Goal Keeper rules...

Goal Keeper rules...

Boardroom

Member
Joined
Dec 28, 2012
Posts
76
Reaction score
11
Vipi ukiishi na mwanamke asiye na kazi wala elimu say maximum form iv... Inakuwaje?
 
Hakuna mwanamke goal keeper siku hizi, sijui huyo wa kwako umemtoa kijiji gani hicho ambacho mpaka leo bado wako usingizini?
 
Vipi ukiishi na mwanamke asiye na kazi wala elimu say maximum form iv... Inakuwaje?

Kwanza fafanua kazi ni nini?
Pili form IV sio kigezo cha kutokuwa na kazi; kama mwanaume utakuwa umeelimika hata kama mwanamke hana ajira ya kuajiriwa wewe mwenyewe inabidi umwajiri. Zipo ajira nyingi binafsi ambazo ukimtumia mke wako (uliyemwita Goli kipa) atakusaidia sana kwenye hizo shughuli.
 
Sijui unaliangalia vipi hili suala, lakini kama ni katika nyanja ya kifedha tu, sio tofauti na ukiwa na mke "goalkeeper" lakini ana PhD
 
pia jua kuwa kulea nako ni kazi,kama analea watoto home,kwanza biblia inasema wababa ndo mtakula kwa jasho,wanawake wao ni kulea,sema sisi tunawasaidia tu,Refer ADAMU NA EVA
 
unapata muda mzuri kweli wa kufunga magoli mazuri coz yupo available any time!
 
Dunia haijawahi kushuhudia mwanamke/mke golikipa.

statement yako inadhalilisha sana wanawake mkuu, waombe radhi.

Hata mke akikaa nyumbani bado anakuwa kuna kazi anafanya ambazo otherwise zingetakiwa zifanywe na mtu kwa kumlipa. Don't underestimate effort za mwanamke kuweka mazingira ya nyumbani vizuri. Kule kufanya kazi kwako ujue behind the scene mwanamke wako kafanya mengi sana mkuu. Hii tunaita ni traditional role of a woman.

Pili, kama unataka mwanamke wako aingize tangible cash inflow (ambayo naamini wewe ndo unaona kuwa ndio kazi), basi atafute either ajira ya kuajiriwa ama ajiajiri mwenyewe.

Kama kazi ya kuajiriwa utaona ina mshahara mdogo, mwendeleze kielimu afikie hatua unayoona inafaa (It is never too late to learn anything in this world)

Kama vipi, mpe mtaji afungue mradi ambao utawaingizia kipato.

Ukumbuke kazi yoyote atakayofanya iwe ya kuajiriwa au kujiajiri, ili iwe na matunda unayotaka lazima benefits expected from zizidi benefit ambazo angeweza kupata/ungeweza kupata kama yeye asingefanya hiyo kazi ya kuajiriwa.

Mfano, assume anapata mshahara wa sh. 100,000 (mapato baada ya kutoa matumizi ya nauli pamoja na lunch akiwa job)

Gharama zake ni
1. kuajiri house girl ili afanye kazi ambazo hawezi fanya kwa sababu umempa kazi zingine
2. Gharama za matibabu, chakula na usumbufu mwingine kutoka kwa house girl)
3. mke wako kurudi kachoka na vi stress vya hapa na pale toka ofisini na hivyo kushindwa kukuburudisha ipasavyo
4. Mkeo kushikwa shikwa hovyo hovyo na wafanyakazi wenzio ama kama ni mama ntilie, vijana kumshikashika makalio n.k. n.k.

So kabla hamjafanya maamuzi kama familia lazima mzingatie mambo mengi sana. Pia nakushauri uanze kuthamini mchango wa mke wako ndani ya familia. Usipende kutumia majina kama golikipa, unamdhalilisha mkeo.
 
oa msomi, she will drive you you will endup having a std iv kama nyumba yako ndogo. what does a man want in a woman? utakuta many highly educated women lacks them. Mid, low and non educated have plenty of those qualities.
 
Vipi ukiishi na mwanamke asiye na kazi wala elimu say maximum form iv... Inakuwaje?

form four ni elimu kubwa kwa tanzania maana anajua kutumia hata simu..

labda sema darasa la saba.. mpeleke veta..
 
sasa kumbe tufanyaje!
cha kumwita mkewe golikipa nini???
ndo apige tu shuti golini aone uwezo wake!
jeuri mwenzie maksudi dadangu!
umeona eeeh!
yeye kama anampenda aoe tu
watapimana uwezo wa kudaka mashuti huko huko
 
Back
Top Bottom