliendelea kufanya nilichokuwa nafanya. Nilipomaliza nikaichukua nikaangalia kwenye kioo cha simu, alikuwa ni Ingrid, ujumbe ulisomeka ‘Hi Barry’.

‘Hi ingrid’ nikamjibu

‘umerudi?’ aliuliza

‘yeeep’

‘unafanyaje now?’

‘napika’

‘mmmh! Si ungeniita nije nikupikie’ aliandika Ingrid huku akiambatanisha na emoji tatu za kinyani kimefunika macho.

‘njoo basi’ nilimjibu huku nikiambatanisha emoji moja ya kucheka.

‘hadi nijipendekeze?’

‘we hutaki kuja acha maneno mingi, ngoja mi nipike uje ule, mwanamke gani wewe unakuwa mvivumvivu’ nilimtania.

‘weee koma, nani mvivu’ nilicheka majibu yake japokuwa huwa sipendi kuambiwa neno ‘koma’. Lakini kwa kuwa alikuwa ni Ingrid, rafiki yangu kipenzi..nililimezea hili.

“wewe piga domo tu…ukiwa mvivu utabaki kutoa michango na kuhudhuria sherehe za harusi za mashoga zako” niliambatanisha emoji za kicheko ili ajue nilikuwa natania.

“barry jamani, kwani mimi ni mvivu kiasi cha kuniambia maneno makali kiasi hicho?” aliandika Ingrid huku akiambatanisha na emoji za kununa.

“sasa kama hata hutaki kuja kunipikia, si uvivu huo?”

“kwa hiyo chakula cha siku ile ni wewe ulipika sio?”

“daaaah!.....kwa hiyo kile ulipika wewe?” nilimuuliza

“sasa je?”

“kwa chakula kile kilivyokuwa kitamu, naomba kutengua kauli yangu kuwa wewe ni mvivu. Nisamehe tu bibie, wewe ni wife material kabisa….”

“hahahaha…”

“kipii kikuchekechechacho?”

“si kwa kujitetea huko, sawa lakini…but ukimaliza kupika niambie, kuna jambo la kuongea na wewe”. jambo la kuongea na mimi. Nilistuka

“poa” niliamua kumjibu.

Niliendelea kupika huku akili akiwa imehama kidogo, ni nini alikuwa anataka kuongea na mimi? Nilijiuliza nikakosa jibu, nikaona sikuwa na haja kujitesa kutaka kujua ni nini alikuwa anataka kuniambia wakati muda si mrefu angeniambia. Nikawa mpole.

Nilipika, nikala, nikaosha vyombo, kisha nikajilaza kwenye godoro langu. Nikachukua simu kisha nikamtumia ujumbe.

‘tayari, karibu tule’ japokuwa nilikuwa tayari nimeshakula.

‘thanks’ alijibu.

“unasema tu thanks…, unakuja au?’.

‘ndiyo’

‘ukija kula usisahau kuniambia kile ambacho ulisema unataka kunambia’
‘nakuambia kwanza, ndo nije nile’

‘bwana weee sasa si utakuta nimeshamaliza kula?’

‘nitapika tena’

‘aaah kumbe nishajua, hutaki kula chakula changu’

‘mmmmmh’

‘mbona mguno mrefu hivyo!’

‘bwana weee, tuachane na hayo…”

“nakusikiliza madame”

“are you in relationship?” nilishtuka sana nilipouona ujumbe huo. Nilijiuliza ni nini kilimfanya aniulize swali hilo lakii sikupata jibu la haraka haraka.

“kwani vipi?” nilimuuliza baada ya kufikiri kwa muda.

“we nijibu ndo utajua”

“yeah,” niliamua kumjibu hivyo japokuwa ki ukweli sikuwa katika mahusiano.

“mhh, mbona sijawahi kumwona hata ukimpost status wifi?” aliuliza .

“ni mpenzi wangu, yeye siyo mali ya umma” nilimjibu.

“mhh.. haya bwana. msalimie”

“haya nimeshakujibu, sasa niambie ulichokuwa unataka kuniambia”

“tayari nimeshakwambia kuwa msalimie”

“hivyo tu?”

“ndiyo”

Jibu lake hilo lilinifanya nihisi kuwa pengine hakuwa amefurahishwa na majibu yangu au pengine hakutegemea kama ningemjibu kivyo. Jumbe zake za mwisho zilionyesha wazi hakuwa mwenye furaha kabisa. Japokuwa sikuwa na historia ya kuwa na uhusiano wa karibu sana na wasichana katika maisha yangu lakini nilikuwa na uwezo wa kutambua fikra zao kirhisi kabisa.

Hivyo, baada ya kugundua kuwa pengine hakupenda kile nilichomjibu basi nikaamua kugeuza upande wa pili wa shilingi.

“hahahaha, nakuzingua bwana..mimi bado niponipo kwanza” Nilimjibu huku nikiwa na hamu ya kutaka kujua yeye angenijibu nini.

“nilitaka kushangaa, mbona sijawahi kuona hata dalili!” alijibu ingrid. Niliona nuru katika maandishi yake na hivyo nikatambua ni wazi nilkkuwa natembea kwenye njia ambayo yeye alitaka nipite.

“kwa hiyo kumbe huwa unanichora tu, sio”

“walaah, hivyo ni vitu vya kuonekana tu mbona”

“haya bhana madame, umeshinda”

“sawa...nikuambie kitu barry?”

"Duh, inaonekana leo una vitu vingi sana vya kusema. Enhe nakusikiliza” Nilimjibu huku nikijiuliza ni nini kingine tena alitaka kukisema huyu binti.

“barry, sorry kama utanielewa vibaya, Barry nimeshindwa kujizuia, I love you so much.’ Aliandika Ingrid huku akiambatanisha na emoji za makopakopa. Nilistuka sana baada ya kuuona ujumbe huu. Akili ikafunguka na kuwaza mambo mengi kwa wakati mmoja, lakini bado sikuweza kupata jibu la harakaharaka. Katika kipindi chote ambacho tulikuwa katika dimbwi la urafiki na yeye sikuwahi kufikiri kuwa ipo siku tutahitaji kuingia katika mahusiano. Neno mapenzi halikuwapo kabisa ndani ya kichwa changu.

Nilizidi kufikiri kwa muda, sikujua nimjibu nini. Wakati najiuliza ni nini nimjibu nikaona ujumbe mwinngine kutoka kwake.

"Mbona kimya barry?" Ujumbe huu uliniamsha kutoka katika katika tafakari nzito ambayo nilikuwa naifanya kuhusu jambo lililokuwa mbele yangu kwa wakati huo.

Nilibonyeza kwenye uwanja wa kuandika jumbe, herufi zikatokea kwenye kioo kuashiria kuwa zilikuwa tayari kupokea maelekezo kutoka kwangu. Nilibaki kuzitizama huku nikiwa natafakari ni nini cha kuandika.

Itaendelea…
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI


SEHEMU YA 4

lipoishia..
nilichukua peni kisha nikaanza kuandika mistari kadhaa ambayo ilinijia kichwani..

“Nilikuumiza kihisia pia kimwili/
Licha ya upendo wako nilikulipa ukatili/
Nilifurahi kuona machozi yako/
Ni kama niliichukia furaha yako/
Kwa nguvu ya pendo lako ulivumilia yote/
Ukiamini kuwa…”


Nilishindwa kupata maneno ya kujazia ili kukamilisha mstari, nikaweka pei katikati ya daftari kisha nikalifukika na kuliweka lilipokuwa kisha nikajilaza kwenye godoro nikisubiri usingizi unipitie.

Endelea..
Miezi miwili ilikatika, maisha yakazidi kusonga mbele, nikaanza kuzoeleka kwa watu hasa wateja wa bidhaa niliyokuwa nauza. Niliendelea kupiga kazi kwa kujituma, japokuwa pia sikuwa nyuma kufuatilia mipango yangu ya kutoka kimuziki japokuwa sikuwa nafanya kwa nguvu sana. Nilikuwa nasubiri nikusanye angalau pesa za kunitosha ili nikianza harakati zangu, ziwe ni harakati kweli. Ingrid naye hakuwa nyuma, alinizoea hasa, tukawa kama marafiki wakubwa sana kwa kipindi kile kifupi nilichofahamiana naye. Na nilikuwa nafurahia uwepo wake kila wakati. Alikuwa ni mwanye kujali sana, alikuwa mwema sana kwangu. Ni kama alikuja kubadili mtizamo wangu juu ya uhusiano wangu na wasichana.

Siku moja wakati nikiwa naandaa chakula changu cha usiku nilisikia sauti ya ujumbe kutoka whatsapp kwenye simu yangu. Sikuwa na haraka kujua ni nani aliyekuwa amenitumia ujumbe kwa muda huo. Niliendelea kufanya nilichokuwa nafanya. Nilipomaliza nikaichukua nikaangalia kwenye kioo cha simu, alikuwa ni Ingrid, ujumbe ulisomeka ‘Hi Barry’.

‘Hi ingrid’ nikamjibu

‘umerudi?’ aliuliza

‘yeeep’

‘unafanyaje now?’

‘napika’

‘mmmh! Si ungeniita nije nikupikie’ aliandika Ingrid huku akiambatanisha na emoji tatu za kinyani kimefunika macho.

‘njoo basi’ nilimjibu huku nikiambatanisha emoji moja ya kucheka.

‘hadi nijipendekeze?’

‘we hutaki kuja acha maneno mingi, ngoja mi nipike uje ule, mwanamke gani wewe unakuwa mvivumvivu’ nilimtania.

‘weee koma, nani mvivu’ nilicheka majibu yake japokuwa huwa sipendi kuambiwa neno ‘koma’. Lakini kwa kuwa alikuwa ni Ingrid, rafiki yangu kipenzi..nililimezea hili.

