Habari Corparation imezaliwa Upya?

Hivi kwani hamfahamu camp ya RA na EL wamekuwa na strategy ya kuichafua serikali ya mkwere na kuiondolea imani kwa umma, imani ambayo tayari haipo...in short wanafanya kila wawezalo kufanya kazi ya serikali iwe ngumu mara mia!!

Ni kweli mwanangu Hekima inasema mamlaka yeyote ikijifitini LAZIMA ISAMBARATIKE Hasira ya mkizi ni furaha kwa mvuvi!
 
Mwenzet katoa mada cha maan ni kuijadili siyo kumtukana na kutaka mtu afikiri jinsi wewe unavyofikiri kitu ambacho hakiwezekani. Tumpe mawako kama alivyosema mwingine kuwa mmiliki wa New Habari cooperation ni mjanja sana na anatumia chombo kile kueneza propaganda za kuwabeza maadui zake na kuwapongeza marafiki zake bila kujali wako chama gani hasa kwa chama tawala ambao ndiyo wana mpa kula. ukiangalia amemuweka Hussein Bashe Pale kuwa mkurugenzi mtendaji anamlipa mshahara mkubwa wakati mapato ya pale ni madogo. Ukweli ni kwamba ukiacha propaganda Rostam hana cha ziada anachofaidi pale. New Habari cooperation ipo pale kwa maslahi ya rostam liaziz ingawa kwenye umiliki hamna jina wala sahihi yake. atampamba anayetimiza matakwa yake na kumponda aliyekinyume chake. Na si kwa watu tu hata sera zinazoelekea kuua maslahi yake. rostam aziz anamiliki makampuni zaidi ya 17 hapa nchini lakini hakuna hata moja lenye jina au sahihi yake sasa JK sijui hajui au amelogwa au naye fisadi sijui maana kama ndivyo basi huyo jamaa jake (rose mtam) atakua jambazi basi maana nimesikia ila sina uhakika kuwa amefungua makmpuni manne hapo jirani KENYA na yote ameasajili kwa jina lake. Sisi waTZ ni majuha au shamba la bibi?????
 
wapo waliokosa malezi mazuri ya wazee huingia jf

Ni kweli kabisaaaa.

Jamani mimi jana nimesoma Mtanzania nikafikiri nasoma Mwananchi na nikapata mshtuko. Ni kweli hili gazeti ni kama limebadilisha mwelekeo lakini siwezi amini mpaka machapisho 20 yapite ndo tuta conclude vizuri. Ila kutukana si vizuri wakuu
 
JF siyo marketing board.

Lakini Nyie vipi,mtoa mada kakosa nini jamani.

Kama HP wamejirekwebisha walipokuwa wamekosea hilo ni SAFI SANA kitaaluma nadhani la mmoja wetu anajua hilo.Pia wao wanaona mwitikio wa jamii,wanatoa gazeti halinunuliwi,mauzo haku8na,matangazo hakuna kisha wanakaa chini wanagundua tatizo na kuilipatia ufumbuzi basi.

Nadhani kwanza tuwapongeze HP kwa kubadilika kisha tuwape onyo la kutorudi kule kule walikokuwa mwanzo kwani watasababisha gazeti life.

Mambo ya umiliki na yaliyomo ni vitu 2 tofauti,tujadili yaliyomo badala ya umiliki.

Mnaponda ITV,TBC,Channel ten,Star TV sasa mnataka tutazame tv ipi,acheni Unazi bwana
 
kila nikisoma magazeti ya Rai na Mtanzania naona sasa tofauti, yanaichambua ccm, kuna tetesi kwamba bodi ya habari corparation imekaa na imeamua kuichambua ccm kama Karanga, hata wale magwiji wa makala zinazoichambua ccm kama vile hilal k. Sued amerudishwa tena kuandika makala ktk gazeti la rai na sasa ameambiwa atumie ipasavyo kalamu yake kuichambua ccm na ameicha solemba mwanahalisi ambayo alitimkia.hii inatokana na magazeti hayo hapo mwanzo kuelemea sana ccm jambo ambalo wachambuzi imeona itakuwa pigo kwa wale wanaowania urais na kuungwa mkono na magazeti hayo. sharti kubwa kutomgusa mmiliki wake

