pilipili kichaa
JF-Expert Member
- Sep 3, 2013
- 19,030
- 15,232
POle sana kamanda Lema, Mungu ndie tegemeo lako katu usirudi nyuma!
Ahsante MUNGU Kwa Kuwaponya Lema Na Wenzanke Kwani Bado Tunaitaji Nguvu Zao Katika Kuundea Ukombozi Wa Taifa Hili
Mbunge wa Arusha mjini, Mhe.Godbles Lema amepata ajali ya gari alasiri hii. Ajali hiyo imetokea katika eneo la Burka, karibu na Uwanja wa ndege wa Arusha. Alikuwa akielekea bungeni-Dodoma.
Gari lake-Land Cruiser limegongana na Suzuki. Magari yote mawili yameumia vibaya, hasa Suzuki, kiasi cha kutoamini kama kuna mtu katoka salama. Hata hivyo Mungu ni mkubwa, Mbunge, Dereva wake na watu wengine wako salama.
Ameahirisha safari, amerejea mjini kwa taratibu nyingine, ikiwa ni pamoja na kucheki afya hospitali.
![]()
Ushauri wangu kwa wabunge wa CHADEMA, hasa hawa vijana,
- Ajirini madereva waliosomea kazi hiyo acheni kuokoteza wahuni huko mtaani na kuwafanya ndio madereva wenu.
Wengi wao ni walevi wa pombe na bangi.
Tumeshuhudia SUGU ameshapata ajali zaidi ya nne toka awe Mbunge, ya mwisho ilikuwa ni pale Kitonga. Pia tusisahau tulishampoteza Kamanda Regia(R.I.P) kwenye ajali pale RUVU.
Wabunge huwa wanalipwa fedha kwa ajili ya dereva, ajirini!!
View attachment 259144
Pole sana Lema pamoja na makamanda wengine majeruhi Allah atawaafu.
MUSSA ALLAN, msikilize mwenzio Ritz hapo first page..!
Ukisha msikiliza, niambie ajari hizi zilitokana na nini? Je ni madereva Kanjanja au kuna kitu nyuma ya pazia? Au ni ajari kama zilivyoajri zingine?
1.Ajari ya Salome Mbatia alipokuwa njia kwenda Songea kama sikosei..
2.Ajari ya Mudhihri Mudhihiri alipokuwa akitoka Bungeni kurudi Jimboni kwake.
3.Ajari ya Herson Mwakyembe pale Iringa toka Dar kwenda Mbeya.
4.Ajari ya Edward Sokoine Kitonga akielekea Dareslaam.
5.Ajari ya Juma Akukweti kwa Ndege akitokea Mbeya kwenda Dar.
Ushabiki ni kitu kibaya sana hasa kwenye vitu serious kama hizi Ajari. Hapa tunaona wakati Ajari zilizohusisha wabunge wa Chadema zikiwa Takribani tatu mpaka sasa, Sugu, Regia na Lema,Na waliopoteza maisha ni Mbunge mmoja tu (R.I.P COMRADE) Regia Mtema. Humo ccm Wabunge watatu tumeshawapoteza (R.I.P) Kutokana na ajari hizo huku mmoja akiachwa na kilema cha kudumu.!!
Sasa sijui kama hao wote walipata ajari hizo kutokana na 'Uhuni' wa madereva wao au kunasababu nyingine tofauti na Ulanjanja wa Madereva hao.
Ulimi ukiutumia vizuri ni kiungo Muhimu sana kwa Binadamu, lakini kikitumika vibaya ni kiungo hatari sana kwa Uwepo wa binadamu licha ya kwamba ni yeye mwenyewe ndiye anayekimiliki.!
Watch your Tongue Mister..!!!
BACK TANGANYIKA
ana stress baada ya kujua harudi bungeni tena october anyway pole lema
Mkuu hapa tunashauriana tu, sio mashindano, Kunywa Pombe na kuendesha chombo cha moto ni hatari sana, Muulize Joseph Selasini anafahamu.