“wewe piga domo tu…ukiwa mvivu utabaki kutoa michango na kuhudhuria sherehe za harusi za mashoga zako” niliambatanisha emoji za kicheko ili ajue nilikuwa natania.

“barry jamani, kwani mimi ni mvivu kiasi cha kuniambia maneno makali kiasi hicho?” aliandika Ingrid huku akiambatanisha na emoji za kununa.

“sasa kama hata hutaki kuja kunipikia, si uvivu huo?”

“kwa hiyo chakula cha siku ile ni wewe ulipika sio?”

“daaaah!.....kwa hiyo kile ulipika wewe?” nilimuuliza

“sasa je?”

“kwa chakula kile kilivyokuwa kitamu, naomba kutengua kauli yangu kuwa wewe ni mvivu. Nisamehe tu bibie, wewe ni wife material kabisa….”

“hahahaha…”

“kipii kikuchekechechacho?”

“si kwa kujitetea huko, sawa lakini…but ukimaliza kupika niambie, kuna jambo la kuongea na wewe”. jambo la kuongea na mimi. Nilistuka

“poa” niliamua kumjibu.

Niliendelea kupika huku akili akiwa imehama kidogo, ni nini alikuwa anataka kuongea na mimi? Nilijiuliza nikakosa jibu, nikaona sikuwa na haja kujitesa kutaka kujua ni nini alikuwa anataka kuniambia wakati muda si mrefu angeniambia. Nikawa mpole.

Nilipika, nikala, nikaosha vyombo, kisha nikajilaza kwenye godoro langu. Nikachukua simu kisha nikamtumia ujumbe.

‘tayari, karibu tule’ japokuwa nilikuwa tayari nimeshakula.

‘thanks’ alijibu.

“unasema tu thanks…, unakuja au?’.

‘ndiyo’

‘ukija kula usisahau kuniambia kile ambacho ulisema unataka kunambia’
‘nakuambia kwanza, ndo nije nile’

‘bwana weee sasa si utakuta nimeshamaliza kula?’

‘nitapika tena’

‘aaah kumbe nishajua, hutaki kula chakula changu’

‘mmmmmh’

‘mbona mguno mrefu hivyo!’

‘bwana weee, tuachane na hayo…”

“nakusikiliza madame”

“are you in relationship?” nilishtuka sana nilipouona ujumbe huo. Nilijiuliza ni nini kilimfanya aniulize swali hilo lakii sikupata jibu la haraka haraka.

“kwani vipi?” nilimuuliza baada ya kufikiri kwa muda.

“we nijibu ndo utajua”

“yeah,” niliamua kumjibu hivyo japokuwa ki ukweli sikuwa katika mahusiano.

“mhh, mbona sijawahi kumwona hata ukimpost status wifi?” aliuliza .

“ni mpenzi wangu, yeye siyo mali ya umma” nilimjibu.

“mhh.. haya bwana. msalimie”

“haya nimeshakujibu, sasa niambie ulichokuwa unataka kuniambia”

“tayari nimeshakwambia kuwa msalimie”

“hivyo tu?”

“ndiyo”

Jibu lake hilo lilinifanya nihisi kuwa pengine hakuwa amefurahishwa na majibu yangu au pengine hakutegemea kama ningemjibu kivyo. Jumbe zake za mwisho zilionyesha wazi hakuwa mwenye furaha kabisa. Japokuwa sikuwa na historia ya kuwa na uhusiano wa karibu sana na wasichana katika maisha yangu lakini nilikuwa na uwezo wa kutambua fikra zao kirhisi kabisa.

Hivyo, baada ya kugundua kuwa pengine hakupenda kile nilichomjibu basi nikaamua kugeuza upande wa pili wa shilingi.

“hahahaha, nakuzingua bwana..mimi bado niponipo kwanza” Nilimjibu huku nikiwa na hamu ya kutaka kujua yeye angenijibu nini.

“nilitaka kushangaa, mbona sijawahi kuona hata dalili!” alijibu ingrid. Niliona nuru katika maandishi yake na hivyo nikatambua ni wazi nilkkuwa natembea kwenye njia ambayo yeye alitaka nipite.

“kwa hiyo kumbe huwa unanichora tu, sio”

“walaah, hivyo ni vitu vya kuonekana tu mbona”

“haya bhana madame, umeshinda”

“sawa...nikuambie kitu barry?”

"Duh, inaonekana leo una vitu vingi sana vya kusema. Enhe nakusikiliza” Nilimjibu huku nikijiuliza ni nini kingine tena alitaka kukisema huyu binti.

“barry, sorry kama utanielewa vibaya, Barry nimeshindwa kujizuia, I love you so much.’ Aliandika Ingrid huku akiambatanisha na emoji za makopakopa. Nilistuka sana baada ya kuuona ujumbe huu. Akili ikafunguka na kuwaza mambo mengi kwa wakati mmoja, lakini bado sikuweza kupata jibu la harakaharaka. Katika kipindi chote ambacho tulikuwa katika dimbwi la urafiki na yeye sikuwahi kufikiri kuwa ipo siku tutahitaji kuingia katika mahusiano. Neno mapenzi halikuwapo kabisa ndani ya kichwa changu.

Nilizidi kufikiri kwa muda, sikujua nimjibu nini. Wakati najiuliza ni nini nimjibu nikaona ujumbe mwinngine kutoka kwake.

"Mbona kimya barry?" Ujumbe huu uliniamsha kutoka katika katika tafakari nzito ambayo nilikuwa naifanya kuhusu jambo lililokuwa mbele yangu kwa wakati huo.

Nilibonyeza kwenye uwanja wa kuandika jumbe, herufi zikatokea kwenye kioo kuashiria kuwa zilikuwa tayari kupokea maelekezo kutoka kwangu. Nilibaki kuzitizama huku nikiwa natafakari ni nini cha kuandika.

Itaendelea…
Kazi nzuri mkuu.
Tuko pamoja sana kiongozi.
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI

SEHEMU YA 5

Ilipoishia…

Nilizidi kufikiri kwa muda, sikujua nimjibu nini. Wakati najiuliza ni nini nimjibu nikaona ujumbe mwinngine kutoka kwake.

"Mbona kimya barry?" Ujumbe huu uliniamsha kutoka katika katika tafakari nzito ambayo nilikuwa naifanya kuhusu jambo lililokuwa mbele yangu kwa wakati huo.

Nilibonyeza kwenye uwanja wa kuandika jumbe, herufi zikatokea kwenye kioo kuashiria kuwa zilikuwa tayari kupokea maelekezo kutoka kwangu. Nilibaki kuzitizama huku nikiwa natafakari ni nini cha kuandika.

Endelea….

‘thanks,I love you too, Ingrid’ Nikaamua kumjibu kirahisi ili nione atasema nini. Jibu langu hili lililenga kutegeneza mazingira ya yeye kulazimika kujieleza zaidi na hilo lingefanya mimi niweze kung’amua ni nini hasa kilikuwa kichwani mwake.

“barry, seriously?’’ alijibu Ingrid huku akiambatanisha emoji za kidoli ambacho macho yake yamefunikwa na vikopokopa.

‘Seriously?, kwani yeye alikuwa anamaanisha kipi hasa’ nilijiuliza. Japokuwa nilikuwa nishaanza kuhisi ni nini alikuwa anataka kusema lakini nilingoja ili nijue mwisho wake.

“sasa kama unanipenda kwa nini mimi nisikupende?”

“so unamaanisha kuanzia sasa mimi ni girlfriend wako?”

“girlfriend…unamaanisha mpenzi wangu au?”

“ndio barry”

‘ingrid, mimi huwa napenda utani lakini si kama huu. Wewe ni rafiki yangu mzuri na niko na furaha kwa hilo. Lala maana naona umeanza kuugua’

‘barry, ni kweli naugua. Naugua kwa ajili yako. Nahitaji dawa kutoka kwako , Nifanye nipone, barry’

‘ingrid, hebu acha hizo story basi’ Nilimjibu kwa mkato kuonyesha nilikuwa namaanisha nilichokuwa nakisema.

‘barry hivi unadhani mimi naweza kucheza na hisia za mtu kwa kiasi hiki? jua nipo serious kuliko unavyodhani, nakupenda barry, I want you to be my man’. Nilitoa macho kuingalia simu. Nilikuwa siamini kile nilichokuwa nakiona. Nilirudia kusoma tena na tena. Nikashindwa nimjibu nini. Japokuwa nilikuwa na urafiki naye kwa muda sasa sikuwahi kuwaza kuwa kuna siku atakuja kuwa mpenzi wangu.

Muda kidogo simu ikaita….alikuwa ni Ingrid anapiga. Nilipata kigugumizi kuipokea. Nikawaza ni nini nitamwambia kama ni kweli atakuwa yupo serious na anachokisema. Je, nikimwambia hapana atajisikiaje?.katika mazingira ya kawaida ni vigumu sana kwa msichana kumtamkia mwanaume kuwa anampenda japokuwa mimi nimekuwa na bahati hiyo mara kadhaa. Kuna kipindi rafiki yangu mmoja alikuwa ananitania kuwa eti nina nyota ya chipsi mayai, kupendwa na watoto wa kike. Lakini nikajiuliza ni nini kinamvuta kwangu. Lakini kwa dhamiri ya dhati kabisa kutoka katika moyo wangu, sikuwa nataka kuwa na mahusiano na ingrid, wala msichana yeyote Yule. Ni kwa sababu kuna jambo lililonikuta na likanifanya nikose tamanio la kuwa na msichana kabisa katika maisha yangu japokuwa mara kadhaa hisia zilikuwa zinakaribia kunishinda lakini niliendelea kushikilia msimamo.

Sikuwa namtamani msichana mwingine yeyote, bali bali mmoja tu, ambaye naye kwa muda huo na hata baadaye nisingeweza kumpata tena. Sikuwa na uhakika kuwa huko aliko alikuwa ananikumbuka na mimi, lakini yeye ndiye aliyenifanya nisimpende msichana yeyote tena.

Simu iliendelea kuita lakini nilishindwa kuipokea. Ikakata, muda kidogo ikaanza kuita tena. Nikaamua kupokea.

‘adje’ nilisema kwa sauti ya utulivu wa hali ya juu

‘kwa nini hupokei simu yangu?’

“kwani hapa nimefanyaje?” nilimjibu

“si nimepiga mara ya kwanza hujapokea, ni nii kilikufanya usipokee?” aliongea igrid kwa sauti ya kulalamika.

“nilitoka kwenda maliwatoni” nilidanganya ili hilo liishe haraka.

“ok sawa, barry najua unaniwazia tofauti lakini nisingeweza kukaa na siri hii kwa muda mrefu, nakupenda sana barry, siwezi kueleza ni jinsi gani, but please nielewe tu hivyo barry. Hata mimi nashindwa kuelewa huu ujasiri wa kukutamkia nimeutoa wapi, ila naamini hisia zimenizidi na siwezi kuzihimili tena.” Aliongea Ingrid kwa sauti nyororo ambayo ilipenya katika masikio yangu na kuifanya nipatwe na hisia ambazo sikuwa nimezipata kwa muda mrefu sana.

“sikuwahi kufikiria mimi na wewe kuwa katika mahusiano ya kimapenzi, ni nini kinakufaya useme hivyo?” nilimuuliza kwa sauti iliyojaa utulivu, sauti iliyoonyesha kuwa nilikuwa najali kile alichokuwa anakisema.

“ukaribu wangu mimi na wewe ndo umesababisha yote haya….kila mara nawaza kuhusu wewe, pia nahisi utakuwa mtu sahihi kwangu” aliongea Ingrid kwa sauti ile ile nyororo na mara hii alimaliza kwa kushusha pumzi laini iliyojaa hisia kali za mapenzi. Taratibu nilianza kuona ni jinsi gani indrid alikuwa na hisia kali juu yangu.

“unahisi, huna uhakika” nilimjibu kwa mkato ili nizidi kujipa nafasi ya kufikiri ni jibu gani zuri la kumpa kwa sababu bado sikuwa na mpango wowote wa kumfanya yeye kuwa mpenzi wangu.

“but hisia huwa zinasema ukweli barry, sivyo?”

“si mara zote, anyway hicho kitu hakiwezekani na nasikitika kuongeza kuwa hakitowezekana kamwe. Futa kila kitu kukihusu, samahani sana Ingrid. ” nilimjibu kwa sauti dhabiti kuonyesha sikuwa natania hata kidogo. Niliamua kumuweka wazi ili asiendelee kuwa na matumaini hewa ambayo yangemuumiza hapo baadaye.

“jamani barry, kwa nini lakini? Kwa nini unanifanyia hivi?” aliuliza kwa sauti ya kinyonge sana, hadi nikajihisi kuumia. Lakini nisingeweza kubadili maamuzi yangu hata kidogo.

“ni kwa sababu haiwezekani…mimi nadhani kuwa marafiki kuna manufaa makubwa kwetu kuliko kuwa wapenzi”

“barry, tumeshakuwa marafiki kwa muda sasa, inatosha. Na kama unakiri kuwa urafiki wetu una manufaa, sasa fikiri kama tukisogea mbele zaidi, ni wazi kutakuwa na manufaa makubwa zaidi ya haya.” Aliongea Ingrid kwa msisitizo.

“Ingrid, najua ni nngumu kukubaliana na hili, ila nakuomba ulipokee.”

“barry why lakini, au mimi ni mbaya, sikuvutii. Na kila siku ulikuwa unanisifia kuwa mimi ni mrembo, na muda mfupi uliopita umetoka kuniambia kuwa mimi ni wife material. Barry, kama mimi ni mrembo, mkarimu na wife material kama ulivyokuwa unaniambia kila siku sasa ni kwa nini hutaki kuwa na mimi? Unamaanisha ulikuwa unanipaka mafuta kwa mgongo wa chupa, sio?” daaaah……hakuna kipindi kigumu kwa mwanume kama kutaka kumkatalia mwanamke ambaye hupendi kumuona akiwa na huzuni. Ingrid aliongea kwa hisia kali sana. Akili yangu ililazimika kufanya kazi ya ziada kutafuta majibu yatakayomfanya Ingrid atulie.

“hapana Ingrid…wewe ni mzuri. Wewe ni mrembo, una sifa zote za kuwa mpenzi, mchumba hadi kuwa mke wa mtu. Lakini si kwa mtu kama mimi. Sikufai, siendani na wewe. Samahani sana kwa hilo” niliamua kujishusha zaidi mbele yake. Hii mbinu ya kujiharibu mwenyewe na kumremba mwingine ilikuwa inanisaidia sana. Ni njia ambayo ilikuwa inanisaidia kumaliza matatizo mengi na niliiamini ingefanya kazi katika hili la Ingrid.

“nani amesema hunifai, huwafai wengine lakini unanifaa mimi pekeyangu” aliijibu Ingrid.

“Ingrid, hujui chochote kuhusu historia yangu ya nyuma, kwa hiyo ninaposema sikufai najua utakuwa huelewi ni nini namaanisha, ila elewa hivyo tu. Kwanza mimi ni mtu ambaye sina kipato cha kutosha kukuhudumia. Na sitokuwa najisikia furaha pale nitakapokuwa nashindwa kutatua matatizo yako madogo madogo. Sipendi uteseke, Ingrid ni dhambi kubwa sana kumchukua ndege kutoka porini ambako alikuwa anaishi kwa furaha na uhuru na kumpeleka nyumbani huku ukiwa unajua kuwa huwezi kumtunza vizuri. Maisha ninayoyaishi wewe mwenyewe unayaona, ni vipi ninaweza kukupa wewe furaha?”

“barry, mimi nakuhitaji wewe tu. Nikiwa na wewe hiyo inatosha kunipa furaha yote ninayoihitaji. Barry, can’t you feel what I feel?” aliongea kwa sauti ya kubembeleza, Ingrid alikuwa na sauti tamu sana. Maneno yake yalizidi kufanya nione halikuwa jambo rahisi kumtoka.

“najua fika kuwa unayasema haya kwa kuwa huu ni mwanzo tu”

“hapana barry, mapenzi sio pesa, mapenzi ni hisia. Hivyo vingine vinatafutwa.”

“Sikiliza Ingrid, hayo ni maneno tu kwa sababu upo katika kilele cha hisia kali, lakini siku za mbele utakuja kugundua kuwa kuna vitu vingine zaidi ya hisia za mapenzi. Lakini hata kama ni kweli unanipenda jinsi nilivyo na nikawa sikupatii huduma nyingine zaidi ya muda wangu na kukujali kibinadamu, bado nitakuwa najisikia vibaya. Hakuna mwanaume anapenda kutokumhudumia mpenzi wake. Nitakuwa naishi kwa wasiwasi muda wote. “

“barry, au unafurahia mimi ninavyoteseka kwa ajili yako. Mimi nimekwambia hilo sio tatizo but wewe bado umeng’ang’ania tu. Au mimi kukwambia nakupenda unahisi mimi ni Malaya?” aliongea kwa sauti yenye ukali kidogo. Nilishusha pumzi kwa nguvu. Ulikuwa ni wasaa mgumu sana kwangu. Kila neno nililokuwa natamka lilikujwa linapanguliwa kirahisi sana. Ililazimika nitumie ujuzi wa ziada kumtuliza.

“hapana Ingrid, usifike huko” nilijaribu kumtuliza.

“Lazima nifike tu, maana unang’ang’ania kitu ambacho tayari mi nasema si shida kwangu”

“ni kweli hilo laweza kuwa sio tatizo”

“kwa hiyo tunaweza kuwa pamoja si eti barry” aliuliza kwa sauti ya mahaba yaliyotukuka.

“hapana, nina tatizo kubwa zaidi ya hilo” nilimjibu

“barry, lipi hilo tena? Mbona sikuelewi lakini?” aliongea kwa sauti iliyoonyesha kuchanganyikiwa.

“siwezi kukwambia…..ni jambo la binafsi sana, siwezi kukwambia….na hilo hasa ndo linasababisha mimi na wewe tusiweze kuwa pamoja, nisamehe sana Ingrid.” Nilimwambia kwa upole ili ajue kuwa sikuwa natania hata kidogo.

“barry we niambie ili kama naweza kukusaidia nikusaidie ili tu mimi niwe na wewe. Hakuna jambo lisilo na suluhisho. Barry kuwa na huruma na hisia zangu” aliongea kwa sauti iliyosindikizwa na kwikwi ya kilio kwa mbali. Niliumia sana. Niliumia kuona msichana analia kwa sababu yangu. Nilishindwa kuelewa ni nini kilimfanya anipende sana kwa kiasi kile. Sikuwa na elimu, sikuwa na pesa pia. Ni nini hasa kilimvuta kwangu. Sikutaka aendelee kuumia zaidi . niliamua kumpa majibu ya kumpoza.

“ok, Ingrid nimekuelewa. Wacha niipe hekima itende kazi yake. Nitaamua kadri nitavyoona inafaa.”

“barry please, usiniache solemba please…..hujui tu jinsi huwa najisika furaha nikiisikia sauti yako. Ya upole, inafariji. Najihisi kutulizwa kabisa kimawazo usiku wa leo japo bado unazinyanyasa hisia zangu. Nakupenda sana barry, usisahau hili” aliongea kwa sauti ambayo kwa mwanaume yeyote rijali angeweza kusisimka. Ingrid alikuwa anajua kuitumia sauti yake vizuri. Alikuwa ni mtaalamu wa kuteka hisia, nadhani.

