Nimepokea sms kwenye simu yangu ya mkononi ikiwa na ujumbe huu na nimeona ni vizuri niwashirikishe harakati hizi zinazoendeshwa na undisclosed sources.
"Nzi na nyuki hufa kwa kulazimisha kupenya kwenye kioo angavu, na ndivyo watakavyoangamia wasomi, wafanyakazi na wakulima wanaolazimisha kutimiza ndoto zao kupitia chama cha mafisadi (ccm).
Sasa tuunge mkono kwenye kampeni maalumu dhidi ya Kikwete 2010, maana aliingia kwa mbinu atatoka kwa mbinu. Mtenda utendewa, tuwasapoti wadai haki na oparesheni SANGARA, Tanzania bila Kikwete inawezekana.
Tuma ujumbe huu kwa walio choshwa na Kikwete. Hasa Walimu, NMB, TRL, Wazee wastaafu wa EAC, Wanafunzi vyuoni, Madaktari, Polisi, Maaskofu, Mapadri, Makadhi, Mashehe, Wavuvi, Waumini wa dini zote na Wakurugenzi wa vyombo vya habari."
Nasisitiza kwamba huu ujumbe nimeupokea kwenye simu yangu na sijui ni nani kanitumia.
MF
I don't think whether this is a constructive strategy!!i've been working with nmb for more than 4 years, na sikuwahi hata mara moja kusikia watu wakimlalamikia Kikwete!!!! Walimu?! walimu gani? hawahawa ambao hata ukiwasikiliza wanapishana maoni kwenye masuala yao wenyewe au kuna wengine?! Labda TRL, lakini nahofia kama sehemu iliyo na lundo la wazee namna ile wanaweza kuwa tayari kwa mabadiliko kupita njia ya simu!!! Labda Maaskofu na mapadri, kwavile tutake tusitake, udini Tanzani upo, hususani ule wa chinichini!!! eti wakurugenzi wa vyombo vya habari!!!? lol! vyombo vipi? hivi vya TZ au vingine!!!? Mengi anayejitia kupiga vita ufisadi, magazeti yake yote nayo yanajitia kupiga vita ufisadi!!! Rostam Azizi anayeonekana papa la ufisadi, vyombo vyake vyote vina msimamo tofauti na ule wa vya IPP!! umenipata hapo mkuu?! Vyombo vya habari vyetu vinaegemea kule walikoegemea wamiliki wake!!!