Mimi binafsi huwa ninazikubali Xiaomi, Samsung, Motorola, Oppo, Realme, Huawei, Vivo na Google Pixel ila iPhone nazo ni nzuri sana na nilianza kuzipenda hizi simu bila kufuata mkumbo ila limitations za ajabuajabu ndio zilifanya upendo upungue kidogo kwa iPhone
- iPhone kwenye design yupo vizuri hasa kwenye hii ya flat bar (2.5D), macho matatu na haya mawili ya kulala kama ya iPhone 14 plain. Ila tu sasahivi ananikera, sijui ameishiwa design maana tangu 2019 hadi leo ni macho matatu yaleyale
- Kwenye iPhone camera zake ni kweli zina saturation kubwa lakini mimi naona hii level ya saturation ni nzuri sana kwa kupiga hata picha za mazingira. Sio tu kwa watu hadi wadada wengi wakazipenda, bali hata kwa picha za environment, wanyama, majengo na kila kitu huwa zinaappear vizuri sana.
- Display ya iPhone 14 Pro Max inafikia brightness hadi 2000nits. Hili suala ni amazing.
- iPhone zinatoa video nzuri sana na feature yake kali ya Cinematic Mode
- iOS nayo haina mpinzani. Hata shapes za icons tu zinavutia. Security ni kubwa kwa sababu inalimit vitu vingi sana, japo hili suala siliafiki. Hii software haina mpinzani aisee.
- iPhone 14 Pro Max inaweza kukaa chini ya kina cha maji cha 6m kwa dakika 30. Mkuu mita 6 ni nyingi sana
- Pia kwa flagship, iPhone kwa sasa zinafunika flagship nyingi sana kwenye suala la ukaaji wa charge
- Messaging na Calling apps za iPhone ni nzuri sana kuliko hizi za Google
- Ingawa Google Assistant ndio best, ila Siri nayo inakosha aisee
- Software ya iOS inakuwa supported hadi 6 to 8 years
- Chipset zao za Bionic nazo ni powerful sana, ingawa RAM analimit kwenye 6GB ila perfomance ni kubwa kuliko baadhi ya simu zenye 12GB RAM
Sasa mkuu kwa nini unasema iPhone sio simu, hebu nielimishe na mimi nipate uelewa juu ya hizi simu.