Leo, Jumatatu ya PASAKA, takribani Magazeti yote yamepambwa na vichw vya habari vinavyomnukuu JOSEPHAT GWAJIMA akisema: "SITAWAACHA LOWASSA, SLAA".
Ameyasema hayo wakati wa ibada ya Pasaka, aliyoiongoza akiwa kwenye kile na hoja yake ikiwa ni kiwa anasikia UVUMI kuwa aliitwa kuhojiwa na POLISI kwa sababu aliwakaribisha LOWASSA na SLAA kanisani kwake.
Labda GWAJIMA amechanganyikiwa. Namkumbusha kuwa alitwa kuhojiwa na Polisi kwa sababu alimtukana Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Dar es Salaam, Muhadhama Polycarp Kardinari Pengo.
Jambo la Msingi Kabisa kutokana na hii kauli yake iliyopamba vichwa vya Magazeti ya leo: Ni wazi Kabisa Kauli hii inalenga kumaanisha kuwa hatawaacha LOWASSA na SLAA katika mbio za Urais. Kama ni kweli basi amewaangamiza kisiasa. Gwajima kwa matukio ya hivi karibuni ni Mchafu sana na hawezi kuwasaidia chochote wagombea wake kufikia malengo yao.
RAIS CHAGUO LA WATANZANIA ATATOKA KWA MUNGU NA SIYO KWA WACHUNGAJI WACHAFU KAMA GWAJIMA.