Huwa siyanunui magazeti haya mara kwa mara kwa hiyo kusema ukweli siwezi kusema lolote kuhusu mabadiliko unayoyasema. Lakini mimi suala langu kubwa litakuwa ni kwa nini waanze kuichambua CCM (kama unavyodai) sasa wakati siku chache zilizopita walitumia nguvu zao zote kuipigia debe hata kwa kutunga habari za uongo kuhusu wapinzani wa CCM?

Isije ikawa ni ile vita yao ya mafisadi ya ndani kwa ndani ambayo huwa inakuwepo mpaka unapokaribia uchaguzi mkuu. Ikifika uchaguzi wanaungana wote kupambana na yoyote anayetishia uhai wa genge lao kubwa la kifisadi.

Kwa ufupi ndugu yangu usidanganyike hiyo ni vita ya uteuzi wa nafasi mbalimbali za CCM za mwaka 2015 imeanza na tunajua Rai wako upande gani tayari.
 
Msijaribu kutudanganya hapa. New Habari Corporation ambayo inachapisha magazeti ya RAI, Mtanzania, The African na mengineyo inamilikiwa na fisadi nambari wani hapa Tanzania -- Rostam Aziz. Habari zao kila siku ni kuwasakama wapambanaji wa ufisadi kama Samuel Sitta, Harison Mwakyembe, na wengineo na kujaribu kuwakosha mafisadi wakuu wa Tanzania - Rostam, Edward Lowassa, Andrew Chenge, Nazir Karamagi na wengineo.

Kudiriki kununua au kusoma magazeti haya ni sawa na kuunga mkono UFISADI hapa Tanzania.

Magazeti ya kununua ni MwanaHalisi, Mwananchi, RaiaMwema, Dira na Majira. Haya yanajitahidi kuandika habari za kweli. Mengine yaliyobaki ni kuwa aidha wamiliki au wahariri wao wamewekwa sawa na mafisadi, serikali ya JK au hawana ujasiri kupambana nao. Ukweli ndiyo huo.
 
kuna mabadiliko gani? nilisikia kichwa cha habari kwenye tv(maana huwa sinunui) baada ya yale mauaji ya polisi kwa raia arusha kwamba 'mchumba wa dr slaa ajeruhiwa' haya ndo mabadiliko? kama hamuuzi toeni copy chache sie hatudanganyiki
 
Mimi nachukia mmiliki wa haya magazeti kwa sababu ametuibia vya kutosha, ametudhalilisha kiasi cha kutosha hata najikuta kuchukia magazeti yeyewe na waandishi wake. Waandishi wa habari Corp wananuka kama anavyoinuka mmiliki wao!!! Hata waandike nini siwezi kusoma magazeti yao, labda wahame waende vyumba vingine vya habari na waache uozo walioambukizwa na Muejemi wao! Phu...... tuondolee takataka za kuwapamba mafisadi na mali zao!!!!!!!!!!!!!
jee huyu hilal huoni karudi rai na makala zake huzioni?
 
Okay muhogomchungu, sasa tuambie lengo lako la kuleta hii hoja jamvini - je ni kwamba unatushauri tuanze kuyanunua hayo magazeti ? Kama ni hivyo mimi nakuambia bila kumung'unya maneno - siyanunui ng'o ! Unataka kujua sababu ? Haya nitakuambia - wanaoendesha hayo magazeti wananuka ! Bila shaka unajua ni viumbe gani vinapenda kuogelea penye uvundo na uchafu, haya nitakuambia - ni inzi ! Magazeti ya Habari Corporation ? you must be kidding !

Mkuu nakubaliana na wewe anything to do with RA ni cha kuogopwa na kukimbiwa kuliko ukoma. Huyu RA ameona magazeti yake hayapendwi tena kwa kuikandia cdm sasa anajidai kukuna kuna ccm kutuhadaa. Mwambieni AMENOA.
 
Back
Top Bottom