- Thread starter
- #21
Mtoa mada umeuliza swali zuri japo mifano yako haihusiani na jambo ulilouliza. Katika mifano yako umetaja mboni ya jicho na kutoa mate ambazo ni reflex actions. Reflex actions nyingine ni kama kupiga chafya na kujikuna unapowashwa. Hayo ni matendo ambayo mwanadamu anayafanya bila kufikiria. Na yanaongozwa na central nervous system. Sidhani kama kuna kiumbe yoyote anayeweza kufikiria kuwa sasa nipige chafya. Ila inatokea pale mfumo wa hewa unapojisafisha. Kwa maelezo hayo basi tukirudi kwenye swali lako ni kwamba matukio kama kufukuzwa kazi au tukio lolote la kuitikia kichokoo linaongozwa na ubongo. Hivyo ni kweli kabisa kama utakuwa na uelewa wa kutokukurupuka katika kufanya maamuzi basi itakuwa rahisi kwako kuweza kufanya maamuzi ya busara bila kujidhuru wala kuathiri afya yako. Binadamu tumepewa akili na utashi. Na huo ndio hutuongoza katika mambo yote yanayotumia akili. Kikubwa katika yote ni kujua jinsi ya kukontrol mapigo ya moyo wako. Hili ni somo jingine. Namalizia kwa kusema Fikiri kabla ya kutenda.
Nilipotoa mifano ya reflex action nilikuwa nina maana yangu. Maana yangu nikuwa God/nature is correct to create us with those reflex action because they are there to help us. Sasa kama hayo ni sahihi, iweje tujaribu kukinzana na ku-PANIC?