“usijali, Ingrid ….but nikuulize kitu”

“uliza tu sweetie” eti sweetie, linapokuja suala la hisia, mara zote wanawake huwa wapo hatua kadhaa mbele kutuzidi sisi wanaume.

“kwa nini unanipenda, nina nini cha zaidi labda?”

“sikiliza barry, una busara sana…unajali, pia najua wewe utakuwa mchumba mzuri na hatimaye mume mzuri pia”. Mimi niwe mchumba mzuri na hatimaye mume mruri. Mimi niwe mume mzuri, nadhani kwa sababu alikuwa hanijui vizuri. Laiti kama angekuwa ananifahamu japo kidogo asingesema hayo.

“una uhakika gani kuwa mimi nitakuwa mume mzuri?”

“barry wewe unajionaje?”

“sifahamu lolote kwa sababu siweji kujisoma mwenyewe, usiku mwema Ingrid, ulale sasa”

“daaah, natamani niendelee tu kuongea na wewe hata usiku mzima ili niendelee kuisikia sauti yako nzito inayoniliwaza na kunibembeleza, natamani niwe na wewe katika usiku huu tulivu nikiwa nimejilaza kifuani mwako, nikisikiliza kila pigo la moyo wako na mikono yako ikiwa ikitembea kwa taratibu katika kiuno changu. What a wonderful feeling.” Aliongea Ingrid huku akihema kimahaba. Maneno aliyoyatamka yalifanya nisisimke kiasi cha mkonga wangu kuanza kuamka kwa fujo. Nikiwa sijui ni nini nijibu Ingrid aliendelea “furaha yangu ni kuona mimi na wewe tunakuwa pamoja milele, Barry. Furaha yangu iko mikononi mwako ni maamuzi yako kuitunza ama kuiharibu. Barry utaweza kufanya furaha ya rafiki yako ikaharibika kweli?”

“nitafanya kadri ntakavyoona inafaa. Usiku mwema Ingrid” kisha nikakata simu. Sikutaka aendelee kuniongelesha zaidi.

Baada ya kukata simu kichwa kilikuwa na mawazo lukuki. Kila nikilipokuwa najaribu kuutafuta usingizi nilishindwa. Kila nikikumbuka maneno ya mwisho ya Ingrid mkonga ulizidi kuimarika na hakukuwa na dalili kama ungetulia muda mfupi baadaye na ikizingatiwa ni muda mrefu sikuwahi kupata hisia kama za siku hiyo.

Baada ya kuona itakuwa ngumu kutuliza hali ya hewa, nikabeba maji na sabuni nikaenda bafuni. Kabla ya kuoga nikapiga punyeto kushusha mzuka kisha nikaoga huku nikitafakari ni vipi jambo lililoanza siku hiyo lingeishaje.

Itaendelea….
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI

SEHEMU YA 5

Ilipoishia…

Nilizidi kufikiri kwa muda, sikujua nimjibu nini. Wakati najiuliza ni nini nimjibu nikaona ujumbe mwinngine kutoka kwake.

"Mbona kimya barry?" Ujumbe huu uliniamsha kutoka katika katika tafakari nzito ambayo nilikuwa naifanya kuhusu jambo lililokuwa mbele yangu kwa wakati huo.

Nilibonyeza kwenye uwanja wa kuandika jumbe, herufi zikatokea kwenye kioo kuashiria kuwa zilikuwa tayari kupokea maelekezo kutoka kwangu. Nilibaki kuzitizama huku nikiwa natafakari ni nini cha kuandika.

Endelea….

‘thanks,I love you too, Ingrid’ Nikaamua kumjibu kirahisi ili nione atasema nini. Jibu langu hili lililenga kutegeneza mazingira ya yeye kulazimika kujieleza zaidi na hilo lingefanya mimi niweze kung’amua ni nini hasa kilikuwa kichwani mwake.

“barry, seriously?’’ alijibu Ingrid huku akiambatanisha emoji za kidoli ambacho macho yake yamefunikwa na vikopokopa.

‘Seriously?, kwani yeye alikuwa anamaanisha kipi hasa’ nilijiuliza. Japokuwa nilikuwa nishaanza kuhisi ni nini alikuwa anataka kusema lakini nilingoja ili nijue mwisho wake.

“sasa kama unanipenda kwa nini mimi nisikupende?”

“so unamaanisha kuanzia sasa mimi ni girlfriend wako?”

“girlfriend…unamaanisha mpenzi wangu au?”

“ndio barry”

‘ingrid, mimi huwa napenda utani lakini si kama huu. Wewe ni rafiki yangu mzuri na niko na furaha kwa hilo. Lala maana naona umeanza kuugua’

‘barry, ni kweli naugua. Naugua kwa ajili yako. Nahitaji dawa kutoka kwako , Nifanye nipone, barry’

‘ingrid, hebu acha hizo story basi’ Nilimjibu kwa mkato kuonyesha nilikuwa namaanisha nilichokuwa nakisema.

‘barry hivi unadhani mimi naweza kucheza na hisia za mtu kwa kiasi hiki? jua nipo serious kuliko unavyodhani, nakupenda barry, I want you to be my man’. Nilitoa macho kuingalia simu. Nilikuwa siamini kile nilichokuwa nakiona. Nilirudia kusoma tena na tena. Nikashindwa nimjibu nini. Japokuwa nilikuwa na urafiki naye kwa muda sasa sikuwahi kuwaza kuwa kuna siku atakuja kuwa mpenzi wangu.

Muda kidogo simu ikaita….alikuwa ni Ingrid anapiga. Nilipata kigugumizi kuipokea. Nikawaza ni nini nitamwambia kama ni kweli atakuwa yupo serious na anachokisema. Je, nikimwambia hapana atajisikiaje?.katika mazingira ya kawaida ni vigumu sana kwa msichana kumtamkia mwanaume kuwa anampenda japokuwa mimi nimekuwa na bahati hiyo mara kadhaa. Kuna kipindi rafiki yangu mmoja alikuwa ananitania kuwa eti nina nyota ya chipsi mayai, kupendwa na watoto wa kike. Lakini nikajiuliza ni nini kinamvuta kwangu. Lakini kwa dhamiri ya dhati kabisa kutoka katika moyo wangu, sikuwa nataka kuwa na mahusiano na ingrid, wala msichana yeyote Yule. Ni kwa sababu kuna jambo lililonikuta na likanifanya nikose tamanio la kuwa na msichana kabisa katika maisha yangu japokuwa mara kadhaa hisia zilikuwa zinakaribia kunishinda lakini niliendelea kushikilia msimamo.

Sikuwa namtamani msichana mwingine yeyote, bali bali mmoja tu, ambaye naye kwa muda huo na hata baadaye nisingeweza kumpata tena. Sikuwa na uhakika kuwa huko aliko alikuwa ananikumbuka na mimi, lakini yeye ndiye aliyenifanya nisimpende msichana yeyote tena.

Simu iliendelea kuita lakini nilishindwa kuipokea. Ikakata, muda kidogo ikaanza kuita tena. Nikaamua kupokea.

‘adje’ nilisema kwa sauti ya utulivu wa hali ya juu

‘kwa nini hupokei simu yangu?’

“kwani hapa nimefanyaje?” nilimjibu

“si nimepiga mara ya kwanza hujapokea, ni nii kilikufanya usipokee?” aliongea igrid kwa sauti ya kulalamika.

“nilitoka kwenda maliwatoni” nilidanganya ili hilo liishe haraka.

“ok sawa, barry najua unaniwazia tofauti lakini nisingeweza kukaa na siri hii kwa muda mrefu, nakupenda sana barry, siwezi kueleza ni jinsi gani, but please nielewe tu hivyo barry. Hata mimi nashindwa kuelewa huu ujasiri wa kukutamkia nimeutoa wapi, ila naamini hisia zimenizidi na siwezi kuzihimili tena.” Aliongea Ingrid kwa sauti nyororo ambayo ilipenya katika masikio yangu na kuifanya nipatwe na hisia ambazo sikuwa nimezipata kwa muda mrefu sana.

“sikuwahi kufikiria mimi na wewe kuwa katika mahusiano ya kimapenzi, ni nini kinakufaya useme hivyo?” nilimuuliza kwa sauti iliyojaa utulivu, sauti iliyoonyesha kuwa nilikuwa najali kile alichokuwa anakisema.

“ukaribu wangu mimi na wewe ndo umesababisha yote haya….kila mara nawaza kuhusu wewe, pia nahisi utakuwa mtu sahihi kwangu” aliongea Ingrid kwa sauti ile ile nyororo na mara hii alimaliza kwa kushusha pumzi laini iliyojaa hisia kali za mapenzi. Taratibu nilianza kuona ni jinsi gani indrid alikuwa na hisia kali juu yangu.

“unahisi, huna uhakika” nilimjibu kwa mkato ili nizidi kujipa nafasi ya kufikiri ni jibu gani zuri la kumpa kwa sababu bado sikuwa na mpango wowote wa kumfanya yeye kuwa mpenzi wangu.

“but hisia huwa zinasema ukweli barry, sivyo?”

“si mara zote, anyway hicho kitu hakiwezekani na nasikitika kuongeza kuwa hakitowezekana kamwe. Futa kila kitu kukihusu, samahani sana Ingrid. ” nilimjibu kwa sauti dhabiti kuonyesha sikuwa natania hata kidogo. Niliamua kumuweka wazi ili asiendelee kuwa na matumaini hewa ambayo yangemuumiza hapo baadaye.

