Hadithi hadithi.?

Hadithi hadithi.?

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
27,483
Reaction score
61,851
Hapo zamani kuku na mwewe walikuwa marafiki. Siku moja kuku akaenda kuazima sindano ya kushona nguo kwa mwewe iliyokuwa ikitumiwa na ukoo mzima wa mwewe.
Kwa bahati mbaya ile sindano ikapotea. Mwewe alikasirika sana akataka alipwe sindano yake ya ukoo la sivyo atajilipiza kwa kuchukua vifaranga vya kuku na kupeleka kwenye ukoo wake hadi sindano itakapo patikana. Ndo maana hadi leo kuku anatafuta sindano kwa kufukua fukua kila sehemu ili kuokoa kizazi chake.
Hadithi yangu inaishia hapo. Mia
 
ha ha ha ha....dah kumbe ndio sababu ya kisa cha kuku kufukua chini.....aisee makes sense
 
Kitabu CHA kwanza CHA kusoma. HATUA YA kwanza
HUYU NI Juma;
Juma ANA Dada;
Dada YA Juma NI Roza;
Roza NI MTOTO mdogo;
Roza ni mdogo KULIKO Juma.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom