Six Man
JF-Expert Member
- Dec 19, 2017
- 253
- 893
NAKUCHUKIA SHADYA
Juma Hiza
0712988278
Najua utajiuliza ni kwanini namchukia Shadya. Naam! Nafahamu hili ndilo litakuwa swali la kwanza litakalokujia katika ufahamu wako. Hata hivyo sishangai kupokea swali kama hili kutoka kwako kwani kichwa cha mkasa huu kinazungumza kuwa namchukia Shadya. Ni kweli namchukia sana Shadya wala sijui kama chuki yangu dhidi yake itakuja kutoweka. Namchukia sana tena sana tu.
Ngoja nikueleze kitu ndugu yangu, mpenzi msikilizaji wa mkasa huu. Katika mapenzi kuna mambo mengi sana huwa yanatokea. Mengi kati ya hayo huwa ni yenye kuleta furaha moyoni na mengine huweza kukusababishia maumivu makali kiasi kwamba ikatokea ukayachukia mapenzi kabisa, ukaona hukustahili kupenda au kupendwa.
Mapenzi yanaweza yakakusababisha ukajikuta unaishi katika dunia usiyoweza kuitambua, dunia ya kukosa amani muda wote karaha ndio akawa ndugu yako wa karibu. Unaweza ukawa chizi usiyeokota makopo lakini sababu kubwa ikawa ni mapenzi.
Laiti kama mapenzi yangepewa umbo la kuwa kiumbe kilicho hai, yasadiki maneno yangu kuwa leo hii ninapokusimulia haya yasingekuwa hai kama siokuwa maututi hospitalini kwa kujeruhiwa vibaya na binadamu mwenye hasira kali ambaye kila siku anayachukia mapenzi kuliko kitu chochote kile katika hii dunia yenye kila jema na baya unalo lifahamu.
Asikwambie mtu mapenzi ni kitu kingine kabisa. Sijui niyaweke katika fungu gani kwani kila ninapojaribu kuyatafakari hujikuta naishia kuumwa kichwa mwisho nalala pasipo kujijua.
Kama si mapenzi nafikiri leo hii nisingekuwepo hapa nikakusimulia mkasa huu ambao naamini utabaki kama kumbukumbu kwa vizazi hadi vizazi ili nao waweze kujifunza mambo mengi kutoka kwangu na nisingependa wayarudie makosa niliyowahi kuyafanya. Nataka simulizi hii ibaki kuwa yangu ya peke yangu.
Nisingependa baada ya mkasa huu masikio yangu yasikie eti! Kuna akina Shadya wengine ambao wanaochukiwa zaidi ya huyu aliyeniumiza mimi. Aliyenipa jeraha la moyo litakaloacha kovu la milele katika moyo wangu wa nyama. Kovu ambalo litaniumiza siku zote za uhai wa maisha yangu mpaka pale mwisho wa pumzi zangu utakapowadia.
Simulizi hii ikuache na fundisho kubwa katika maisha yako.
****
Muda:Saa 4:00 usiku.
Ally anasimulia;
Nakumbuka mambo mengi sana yaliyowahi kutokea katika maisha yangu na Shadya. Nilimpenda sana Shadya kwa kuwa niliamini ni mwanamke pekee ambaye angeweza kuishi na mimi siku zote za uhai wa maisha yangu. Alikuwa ni mwanamke ambaye alivumilia mambo mengi sana, nakumbuka ugumu wa maisha niliyokuwa nao lakini bado hakuchoka kunipenda, alizidi kunionyesha mapenzi ya dhati ambayo kiukweli sikuwahi kuwaza wala kutegemea kwamba kuna siku itafika atakuja kuniumiza maishani, nilimuamini sana. Nilijinyima sana kwasababu yake. Alinikabidhi dhamana ya kuutunza moyo wake wa mapenzi uliyokuwa kwangu japo kutokana na uzuri aliyokuwa amejaaliwa alikuwa akisumbuliwa na wanaume wengi lakini hakusita kuniambia kuwa alikuwa akinipenda mimi na ni mimi pekee ambaye alikuwa akinisubiria katika maisha yake.
Ama kweli maneno ya wahenga waliyosema “Maisha ni safari ndefu iliyokuwa na kiza mbeleni”, usemi huu uliweza kujidhihirisha katika maisha yangu, sikuwa na kazi ya maana, maisha yangu niliyaendesha kwa kuungaunga kwa vibarua vya kujishikiza ilimradi maisha yasonge mbele.
Nilikuwa nikipigika haswaa! ilimradi niweze kumridhisha Shadya mwanamke wa maisha yangu. Niliamini bila ya yeye hakukuwa mimi maishani. Mtaa niliyokuwa naishi nilikuwa ni mwanaume pekee ambaye niliyebahatika kutembea na msichana mrembo sana, marafiki zangu walikuwa wakinisifia sana huku wengine wakinigeuka na kwenda kumfuata kwa lengo la kuniharibia lakini hakuna walichoambulia, Shadya alikuwa akinipenda sana, kiukweli kwa wakati ule nilikuwa nikimuamini kupita kawaida.
Kichwa changu bado kinayakumbuka vyema maneno yake aliyokuwa akiniambia kila mara kuwa alikuwa akinipenda hivyo nizidi kuishi na imani thabiti juu yake, alikuwa hapendi kuniona nikimuhisi vibaya, alifanya kila awezalo ilimradi nimuamini na kweli alifanikiwa katika hilo.
Baada ya mwaka mmoja kupita tangu uhusiano wetu ulipoanza, Shadya alianza kuitamani ndoa, kila alipopata nafasi ya kukaa na mimi alikuwa akinisihi sana suala la ndoa.
“Baby na mimi nataka kuwa mke wa mtu,” aliniambia Shadya huku akiilegeza Sauti yake iliyobadilika na kuwa kama ya kitoto.
“Shadya mpenzi wangu, mipango bado haijakaa sawa nivumilie kidogo nitakuoa tu! mpenzi,” nilimjibu huku nilimtazama usoni ni hapa ambapo nikazidi kuuona uzuri wa msichana huyu ambaye alikuwa ameziteka hisia zangu katika gereza la mapenzi, nilikuwa kipofu kwake.
“Marafiki zangu wote wameshaolewa bado mimi tu! yani watu wananishangaa,” aliniambia Shadya huku akiubetua mdomo wake. Alionekana kuchukizwa sana na maneno yangu.
“Inakupasa uwe mvumilivu mpenzi wangu,” nilimwambia.
“Sitaki mimi nataka kuolewa.” aliniambia Shadya.
Maneno ya Shadya yalizidi kuniweka katika wakati mgumu sana. Sikuwa na kazi ambayo ilikuwa ikiyaendesha maisha yangu, sasa ingekuwaje kama ningeamua kumuoa? Hili lilikuwa ni swali ambalo lilikuwa likiniumiza sana kichwa. Niliwaza mambo mengi sana juu ya hili lakini hakuna nilichong’amua sanasana nilizidi kujiumiza tu!.
Niliamua kumueleza Mama yangu kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Nakumbuka aliniambia nitafute maisha kwanza kwani mapenzi yapo tu! na ningeyakuta mbeleni.
“Lakini Mama nina malengo naye kumbuka,” nilimwambia Mama.
“Hata kama unamalengo naye kitu cha umuhimu ni kuandaa mazingira, tafuta kazi kwanza mwanangu, kama kweli anakupenda atakusubiri.” aliniambia Mama. Mwanamke pekee ambaye alikuwa mshauri wangu mkubwa, Kauli yake ilikuwa na uzito mkubwa sana kwangu katika kufanya maamuzi.
Nilizidi kupambana kutafuta maisha usiku na mchana huku nikiamini Shadya alikuwa akinisubiri ili niweze kumuoa. Maneno yake ya kunifariji kila siku ndiyo ambayo yalikuwa yakinipa nguvu ya kuzidi kutafuta hata pale nilipokuwa nataka kukata tama niliweza kuamka na kutafuta tena bila kuchoka.
“Nimefiwa na Shangazi yangu wa Morogoro hivyo itanibidi niende kule msibani,” aliniambia Shadya siku moja alipokuja kunipa taarifa za msiba. Zilikuwa ni taarifa mbaya sana kuzipokea na kama mwanadamu ziliweza kuniumiza sana. Nilimruhusu aende msibani ambapo aliniambia angeweza kukaa kwa muda wa mwezi mmoja, aliniambia kuwa aliwakumbuka sana ndugu zake waliokuwepo huko. Safari hiyo pia aliitumia kwa kwenda kukaa na ndugu zake.
****
Baada ya mwezi mmoja kupita niliweza kupokea taarifa zilizoniumiza sana moyo wangu, nilipata taarifa kuwa Shadya alikuwa ameolewa na mwanaume mwingine huko Morogoro. Kwakweli sikutaka kuamini kile nichokuwa nikiambiwa kwa wakati huo, waliobahatika kwenda harusini waliweza kunionyesha picha zake. Nilihisi kuchanganyikiwandugu msikilizaji.
Tangu hapo sikuweza tena kumuona Shadya machoni mwangu wala Sikuweza tena kusikia japo sauti yake ikirandaranda masikioni mwangu, ameondoka na mapenzi yangu, ameiacha na kidonda kilichoacha kovu linalozidi kuniumiza kila siku maishani mwangu.
NAMCHUKIA SANA!!” alimaliza kusimulia Ally alipokuwa akihojiwa na kipindi cha redio kilichokuwa kikipendwa na watu wengi sana. Kilikuwa ni kipindi cha Mikasa ya Kimapenzi na Maisha.
Mtangazaji wa kipindi hicho aliyejulikana kwa jina moja la Salma aliruhusu maswali na ushauri kwa wasikilizaji wa kipindi hicho pendwa. Wasikilizaji wengi walikuwa wakipiga simu huku wengine wakituma ujumbe mfupi wa kumpa pole Ally kwa mkasa huo uliyomkuta katika maisha yake.
MWISHO.
Juma Hiza
0712988278
Najua utajiuliza ni kwanini namchukia Shadya. Naam! Nafahamu hili ndilo litakuwa swali la kwanza litakalokujia katika ufahamu wako. Hata hivyo sishangai kupokea swali kama hili kutoka kwako kwani kichwa cha mkasa huu kinazungumza kuwa namchukia Shadya. Ni kweli namchukia sana Shadya wala sijui kama chuki yangu dhidi yake itakuja kutoweka. Namchukia sana tena sana tu.
Ngoja nikueleze kitu ndugu yangu, mpenzi msikilizaji wa mkasa huu. Katika mapenzi kuna mambo mengi sana huwa yanatokea. Mengi kati ya hayo huwa ni yenye kuleta furaha moyoni na mengine huweza kukusababishia maumivu makali kiasi kwamba ikatokea ukayachukia mapenzi kabisa, ukaona hukustahili kupenda au kupendwa.
Mapenzi yanaweza yakakusababisha ukajikuta unaishi katika dunia usiyoweza kuitambua, dunia ya kukosa amani muda wote karaha ndio akawa ndugu yako wa karibu. Unaweza ukawa chizi usiyeokota makopo lakini sababu kubwa ikawa ni mapenzi.
Laiti kama mapenzi yangepewa umbo la kuwa kiumbe kilicho hai, yasadiki maneno yangu kuwa leo hii ninapokusimulia haya yasingekuwa hai kama siokuwa maututi hospitalini kwa kujeruhiwa vibaya na binadamu mwenye hasira kali ambaye kila siku anayachukia mapenzi kuliko kitu chochote kile katika hii dunia yenye kila jema na baya unalo lifahamu.
Asikwambie mtu mapenzi ni kitu kingine kabisa. Sijui niyaweke katika fungu gani kwani kila ninapojaribu kuyatafakari hujikuta naishia kuumwa kichwa mwisho nalala pasipo kujijua.
