GPS navigation katika gari za bongo

GPS navigation katika gari za bongo

hii kitu mm nilikuwa nawaza sana nasikuipatia jibu coz sio mtaalam wa computer au wa program lakini mm ni FUNDI UMEME WA magari hii kitu nishakutana nayo sana na huwa natamani sana kuifaham ili nipige Hera coz wabongo wengi wakinunua Gari wanaitamani sana lakini huwa tunaishia kuwajibu ni kwamatumizi ya China na japani.

lakini huwa na sutwa na nafsi KWA kuwa kuna wale ambao huwa wanalalamika juu ya kubadili lugha aisee kwenye redio za paso zenye navigation huwa nawapiga pesa coz kuna CD ninayo unaiweka kwenye redio kama inasoma kichina ina load na kubadili lugha inafanyia setting.

ila hapa kwenye navigation najua inawezekana sema wataalam wetu au wanaojua mambo hawajaweza kufuatilia na ninamaswali mengi sana kama mwongozo ambayo nahisi yanaweza kuwa msingi wa kutafuta solutions la hili lkn huwa sipati wa kumuuliza na hata mafundi ninao waamini nao huwa hawana cha kunijibu.

KWA kuwa hizi navigation kwa wenzetu huwa zinafanyiwa update KWA kuinsert CD ya Raman husika.

ninachokijua mm ni kuwa kwenye zile navigation wame install ramani za nchi /bara husika je haiwezekani ku unstall hizo ramani zao na kuinstall ramani za bongo?? Tanzania??

au kama inawezekana application kama mnayoisema ya kwenye simu haiwezekani ikapatikanika ukaiweka kama kwenye CD hivi na kuinstall kwenye gari!?? maana kuna mahali naona mmesema unaweza ukaidownload na kuitumia kwenye phone hata ukiwa haupo hewani.

Chifu mkwawa hembu naomba unijibu maswali hayo machache kama kuna uwezekana wa kuinstal hiyo application kwenye CD?? natamani sana siku nionane na ww maana na mengi sana yananitatiza tatizo nikianzishaga Uzi hapa wachangiaji huwa wanakuwa hawapo.sijui kwa kuwa hakuna jukwaa LA mafundi magari
 
Last edited by a moderator:
inaitwa here maps.

nenda store ya simu yako search neno HERE MAPS halafu idownload, here maps si kama app nyengine katika kila magari 5 yenye ramani manne yanatumia hizi ramani.
Route-and-Drive-S5.jpg


ili upate experience nzuri
-eka view iwe 45 degree angle
-download ramani ya Tanzania ili baadae uweze tumia offline, na kama siku unapata safari ya nje ya nchi download nchi unayoenda
-eka turn by turn navigation ili iwe inakueleza kwa sauti kuepuka kila mara kuangalia ramani
-ipo hadi lugha ya kiswahili kwenye turn by turn navigation

kuhusu mounting nimecheki kaymu zipo as cheap as shilingi 15,000
car mount | Kaymu

Nimepata here maps naomba hio ramani ya Tanzania inaitwaje
 
LEGE kama nilivyosema hapo juu kila magari 5 yenye ramani basi manne yanatumia ramani hizi za here maps, website yao hii hapa kama unaweza pata mambo mawili matatu.
Home - HERE 360

hivyo inamaana kuna asilimia 80% hizo ramani unazoziona ni here maps, ambazo unaweza ukazidownload. cha muhimu jaribu mambo haya

1.angalia kama hio navigation ina network kama wifi halafu connect then jaribu ku update location kama utaweza pata map data za location mpya
2. jaribu kueka map data manual kwa kuhamisha za simu, sababu here maps ipo kwenye simu na unaweza kudownload hizo ramani jaribu kuzichukua za kwenye simu na kuzi update manual

kama step ya pili itakataa itabidi wewe sasa utuambie extension ya hizo ramani za kwenye gari, mfano map-data.xxx then sisi tutatafuta namna ya kuconvert ramani zetu kwenda hio format yako.

pia kuna baadhi ya makampuni ya ramani wanauza hizo map data hivyo huwenda ukahitajika kulipa kiasi fulani cha fedha.
 
Last edited by a moderator:
Thanks mkuu...na hio ya kuweka 45 angle nawekea wapi

kwangu kuna mshale/vimshale chini kushoto nikitap ina inabadili baina ya aerial view na 45 degree view. sema mimi natumia windows phone sina uhakika kama android ni sawa.

pia kuna feature nyengine nimesahau kuisema ya here maps, ambayo ni find my car, incase umepaki gari sehemu yenye watu wengi na umesahau umepaki wapi gari hii ramani inaweza kukuonyesha na ikakupeleka hadi mahali gari lilipo. ila pia sina uhakika kama ipo kwenye android
 
Hoya mzee mi nishashida na hiyo language setting mi ninayo toyota passo yaani full chinise nashindwa hata kusach chanell radio moja ndio yashika halafu mi mwenyewe ni fundi wire but sio kivile, iyo navigation nashida nayo kama kiroho mbaya yaani inabidi tupekue pekue ili tupate ufumbuzi ila nijuze juu ya kuchange lugha.
 
we unataka ikwambie hapa manzese.kimara,tegeta. raman ya tz haitambuliki dunian

Tukisema tumataka mabadiliko hawatuelewi!ni aibu kwa dunia ya leo watu tunaishi kama swala!

Kuna gari nilikuwa naitumia Joberg,huitaji kuumia kichwa kujua unapokwenda.

Unaandika au unaongea unataka kwenda wapi then inakupa shortest root unayoweza kupita na pia inakupa taarifa za msongamano nk
 
Hoya mzee mi nishashida na hiyo language setting mi ninayo toyota passo yaani full chinise nashindwa hata kusach chanell radio moja ndio yashika halafu mi mwenyewe ni fundi wire but sio kivile, iyo navigation nashida nayo kama kiroho mbaya yaani inabidi tupekue pekue ili tupate ufumbuzi ila nijuze juu ya kuchange lugha.

sasa hivi translator zote kubwa yaani google translator na microsoft translator zinaweza kutafsiri lugha kupitia camera. ingia playstore halafu search google translator then tafsiri hadi ufike sehemu ya kubadili lugha (kama ipo).

0d34874c-9c2c-11e4-_837104c.jpg
 
Mkuu Chief Mkwawa hizo dish za azam na continental zenyewe zinahusikaje kwenye Gps msaada wako tafadhali
 
Hoya mzee mi nishashida na hiyo language setting mi ninayo toyota passo yaani full chinise nashindwa hata kusach chanell radio moja ndio yashika halafu mi mwenyewe ni fundi wire but sio kivile, iyo navigation nashida nayo kama kiroho mbaya yaani inabidi tupekue pekue ili tupate ufumbuzi ila nijuze juu ya kuchange lugha.

mkuu upo wapi wewe?? mm nipo dar 0717228064 .tusaidiane
 
Acheni upumbavu wene navigation hahitaji internet na wala haihusiani ingia kwenye menu ila kwa tz hakuna sistym hiyo huwezi itumia
 
Mkuu Chief Mkwawa hizo dish za azam na continental zenyewe zinahusikaje kwenye Gps msaada wako tafadhali

havina mahusiano ila naprove tu point kama hatuwezi kutumia gps basi tusingeweza kuwa na madish kama azam pia sababu vyote vinategemea satelite.
 
Sijajua sababu ya huyu mmiliki wa paso.. uko Manzese unaendesha gari yako halafu kwenye device yako hapo kwenye dashboard inakuonesha uko Manzese. so what??? Sijajua maana ya hii kitu.
 
Sijajua sababu ya huyu mmiliki wa paso.. uko Manzese unaendesha gari yako halafu kwenye device yako hapo kwenye dashboard inakuonesha uko Manzese. so what??? Sijajua maana ya hii kitu.

mtu ananunua gari ili limtembeze kama hutoki manzese ulitakiwa usinunue gari kabisa sababu kazi ya gari ni kutembea, ila kama utatoka utaenda maeneo usiyoyafahamu na hapo ndio utaona faida ya ramani.
 
Kma huoni umuhimu wa gps we kaa pembeni, hata wabunge wakiwa hawana hoja hulala bungeni.
 
Back
Top Bottom