Unapomwambia mtu calm down,easy,chukulia poa n.k unamtoa mtu kwenye hatari ya kuudhuru mwili wake,binadamu anapokuwa kwenye state ya uchungu kwa muda mrefu organs za mwili wake zinadhurika,mf.Moyo,Figo,Maini n.k.kwani unapokuwa kwenye hizo hali vitu hivyo hufanya kazi ya ziada,na hiyo kazi ya ziada inapodumu muda mrefu vinaanza kuumia,ni taratibu lakini hatimaye utaishia kuumwa na hatimaye kufa.Kwa sisi wakristo kwenye Biblia Mithali 4:23 inasema,Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo,maana ndiko zitokako chemichemi za uzima.Kwahiyo pamoja na kwamba tunakutana na mambo yanayoumiza hatutakiwi kuyaacha yaendelee kutuumiza kwakuwa mwili umeumbwa ili upambane navyo,kinachotakiwa hizo hali zikishatokea tufarijiane na sisi wenyewe tujitahidi tuwezavyo kujisahaulisha ili maisha yaendelee...
Sent using
Jamii Forums mobile app