“jamani barry, kwa nini lakini? Kwa nini unanifanyia hivi?” aliuliza kwa sauti ya kinyonge sana, hadi nikajihisi kuumia. Lakini nisingeweza kubadili maamuzi yangu hata kidogo.

“ni kwa sababu haiwezekani…mimi nadhani kuwa marafiki kuna manufaa makubwa kwetu kuliko kuwa wapenzi”

“barry, tumeshakuwa marafiki kwa muda sasa, inatosha. Na kama unakiri kuwa urafiki wetu una manufaa, sasa fikiri kama tukisogea mbele zaidi, ni wazi kutakuwa na manufaa makubwa zaidi ya haya.” Aliongea Ingrid kwa msisitizo.

“Ingrid, najua ni nngumu kukubaliana na hili, ila nakuomba ulipokee.”

“barry why lakini, au mimi ni mbaya, sikuvutii. Na kila siku ulikuwa unanisifia kuwa mimi ni mrembo, na muda mfupi uliopita umetoka kuniambia kuwa mimi ni wife material. Barry, kama mimi ni mrembo, mkarimu na wife material kama ulivyokuwa unaniambia kila siku sasa ni kwa nini hutaki kuwa na mimi? Unamaanisha ulikuwa unanipaka mafuta kwa mgongo wa chupa, sio?” daaaah……hakuna kipindi kigumu kwa mwanume kama kutaka kumkatalia mwanamke ambaye hupendi kumuona akiwa na huzuni. Ingrid aliongea kwa hisia kali sana. Akili yangu ililazimika kufanya kazi ya ziada kutafuta majibu yatakayomfanya Ingrid atulie.

“hapana Ingrid…wewe ni mzuri. Wewe ni mrembo, una sifa zote za kuwa mpenzi, mchumba hadi kuwa mke wa mtu. Lakini si kwa mtu kama mimi. Sikufai, siendani na wewe. Samahani sana kwa hilo” niliamua kujishusha zaidi mbele yake. Hii mbinu ya kujiharibu mwenyewe na kumremba mwingine ilikuwa inanisaidia sana. Ni njia ambayo ilikuwa inanisaidia kumaliza matatizo mengi na niliiamini ingefanya kazi katika hili la Ingrid.

“nani amesema hunifai, huwafai wengine lakini unanifaa mimi pekeyangu” aliijibu Ingrid.

“Ingrid, hujui chochote kuhusu historia yangu ya nyuma, kwa hiyo ninaposema sikufai najua utakuwa huelewi ni nini namaanisha, ila elewa hivyo tu. Kwanza mimi ni mtu ambaye sina kipato cha kutosha kukuhudumia. Na sitokuwa najisikia furaha pale nitakapokuwa nashindwa kutatua matatizo yako madogo madogo. Sipendi uteseke, Ingrid ni dhambi kubwa sana kumchukua ndege kutoka porini ambako alikuwa anaishi kwa furaha na uhuru na kumpeleka nyumbani huku ukiwa unajua kuwa huwezi kumtunza vizuri. Maisha ninayoyaishi wewe mwenyewe unayaona, ni vipi ninaweza kukupa wewe furaha?”

“barry, mimi nakuhitaji wewe tu. Nikiwa na wewe hiyo inatosha kunipa furaha yote ninayoihitaji. Barry, can’t you feel what I feel?” aliongea kwa sauti ya kubembeleza, Ingrid alikuwa na sauti tamu sana. Maneno yake yalizidi kufanya nione halikuwa jambo rahisi kumtoka.

“najua fika kuwa unayasema haya kwa kuwa huu ni mwanzo tu”

“hapana barry, mapenzi sio pesa, mapenzi ni hisia. Hivyo vingine vinatafutwa.”

“Sikiliza Ingrid, hayo ni maneno tu kwa sababu upo katika kilele cha hisia kali, lakini siku za mbele utakuja kugundua kuwa kuna vitu vingine zaidi ya hisia za mapenzi. Lakini hata kama ni kweli unanipenda jinsi nilivyo na nikawa sikupatii huduma nyingine zaidi ya muda wangu na kukujali kibinadamu, bado nitakuwa najisikia vibaya. Hakuna mwanaume anapenda kutokumhudumia mpenzi wake. Nitakuwa naishi kwa wasiwasi muda wote. “

“barry, au unafurahia mimi ninavyoteseka kwa ajili yako. Mimi nimekwambia hilo sio tatizo but wewe bado umeng’ang’ania tu. Au mimi kukwambia nakupenda unahisi mimi ni Malaya?” aliongea kwa sauti yenye ukali kidogo. Nilishusha pumzi kwa nguvu. Ulikuwa ni wasaa mgumu sana kwangu. Kila neno nililokuwa natamka lilikujwa linapanguliwa kirahisi sana. Ililazimika nitumie ujuzi wa ziada kumtuliza.

“hapana Ingrid, usifike huko” nilijaribu kumtuliza.

“Lazima nifike tu, maana unang’ang’ania kitu ambacho tayari mi nasema si shida kwangu”

“ni kweli hilo laweza kuwa sio tatizo”

“kwa hiyo tunaweza kuwa pamoja si eti barry” aliuliza kwa sauti ya mahaba yaliyotukuka.

“hapana, nina tatizo kubwa zaidi ya hilo” nilimjibu

“barry, lipi hilo tena? Mbona sikuelewi lakini?” aliongea kwa sauti iliyoonyesha kuchanganyikiwa.

“siwezi kukwambia…..ni jambo la binafsi sana, siwezi kukwambia….na hilo hasa ndo linasababisha mimi na wewe tusiweze kuwa pamoja, nisamehe sana Ingrid.” Nilimwambia kwa upole ili ajue kuwa sikuwa natania hata kidogo.

“barry we niambie ili kama naweza kukusaidia nikusaidie ili tu mimi niwe na wewe. Hakuna jambo lisilo na suluhisho. Barry kuwa na huruma na hisia zangu” aliongea kwa sauti iliyosindikizwa na kwikwi ya kilio kwa mbali. Niliumia sana. Niliumia kuona msichana analia kwa sababu yangu. Nilishindwa kuelewa ni nini kilimfanya anipende sana kwa kiasi kile. Sikuwa na elimu, sikuwa na pesa pia. Ni nini hasa kilimvuta kwangu. Sikutaka aendelee kuumia zaidi . niliamua kumpa majibu ya kumpoza.

“ok, Ingrid nimekuelewa. Wacha niipe hekima itende kazi yake. Nitaamua kadri nitavyoona inafaa.”

“barry please, usiniache solemba please…..hujui tu jinsi huwa najisika furaha nikiisikia sauti yako. Ya upole, inafariji. Najihisi kutulizwa kabisa kimawazo usiku wa leo japo bado unazinyanyasa hisia zangu. Nakupenda sana barry, usisahau hili” aliongea kwa sauti ambayo kwa mwanaume yeyote rijali angeweza kusisimka. Ingrid alikuwa anajua kuitumia sauti yake vizuri. Alikuwa ni mtaalamu wa kuteka hisia, nadhani.

“usijali, Ingrid ….but nikuulize kitu”

“uliza tu sweetie” eti sweetie, linapokuja suala la hisia, mara zote wanawake huwa wapo hatua kadhaa mbele kutuzidi sisi wanaume.

“kwa nini unanipenda, nina nini cha zaidi labda?”

“sikiliza barry, una busara sana…unajali, pia najua wewe utakuwa mchumba mzuri na hatimaye mume mzuri pia”. Mimi niwe mchumba mzuri na hatimaye mume mruri. Mimi niwe mume mzuri, nadhani kwa sababu alikuwa hanijui vizuri. Laiti kama angekuwa ananifahamu japo kidogo asingesema hayo.

“una uhakika gani kuwa mimi nitakuwa mume mzuri?”

“barry wewe unajionaje?”

“sifahamu lolote kwa sababu siweji kujisoma mwenyewe, usiku mwema Ingrid, ulale sasa”

“daaah, natamani niendelee tu kuongea na wewe hata usiku mzima ili niendelee kuisikia sauti yako nzito inayoniliwaza na kunibembeleza, natamani niwe na wewe katika usiku huu tulivu nikiwa nimejilaza kifuani mwako, nikisikiliza kila pigo la moyo wako na mikono yako ikiwa ikitembea kwa taratibu katika kiuno changu. What a wonderful feeling.” Aliongea Ingrid huku akihema kimahaba. Maneno aliyoyatamka yalifanya nisisimke kiasi cha mkonga wangu kuanza kuamka kwa fujo. Nikiwa sijui ni nini nijibu Ingrid aliendelea “furaha yangu ni kuona mimi na wewe tunakuwa pamoja milele, Barry. Furaha yangu iko mikononi mwako ni maamuzi yako kuitunza ama kuiharibu. Barry utaweza kufanya furaha ya rafiki yako ikaharibika kweli?”

“nitafanya kadri ntakavyoona inafaa. Usiku mwema Ingrid” kisha nikakata simu. Sikutaka aendelee kuniongelesha zaidi.

Baada ya kukata simu kichwa kilikuwa na mawazo lukuki. Kila nikilipokuwa najaribu kuutafuta usingizi nilishindwa. Kila nikikumbuka maneno ya mwisho ya Ingrid mkonga ulizidi kuimarika na hakukuwa na dalili kama ungetulia muda mfupi baadaye na ikizingatiwa ni muda mrefu sikuwahi kupata hisia kama za siku hiyo.

Baada ya kuona itakuwa ngumu kutuliza hali ya hewa, nikabeba maji na sabuni nikaenda bafuni. Kabla ya kuoga nikapiga punyeto kushusha mzuka kisha nikaoga huku nikitafakari ni vipi jambo lililoanza siku hiyo lingeishaje.

