Gwajima na siasa za Ubunge

Gwajima na siasa za Ubunge

Nafuta kauli yangu kuwa wewe siyo mnyonge.

Lakini bado naamini kuwa nchi yetu Tanzania haina dini, bali wananchi wake ndiyo wenye dini. Mara kwa mara kumekuwa kukitokea changamoto zinazohusisha dini (dhehebu kwa dhehebu au dini moja dhidi ya nyingine) binafsi yangu toka moyoni sipendi dini yangu iwe kubwa kuzidi maslahi ya taifa langu hivyo mtu yoyote anayetokea kuanza kukashifu dini ya mwenzake (hata kama mtu huyo ninashiriki naye nyumba moja ya ibada) huwa ninamuangalia kwa jicho la tofauti.

Kwangu mimi naichukulia dini kama njia ya kiroho kutupeleka peponi lakini pia ndani yake imebeba mila na tamaduni za waliotuletea dini hizo mfano majina, mavazi, vyakula, ustaarabu nk. Kulitokea makosa fulani kwa watangulizi wetu (mababu) kukubali kila walichoambiwa na hao waleta dini. Walishikwa akili na kuaminishwa kuwa kila tulichonacho ni kibaya ila vyao ndiyo vizuri matokeo yake tukaacha majina yetu mazuri ya kiafrika, tukaacha na utamaduni wetu mzuri nk.

Leo hii wakitaka kutufitinisha mara nyingi hupenda kutumia misaada pamoja na dini. Binafsi namshukuru MUNGU kwa hili maana kwa Tanzania hawajafanikiwa (ninaomba wasifanikiwe), hivyo nakuomba uwe mshirika wangu kwa kupinga udini Tanzania kwa kuwakemea wanaoendekeza udini na siyo kuwapigia chapuo.
Ikarahani,
Ili Tanzania iwe na serikali ambayo haina dini lazima wafuasi wa dini mbili hizi wawe na uwiano sawa au karibu na sawa katika uendeshaji wa serikali.

Hili halipo Tanzania ratio kama Waraka wa Taasisi na Jumuiya za Kiislam zinavyoonyesha ni 20:80.

Hili Waislam wamekuwa wakiitahadharisha serikali kwa miaka mingi.

Hawa wanaohodhi madaraka kwenye maamuzi ya serikali watafanya maamuzi yenye maslahi na imani zao.

Mifano ipo mingi.
 
Chochote atakachokiunga mkono gwajma lazima kifeli vibaya sana. Subirin ccm mwaka huu itakavyoanguka
 
Ameuliza tamko hilo lingetolewa na Muislam kuzigeuza Sunday Schools zote nchini kua Madrasa ingekuaje?

Hili nadhani ni kinyume chake....

Wakristo wala hatuna visa wala visasi...

Hata kama waislamu wataamua kununua Biblia zote madukani, wakazipiga moto au kuzichana hadharani na kukojolea mikojo, nakuhakikishia hakuna hata mkristo mmoja angenyoosha mkono wake kupambana na yeyote kwa sababu watakuwa hawajui watendalo....!!

Kwanini?

Kwa sababu Neno la Mungu na Mungu mwenyewe muumba haishi/hakai kwenye makaratasi bali anakaa kwenye moyo wa mtu mwenyewe...!

Kwa wenzetu wale, aah balaa....

Hata hili limeletwa na mwandishi huyu ili pengine ajaribu kuamusha hisia zao na pengine waanzishe JIHAD ya kuipigania dini yao kwa nguvu za mwili dhidi ya Mch. Gwajima (mkristo) na wafuasi wake...

Hii siyo sahihi. Hili siyo jema hata kidogo...
 
Ikarahani,
Ili Tanzania iwe na serikali ambayo haina dini lazima wafuasi wa dini mbili hizi wawe na uwiano sawa au karibu na sawa katika uendeshaji wa serikali.

