Gwajima na siasa za Ubunge

Gwajima na siasa za Ubunge

Nguruvi3,
Umedadavua vizuri sana Mkuu..ila kwa mimi sioni ushahidi wa moja kwa moja kama Mamlaka zingemzingatia Sheikh yeyote(asiye rasmi) ambaye angetamka kama alivyotamka Bw Gwajima (kwamba angetamani Makanisa kuwa misikiti n.k).

Maana pia haya hutegemea sana mazingira... na kwa bahati mbaya au nzuri mazingira ya imani hizi mbili yanatofautiana kwa namna moja au nyingine...kwa mfano kwenye ukristo kuna utitiri wa "mabanda" mitaani yanayojitambulisha kama nao ni nyumba za ibada, tofauti na ninavyoona kwa Uislam(labda kama sifahamu zaidi)... hivyo basi anachoongea Kiongozi wa banda fulani sidhani kama italinganishwa na atakachoongea Sheikh iwapo ataongelea kwenye nyumba rasmi ya ibada(Msikiti).

Hivi maneno kama hayo yatamkwe na Askofu wa Katoliki, Anglican au Lutheran unadhani Mamlaka zitakaa kimya? na sidhani kama zitaachiwa mamlaka pekee bali ni jamii yote itaguna.

Kwa hiyo nasisitiza kuwa Mzee Said hana sababu ya kulinganisha mambo yasiyowiana kwenye mizani, Gwajima ni Kiongozi wa kikundi chake tu hapo Dar.
 
May Day, kuna hoja ambayo sijui kama wengi wanaielewa! huenda wanaielewa lakini hawataki kukabiliana nayo. Hilo ni tatizo kubwa kwa Watanzania.

Wazungu wanasema 'ukitaka kupata suluhu ya tatizo lazima kwanza ulitambue tatizo''

Hapa kuna sehemu mbili za kuongelea

Mohamed Said anauliza, je ingalitokea maneno hayo kayasema Sheikh, je, magazeti unayosema yangepuuza?
Je, vyombo rasmi unavyosema vingepuuza kama vinavyompuuza Nabii tito?
Je, wangeacha kutoa uzito kwa mambo yasiyo na afya kwa jamii?

Kwahiyo unatakiwa kumjibu Mohamed Said hoja yake kwa mtazamo wa Askofu Gwajima vs Sheikh X

Wakati ukitafakari kumjibu Mohamed, nikukumbushe kuwa kuna kauli kama ''siasa kali, fundamentalist'' , kwamba kauli hizi zinatoka wapi kama tuna uwezo wa kupuuza kila kitu kutoka kwa hawa viongozi wa dini?

Kwa upande wa pili, kuna tatizo kwa Mohamed Said kugoma ku appreciate'' uwepo wa tatizo kwa watu wake

Mathalan, Juzi katiwa ndani Sheikh Ponda . Siku iliyofuata Sheikh Kundecha kakanusha waraka.
Siku iliyofuata shura inakubali waraka huo ni wao.

Katika mazingira haya unawezaje kusema '' waislam wapo kimya' na si kuwa wamepagawa?

Huwezi kuangalia waraka wa Ponda kwa jicho la waraka wa Maaskofu.
Ukifanya hivyo bila kuangalia tatizo la msingi ni kukwepa ukweli.
Kabla ya ulinganifu unatakiwa ujiulize kwanza, je, kuna ulinganifu miongoni mwa watu wako?