Itaendelea….
Mwamba kaona ajilipue kwanza ili akili ifanye kazi sawia.

Jumatano sio mbali panapo majaliwa kujua kilichojiri.
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI

SEHEMU YA SITA.

Ilipoishia..

Baada ya kuona itakuwa ngumu kutuliza hali ya hewa, nikabeba maji na sabuni nikaenda bafuni. Kabla ya kuoga nikapiga punyeto kushusha mzuka kisha nikaoga huku nikitafakari ni vipi jambo lililoanza siku hiyo lingeishaje.

Endelea…

Asubuhi ilifika, nikaamka ili kujiandaa kwenda kazini huku nikifikiri kile kilichotokea jana usiku. Nilikuwa nahisi pengine ilikuwa ni ndoto. Nikiwa katika maandalizi nilisikia sauti ya simu ikiunguruma. Nikatazama kioo, nikaona jina la Ingrid, na hapo ndipo nilipothibitisha kuwe tukio la jana lilikuwa halisi kabisa.

“Halo Ingrid” nilisema kwa sauti yenye uchovu kidogo.

“mambo vipi barry?” aliongea kwa sauti iliyotulia.

“Mi nipo poa tu sijui wewe.”

“mi nipo salama, umeshaeda kazini?”

“hapana, ndo najiandaa kutoka” niliendelea kumjibu kimkatomkato ili kumkatisha asiongee sana.

“ok poa, but mwenzio nina presha hatari, we hujui tu” aliongea kwa sauti ya mahaba ya kinyonge.

“kuhusu nini?” nilimjibu kama vile sikuwa najua chochote kinachoendelea.

“ni kama nasubiri majibu ya ukimwi vile, please najua umefikiria kuhusu kile tulichokiongea usiku wa jana”. Alisema kwa sauti ya chini sana, iliyojaa huzuni na mahaba. Na mimi nilikuwa nimepitisha uamuzi wa kuwa sintomkubalia mimi na yeye tuwe wapenzi kwa namna yoyote ile ila tatizo nilikuwa natafuta namna bora ya kumwambia ili asihuzunike kwa sababu mbali ya mimi kutotaka kuwa na mahusiano na yeye lakini yeye alikuwa ni rafiki yangu hivyo sikutaka kumpoteza.

“sikiliza Ingrid, binafsi nimeona si vyema kukudanganya au kukupa matumaini ya bandia. Sitaki kukuumiza, najua utaumia lakini maumivu haya ni madogo kuliko yale utakayoyapata pindi pale tutakapokuwa pamoja….sijawahi kupenda, sina roho ya kupenda….na sijui kama nitakuja kujaaliwa moyo huo wa kupenda. Tafadhali niache nitakuwa rafiki yako. Na nakuahidi, nitakuwa mtu mwema kwako kuliko vile ningekuwa kama mpenzi wako.” Nilijikuta naropoka maneno hayo bila kupangilia wala kujali athari zake kwa Ingrid.

“barry, kwa nini lakini unanifanyia hivi, au kwa sababu umeshajua kuwa nakupenda hivyo unanifanyia makusudi” aliongea kwa kulalamika.

“ni vipi kama tusingeonana, ungenipenda mimi?”

“barry, Mungu alikuwa na mpango na sisi ndiyo maana akatukutanisha”

“mpango gani huo?”

“jamani barry, si mimi na wewe tuwe wapenzi, tuwe na familia”

“tuwe wapenzi, tuwe na familia, wewe ni msichana wa aina gani, umekazana tu niwe mumeo mara familia. Kitu ambacho hukifahamu wewe ni kuwa, kwa upande wangu msamiati mapenzi haupo kabisa kwenye dictionary yangu. Sijawahi kumpenda mwanamke hata siku moja. Sitaki yakukute yale yaliyomkuta mwenzako” nilizidi kusisitiza.

“mwenzangu, nani?…kilitokea nini?” aliuliza maswali mawili kwa mkupuo.

“huyo ndiye aliyethibitisha kuwa mimi sina roho ya upendo…huwa naumia sana kila nikilikumbuka sana lile tukio. Nilimkosea sana. Huwa naumia sana kila nikikumbuka lile tukio huwa natamani siku zirudi nyuma ili nisahihishe makosa yangu lakini haiwezekani, na haitowezekana kamwe. Hivyo nina wasiwasi kuwa hili litatokea kwako pia kama tukiwa wapenzi. Hii ndiyo sababu ya mimi sikubaliani na wewe katika hili.” Niliongea katika sauti iliyojaa msisitizo.

“barry…kwani ni nini kilitokea kati yake na wewe?” aliuliza Ingrid kwa sauti iliyojaa shauku.

“siwezi kukwambia……..ni jambo binafsi na kubwa zaidi ni kuwa ni tukio baya sana, huenda ukanichukia?”

“hapana barry…. We nambie tu. Huenda tukalipatia suluhisho kwa sasa”

“niache niende kazini tafadhali….siku njema Ingrid" nilisema na kukata simu.

Nilimalizia kujiaandaa nikatoka nje ili niende katika majukumu yangu. Wakati nanyanyua macho nikakutana na Ingrid amesimama nje akiniangalia. Alikuwa amakaa kihuzuni sana pia niliyaona mahaba mazito aliyokuwa nayo juu yangu. Sikutaka kuonyesha hisia yoyote kwa Ingrid kwa kuwa wapangaji wengine walikuwa tayari wameanza kuamka. Nilipitisha uamuzi wa kupita bila kusalimia kwa kuwa kama kusalimiana tulishasalimiana kwenye simu.

“barry” ingrid aliniita, nilimwangalia huku nikiendelea kutembea kuelekea geti lilipo, nikanyanyua mkono wangu, nikampungia kisha nikachapa mwendo.

Niliendelea na safari yangu huku nikiwa na mawazo tele. Ingrid alinifanya niwaze sana. Kwanza nilijilaumu kwa kuanzisha mazoea naye. Nilijilaumu kwa kumdokezea kuhusu tukio lililotia simanzi kubwa katika maisha yangu. Na juu ya yote hayo, nisingeweza kukubali hisia ziniongoze kufikia hatua ya mimi kuanza uhusiano wa kimapenzi na Ingrid. Mara zote nilikuwa naomba fikra ziniongoze zaidi. lakini kilichokuwa kinaniumiza pia ni kumwona Ingrid akiwa na huzuni. Alikuwa amekuwa rafiki yangu kwa muda sasa, na urafiki wetu ulikuwa ni wenye manufaa sana. Japokuwa nilikuwa na uamuzi tayari lakini sikupenda nimuone na huzuni. Lakini nikaona ni bora nijipe muda ili nione ni nini kitaendelea katika siku zijazo.

***

Siku zilizidi kwenda, Ingrid akiendelea kunisumbua. Nikamzungusha lakini bado alikuwa ameng’ang’ana. Tatizo si kwa sababu nilikuwa simpendi, bali sikuwa na hakika kama mimi nilikuwa nimebadilika. Kwa sababu katika mahusiano yangu ya mwanzo nimekuwa ni mtu mwenye matata matata sana. Wasichana wengi walinilalamikia kuwa sikuwa na haiba ya kujali. Nilikuwa Napata shida sana ni nini nikifanye ili niweze kumtuliza na kumridhisha Ingrid bila ya kumkubali, nikashindwa. Kila siku zilivyokuwa zinasonga mbele ndivyo alivyozidi kukosa amani na kunyong’onyea, yote haya kwa sababu yangu tu. Denis naye hakuwa nyuma kunishauri kuhusu kufanya maamuzi. Mara zote alikuwa akiniambia kuwa nisilaze damu kwa Ingrid maana alikuwa ni msichana mzuri na mwenye haiba nzuri pia. Nakumbuka baadhi ya mazungumzo yetu kuhusu hili jambo.

“hivi barry, unatumia kiungo gani kufikiria? Msichana anakutaka we unamringia, umerogwa?” Denis aliniuliza.

“kwani cha ajabu ni kipi, mbona wao huwa wanatukatalia na huwa ni jambo la kawaida tu, kwa nini iwe ajabu kwangu” nilimjibu.

“kwa hiyo hujampenda?”

“kwani mimi nimeshawahi kupenda mtu?, Denis usijifanye umenisahau. Nadhani unafahamu ni jinsi gani nilivyo sina hisia za karibu kwa wasichana. Unajua fika ni jinsi gani nimekuwa nikiwatendea wasichana niliowahi kuwa nao. Unakumbuka kila kitu kichotokea kati yangu na jenifer, sivyo?. Hivi unadhani nitakuwa nimebadilika? Sipendi mabaya niliyokuwa nawafanyia wengine yamkute Ingrid. Sitaki kumkosea Ingrid.”

“we jamaa kila siku unakumbushia tu hilo jambo. Hata kama lilikuathiri, sasa utajuaje kama umebadilika kama hutaingia kwenye mahusiano?”

“Denis, tatizo linalokusumbua ni kunilazimisha nitumie hisia mahala ambapo fikra inatakiwa itumike. Haya ni maisha yangu, ushauri wako nimeuchukua lakini nakwambia sitowahi kuufanyia kazi”

‘’Endelea kumringia, siku akiwa off wewe upo on ndo utajua”

“haitokaa itokee” nilimjibu denis huku nikimwangalia kwa huku nikicheka.

“sawa, siku yakikushinda nifuate tu ntakusaidia”

“labda mambo mengine lakini siyo hili”

hivi ndivyo danis alikuwa akijaribu kunishawishi ili nikubaliane na Ingrid lakini nilimkatalia katakata. Na mara zote nilizidi kuomba niendelee kuwa na moyo uleule maana mimi kwenye mahusiano najifahamu vizuri sana.