Hili halipo Tanzania ratio kama Waraka wa Taasisi na Jumuiya za Kiislam zinavyoonyesha ni 20:80.

Hili Waislam wamekuwa wakiitahadharisha serikali kwa miaka mingi.

Hawa wanaohodhi madaraka kwenye maamuzi ya serikali watafanya maamuzi yenye maslahi na imani zao.

Mifano ipo mingi.

Siwezi kukupinga wala kukuunga mkono kwa maana sina utafiti nilioufanya, lakini kwa nionavyo mimi baadhi yetu tunahisi kubaguliwa na hii hupelekea kuanza kujitenga na kujibagua wenyewe (hili halipo kwenye dini tu). Tangu nimepata kujitambua sijawahi kuhisi wala kusikia kuwa serikalini watu huchaguliwa/huteuliwa kwa kufuata dini, nijuavyo mimi kuna sifa mtambuka zaidi ya dini na kabila.

Kuna baadhi ya maeneo watu wa dini fulani ni wengi kuliko wa dini nyingine na hii imetokana na mapokeo (wewe unajua), pia kuna usomi wa elimu dunia. Sijawahi kusikia kwamba mtu wa taaluma fulani mwenye sifa za kitaaluma amekataliwa kuajiriwa serikalini kwa sababu ya dini yake.

Huo uwiano unaosema ni 20: 80 sidhani kuwa Serikali imekaa kimya bali kuna maelezo huwa yanatolewa sasa yawezekana baadhi yetu hatukubalinai nayo. nakumbuka enzi za Rais Mwinyi alituhimiza kusomesha watoto baada ya kuulizwa swali lililoonyesha kuna upendeleo kwa dini fulani kiserikali.
 
  • Thanks
Reactions: Pep
Siwezi kukupinga wala kukuunga mkono kwa maana sina utafiti nilioufanya, lakini kwa nionavyo mimi baadhi yetu tunahisi kubaguliwa na hii hupelekea kuanza kujitenga na kujibagua wenyewe (hili halipo kwenye dini tu). Tangu nimepata kujitambua sijawahi kuhisi wala kusikia kuwa serikalini watu huchaguliwa/huteuliwa kwa kufuata dini, nijuavyo mimi kuna sifa mtambuka zaidi ya dini na kabila.

Kuna baadhi ya maeneo watu wa dini fulani ni wengi kuliko wa dini nyingine na hii imetokana na mapokeo (wewe unajua), pia kuna usomi wa elimu dunia. Sijawahi kusikia kwamba mtu wa taaluma fulani mwenye sifa za kitaaluma amekataliwa kuajiriwa serikalini kwa sababu ya dini yake.

Huo uwiano unaosema ni 20: 80 sidhani kuwa Serikali imekaa kimya bali kuna maelezo huwa yanatolewa sasa yawezekana baadhi yetu hatukubalinai nayo. nakumbuka enzi za Rais Mwinyi alituhimiza kusomesha watoto baada ya kuulizwa swali lililoonyesha kuna upendeleo kwa dini fulani kiserikali.
Ikarahasi...
Hii mada huna ujuzi nayo.
 
Kinyungu,
Kweli hebu fikiri sheikh angesema nataka nigeuze Sunday schools zote ziwe madrasa ingekuwaje.

Ndugu yangu kakupa ushauri mzuri.
Fanya hivyo na rejea hapa utupe fikra zako.
Hiyo ni kama Siasa.. CCM wangetamani wanachama wa Chadema wajiunge nao..Hali kadhalika Chadema wangependa CCM members wote wajiunge na chama Chao na hiyo sio dhambi kama Una uwezo wa kushawishi..kama sheikh anawashawishi waumini wa Sunday schools wajiunge na madrasa Kwa wingi ni Jambo la linalofanyika kila siku ila Kwa uchache Sana(watu wanabadili dini kila kukicha).
 
Baadhi ya Watanzania ni wapumbavu wa kutupa. Unashangaa mtu anawapaje kauli mbili tofauti zinazopingana na zote wanazishangilia bila kujiuliza kulikoni?