Na wala huwezi kuangalia waraka wa Ponda kwa jicho la serikali bila kujiuliza serikali hiyo ipoje madarakani?
Utaratibu wa nchi, serikali inatokana na chama, na chama tawala ni CCM

Nitaendelea nikipata nafasi, nalala niwahi shambani kesho.
Magimbi hapa Magila na Kicheba tumejaaliwa mwaka huu
Hua nakuelewa sana mkuu
 
Hili la matamshi ya Gwajima kuhusu kugeuza Madrasa kuwa Sunday Schools na Makanisa inabidi ulaumu utawala uliopo kwa kutomchukulia hatua na BAKWATA kwa kukaa kimya. Huu utawala unaupendeleo wa wazi ka kikabila, kikanda na kidini.
Upo sawa kabisa
 
Mzee wangu acha kujihisi unyonge kiasi hicho, kauli ya Gwajima kusema kuwa atabadilisha madrasa ziwe Sunday school ni kauli za kipumbavu na kichochezi kwa maana nchii haina dini ila watu wake ndiyo wana dini, kwa mtu mwenye upeo wa kuona mbele anajua hilo haliwezekani daima ndiyo maana hata BAKWATA walikaa kimya maana ndiyo jibu la mjinga.

Kama utakumbuka vizuri pia kuna Sheikh mmoja (Nimemsahau jina) aliwahi kusema kuwa Ikulu ya magogoni ni mali ya waislamu hivyo serikali iwarudishie, naye pia hakuna aliyemjibu kwa maana ni jambo lisilowezekana.

Sasa basi kauli za kipuuzi kama za Gwajima na wengineo wenye akili kama zake ukizipuuza hazina madhara ila ukitaka kuzikuza nawe pia waweza onekana mdini mkorofi anayetafuta chanzo cha kufanya ukorofi wake.
 
IKARAHANSI, Ikara...
Sijapata kuwa mnyonge katika uandishi.

Soma hapa chini vipi baadhi ya watafiti wanavyonitafsiri:

NIMEITOA KUTOKA THESIS:
TANZANIAN CHRISTIANS PERCEPTION OF MUSLIMS IN THE CONTEXT OF NATION'S CHRISTIAN - MUSLIMS RELATIONS BY JONATHAN JOUNG SUN LEE 2019

"Among the authors, I found Mohamed Said extremely useful to this study.

Said acted as a representative of the radical Muslims as a member of the Muslim Writers’ Workshop.

Born in 1952 in Dar es Salaam, he has been able to eye-witness and participate in the development of the radical Muslim movement.

His grandfather Salum Abdallah Popo was the founder of the trade union movement and was among the pioneers to establish opposition to colonial rule.

After independence, Salum Abdallah broke his relationship with Nyerere and was detained by the government for his position that trade unions should be free.

As chairman of the Tanganyika Railways African Union (TRAU), he opposed to the government’s policy to place trade unions under TANU (Said 2018).

Said is actively involved in writing and lecturing in Tanzania as well as overseas.

Several of his books and articles have been published in London and Berlin.

Among them, The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924– 1968): The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika (1989), which was published in London, is the work that puts Muslims at the center of nation building of Tanzania (Masebo 2014:24).

Said’s writings are more informative to this study than other literature in terms of providing the raw voices of radical Muslims over the Christian-Muslim relations as well as the Muslim struggle against the government in the history of Tanzania."

Bwana Ikarahansi kuna dalili kuwa mimi ni mnyonge?
 
Huyu mtu na nabii tito utofaut ni kidogo tu, Gwajima ana miujiza ya mazingaombwe ila nabii tito hana ila matendo wote sawa tu.

Hamna alicho ongea kikatimia kila kitu lazima kiende kombo, 2015 team lowassa, 2020 team magufuri, 2025 team makonda

Samahani waumini wa Gwajima
Kitatimiaje wakati ni utapeli ndugu?
hawa jamaa si lolote zaidi ya utapeli!
 
Kuna Sheikh/Ustadh ameshatangulia mbele ya haki katika kutoa elimu alishawahi kusema kwamba Muislam ukikutana na Mlei (Mkristo) mchinje tu, hii kauli Mohamed Said haujaitolea ufafanuzi kama ni sahihi.
 
Labda hujamwelewa Mzee Mohamed Said , yeye ameshakwambia igeuze hiyo kauli iwe kinyume chake ndio ungejua nani ni nani.
Labda watakuelewa kama watataka ila wanawaza na kujibu kwa hisia ndio maana wameshindwa kumuelewa Sheikh Mohamed bin Said.
Ikiwa tu maandiko ambayo wanaamini wanayafuata hawayajui je haya yanayohitaji fikra zisizo na mhemko itakuwaje?
Tazama mada inavyosema na wanachochangia au kujibu utafahamu "upeo" wa waliosoma wetu!!!
 
Mkuu Mohamed Said ni Ustadh Ilunga.
Savimbi...
Mara myingi hapa jamvini watu hutaka mimi niseme kitu kuhusu kauli ile ya Sheikh Ilunga.

Maneno yale kwa hakika si maneno yake Sheikh Ilunga ila ni aya ya Qur'an kuhusu kisasi.

Inawezekana jinsi alivyoeleza Sheikh Ilunga ndiyo imetia hofu kwa watu wengi.

Hii ilikuwa baada ya kuuliwa Sheikh Rogo.
 
Savimbi...
Mara myingi hapa jamvini watu hutaka mimi niseme kitu kuhusu kauli ile ya Sheikh Ilunga.

Maneno yale kwa hakika si maneno yake Sheikh Ilunga ila ni aya ya Qur'an kuhusu kisasi.

Inawezekanajinsi alivyoeleza Sheikh Ilunga ndiyo imetia hofu kwa watu wengi.

Hii ilikuwa baada ya kuuliwa Sheikh Rogo.
Sasa Mkuu mbona Qur'an imahamisha uvunjifu wa amani kwa kulipiza visasi? Kwenye Mafundisho ya kikristo wanahamasisha sana amani.

38 "Mmesikia kwamba ilisemwa: `Jicho kwa jicho, jino kwa jino.`

39 Lakini mimi nawaambieni, usimlipize kisasi mtu mbaya. Mtu akikupiga kofi shavu la kulia, mgeuzie pia shavu la pili.

40 Mtu akikupeleka mahakamani kutaka kukuchukulia shati lako, mwache achukue pia koti lako.

41 Mtu akikulazimisha kubeba mzigo wake kilomita moja, ubebe kilomita mbili.

42 Akuombaye mpe, na mtu akitaka kukukopa kitu usimnyime.

43 "Mmesikia kwamba ilisemwa: `Mpende jirani yako na kumchukia adui yako.`

44 Lakini mimi nawaambieni, wapendeni adui zenu na kuwaombea wale wanaowadhulumu ninyi

Ukipata Muda Pitia Clip Hii ya Mwanakijiji amefafanua jinsi Sheikh alivyoptosha Qur'an inavyosema.

 
  • Thanks
Reactions: Pep
Sasa Mkuu mbona Qur'an imahamisha uvunjifu wa amani kwa kulipiza visasi? Kwenye Mafundisho ya kikristo wanahamasisha sana amani.

38 "Mmesikia kwamba ilisemwa: `Jicho kwa jicho, jino kwa jino.`

39 Lakini mimi nawaambieni, usimlipize kisasi mtu mbaya. Mtu akikupiga kofi shavu la kulia, mgeuzie pia shavu la pili.

40 Mtu akikupeleka mahakamani kutaka kukuchukulia shati lako, mwache achukue pia koti lako.

41 Mtu akikulazimisha kubeba mzigo wake kilomita moja, ubebe kilomita mbili.

42 Akuombaye mpe, na mtu akitaka kukukopa kitu usimnyime.

43 "Mmesikia kwamba ilisemwa: `Mpende jirani yako na kumchukia adui yako.`

44 Lakini mimi nawaambieni, wapendeni adui zenu na kuwaombea wale wanaowadhulumu ninyi

Ukipata Muda Pitia Clip Hii ya Mwanakijiji amefafanua jinsi Sheikh alivyoptosha Qur'an inavyosema.