Usumbufu ulizidi hadi ikafika mahali nikaamua kupitisha uamuzi wa kumwambia kile ambacho hasa kilikuwa kinanifanya nisikubali ombi lake la mimi na yeye kuwa wapenzi. Niliamua kufanya hivyo ili kumpunguza kasi ya kunisumbua kila siku. Nilisubiri anitafute ili nimwambie hicho kilichokuwa kinafanya mimi na yeye iwe vigumu kuwa wapenzi. Na kweli ilikuwa hivyo.

Alifanya hivyo kama kawaida yake, nyakati za usiku alinipigia simu, nikapokea.

“mambo barry” aliongea kwa sauti ya upole.

“safi tu, vipi wewe”

“si salama hata kidogo” alisema kwa sauti ya chini lakini yenye hasira kwa mbali.

“kwa nini?”

“ unajua ni kwa nini….nimejipendekeza kwako sana, nimekubembeleza sana, sasa inatosha. Najilaumu ni kwa nini nilikuambia ukweli wangu. Ni bora nigebaki kuugulia maumivu ya kubaki na siri kuliko haya ninayoyapata sasa. Nilijua ungenisikiliza, ungethamini hisia zangu, lakini imekuwa kinyume barry, nakuchukia……nakuchukia sana barry, sitaki hata kukuona. Ningekuwa na mamlaka ningekuhamisha ukakae sehemu nyingine” alisema Ingrid kwa sauti iliyokuwa na kilio ndani yake. Niliumia sana lakini pia nilifurahi kwani ilikuwa ni nafasi ya kujikomboa katika dimbwi hilo. Kwa kuwa nilikuwa mtaalamu wa kucheza na hisia za wasichana, kauli ile ya Ingrid ilikuwa nafasi adhimu sana kwangu kumfanya Ingrid aachane na mimi na pia aendelee kuwa rafiki yangu.

“Ingrid, unamaanisha hutonipigiaa simu tena?, hatotuchat tena?” niliuliza kwa sauti ya upole na iliyojaa busara.

“kamwe, leo ndiyo mwisho, sahau kila kitu kuhusu mimi…nakuchukia sana barry…sitaki hata urafiki na wewe tena. Niache niishi maisha yangu, siwezi kuwa na urafiki na mtu anayeishi na mimi kinafki. Unashindwa kusikiliza hitaji la nafsi yangu na bado unasema eti twaweza kuwa marafiki” alijibu Ingrid, mara hii akiwa na hasira za dhahiri kaisa.

Baada ya kusikia hivyo, nikaamua niumalize mjadala. Nilitaka kuumaliza mjadala kwa njia ambayo mimi na yeye, wote tungeridhika. Njia yenye busara na hekima huku ikiniacha mimi nikiwa mshindi.

“sawa, nimekuelewa Ingrid. Ila kabla ya kufanya hayo utakayo naomba unipe nafasi niseme maneno yangu ya mwisho kwako. Najua inawezekana ni kweli leo ikawa ni siku ya mwisho kusikia sauti yako ambayo mara zote nimekuwa nafarijika sana kuisikia. Huenda ni kweli leo ukawa ndo mwisho wa urafiki kati yangu mimi na wewe, urafiki ambao siku zote nimekuwa nikitegemea kuwa ungekuwa ni wenye manufaa makubwa sana kati yetu. Sikupingi katika maamuzi yako, hayo ni maamuzi yako na yanafaa kuheshimiwa…na nakiri kuwa nitayaheshimu. Pia umesema unanichukia, kwa kuwa eti mimi sijali hisia zako. Laiti ungejua ni mabaya mangapi ambayo mimi nitakuwa nimekuepusha kwa mimi kukukatalia pengine usingesema hivyo. Na sikukatalia kwa sababu eti sikupendi au nakuchukia lakini kuna kitu ambacho kinafanya yote haya.
“ Ingrid, hivi unadhani mimi si mwanadamu? Au unadhani mimi nafurahi kukuona una huzuni kwa ajili yangu? Hata mimi naumia pia, lakini ni bora maumivu haya unayoyapata sasa kuliko hayo ambayo utayapata baadae kwa kuwa na mimi. Umeamua kutangaza kuvunja urafiki wetu kwa jambo hili dogo, sawa. Lakini nakuomba utambue kuwa unanionea, haunitendei haki hata kidogo. Najua hatuwezi acha kuonana kila siku…lakini jaribu kufikiria mimi nitakuwa najisikiaje pale ambapo nitakuwa nakuona? Anyway… nipo tayari kukupa ukweli wangu wote nyuma ya maamuzi yangu siku yoyote ile ambapo utahitaji na kama ratiba yangu itaruhusu. Baada ya hapo unaweza kuendelea na msimamo wako wa kukata mahusiano na ukaribu wetu. Vinginevyo, nita’miss’ vitu vingi kutoka kwako rafiki yangu, Ingrid” sikutaka kumpa nafasi aijibu hoja hii,ilikata simu, nikaizima, nikalala.
Itaendelea…
 
MAISHA YANGU NYUMA YA PAZIA JEUSI

SEHEMU YA SITA.

Ilipoishia..

Baada ya kuona itakuwa ngumu kutuliza hali ya hewa, nikabeba maji na sabuni nikaenda bafuni. Kabla ya kuoga nikapiga punyeto kushusha mzuka kisha nikaoga huku nikitafakari ni vipi jambo lililoanza siku hiyo lingeishaje.

Endelea…

Asubuhi ilifika, nikaamka ili kujiandaa kwenda kazini huku nikifikiri kile kilichotokea jana usiku. Nilikuwa nahisi pengine ilikuwa ni ndoto. Nikiwa katika maandalizi nilisikia sauti ya simu ikiunguruma. Nikatazama kioo, nikaona jina la Ingrid, na hapo ndipo nilipothibitisha kuwe tukio la jana lilikuwa halisi kabisa.

“Halo Ingrid” nilisema kwa sauti yenye uchovu kidogo.

“mambo vipi barry?” aliongea kwa sauti iliyotulia.

“Mi nipo poa tu sijui wewe.”

“mi nipo salama, umeshaeda kazini?”

“hapana, ndo najiandaa kutoka” niliendelea kumjibu kimkatomkato ili kumkatisha asiongee sana.

“ok poa, but mwenzio nina presha hatari, we hujui tu” aliongea kwa sauti ya mahaba ya kinyonge.

“kuhusu nini?” nilimjibu kama vile sikuwa najua chochote kinachoendelea.

“ni kama nasubiri majibu ya ukimwi vile, please najua umefikiria kuhusu kile tulichokiongea usiku wa jana”. Alisema kwa sauti ya chini sana, iliyojaa huzuni na mahaba. Na mimi nilikuwa nimepitisha uamuzi wa kuwa sintomkubalia mimi na yeye tuwe wapenzi kwa namna yoyote ile ila tatizo nilikuwa natafuta namna bora ya kumwambia ili asihuzunike kwa sababu mbali ya mimi kutotaka kuwa na mahusiano na yeye lakini yeye alikuwa ni rafiki yangu hivyo sikutaka kumpoteza.

“sikiliza Ingrid, binafsi nimeona si vyema kukudanganya au kukupa matumaini ya bandia. Sitaki kukuumiza, najua utaumia lakini maumivu haya ni madogo kuliko yale utakayoyapata pindi pale tutakapokuwa pamoja….sijawahi kupenda, sina roho ya kupenda….na sijui kama nitakuja kujaaliwa moyo huo wa kupenda. Tafadhali niache nitakuwa rafiki yako. Na nakuahidi, nitakuwa mtu mwema kwako kuliko vile ningekuwa kama mpenzi wako.” Nilijikuta naropoka maneno hayo bila kupangilia wala kujali athari zake kwa Ingrid.

“barry, kwa nini lakini unanifanyia hivi, au kwa sababu umeshajua kuwa nakupenda hivyo unanifanyia makusudi” aliongea kwa kulalamika.

“ni vipi kama tusingeonana, ungenipenda mimi?”

“barry, Mungu alikuwa na mpango na sisi ndiyo maana akatukutanisha”

“mpango gani huo?”

“jamani barry, si mimi na wewe tuwe wapenzi, tuwe na familia”

“tuwe wapenzi, tuwe na familia, wewe ni msichana wa aina gani, umekazana tu niwe mumeo mara familia. Kitu ambacho hukifahamu wewe ni kuwa, kwa upande wangu msamiati mapenzi haupo kabisa kwenye dictionary yangu. Sijawahi kumpenda mwanamke hata siku moja. Sitaki yakukute yale yaliyomkuta mwenzako” nilizidi kusisitiza.

“mwenzangu, nani?…kilitokea nini?” aliuliza maswali mawili kwa mkupuo.

“huyo ndiye aliyethibitisha kuwa mimi sina roho ya upendo…huwa naumia sana kila nikilikumbuka sana lile tukio. Nilimkosea sana. Huwa naumia sana kila nikikumbuka lile tukio huwa natamani siku zirudi nyuma ili nisahihishe makosa yangu lakini haiwezekani, na haitowezekana kamwe. Hivyo nina wasiwasi kuwa hili litatokea kwako pia kama tukiwa wapenzi. Hii ndiyo sababu ya mimi sikubaliani na wewe katika hili.” Niliongea katika sauti iliyojaa msisitizo.

“barry…kwani ni nini kilitokea kati yake na wewe?” aliuliza Ingrid kwa sauti iliyojaa shauku.

“siwezi kukwambia……..ni jambo binafsi na kubwa zaidi ni kuwa ni tukio baya sana, huenda ukanichukia?”

“hapana barry…. We nambie tu. Huenda tukalipatia suluhisho kwa sasa”

“niache niende kazini tafadhali….siku njema Ingrid" nilisema na kukata simu.