Mohamed Said, Yaani nikiangalia clip alipokuwa akiponda ubunge kwa dharau zote waumini wanashangilia kwa mbwbwe zote na miluzi halafu clip ya juzi akitangaza kutia nia na kupamba uamuzi wake wa kigeugeu bado waumini wanashangilia pia kwa miluzi, nimeona aibu sana kwa niaba ya waumini hao.

Yani kiongozi wa dini anaweza kuchezea akili za watu apendavyo kwa kigezo cha imani tu jamani!!!!. Imani ya hivi ni kuuza utu na ufahamu wako ambao ni zawadi binafsi kutoka kwa Mungu!!!!

Kama dhana ya dhambi ni halisi, tendo hili ni dhambi pia!!!!
 
Huyu mtu na nabii tito utofaut ni kidogo tu, Gwajima ana miujiza ya mazingaombwe ila nabii tito hana ila matendo wote sawa tu.

Hamna alicho ongea kikatimia kila kitu lazima kiende kombo, 2015 team lowassa, 2020 team magufuri, 2025 team makonda

Samahani waumini wa Gwajima
Samahani ya nini Sasa na wewe? UMENENA. Over
 
Hivi huyo Bw Gwaji ana wafuasi wangapi?, kwa nini unataka ionekane kana kwamba anayofanya au kusema huyo Bwana anawakilisha jamii nzima ya Ukristu?.

Hivi ni mangapi tunakutana nayo mitaani na tunayapuuza...kuna wakati unapita unakuta Mtu kakusanya Watu anaongea mambo yake tena kavaa kanzu na baragashia lakini Mtu unapita na zako unaachana nao...tukianza kushabikia kila kitu kinachofanywa na kila Mtu sidhani kama tutapata muda wa kufanya mambo mengine ya muhimu.

Kama hayo Magazeti yamempuuza kwa nini na wewe unashindwa kumpuuza?, ni wapi umeona Nabii Tito akipewa kipaumbele kwenye vyombo rasmi vya habari zaidi ya mitandaoni?...Kwa nini wewe unatamani wawe wanatoa uzito kwa mambo yasiyo na afya kwa jamii kama hayo?.

Mkuu May Day, tofauti ya Gwajima na hao wengine ni kuwa yeye anatamani kuwa mbunge ambacho ni cheo chenye dhamana na ushawishi mkubwa kwenye jamii yetu.

Kama angesemea hayo maneno kanisani kwake na asitie nia ya kuutaka ubunge nadhani ingekuwa rahisi kumpuuza na hata hizo kanda zake zisingepata umaarufu.

Alafu mkuu niongezee tu kukumbusha kuwa hata Adolf Hitler alianza kama “rable rouser” wa jinsi hii.

Matamko ya kibaguzi kama haya, kutoka kwa mtu mwenye ushawishi fulani ndani ya jamii, hata kama wafuasi wake si wengi yanaweza leta athari mbaya sana na yanapaswa kukemewa kwa nguvu zote.

Naungana na mkuu Mohamed Said kuwa jamii inapaswa kuwa na masikio mazuri!
 
Wajumbe wameshafanya yao! Lets move on.
Sasa hao ndio Watu wanaopaswa kupuuzwa na Wajumbe, wasiangalie rushwa tu za kuneemesha matumbo yao wakatuwekea Mtu asiye na faida kwenye Jamii kubwa...huyo anapaswa kubaki huko kwenye kundi lake.
 
“Ukimya una sauti. Ukiwa na masikio mazuri utasikia sauti ya ukimya”

Kuna swali wanabailojia huwa wanauliza.

Je, mti ukianguka porini na hapakuwepo mtu wa kuusikia, ulitoa sauti?

Swali hili linaulizwa kuweka msisitizo kuwa kinachosikia na kutafsiri sauti ni ubongo na sio masikio ambayo kazi yake ni kupokea mawimbi ya sauti, kuyageuza kuwa mtikisiko, kuyakuza, na kuyafanya kuwa mtiririko wa kiumeme ambao husafirishwa hadi kwenye ubongo na ndipo mawimbi hayo hutafsiriwa kuwa sauti.

Somo hapa ni kuwa jamii( pamoja na mamlaka zake) ijifunze kusikiliza kwa akili zaidi na mamlaka zisichague kusikiliza baadhi ya sauti na kuzikemea/kuzidhibiti wakati zikiachia nyingine kusikika na kuleta tafrani.
 
Inamaana umeshasahau hii kesi? Au ulikuwa hujazaliwa?
 
May Day, kuna hoja ambayo sijui kama wengi wanaielewa! huenda wanaielewa lakini hawataki kukabiliana nayo. Hilo ni tatizo kubwa kwa Watanzania.

Wazungu wanasema 'ukitaka kupata suluhu ya tatizo lazima kwanza ulitambue tatizo''

Hapa kuna sehemu mbili za kuongelea

Mohamed Said anauliza, je ingalitokea maneno hayo kayasema Sheikh, je, magazeti unayosema yangepuuza?
Je, vyombo rasmi unavyosema vingepuuza kama vinavyompuuza Nabii tito?
Je, wangeacha kutoa uzito kwa mambo yasiyo na afya kwa jamii?

Kwahiyo unatakiwa kumjibu Mohamed Said hoja yake kwa mtazamo wa Askofu Gwajima vs Sheikh X

Wakati ukitafakari kumjibu Mohamed, nikukumbushe kuwa kuna kauli kama ''siasa kali, fundamentalist'' , kwamba kauli hizi zinatoka wapi kama tuna uwezo wa kupuuza kila kitu kutoka kwa hawa viongozi wa dini?

Kwa upande wa pili, kuna tatizo kwa Mohamed Said kugoma ku appreciate'' uwepo wa tatizo kwa watu wake

Mathalan, Juzi katiwa ndani Sheikh Ponda . Siku iliyofuata Sheikh Kundecha kakanusha waraka.
Siku iliyofuata shura inakubali waraka huo ni wao.

Katika mazingira haya unawezaje kusema '' waislam wapo kimya' na si kuwa wamepagawa?

Huwezi kuangalia waraka wa Ponda kwa jicho la waraka wa Maaskofu.
Ukifanya hivyo bila kuangalia tatizo la msingi ni kukwepa ukweli.
Kabla ya ulinganifu unatakiwa ujiulize kwanza, je, kuna ulinganifu miongoni mwa watu wako?

Na wala huwezi kuangalia waraka wa Ponda kwa jicho la serikali bila kujiuliza serikali hiyo ipoje madarakani?
Utaratibu wa nchi, serikali inatokana na chama, na chama tawala ni CCM

Nitaendelea nikipata nafasi, nalala niwahi shambani kesho.
Magimbi hapa Magila na Kicheba tumejaaliwa mwaka huu
Kukosekana ulinganifu baina ya watu wa mzee Saidi hakutoi uhalali kwa watu wengine kutoa matamko yenye kuleta hisia hasi kwa watu hao.

Nikukumbushe kuwa Maaskofu wakatoliki waliwahi kutoa waraka wa Kwaresma na Kadinali Pengo akaupinga.

Katika hili ni ipi tofauti ya Sheikh Kundecha na Kadinali Pengo?

Mzee Mohamedi Saidi akitafuta ulinganifu atakuwa anakosea?
 
Gwajima hafai na hajawahi kufaa... huyu anakula mpka kondoo huku akiwachukua na video ...
 
Mimi Ni mkristo,naunga mkono hoja yako.
Pia ongeza Kama maneno hayo yangesemwa na mchungaji mwenye uelekeo wa CHADEMA ama mchungaji mwanachachadema Kama Msigwa hivi,au Shehe ponda pangechimbika.
 
Back
Top Bottom