Savimbi,
Kama Sheikh Ilunga angeendelea mbele angesoma Allah anaeleza ubora wa kusamehe.

Hii kisasi Allah kaileta kuwazuia watu kutotendeana uovu kwa watu kuogopa kuwa endapo mtu ataua basi na yeye atauawa.
 
IKARAHANSI, Ikara...
Sijapata kuwa mnyonge katika uandishi.

Soma hapa chini vipi baadhi ya watafiti wanavyonitafsiri:

NIMEITOA KUTOKA THESIS:
TANZANIAN CHRISTIANS PERCEPTION OF MUSLIMS IN THE CONTEXT OF NATION'S CHRISTIAN - MUSLIMS RELATIONS BY JONATHAN JOUNG SUN LEE 2019

"Among the authors, I found Mohamed Said extremely useful to this study.

Said acted as a representative of the radical Muslims as a member of the Muslim Writers’ Workshop.

Born in 1952 in Dar es Salaam, he has been able to eye-witness and participate in the development of the radical Muslim movement.

His grandfather Salum Abdallah Popo was the founder of the trade union movement and was among the pioneers to establish opposition to colonial rule.

After independence, Salum Abdallah broke his relationship with Nyerere and was detained by the government for his position that trade unions should be free.

As chairman of the Tanganyika Railways African Union (TRAU), he opposed to the government’s policy to place trade unions under TANU (Said 2018).

Said is actively involved in writing and lecturing in Tanzania as well as overseas.

Several of his books and articles have been published in London and Berlin.

Among them, The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924– 1968): The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika (1989), which was published in London, is the work that puts Muslims at the center of nation building of Tanzania (Masebo 2014:24).

Said’s writings are more informative to this study than other literature in terms of providing the raw voices of radical Muslims over the Christian-Muslim relations as well as the Muslim struggle against the government in the history of Tanzania."

Bwana Ikarahansi kuna dalili kuwa mimi ni mnyonge?

Nafuta kauli yangu kuwa wewe siyo mnyonge.

Lakini bado naamini kuwa nchi yetu Tanzania haina dini, bali wananchi wake ndiyo wenye dini. Mara kwa mara kumekuwa kukitokea changamoto zinazohusisha dini (dhehebu kwa dhehebu au dini moja dhidi ya nyingine) binafsi yangu toka moyoni sipendi dini yangu iwe kubwa kuzidi maslahi ya taifa langu hivyo mtu yoyote anayetokea kuanza kukashifu dini ya mwenzake (hata kama mtu huyo ninashiriki naye nyumba moja ya ibada) huwa ninamuangalia kwa jicho la tofauti.

Kwangu mimi naichukulia dini kama njia ya kiroho kutupeleka peponi lakini pia ndani yake imebeba mila na tamaduni za waliotuletea dini hizo mfano majina, mavazi, vyakula, ustaarabu nk. Kulitokea makosa fulani kwa watangulizi wetu (mababu) kukubali kila walichoambiwa na hao waleta dini. Walishikwa akili na kuaminishwa kuwa kila tulichonacho ni kibaya ila vyao ndiyo vizuri matokeo yake tukaacha majina yetu mazuri ya kiafrika, tukaacha na utamaduni wetu mzuri nk.

Leo hii wakitaka kutufitinisha mara nyingi hupenda kutumia misaada pamoja na dini. Binafsi namshukuru MUNGU kwa hili maana kwa Tanzania hawajafanikiwa (ninaomba wasifanikiwe), hivyo nakuomba uwe mshirika wangu kwa kupinga udini Tanzania kwa kuwakemea wanaoendekeza udini na siyo kuwapigia chapuo.
 
  • Thanks
Reactions: Pep
😆😆😆 aliyemteka Dr Ulimboka alikamatwa kwenye kanisa la Gwajima ! nani aliamini ule ujinga ?
 
Back
Top Bottom