Kama si mapenzi nafikiri leo hii nisingekuwepo hapa nikakusimulia mkasa huu ambao naamini utabaki kama kumbukumbu kwa vizazi hadi vizazi ili nao waweze kujifunza mambo mengi kutoka kwangu na nisingependa wayarudie makosa niliyowahi kuyafanya. Nataka simulizi hii ibaki kuwa yangu ya peke yangu.
Nisingependa baada ya mkasa huu masikio yangu yasikie eti! Kuna akina Shadya wengine ambao wanaochukiwa zaidi ya huyu aliyeniumiza mimi. Aliyenipa jeraha la moyo litakaloacha kovu la milele katika moyo wangu wa nyama. Kovu ambalo litaniumiza siku zote za uhai wa maisha yangu mpaka pale mwisho wa pumzi zangu utakapowadia.
Simulizi hii ikuache na fundisho kubwa katika maisha yako.
****
Muda:Saa 4:00 usiku.
Ally anasimulia;
Nakumbuka mambo mengi sana yaliyowahi kutokea katika maisha yangu na Shadya. Nilimpenda sana Shadya kwa kuwa niliamini ni mwanamke pekee ambaye angeweza kuishi na mimi siku zote za uhai wa maisha yangu. Alikuwa ni mwanamke ambaye alivumilia mambo mengi sana, nakumbuka ugumu wa maisha niliyokuwa nao lakini bado hakuchoka kunipenda, alizidi kunionyesha mapenzi ya dhati ambayo kiukweli sikuwahi kuwaza wala kutegemea kwamba kuna siku itafika atakuja kuniumiza maishani, nilimuamini sana. Nilijinyima sana kwasababu yake. Alinikabidhi dhamana ya kuutunza moyo wake wa mapenzi uliyokuwa kwangu japo kutokana na uzuri aliyokuwa amejaaliwa alikuwa akisumbuliwa na wanaume wengi lakini hakusita kuniambia kuwa alikuwa akinipenda mimi na ni mimi pekee ambaye alikuwa akinisubiria katika maisha yake.
Ama kweli maneno ya wahenga waliyosema “Maisha ni safari ndefu iliyokuwa na kiza mbeleni”, usemi huu uliweza kujidhihirisha katika maisha yangu, sikuwa na kazi ya maana, maisha yangu niliyaendesha kwa kuungaunga kwa vibarua vya kujishikiza ilimradi maisha yasonge mbele.
Nilikuwa nikipigika haswaa! ilimradi niweze kumridhisha Shadya mwanamke wa maisha yangu. Niliamini bila ya yeye hakukuwa mimi maishani. Mtaa niliyokuwa naishi nilikuwa ni mwanaume pekee ambaye niliyebahatika kutembea na msichana mrembo sana, marafiki zangu walikuwa wakinisifia sana huku wengine wakinigeuka na kwenda kumfuata kwa lengo la kuniharibia lakini hakuna walichoambulia, Shadya alikuwa akinipenda sana, kiukweli kwa wakati ule nilikuwa nikimuamini kupita kawaida.
Kichwa changu bado kinayakumbuka vyema maneno yake aliyokuwa akiniambia kila mara kuwa alikuwa akinipenda hivyo nizidi kuishi na imani thabiti juu yake, alikuwa hapendi kuniona nikimuhisi vibaya, alifanya kila awezalo ilimradi nimuamini na kweli alifanikiwa katika hilo.
Baada ya mwaka mmoja kupita tangu uhusiano wetu ulipoanza, Shadya alianza kuitamani ndoa, kila alipopata nafasi ya kukaa na mimi alikuwa akinisihi sana suala la ndoa.
“Baby na mimi nataka kuwa mke wa mtu,” aliniambia Shadya huku akiilegeza Sauti yake iliyobadilika na kuwa kama ya kitoto.
“Shadya mpenzi wangu, mipango bado haijakaa sawa nivumilie kidogo nitakuoa tu! mpenzi,” nilimjibu huku nilimtazama usoni ni hapa ambapo nikazidi kuuona uzuri wa msichana huyu ambaye alikuwa ameziteka hisia zangu katika gereza la mapenzi, nilikuwa kipofu kwake.
“Marafiki zangu wote wameshaolewa bado mimi tu! yani watu wananishangaa,” aliniambia Shadya huku akiubetua mdomo wake. Alionekana kuchukizwa sana na maneno yangu.
“Inakupasa uwe mvumilivu mpenzi wangu,” nilimwambia.
“Sitaki mimi nataka kuolewa.” aliniambia Shadya.
Maneno ya Shadya yalizidi kuniweka katika wakati mgumu sana. Sikuwa na kazi ambayo ilikuwa ikiyaendesha maisha yangu, sasa ingekuwaje kama ningeamua kumuoa? Hili lilikuwa ni swali ambalo lilikuwa likiniumiza sana kichwa. Niliwaza mambo mengi sana juu ya hili lakini hakuna nilichong’amua sanasana nilizidi kujiumiza tu!.
Niliamua kumueleza Mama yangu kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Nakumbuka aliniambia nitafute maisha kwanza kwani mapenzi yapo tu! na ningeyakuta mbeleni.
“Lakini Mama nina malengo naye kumbuka,” nilimwambia Mama.
“Hata kama unamalengo naye kitu cha umuhimu ni kuandaa mazingira, tafuta kazi kwanza mwanangu, kama kweli anakupenda atakusubiri.” aliniambia Mama. Mwanamke pekee ambaye alikuwa mshauri wangu mkubwa, Kauli yake ilikuwa na uzito mkubwa sana kwangu katika kufanya maamuzi.
Nilizidi kupambana kutafuta maisha usiku na mchana huku nikiamini Shadya alikuwa akinisubiri ili niweze kumuoa. Maneno yake ya kunifariji kila siku ndiyo ambayo yalikuwa yakinipa nguvu ya kuzidi kutafuta hata pale nilipokuwa nataka kukata tama niliweza kuamka na kutafuta tena bila kuchoka.
“Nimefiwa na Shangazi yangu wa Morogoro hivyo itanibidi niende kule msibani,” aliniambia Shadya siku moja alipokuja kunipa taarifa za msiba. Zilikuwa ni taarifa mbaya sana kuzipokea na kama mwanadamu ziliweza kuniumiza sana. Nilimruhusu aende msibani ambapo aliniambia angeweza kukaa kwa muda wa mwezi mmoja, aliniambia kuwa aliwakumbuka sana ndugu zake waliokuwepo huko. Safari hiyo pia aliitumia kwa kwenda kukaa na ndugu zake.
****
Baada ya mwezi mmoja kupita niliweza kupokea taarifa zilizoniumiza sana moyo wangu, nilipata taarifa kuwa Shadya alikuwa ameolewa na mwanaume mwingine huko Morogoro. Kwakweli sikutaka kuamini kile nichokuwa nikiambiwa kwa wakati huo, waliobahatika kwenda harusini waliweza kunionyesha picha zake. Nilihisi kuchanganyikiwandugu msikilizaji.
Tangu hapo sikuweza tena kumuona Shadya machoni mwangu wala Sikuweza tena kusikia japo sauti yake ikirandaranda masikioni mwangu, ameondoka na mapenzi yangu, ameiacha na kidonda kilichoacha kovu linalozidi kuniumiza kila siku maishani mwangu.
NAMCHUKIA SANA!!” alimaliza kusimulia Ally alipokuwa akihojiwa na kipindi cha redio kilichokuwa kikipendwa na watu wengi sana. Kilikuwa ni kipindi cha Mikasa ya Kimapenzi na Maisha.
Mtangazaji wa kipindi hicho aliyejulikana kwa jina moja la Salma aliruhusu maswali na ushauri kwa wasikilizaji wa kipindi hicho pendwa. Wasikilizaji wengi walikuwa wakipiga simu huku wengine wakituma ujumbe mfupi wa kumpa pole Ally kwa mkasa huo uliyomkuta katika maisha yake.
MWISHO.
Fadhy Mtanga, 2010