Habari njema kwa Vibonge!

Habari njema kwa Vibonge!

Madame B watu wenye shepu za hivyo ni wachache sana. We ukipita barabarani unakutana na wangapi wenye pododo kama lako? wengi wamenenepa hovyo hovyo tu matumbo yametangulia

ni kweli,unakuta mdada kanenepa tumbo mbele,---- kule vurugu tupu, shepu inakua hovyo kabisa,anakosa mvuto zaidi ni kituko!
 
huyu Maty hana nia nzuri na Madame B eti anamshawishi apunguze uoto wa asili aaagrrrrrrrr mi nalipinga hili kwa nguvu zote akipunguza tutashangaa nini sasa jamani Maty?

We nipunguze hazina nife na njaa mjini hapa?
Hakuna hiyo.
Hapa ni nyagi na valuu.
 
Last edited by a moderator:
haya mpwa yana raha yake bana upo nalo maeneo maeneo umekaa nalo unapata moja baridi moja moto likaenda toilet angalia meza za karibu wanaume kwa wanawake wanavyo tumbua mimacho kuangalia Singida Dodoma kama wamebanwa na mlango.

uwiiii eeee mbavu zangu mie,ngoja nikae kimya
 
Huo ndio mpango wa mujini MADAME B,waje wapate maujuzi ya kutoa vitambi huku looolz!

Waje waone Tips za kupunguza vitambi wasije kutuua vitandani bure.
Kila siku chuma mboga tuu.
Akha,
Wakuje...
passion lady, waite.
 
Last edited by a moderator:
ANGALIZO
Hii soup inapunguza mwili kwa haraka sana ila ukishapungua inabidi uangalie mlo wako inabidi upunguze vyakula vya mafuta mawali maugali badala yake ule mboga nyingi kuliko chakula, sio baada ya wiki unaanza kufakamia misosi mfululizo utanenepa zaidi ya mwanzo.
Maty njia bora ya kupunguza unene ni kufanya mazoezi na kurekebisha unachokula na unakula wakati gani.

Pili sielewi ni kwa nini mtu upunguze unene lakini still ukubali kuwa mwili flabby. Tuache visingizio. Mazoezi ni muhimu sana kwa afya zetu.

These short cuts won't lead us anywhere.
 
Last edited by a moderator:
Maty asante mwayaa... mbona lakini hapo kwa avatar wewe ni mwembamba? au huyo ni mdogo wako (joke), BUT nafikiri mtu kabla huja ji commit katika diet au mazoezi kwa ajili ya kupunguza mwili ni bora kujifunza kwanza maisha utakayoishi baada ya diet... as inabidi uchange life style ili umaintain.

Na ni muhimu tutambue kwamba kupunguza na kuongezeka uzito mara kwa mara (kwa njia za short curt) si nzuri kiafya.
 
Dear baadhi ya viungo hujaelezea namna na wakati wa kuviweka, ila kwa kuwa nafahamu upishi kwangu haijawa shida kuelewa...

Sijaiandika mimi mpendwa nimeicopy huko nilikoitoa kama ilivyo na kupaste hapa, mimi niliprint nimefuata maelekezo hayo jinsi yalivyo na imenisaidia, sifanyi matangazo ya biashara nimeiweka ili kama kuna mtu amechoka unene kama ambavyo niliuchoka mimi atumie na inaweza kumsaidia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom