kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,255
- 16,185
Gwajima, Mpina na Polepole wote wanazo sifa zinazorandana. Wote ni wasukuma/wanyamwezi, ni waskristo na walipewa vyeo vikubwa na JPM (msukuma).
Wanachosahau ni kitu kimoja kuwa ndani ya CCM na serikali wapo wasukuma na waskristo wengine wengi sana bado. Hivyo, kama ukimkata Mpina kugombea kisesa yuko msukuma mwingine atagombea kisesa. Kama kanisa la Gwajima limefungiwa Yako makanisa mengine Yako wazi hayajafungiwa.
Akili za Gwajima ni kwamba kinachompata yeye kinawahusu wasukuma wote, waskristo wote na wanaCCM wote. Hivyo woote hawa watamuunga mkono yeye kwenye ugomvi wake na Samia.
Akili za kipuuzi kama hizí alikuwa nazo Gashagwa (mkikiyu) aliyekuwa naibu Rais wa Kenya aliyeondolewa kwa upuuzi wake wa kikabila. Rais Ruto alimteua mkikiyu mwingine kuchukua nafasi ya Gashagwa. Hivyo wakikuyu wachache tu wakamuunga mkono Gashagwa na wengi wakamuunga mkono naibu Rais mpya ambae ni mtoto wao pia.
Gwajima anahesabu idadi ya wasukama na idadi ya waskristo nchini na kudhani kuwa wooote wataungana nae kwenye ujinga wake na kusahau kuwa wapo wasukuma na waskristo wengine kama Biteko, Kasheku Msukuma na wengine wengi bado wanagombea na wako serikalini na ndani ya CCM. Eti Leo hii kanisa la katoliki na kanisa lake la uzima na ufufuo ni kitu kilekile tu. Anasahau kuwa watu wanakumbuka namna alivyomshambulia Kadinali Pengo.
Wanatapatapa, amekata punzi.
Wanachosahau ni kitu kimoja kuwa ndani ya CCM na serikali wapo wasukuma na waskristo wengine wengi sana bado. Hivyo, kama ukimkata Mpina kugombea kisesa yuko msukuma mwingine atagombea kisesa. Kama kanisa la Gwajima limefungiwa Yako makanisa mengine Yako wazi hayajafungiwa.
Akili za Gwajima ni kwamba kinachompata yeye kinawahusu wasukuma wote, waskristo wote na wanaCCM wote. Hivyo woote hawa watamuunga mkono yeye kwenye ugomvi wake na Samia.
Akili za kipuuzi kama hizí alikuwa nazo Gashagwa (mkikiyu) aliyekuwa naibu Rais wa Kenya aliyeondolewa kwa upuuzi wake wa kikabila. Rais Ruto alimteua mkikiyu mwingine kuchukua nafasi ya Gashagwa. Hivyo wakikuyu wachache tu wakamuunga mkono Gashagwa na wengi wakamuunga mkono naibu Rais mpya ambae ni mtoto wao pia.
Gwajima anahesabu idadi ya wasukama na idadi ya waskristo nchini na kudhani kuwa wooote wataungana nae kwenye ujinga wake na kusahau kuwa wapo wasukuma na waskristo wengine kama Biteko, Kasheku Msukuma na wengine wengi bado wanagombea na wako serikalini na ndani ya CCM. Eti Leo hii kanisa la katoliki na kanisa lake la uzima na ufufuo ni kitu kilekile tu. Anasahau kuwa watu wanakumbuka namna alivyomshambulia Kadinali Pengo.
Wanatapatapa, amekata punzi.