Nilimalizia kujiaandaa nikatoka nje ili niende katika majukumu yangu. Wakati nanyanyua macho nikakutana na Ingrid amesimama nje akiniangalia. Alikuwa amakaa kihuzuni sana pia niliyaona mahaba mazito aliyokuwa nayo juu yangu. Sikutaka kuonyesha hisia yoyote kwa Ingrid kwa kuwa wapangaji wengine walikuwa tayari wameanza kuamka. Nilipitisha uamuzi wa kupita bila kusalimia kwa kuwa kama kusalimiana tulishasalimiana kwenye simu.

“barry” ingrid aliniita, nilimwangalia huku nikiendelea kutembea kuelekea geti lilipo, nikanyanyua mkono wangu, nikampungia kisha nikachapa mwendo.

Niliendelea na safari yangu huku nikiwa na mawazo tele. Ingrid alinifanya niwaze sana. Kwanza nilijilaumu kwa kuanzisha mazoea naye. Nilijilaumu kwa kumdokezea kuhusu tukio lililotia simanzi kubwa katika maisha yangu. Na juu ya yote hayo, nisingeweza kukubali hisia ziniongoze kufikia hatua ya mimi kuanza uhusiano wa kimapenzi na Ingrid. Mara zote nilikuwa naomba fikra ziniongoze zaidi. lakini kilichokuwa kinaniumiza pia ni kumwona Ingrid akiwa na huzuni. Alikuwa amekuwa rafiki yangu kwa muda sasa, na urafiki wetu ulikuwa ni wenye manufaa sana. Japokuwa nilikuwa na uamuzi tayari lakini sikupenda nimuone na huzuni. Lakini nikaona ni bora nijipe muda ili nione ni nini kitaendelea katika siku zijazo.

***

Siku zilizidi kwenda, Ingrid akiendelea kunisumbua. Nikamzungusha lakini bado alikuwa ameng’ang’ana. Tatizo si kwa sababu nilikuwa simpendi, bali sikuwa na hakika kama mimi nilikuwa nimebadilika. Kwa sababu katika mahusiano yangu ya mwanzo nimekuwa ni mtu mwenye matata matata sana. Wasichana wengi walinilalamikia kuwa sikuwa na haiba ya kujali. Nilikuwa Napata shida sana ni nini nikifanye ili niweze kumtuliza na kumridhisha Ingrid bila ya kumkubali, nikashindwa. Kila siku zilivyokuwa zinasonga mbele ndivyo alivyozidi kukosa amani na kunyong’onyea, yote haya kwa sababu yangu tu. Denis naye hakuwa nyuma kunishauri kuhusu kufanya maamuzi. Mara zote alikuwa akiniambia kuwa nisilaze damu kwa Ingrid maana alikuwa ni msichana mzuri na mwenye haiba nzuri pia. Nakumbuka baadhi ya mazungumzo yetu kuhusu hili jambo.

“hivi barry, unatumia kiungo gani kufikiria? Msichana anakutaka we unamringia, umerogwa?” Denis aliniuliza.

“kwani cha ajabu ni kipi, mbona wao huwa wanatukatalia na huwa ni jambo la kawaida tu, kwa nini iwe ajabu kwangu” nilimjibu.

“kwa hiyo hujampenda?”

“kwani mimi nimeshawahi kupenda mtu?, Denis usijifanye umenisahau. Nadhani unafahamu ni jinsi gani nilivyo sina hisia za karibu kwa wasichana. Unajua fika ni jinsi gani nimekuwa nikiwatendea wasichana niliowahi kuwa nao. Unakumbuka kila kitu kichotokea kati yangu na jenifer, sivyo?. Hivi unadhani nitakuwa nimebadilika? Sipendi mabaya niliyokuwa nawafanyia wengine yamkute Ingrid. Sitaki kumkosea Ingrid.”

“we jamaa kila siku unakumbushia tu hilo jambo. Hata kama lilikuathiri, sasa utajuaje kama umebadilika kama hutaingia kwenye mahusiano?”

“Denis, tatizo linalokusumbua ni kunilazimisha nitumie hisia mahala ambapo fikra inatakiwa itumike. Haya ni maisha yangu, ushauri wako nimeuchukua lakini nakwambia sitowahi kuufanyia kazi”

‘’Endelea kumringia, siku akiwa off wewe upo on ndo utajua”

“haitokaa itokee” nilimjibu denis huku nikimwangalia kwa huku nikicheka.

“sawa, siku yakikushinda nifuate tu ntakusaidia”

“labda mambo mengine lakini siyo hili”

hivi ndivyo danis alikuwa akijaribu kunishawishi ili nikubaliane na Ingrid lakini nilimkatalia katakata. Na mara zote nilizidi kuomba niendelee kuwa na moyo uleule maana mimi kwenye mahusiano najifahamu vizuri sana.

Usumbufu ulizidi hadi ikafika mahali nikaamua kupitisha uamuzi wa kumwambia kile ambacho hasa kilikuwa kinanifanya nisikubali ombi lake la mimi na yeye kuwa wapenzi. Niliamua kufanya hivyo ili kumpunguza kasi ya kunisumbua kila siku. Nilisubiri anitafute ili nimwambie hicho kilichokuwa kinafanya mimi na yeye iwe vigumu kuwa wapenzi. Na kweli ilikuwa hivyo.

Alifanya hivyo kama kawaida yake, nyakati za usiku alinipigia simu, nikapokea.

“mambo barry” aliongea kwa sauti ya upole.

“safi tu, vipi wewe”

“si salama hata kidogo” alisema kwa sauti ya chini lakini yenye hasira kwa mbali.

“kwa nini?”

“ unajua ni kwa nini….nimejipendekeza kwako sana, nimekubembeleza sana, sasa inatosha. Najilaumu ni kwa nini nilikuambia ukweli wangu. Ni bora nigebaki kuugulia maumivu ya kubaki na siri kuliko haya ninayoyapata sasa. Nilijua ungenisikiliza, ungethamini hisia zangu, lakini imekuwa kinyume barry, nakuchukia……nakuchukia sana barry, sitaki hata kukuona. Ningekuwa na mamlaka ningekuhamisha ukakae sehemu nyingine” alisema Ingrid kwa sauti iliyokuwa na kilio ndani yake. Niliumia sana lakini pia nilifurahi kwani ilikuwa ni nafasi ya kujikomboa katika dimbwi hilo. Kwa kuwa nilikuwa mtaalamu wa kucheza na hisia za wasichana, kauli ile ya Ingrid ilikuwa nafasi adhimu sana kwangu kumfanya Ingrid aachane na mimi na pia aendelee kuwa rafiki yangu.

“Ingrid, unamaanisha hutonipigiaa simu tena?, hatotuchat tena?” niliuliza kwa sauti ya upole na iliyojaa busara.

“kamwe, leo ndiyo mwisho, sahau kila kitu kuhusu mimi…nakuchukia sana barry…sitaki hata urafiki na wewe tena. Niache niishi maisha yangu, siwezi kuwa na urafiki na mtu anayeishi na mimi kinafki. Unashindwa kusikiliza hitaji la nafsi yangu na bado unasema eti twaweza kuwa marafiki” alijibu Ingrid, mara hii akiwa na hasira za dhahiri kaisa.

Baada ya kusikia hivyo, nikaamua niumalize mjadala. Nilitaka kuumaliza mjadala kwa njia ambayo mimi na yeye, wote tungeridhika. Njia yenye busara na hekima huku ikiniacha mimi nikiwa mshindi.

“sawa, nimekuelewa Ingrid. Ila kabla ya kufanya hayo utakayo naomba unipe nafasi niseme maneno yangu ya mwisho kwako. Najua inawezekana ni kweli leo ikawa ni siku ya mwisho kusikia sauti yako ambayo mara zote nimekuwa nafarijika sana kuisikia. Huenda ni kweli leo ukawa ndo mwisho wa urafiki kati yangu mimi na wewe, urafiki ambao siku zote nimekuwa nikitegemea kuwa ungekuwa ni wenye manufaa makubwa sana kati yetu. Sikupingi katika maamuzi yako, hayo ni maamuzi yako na yanafaa kuheshimiwa…na nakiri kuwa nitayaheshimu. Pia umesema unanichukia, kwa kuwa eti mimi sijali hisia zako. Laiti ungejua ni mabaya mangapi ambayo mimi nitakuwa nimekuepusha kwa mimi kukukatalia pengine usingesema hivyo. Na sikukatalia kwa sababu eti sikupendi au nakuchukia lakini kuna kitu ambacho kinafanya yote haya.
“ Ingrid, hivi unadhani mimi si mwanadamu? Au unadhani mimi nafurahi kukuona una huzuni kwa ajili yangu? Hata mimi naumia pia, lakini ni bora maumivu haya unayoyapata sasa kuliko hayo ambayo utayapata baadae kwa kuwa na mimi. Umeamua kutangaza kuvunja urafiki wetu kwa jambo hili dogo, sawa. Lakini nakuomba utambue kuwa unanionea, haunitendei haki hata kidogo. Najua hatuwezi acha kuonana kila siku…lakini jaribu kufikiria mimi nitakuwa najisikiaje pale ambapo nitakuwa nakuona? Anyway… nipo tayari kukupa ukweli wangu wote nyuma ya maamuzi yangu siku yoyote ile ambapo utahitaji na kama ratiba yangu itaruhusu. Baada ya hapo unaweza kuendelea na msimamo wako wa kukata mahusiano na ukaribu wetu. Vinginevyo, nita’miss’ vitu vingi kutoka kwako rafiki yangu, Ingrid” sikutaka kumpa nafasi aijibu hoja hii,ilikata simu, nikaizima, nikalala.
Itaendelea…
Game la hisia linaanza sasa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom